Je, Makonda kavunja mwiko?

Je, Makonda kavunja mwiko?

Nafikili police wanatakiwa wajifunze zaidi kuwa wanasiasa sio wakuwaamini hata siku moja mchana rafiki usiku mnafiki sasa ni muda wa jeshi kujiweka mbali na siasa
 
Uyu bibi leo sijui amekula maharage ya wapi tangu lini police alishakuwa rafiki na raia? Et baada ya Azimio la Arusha ndio polisi walibadilika hiyo historia uliyosoma nahisi imeandikwa kikureshi yani kuruani
 
Polisi wa Leo wauwaji RIP mwangosi...kweli cha kale dhahabu.!!?
 
"Ushujaa" nadhani hata Makonda alidhani hivyo..,,anzia kwa Kabwe.....ngoja nikueleze Makonda angekuwa shujaa Kama angesema hayo katika hali gani...
1. Mpinzani wa serikali.
2. Angekuwa Na cheo cha chini kabisa nje ya kamati ya ulinzi Na Usalama.
3. Angekuwa yeye Mwenyewe Ni polisi...
Neno "Shujaa" lingefi"t Sana hapo

Kwa ujumla, Makonda sio "Shujaa" na huwezi kuwa "shujaa" kwa kusema Tu, Na kitafuta umaarufu hewa.....
Ngoja nikwambie baadhi ya mashujaa WA siasa za Bongo baada ya uchaguzi mkuu hadi Leo Nov. 2016.
1.Bashe
2.Lema
3.Lissu
4.NA wengine wengi...

Hivi anatafuta umaarufu ili awe nani? kwani ana cheo gani?? ni cheo rahisi rahisi tu hicho??

wivu unawasumbua sana

mpaka shoga Lema unamwita shujaa, mziraji wa chakula
 
Afrika kwa ujumla na hususan Tanzania (baada ya Uhuru) Polisi wamekuwa ni watu wa kuogopewa na jamii kama vile nyoka.

Nnakumbuka miaka ya mwanzoni mwa nchi yetu kupata Uhuru Polisi walikuwa ni watu wanaopendwa na jamii, enzi hizo ilikuwa utawakuta polisi wa Kizungu, Kihindi, Kiarabu na Kiafrika.

Kama watoto, kila mmoja wetu alikuwa anatamani siku moja awe askari Polisi. Kilichotupelekea kuwa hivyo ni jinsi enzi hizo polisi walivyokuwa na upole kwa watoto, nnakumbuka wakija mashuleni kutupa mafunzo ya kila aina na kutueleza vipi tuwe raia wema wenye kusaidia wengine. Nnakumbuka pia polisi wakituvusha barabara kwa upole na ingawa magari yalikuwa si mengi.

Nnachokikumbuka zaidi kwa polisi wa siku hizo ni tabasamu zao, awe wa kiume au wa kike (wa kike walikuwa wachache sana), ilikuwa siku zote nikiwaona polisi amma njiani amma wakija mashuleni walikuwa na tabasamu lisilokwisha na wenye nyuso za furaha kiasi cha kukufanya uliye karibu nao uwe na amani.

Hayo yaliisha mara tu baada ya kutangazwa azimio la Arusha.

Baada ya hapo mpaka hii leo, Polisi wamekuwa ni watu wasiocheka na watu, polisi imekuwa ndiyo tishio kwa watoto, mtoto wako akikosa ukimtajia polisi basi anaingiwa na uoga.

Jee, tumejiuliza kwanini? Mimi nna-majibu mengi sana kuhusu hilo lakini nnawaachia wachangia mada nanyi mjinafasi na kutoa dukuduku lenu kwa mtazamo wenu.

Paul Makonda, ameweza kuwasema polisi hadharani, tena kinaga ubaga. Mwiko ambao hata wakubwa zaidi ya Makonda kwenye uongozi wameshindwa kuuvunja kwa hapa kwetu Tanzania na nchi nyingi za Kiafrika kwa ujumla. Jee, kwanini?

Binafsi nnaona kitendo cha Makonda ni cha kishujaa sana. Wewe jee?

