mjingamimi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2015
- 46,337
- 57,160
Torati ipi?Mkuu bila shaka maneno haya yako kwenye koran, sasa iweje kwenye torati aseme anamfanya mtu kwa sura yake alafu baadaye ije Koran iseme hafanani na chochote?
Torati ipi?Mkuu bila shaka maneno haya yako kwenye koran, sasa iweje kwenye torati aseme anamfanya mtu kwa sura yake alafu baadaye ije Koran iseme hafanani na chochote?
Tofauti ni uelewa
Mwanzo 1:26-27
“Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.
Kwa mfano wetu ni kusema utu na tabia mienendo.
Mungu alimuumba mwanadamu akampa pumzi, akili, maarifa nk na kumpa majukumu ya kutawala na kuendeleza uumbaji wa vitu duniani. Na ndio maana wanadamu wote tunapata kibali cha kuzaliwa tunatakiwa kuishi kwa kufanya na kukamilisha kile Mungu alichokusudia kwetu mwisho tuondoke.
Na uumbaji katika ulimwengu huu unaendelea kwa wanadamu kutumia karama/vipaji akili na maarifa waliyogaiwa na Mungu. Sasa hivi mwanadamu nae anaumba machines mbalimbali na robots kufanya kile anachokitaka yeye. Na anaziprogram hizo machines na roborts kufanya tuu yale aliyoagiza yeye na sio vinginevyo; kama vile wanadamu tulivyokua programmed na Mungu kupitia maandiko matakatifu ya imani zetu
Je, tunaweza kusema gari linalofanya safari na kubeba mizigo kwa niaba ya mwanadamu au machines, au robots mbalimbali zina kichwa, macho, miguu na moyo kama alivyo mwanadamu??
Torati ipi?
Torati ya Musa
Ni lini Mwenyezi Mungu aliwapa malaika/maserafi/makerubi uwezo wa kushirikiana naye (Mungu) katika kuumba/kufanya?Kwanza na declair interest mimi ni Mkristo na nitatumia Biblia, maandiko mbalimbali ya kikristo, wanatheolojia mbalimbali, maono mbalimbali ya kikristo na yangu Binafsi kuhusu Mungu na kufanana na mwanadamu/Mtu.
NENO: MWANZO 1:26-28 Mungu anasema na tumfanye mtu kwa sura na mfano wetu. Hapa aliongea na watoto wake wa kimbingu kabla ya uumbaji wa mwanadamu. Wana aliokuwa anaongea nao ni viumbe wa kiroho yaani malaika, maserafi, makerubi n.k. Ukisoma Biblia watumishi wa Mungu waliowahi Kutana na malaika walikuwa na sura (Image) na maumbo ya kibinadamu(Image) na sio wanyama.
Watumishi wa Mungu manabii na mitume waliobahatika kumuona Mungu alijifunua kwao kama (Image) mtu/mwanadamu Toka Isaya, Daniel tena alimuona "kama mzee wa siku" hadi Nabii Yohana walimuona "mmoja aliye mfano wa Mwanadamu"(Image)
Hata mimi binafsi nishawahi muona "mmoja aliye mfano wa Mwanadamu (Image)
Kwa hiyo, Mungu anafanania (Image) mwanadamu na hii ipo wazi kwani kabla ya anguko la mwanadamu. Mwanadamu alikuwa mtawala wa dunia na Mungu alimpa atawale kama ambavyo yeye anatawala Mbinguni na hata mwanaye wa pekee a.k.a mwana wa Mmiliki alikuja na kukaa duniani kwa Image kama mwanadamu.
Mkristo ni nani?Kwani Musa alikuwa ni mkristo?
Mkristo ni nani?
[emoji736][emoji736][emoji736]Kwanza na declair interest mimi ni Mkristo na nitatumia Biblia, maandiko mbalimbali ya kikristo, wanatheolojia mbalimbali, maono mbalimbali ya kikristo na yangu Binafsi kuhusu Mungu na kufanana na mwanadamu/Mtu.
NENO: MWANZO 1:26-28 Mungu anasema na tumfanye mtu kwa sura na mfano wetu. Hapa aliongea na watoto wake wa kimbingu kabla ya uumbaji wa mwanadamu. Wana aliokuwa anaongea nao ni viumbe wa kiroho yaani malaika, maserafi, makerubi n.k. Ukisoma Biblia watumishi wa Mungu waliowahi Kutana na malaika walikuwa na sura (Image) na maumbo ya kibinadamu(Image) na sio wanyama.
