Je, Mungu ndiye aliyeumba dhambi?

Je, Mungu ndiye aliyeumba dhambi?

Asante mkuu kwa kujibu!

Kwanza kabla ya kutoa hoja zangu, namimi niseme kitu!
Unajua mkuu, haya mambo ukiyajadili bila kuegamia upande wowote yanaleta raha sana. Kwa kweli kwangu mimi ni burudani tosha hii ninapoona watu kila hoja inayotolewa lazima ihojiwe. Safi sana na huu ndio u great thinker, hakuna kukubali kirahisi rahisi.

Sasa niende kwenye hoja!
Hili la kwanza unalozungumzia, ni kuwa kadiri ya wanaoamini Mungu, ni kuwa Mungu hana mwanzo wala mwisho, maana yake ni wa milele. Yaani kabla ya kuumba hata kitu kumoja, tayari alishakuwepo kwa kipindi Infinity kurudi nyuma. Sasa atuwezi tukasema kipindi infinity ni muda gani kwa kutaja kwa namba!! Yaani ni muda usiotamatika!!. Ona ilivyongumu ku visualize!!

Hoja yako ya pili, mkuu kadiri ya imani yako ni kuwa Mungu ni chanzo cha vitu vyooote. Sasa hapa pia tutahitaji utuelezee, Je, chanzo cha chanzo hicho ni kipi!?
Ndio, kila chanzo kina chanzo, angalia mfano huu, labda tuseme Chanzo cha kifo cha John Doe ni ajali, chanzo cha ajalu hiyo ni mwendo kasi wa dereva, chanzo cha mwendo kasi huo ni kulewa, chanzo cha ulevi wa dereva ni stress, chanzo cha stress, ni usaliti wa mkewe, chanzo cha usaliti wa mkewe ni... chanzo chanzo chanzo mpaka mwisho, na kujirudia rudia humohumo.

Mambo haya yanafurahisha sana!!

Shida iliyopo mkuu ni kwamba sio ya kwamba muda hautamkiki bali ni muda usiojulikana na hii yote ni kutokana na namna binadamu tumeishia kutambua/ kukadiria muda baada ya kuwepo kwa ulimwengu na vilivyomo ndani ya ulimwengu. Hatuna uwezo wa kurudi nyuma kabla ya ulimwengu kuwepo na kutambua muda. Hata wanasayansi wanakadiria umri wa universe kwa kutumia reference ya tukio la bing bang, hawana uwezo wa kujua muda kabla ya tukio la bing bang. Kwahiyo kutojua muda uliotumika kabla hakutaweza kupata jibu la kile alichokuwa akikifanya ni kipi kwasababu inawezekana kumepishana sekunde tu mathalani.

Hoja ya pili ni kwamba ni kweli kwa mujibu wa mawazo yangu; Mungu maana yake ni chanzo cha uwepo wa vyote vilivyopo ulimwenguni. Yawezekana na yeye akawa na chanzo au asiwe na chanzo. kama atakuwa na chanzo basi hicho chanzo chake yeye kitakuwa na neno lingine kutofautisha kati yao. Uwezo wa binadamu umeishia kutambua ya kwamba chanzo/kisababishi cha ulimwengu na vilivyopo ulimwenguni linatumika neno Mungu. Je wewe waona ni kipi kilichosababisha uwepo wa vyote vilivyopo ulimwenguni?
 
Shida iliyopo mkuu ni kwamba sio ya kwamba muda hautamkiki bali ni muda usiojulikana na hii yote ni kutokana na namna binadamu tumeishia kutambua/ kukadiria muda baada ya kuwepo kwa ulimwengu na vilivyomo ndani ya ulimwengu. Hatuna uwezo wa kurudi nyuma kabla ya ulimwengu kuwepo na kutambua muda. Hata wanasayansi wanakadiria umri wa universe kwa kutumia reference ya tukio la bing bang, hawana uwezo wa kujua muda kabla ya tukio la bing bang. Kwahiyo kutojua muda uliotumika kabla hakutaweza kupata jibu la kile alichokuwa akikifanya ni kipi kwasababu inawezekana kumepishana sekunde tu mathalani.

