MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,256
- 22,322
Sio masikhara kuhusu hili swali. Inawezekana mwanaharakati huru Cprin Musiba ni mtu anayehusudiwa (role model) na vijana wa chama cha Mbowe (CCM B). Kwanini natamka hivi? Kwanza ikumbukwe mwanaharakati huru alikuwa akitukana yeyote aliyehisi ni kikwazo kwenye utawala wa awamu ya 5. Tumeona vijana wa Mbowe nao wakitukana na kumdhalilisha yeyote yule wanayeona ni kikwazo kwa Mbowe. Mbaya zaidi baadhi yao wamekuwa wakinukuu habari zilizowahi kuandikwa na magazeti ya mwanaharakati huru ili kutimiza malengo yao ya kutukana (refer vita ya Mange na MMM). Hata kwenye uzi wangu uliohusu Nabii feki Lema kujibiwa vibaya na mmoja wa vijana wa Mbowe kuna mwanachama wa CHADEMA alijitokeza kwenye comments na kudai anaona ni sawa kwa sababu hata Musiba alikuwa akitukana.
Ni wakati sahihi wa vijana wa CHADEMA kutafuta role model mpya ambaye hujenga hoja nzito kuliko kuendelea kuiga alichokuwa akifanya Musiba kwenye utawala uliopita. Nadhani hata komredi Lucas Mwashambwa anafaa kuwa role model mzuri kwenu kwenye kujenga hoja na sio matusi. Mwisho ninamtupia lawama mwanaharakati huru Musiba kwa alichokifanya wakati wa awamu ya 5 kiasi cha kufanya maelfu ya vijana wa CHADEMA nao kuiga alichokuwa akifanya. Yaani kwa sasa kila uzi ulio na hoja tofauti na wanayopenda kusikia lazima ukute comments zao za matusi.
Ni wakati sahihi wa vijana wa CHADEMA kutafuta role model mpya ambaye hujenga hoja nzito kuliko kuendelea kuiga alichokuwa akifanya Musiba kwenye utawala uliopita. Nadhani hata komredi Lucas Mwashambwa anafaa kuwa role model mzuri kwenu kwenye kujenga hoja na sio matusi. Mwisho ninamtupia lawama mwanaharakati huru Musiba kwa alichokifanya wakati wa awamu ya 5 kiasi cha kufanya maelfu ya vijana wa CHADEMA nao kuiga alichokuwa akifanya. Yaani kwa sasa kila uzi ulio na hoja tofauti na wanayopenda kusikia lazima ukute comments zao za matusi.