Nnaomba tuchangie hii mada huku tukielekeza maoni yetu kwa viongozi wa nchi pamoja na viongozi wa majeshi ya polisi kwa nia ya kuitaka polisi iwe rafiki zaidi wa wananchi na iwe ni kwa ajili ya wananchi na si kwa ajili ya viongozi wa nchi au watawala wa nchi pekee.
AMEWEZA KUWA WA KWANZA KUWA NA UJASIRI WA KUWAPIGA WATU WAZIMA-------- cc Warioba
 
Nafikili police wanatakiwa wajifunze zaidi kuwa wanasiasa sio wakuwaamini hata siku moja mchana rafiki usiku mnafiki sasa ni muda wa jeshi kujiweka mbali na siasa

= nafikiri
 
Makonda anastahili pongezi tena hakuangalia ukubwa wa mtu na kitengo chake,
Lazima tuache unafiki
Penye ukweli pawekwe wazi
Tunahitaji Tanzania yenye viongozi wasio wanafiki
Wafanye kazi kulingana na kiapo chake ,
Umeapa kuwatumikia Watanzania sio vitu vingine.
Kwani makonda na sirro nani mkubwa? Yaani ni km baba amshitaki mtt huyo ni kama wendawazimu
 
= nafikiri

Zingatia Dunia nzima polisi hajawahi kupendwa na raia kwa kipindi kirefu, kwa hapa Tanzania jeshi la mkoloni ndio lilikuwa tatizo kuliko hili la wakina Mura kabla na baada ya hilo azimio lako. Kama well trained police wa US hapendwi itakuwa wa Bongo anaefanya crash programme!?

Matter of fact, nimemuona Kamanda Sirro akiwa Kamanda wa mikoa kadhaa hapa Tanzania na sijawahi kusikia wala kuwa na mashaka na utendaji wake..ana busara, hekima, jasiri, na pia ni mtu anaejituma saana n.k kwa huyu kijana kumdhalilisha kamanda mbele ya kadamnasi ili apate cheap popularity haikubaliki hata kidogo.

Kamanda halali usiku wote anaita radio call na kuhakikisha mkoa huko salama na mkuu wa mkoa kalala salama then from nowhere mkuu huyo huyo wa mkoa ambae kwa umri ni kama mtoto wa kamanda anatomboka maneno mbofu. Pole saana kamanda watu hawajui na hawathamini kazi unayowafanyia..umetoa kafara usingizi wako..kwenye press conference macho ni mekundu..kwa kukosa usingizi ukiwa umekesha vikindu kwenye oparesheni za ngumu. Then kijana mmoja ambae anaamka saa moja na kufika kazini SAA mbili anaamua tu kukudhalilisha.
 
Hii imetokea wakati muafaka kutuma meseji kwa polisi kuwa wasikubali kufanya kazi kwa utashi wa wanasiasa!
Polisi wanapaswa kufuata sheria.
Na hao wanasiasa hawako juu ya sheria.
Unapomtuma askari amkamate mtu lazima liwepo kosa la kisheria, askari naye atamkamata mhalifu au mtuhumiwa kwa kufuata kanuni za kisheria na kisha kumshughulikia kwa mujibu wa sheria.
Askari hapaswi hata siku moja kumkamata mtu au kufanya kazi yake kwa mujibu wa mwanasiasa awe Makonda, awe Mh. Majaliwa.
Wengi waliokamatwa kwa makosa ya shisha imeshindikana kuwafikisha mahakamani kwani mwendesha mashataka ameshindwa kupata "charge" halisi kisheria.

Ni ukweli ulio wazi kuwa shisha sio madawa ya kulevya....ila kuna wapuuzi wachache wanaweza zichanganya na madawa na kudhuru watu.
Hili huweza tokea hata kwa sigara pia.
Lakini ingekuwa busara zaidi kuliko kuwakamata watu wenye leseni za biashara zinazowaruhusu kuuza shisha badala ya kushughulika na watu wa madawa halisi ya kulevya.
 
Makonda amekosa maadili na hana haya hata kidogo.Sirro ni jembe lakini Makonda ni mpenda sufa tu.
 
Wewe bibi unaumwa ugonjwa flani unaitwa PTSD hima fika pale Regency Hospital kwa msaada zaidi.

Zingatia Dunia nzima polisi hajawahi kupendwa na raia kwa kipindi kirefu, kwa hapa Tanzania jeshi la mkoloni ndio lilikuwa tatizo kuliko hili la wakina Mura kabla na baada ya hilo azimio lako. Kama well trained police wa US hapendwi itakuwa wa Bongo anaefanya crash programme!?

