View attachment 1469189
Hongereni Takukuru; na ndio maana tunasema kuna haja ya kuwafanya Meja na Brigedias kuwa wasimamizi wa taasisi za Umma, muhimu wawe na taaluma. Nchi hiyo ya TZ ilishaoza, bila ujeshi ujeshi mambo hayatoenda.
Wananchi oneni kazi ya JPM na tunaposema JPM anapambana na Rushwa muelewe.
Wahusika wanakabiliwa na mashtaka ya kutakatisha fedha zaidi ya bilions of money. Matumizi mabaya ya madaraka ( kujipandisha vyeo hovyo) na kuisababishia hasara serikali.
Pamoja na hayo ; ni wazi kuwa wakurugenzi wengine wachunguzwe; Mkurugenzi wa manunuzi hawezi kuwa salama na hawezi kuwa mbali na matukio ya ubadhilifu wa fedha; Mkurugenzi Mkuu —- Mkurugenzi wa Manunuzi —— Mkurugenzi wa Logistics ( tayari yupo kikaangoni)——- Mkurugenzi wa Rasilimali watu ——— Mkurugenzi wa Fedha. Hii timu inafanya kazi kwa pamoja katika ubadhilifu hivo timu yote hii itapashwa kuingizwa Mahakamani kumsaidia Mkurugenzi wao kujibu mashtaka na wao pia washitakiwe kisheria.
Hawa watu ni matajiri na haijulikani utajiri wao unatoka wapi. Ukitaka kujua shida ya Manunuzi kwa Bohari ya Madawa MSD, tuulizeni sisi tuliowahi kufanya kazi Halmashaui zaidi miaka 3.
Dawa ambayo mtaani utanunua elf 5 , MSD utauziwa elf 30; Na kwakuwa wanakata pesa kwenye ac za hospitali, unakuta huna jinsi.
Hili litazamwe snaa wanatabia ya kuchomeka bei kubwa na kuchukua mzigo mkubwa mwisho wa siku utasikia bohari inateketeza dawa zilizoexpiry zenye thamani ya bilioni nne; whaaaaaaaat , Nakufa!
Expiring zote zichunguzwe kwanini dawa zife na MSD inawateja wa uhakika? Ni kitu ambacho hakiingii akilini; Dawa zinakufa vipi wakati Hosp hakuna dawa!!!!
Ndio maana tunasema hiyo cheni hapo juu ikatwe na watu waanze fresh; vinginevyo Gabriel Sauli hao watu watakuzidi kete kwa vitimbi vyao.
Hii sio chuki kama baadhi ya comment hapo juu; bali Uzalendo wa kweli na pesa zinazopotea huku wazee wetu vijijini wakiendelea kukosa dawa.
Kwa maana hiyo GPSA nayo ifanyiwe kazi ; hizi taasisi za manunuzi hazipo kwa ajili ya kunufaisha watu, zipo kwa ajili ya kutumikia taifa. Ifahamike hivo; Ni wakati sasa wa kuanza kufuatilia ac za wakurugenzi wa GPSA na ku block hizo pesa mapema.
Wengine wanaficha pesa majumbani kwao kwenye mashimo na kuchimbia huko ;transactions zao zote ziangaliwe na kuchunguzwa. Tunataka JPM atoke kifua mbele na hii vita. Mungu Ibariki TZ ; Mungu Wabariki wa TZ , Mungu mbariki JPM.
Brigedia Jen Sauli Mhidize kazi unayo lakini utaweza na ukitaka kuweza kata huo uzi uliokuwa unawaunganisha.
Toa hao wakurugenzi kabisa weka watu utakaofanya nao kazi kizalendo.
Takukuru hongereni; Matunda ya Awamu ya 5 : TZ mbele kwa mbele, Corona tumeishinda : Corona ilikuwa ni Mental Game !