Watumishi wa Mungu manabii na mitume waliobahatika kumuona Mungu alijifunua kwao kama (Image) mtu/mwanadamu Toka Isaya, Daniel tena alimuona "kama mzee wa siku" hadi Nabii Yohana walimuona "mmoja aliye mfano wa Mwanadamu"(Image)
Hata mimi binafsi nishawahi muona "mmoja aliye mfano wa Mwanadamu (Image)
Kwa hiyo, Mungu anafanania (Image) mwanadamu na hii ipo wazi kwani kabla ya anguko la mwanadamu. Mwanadamu alikuwa mtawala wa dunia na Mungu alimpa atawale kama ambavyo yeye anatawala Mbinguni na hata mwanaye wa pekee a.k.a mwana wa Mmiliki alikuja na kukaa duniani kwa Image kama mwanadamu.
Namalizia kuandaa script ya kukutongoza uwe demu wangu
Hujaelezea kwa Sura yetu
Alikuwa na kina nani?Ukijua wakati Mungu anaumba alikua na kina nani ungeelewa jibu langu
Sawa twende kwenye swali la msingiMkristo ni mfuasi wa yesu kristo
Umepinda kweli wewe ahahahMahari ya huyu demu anapokea mwenyewe fanya haraka
Umepinda kweli wewe ahahah
Ahahahahahahah..Fanya haraka weweeee
Sawa twende kwenye swali la msingi
kiufupi MUNGU hana umbile la aina yoyote,si mtu,si mnyama,si upepo Wala si chochote.
Ila YUPO.
Asante.
Ni kweli Yohana kipindi hiki alikuwa katika kisiwa cha patmo, na kuwa katika Roho alikomaanisha ni HALI YA KUWA KARIBU NA MUNGU, KUWA KATIKA USAFI, UCHAJI NA UTAUWA WA KIWANGO CHA JUU KIROHO, mtu akiwa katika hali hii tunasema yupo katika ulimwengu wa roho, ulimwengu ambao Mungu (Ambaye ni ROHO kamili) huwasiliana/kuzungumza na wanae kiroho... Hivyo Basi Yohana akiwa katika Roho, alipata kumuona huyo mtu mfano wa mwanadamu.. Pengine angekua katika hali ya mwili asingeweza kumuona.
Je mtu huyu alikua ni nani? Jibu liko hapa chini...
Ufunuo wa Yohana 1:17-18
"Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,
na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu."
Mtu huyo ili tumjue hebu tuangalie sifa zake, kimuonekano na zile alizotaja kwa maneno yake kama ilivyosikika kwa masikio na kuandikwa kwa mikono ya Yohana..
Mtu huyu kwanza, Anamuambia Yohana USIOGOPE... Hii ina maana Yeye Hana Hofu (Ameishinda hofu), Tujiulize ni mwanadamu gani hana hofu? Bila shaka yule hakuwa mwanadamu na ndio maana Yohana alisema aliona mtu, mfano wa mwanadamu.
Sifa ya pili, MIMI NI WA KWANZA NA WA MWISHO (ALPHA AND OMEGA), Je ni mwanadamu gani ambaye ni alpha and Omega? Hayupo.. Basi huyu hakuwa mwanadamu Bali ni mtu mfano wa mwanadamu..
Sifa ya tatu, ALIYE HAI, NAMI NALIKUWA NIMEKUFA... Huyu Bwana mkubwa bila shaka yeye ndiye MASIHA, Mwamba wa miamba, Alpha and Omega, Asiye na Hofu.
Sifa ya Nne, Yuko hai hata milele na milele.. Huyu ndiye MFALME wetu Yesu Kristo wa Nazareth.
Sifa ya tano, NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI NA ZA KUZIMU.. Hapa ndipo anapojitambulisha kwa UMUHIMU WA KULE KUFA NA KUFUFUKA KWAKE SIKU YA TATU... Yesu alikufa, Akazikwa AKASHUKA KATIKA WAFU, Huko alienda Kumnyang'anya shetani Mamlaka na Umiliki wa hizo funguo.
Basi bila shaka, Yohana akiwa katika ulimwengu wa roho alionana na kuongea na YESU KRISTO WA NAZARETH, BWANA WA MABWANA, MFALME WA WAFALME, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI, AKETIYE KUUME KWA MUNGU BABA, MWENYE USHIRIKA PAMOJA NASI KUPITIA ROHO MTAKATIFU, AMBAYE KWAKE TWAPATA UZIMA WA MILELE NA TUMAINI LA UHAI WETU..
Bila shaka nimejibu/Nimeeleza ulichotaka, Kama sivo ULIZA TENA.
Kwa hiyo tofauti ni kwamba quran ipo katika lugha ya kiarabu na injili na torati zipo katika lugha za mataifa tofauti, swali ni je una uhakika gani kwamba torati na injili zenye lugha asilia hazipo?
Pili kusoma quran koran kwa lugha ya kiarabu sio hoja, hoja ni je unailewa?