Mkuu asante kwa jibu lako fikirishi lakini naweza kujibu kama ifuatavyo:
La kwanza, kama kweli Mungu amekuwepo milele na milele maana yake kabla ya kuumba kitu chochote amekuwepo hapo kwenye space(kadiri ya mdau mmoja hapo juu, kuwa Mungu alikuwa kwenye space kabla ya kuumba chochote) kwa muda infinity(maana yake hana mwanzo). Sasa swali linakuja kwa wanaomuamini, katika Muda huu infinity, Mungu alikuwa anafanya nink hapo kwenye space peke yake? (Kumbuka hiyo ni kabla hajaumba chochote hata malaika)
La pili, mkuu hauwezi ukasema kuwa Mungu yupo pasi na kutanabaisha sifa zake. Yaani sifa ni kama identity ya uwepo wake, kwa mfano, wewe unaamini kuwa mungu ni chanzo cha vitu vyoote. Tayari hiyo ni sifa unayoamini anayo, na hapohapo swali linazuka, Je kama Mungu ni chanzo cha vyoote, je Mungu ni chanzo cha shetani, dhambi na uovu uliomo duniani!?
Nadhani utaona ni jinsi gani watu wanatumia sifa wampazo Mungu kupinga uwepo wake!