Hoja ya pili ni kwamba ni kweli kwa mujibu wa mawazo yangu; Mungu maana yake ni chanzo cha uwepo wa vyote vilivyopo ulimwenguni. Yawezekana na yeye akawa na chanzo au asiwe na chanzo. kama atakuwa na chanzo basi hicho chanzo chake yeye kitakuwa na neno lingine kutofautisha kati yao. Uwezo wa binadamu umeishia kutambua ya kwamba chanzo/kisababishi cha ulimwengu na vilivyopo ulimwenguni linatumika neno Mungu. Je wewe waona ni kipi kilichosababisha uwepo wa vyote vilivyopo ulimwenguni?
Kwanza Heri ya Krismas mkuu!

Basi kumbe kwa sasa tuachane na hoja ya kwanza, kwamba Mungu amekuwepo kwa muda gani kabla ya kuumba chochote.

Basi, kwenye hoja hiyo ya pili, kuhusiana na imani yako kwa Mungu, kwamba Mungu ndiye chanzo.cha vyote!!

Labda ungetuambia na sisi kinagaubaga ili tuamini sasa kuwa pengine usemayo ndiyo sahihi na watu.wamepoteza muda wao kum model Mungu kwa jinsi waonavyo.

Sasa mimi na maswali kadhaa kumuhusu huyo Mungu ambaye ni chanzo cha yote.

1. Ana weza yote, ana upendo wote na ana nguvu zote mpaka leo!?

2. Ana jinsia? (Yaaani ni ruksa kumuita Mungu bab)

3. Matukio yanayotokea leo, ni yeye ndiye anaya control?

4. (Ntaendeleza mengine kadiri tunavoendelea)
 
Ipo siku ukweli utakua wazi...

Kuna msemo unaosema, if you want to rule them divide them...


Cc: mahondaw
Iwapo ukweli ukawa wazi na ikabainika kuwa ni kweli Mungu yupo na ndiye mwenye upendo mkuu, Je akiwahukumu kwa kuwachoma moto wa milele wale wote ambao hawakumuamini hapo kabla, atakuwa amedhihirisha upendo wake?
 
Mkuu wewe Unaweza kuwa ulisoma chuo kikubwa kama havard au Cambridge,,lakini ukija kutafuta kazi hapa tz au popote lazima ufanyiwe interview.

Swali ni je unapofanyiwa ile interview ina maana kile chuo kikubwa ulichosoma kilikupa cheti ukiwa hujakamilika??

Je, huyu anaekupa mtihani wa interview ana level inayostahili kukupa mtihani kumlinganisha hata na tutor wa pale havard au Cambridge?

Kitu kizuri hujaribiwa ili kuthibitisha ubora wake?

La sivyo wewe na cheti chako cha havard havard ungekuwa unaingia Kazini moja kwa moja maana uko 100% perfect
Sijui kama umeelewa nilichokuuliza. Unampimaje binadamu kwa kumpa mtihani ilihali huyo huyo anayepima ndio huyo huyo aliyemuumba mpimwaji. Kwahiyo kamuumba makusudi awe na mapungufu ili afeli mitihani? Kwani alishindwa nini kumuumba huyo mtu akiwa mkamilifu? Ikiwa wewe ni designer wa magari, umeunda gari kisha ukalipeleka barabarani kwajili ya kulifanyia majaribio na ukagundua gari linamapungufu kwenye matairi lakini hukurekebisha hayo mapungufu. ukaliacha gari litumike hivyo hivyo. Je ikitokea gari limesababisha ajali wewe designer utalilaumu vipi gari wakati wewe ndiye chanzo?
 
Kwanza Heri ya Krismas mkuu!

Basi kumbe kwa sasa tuachane na hoja ya kwanza, kwamba Mungu amekuwepo kwa muda gani kabla ya kuumba chochote.

Basi, kwenye hoja hiyo ya pili, kuhusiana na imani yako kwa Mungu, kwamba Mungu ndiye chanzo.cha vyote!!

Labda ungetuambia na sisi kinagaubaga ili tuamini sasa kuwa pengine usemayo ndiyo sahihi na watu.wamepoteza muda wao kum model Mungu kwa jinsi waonavyo.

Sasa mimi na maswali kadhaa kumuhusu huyo Mungu ambaye ni chanzo cha yote.

1. Ana weza yote, ana upendo wote na ana nguvu zote mpaka leo!?

2. Ana jinsia? (Yaaani ni ruksa kumuita Mungu bab)

3. Matukio yanayotokea leo, ni yeye ndiye anaya control?

4. (Ntaendeleza mengine kadiri tunavoendelea)

1.Kuhusu kuweza yote, upendo na nguvu hilo silifahamu.

