Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 26,313
- 39,699
Nimemsikiliza mzee Butiku hivi karibuni akiwataka vijana kupuuza ushauri wa wanasiasa wanaodai Haki, Uwajibikaji na Katiba ya Wananchi (anaouita ni ushauri potoshi), badala yake anawaasa vijana kumsikiliza na kumheshimu Samia ambaye yeye anasema ANA NIA NJEMA.
Huyu mzee Butiku. Anastahili kuheshimiwa kwa kauli zake hizi? Je Tumuheshimu Samia ambaye
Huyu Butiku haoneshi kuguswa na matatizo na mkwamo unaolikabili Taifa. Anaongea kauli ya kuwa yamepita hayo tugange yajayo na kusamehe aliyoyafanya Samia.
Je Butiku anastahili heshima ama tumpuuze?
Karibu tujadili
Huyu mzee Butiku. Anastahili kuheshimiwa kwa kauli zake hizi? Je Tumuheshimu Samia ambaye
- Hajawahi kuoneshwa kuguswa na matukio ya unyama, ukatili na mauaji ya raia chini ya uratibu wa vyombo vya ulinzi na usalama
- Aliliandaa Jeshi kushiriki uchaguzi Mkuu 2025 kwamba lipo tishio la usalama
- Alitoa amri kwa majeshi kuua kwa kimbari raia hapo Oktoba 29.
- Juzi hapa amenukuliwa akiwasifia raia wa Zanzibar kuwa hawakuuliwa Oktoba 29
- Na mengine mengi
Huyu Butiku haoneshi kuguswa na matatizo na mkwamo unaolikabili Taifa. Anaongea kauli ya kuwa yamepita hayo tugange yajayo na kusamehe aliyoyafanya Samia.
Je Butiku anastahili heshima ama tumpuuze?
Karibu tujadili