2. Kuhusu jinsia ni kwamba hana jinsia yeyote. Kama vile ilivyo energy inaweza kubadilika kwenye hali moja kwenda nyingine.

3.kuhusu matukio yanayotokea leo, ni kwamba yeye ha control tena chochote. Kazi ilishamalizaga kipindi kile kile cha kuumbwa kwa ulimwengu na vilivyomo.
 
1.Kuhusu kuweza yote, upendo na nguvu hilo silifahamu.

2. Kuhusu jinsia ni kwamba hana jinsia yeyote. Kama vile ilivyo energy inaweza kubadilika kwenye hali moja kwenda nyingine.

3.kuhusu matukio yanayotokea leo, ni kwamba yeye ha control tena chochote. Kazi ilishamalizaga kipindi kile kile cha kuumbwa kwa ulimwengu na vilivyomo.
Sawa mkuu, umejibu vyema!

Sasa je,

# kazi yake ni ipi kwa sasa!?

#Je yafaa kumuabudu na kumtukuza kwa sasa?!
 
Kwahiyo kadiri ya hii imani yako ni kuwa hapaswi kuabudiwa, sawa!!

Lakini mkuu, unajua chanzo cha kila kitu, ni vitu vingi sana!?

Kwa maana, kila kitu kina chanzo chake:

Mfano, chanzo cha maralia ni Mbu, chanzo cha kulewa ni pombe, chanzo cha mimba ni ngono, chanzo cha ulimwengu ni bigbang(kadiri ya sayansi) n.k, n.k

Kwa muktadha huu, je hivyo pia ni Mungu wako!? Yaani Mbu, Pombe, Ngono, Big bang n.k, vitu hivi pia umevijumuisha kama ni Mungu wako mkuu!?
Mkuu, kwani huko Kuabudu na kumtukuza kuna mfaidisha/kumuongeza kipi Mungu hadi kwake iwe ni cha lazima?
 
Mkuu, mimi sijajichanganya sehemu yoyote. Kusema kwamba yawezekana mungu yupo, au yawezekana hayupo, huko si kujichanganya. Ila ni kuthibitisha jinsi gani sijui. Kwa kifupi mimi sijui kiuhakika kama Mungu yupo au hayupo.

Ila nyie ambao mnasema kwamba mna uhakika Mungu yupo ndio hapo tunahitaji mtuhakikishie au mtuthibitishie.

Mnaposema Mungu yupo na anaupendo mkuu kwa viumbe vyake, ilihali baadhi ya viumbe wake wasio na hatia wanaangamia kwa majanga ya asili yaliyo ndani ya uwezo wake kuyadhibiti, hapo ndio mnatuchanganya kabisa.

Mnaposema kaumba kila kitu kasoro space (rejea jibu la mmoja hapo juu), kumbe kuna vitu hajaumba, sasa ni nani kaumba space!? Bado mnatuvuruga!!

Tuthibitishieni na tuone kwamba Mungu ndio mwenye sifa hizo, ili wote tuamini kuwa yupo!!
Wewe unasema kwa jinsi Mungu anavyoelezwa na waislamu na wakristo hayupo ila hapo hapo unasema Mungu anaweza kuwepo ila sio huyu wa waislamu na wakristo.

Hapo tupo tunaenda sawa kwanza?
 
Kwahiyo kadiri ya hii imani yako ni kuwa hapaswi kuabudiwa, sawa!!

Lakini mkuu, unajua chanzo cha kila kitu, ni vitu vingi sana!?

Kwa maana, kila kitu kina chanzo chake:

Mfano, chanzo cha maralia ni Mbu, chanzo cha kulewa ni pombe, chanzo cha mimba ni ngono, chanzo cha ulimwengu ni bigbang(kadiri ya sayansi) n.k, n.k

Kwa muktadha huu, je hivyo pia ni Mungu wako!? Yaani Mbu, Pombe, Ngono, Big bang n.k, vitu hivi pia umevijumuisha kama ni Mungu wako mkuu!?

Mkuu unasahau nyuma nilikwambia Mungu ni chanzo cha uwepo wa kitu gani? Je ulivyovitaja hapo unaweza kunitajia ni kipi kimeumba vilivyomo ulimwenguni hadi aitwe ni Mungu?
 
Mkuu unasahau nyuma nilikwambia Mungu ni chanzo cha uwepo wa kitu gani? Je ulivyovitaja hapo unaweza kunitajia ni kipi kimeumba vilivyomo ulimwenguni hadi aitwe ni Mungu?
Sijasahau mkuu, nafikiri ww ndio unasahau kuwa vitu vyote hapa ulimwenguni havikutokea au kuanzishwa kwa wakati mmoja.

Kama kweli chanzo ni big bang, basi wakati ule ilipotokea hakukutokea vitu vingine wakati uleule, mfano miti, viatu na pombe.

Vitu vingine viliendelea kutokea baadaye kutokana na mazingira yalivyoruhusu.

Kwa muktadha huo, hauwezi ukasema chanzo cha vitu vyoooote hapa ulimwenguni ni kimoja, hapana. Kila kitu kina chanzo chake.

Labda useme Mungu unayemuamini ni yule aliyetokeza kitu cha kwanza kabisa, say ulimwengu!!
 
Mkuu, ni mungu yupi huyo ambaye hauwezi kumuelewa!?

Ni huyu wa wakristu? Au wa waislamu? Au wa wabudha? Au wa wahindu!? Au wa mkuu Smt016 ?

Ni yupi unayemaanisha haeleweki kwa akili za mwanadamu?
Huwezi kumuelewa Mungu kwa akili ya kawaida ya kibindam
 
Kila mtu ana uelewa wake kuhusu neno Mungu. Mungu maana yake ni kianzilishi/chanzo (source) cha ulimwengu kuwepo. Hata kisayansi huwezi kuambiwa ulimwengu umejitokeza bila kuwa na chanzo kama vile energy, n.k kwahiyo ile chanzo cha kutokea ndio inatumika neno Mungu kwa maana kilichosababisha/anzisha uwepo wa ulimwengu.

Swali lako la pili ni kwamba muda unaanza kuhesababika baada ya tukio na sio kabla ya tukio kwahiyo huwezi kusema kuwa imepita makarne na makarne wakati hakukuwa na hesabu yoyote ya muda. Inawezekana ikawa hata sekunde haikupita Mungu akaumba ulimwengu hapo hapo. Au mwenzangu unaweza kuniambia Mungu kakaa muda gani kisha ndio akaumba ulimwengu? Au ni karne ngapi zimepita ndipo akaumba ulimwengu?
Sijasahau mkuu, nafikiri ww ndio unasahau kuwa vitu vyote hapa ulimwenguni havikutokea au kuanzishwa kwa wakati mmoja.

Kama kweli chanzo ni big bang, basi wakati ule ilipotokea hakukutokea vitu vingine wakati uleule, mfano miti, viatu na pombe.

Vitu vingine viliendelea kutokea baadaye kutokana na mazingira yalivyoruhusu.

Kwa muktadha huo, hauwezi ukasema chanzo cha vitu vyoooote hapa ulimwenguni ni kimoja, hapana. Kila kitu kina chanzo chake.

Labda useme Mungu unayemuamini ni yule aliyetokeza kitu cha kwanza kabisa, say ulimwengu!!
Post 251 nilishakwambia nini maana ya Mungu. Inabidi uwe unakumbukumbu pia maana tutakuwa tunaenda mbele kisha tunarudi nyuma tena. Ulimwengu na vilivyomo ulimwenguni chanzo ni Mungu.
 
Post 251 nilishakwambia nini maana ya Mungu. Inabidi uwe unakumbukumbu pia maana tutakuwa tunaenda mbele kisha tunarudi nyuma tena. Ulimwengu na vilivyomo ulimwenguni chanzo ni Mungu.
Mkuu, kwa kifupi nilikuelewa hivii:

Mungu ni chanzo cha kila kitu yaani ulimwengu na vilivyomo ulimwenguni.

Nilikuelewa vizuri au sio hivyoo!?
 
Kuna MTU mmoja alishawahi kusema hivi. Kwa Uwezo alionao binadamu, Kuhoji kuhusu Mungu Ni sawa na kuchimba kashimo kwa Mkono pembezoni mwa bahari na kutaka kuhamishia bahari yote katika kale kashimo.

Ova and Out.
 
Back
Top Bottom