Matter of fact, nimemuona Kamanda Sirro akiwa Kamanda wa mikoa kadhaa hapa Tanzania na sijawahi kusikia wala kuwa na mashaka na utendaji wake..ana busara, hekima, jasiri, na pia ni mtu anaejituma saana n.k kwa huyu kijana kumdhalilisha kamanda mbele ya kadamnasi ili apate cheap popularity haikubaliki hata kidogo.

Kamanda halali usiku wote anaita radio call na kuhakikisha mkoa huko salama na mkuu wa mkoa kalala salama then from nowhere mkuu huyo huyo wa mkoa ambae kwa umri ni kama mtoto wa kamanda anatomboka maneno mbofu. Pole saana kamanda watu hawajui na hawathamini kazi unayowafanyia..umetoa kafara usingizi wako..kwenye press conference macho ni mekundu..kwa kukosa usingizi ukiwa umekesha vikindu kwenye oparesheni za ngumu. Then kijana mmoja ambae anaamka saa moja na kufika kazini SAA mbili anaamua tu kukudhalilisha.

Imbecillic!

Hapana, haukuwepo ukoloni, nami nimeongelea polisi hata baada ya ukoloni, from experience au unachokisoma hukielewi?

US nimefika mara kadhaa, si mara moja wala mbili na huwezi nidanganya kuhusu Police wa US. Police wa US hajawahi kuogopwa na wasiovunja sheria.

Police wa Tanzania unaweza mfanyia hivi, hususan FFU?:

2016-10-25T213202Z_1_LYNXNPEC9O1LJ_RTROPTP_0_USA-POLICE_1.jpg


a-football-fan-greets-police-in-riot-gear-as-she-leaves-the.jpg
 
"Ushujaa" nadhani hata Makonda alidhani hivyo..,,anzia kwa Kabwe.....ngoja nikueleze Makonda angekuwa shujaa Kama angesema hayo katika hali gani...
1. Mpinzani wa serikali.
2. Angekuwa Na cheo cha chini kabisa nje ya kamati ya ulinzi Na Usalama.
3. Angekuwa yeye Mwenyewe Ni polisi...
Neno "Shujaa" lingefi"t Sana hapo

Kwa ujumla, Makonda sio "Shujaa" na huwezi kuwa "shujaa" kwa kusema Tu, Na kitafuta umaarufu hewa.....
Ngoja nikwambie baadhi ya mashujaa WA siasa za Bongo baada ya uchaguzi mkuu hadi Leo Nov. 2016.
1.Bashe
2.Lema
3.Lissu
4.NA wengine wengi...
Wengine wengi kina nani
 
Hivi anatafuta umaarufu ili awe nani? kwani ana cheo gani?? ni cheo rahisi rahisi tu hicho??

wivu unawasumbua sana

mpaka shoga Lema unamwita shujaa, mziraji wa chakula
Okay, embu niambie inabidi uwe Na sifa gani Ili uwe mkuu wa mkoa? Alafu linganisha na huyo unaemuita ""sho.g.a"
 
Nashukuru Sana kwa uchambuzi uliotukuka,,, utu uzima dawa bi faiza.
 
Afrika kwa ujumla na hususan Tanzania (baada ya Uhuru) Polisi wamekuwa ni watu wa kuogopewa na jamii kama vile nyoka.

Nnakumbuka miaka ya mwanzoni mwa nchi yetu kupata Uhuru Polisi walikuwa ni watu wanaopendwa na jamii, enzi hizo ilikuwa utawakuta polisi wa Kizungu, Kihindi, Kiarabu na Kiafrika.

Kama watoto, kila mmoja wetu alikuwa anatamani siku moja awe askari Polisi. Kilichotupelekea kuwa hivyo ni jinsi enzi hizo polisi walivyokuwa na upole kwa watoto, nnakumbuka wakija mashuleni kutupa mafunzo ya kila aina na kutueleza vipi tuwe raia wema wenye kusaidia wengine. Nnakumbuka pia polisi wakituvusha barabara kwa upole na ingawa magari yalikuwa si mengi.

Nnachokikumbuka zaidi kwa polisi wa siku hizo ni tabasamu zao, awe wa kiume au wa kike (wa kike walikuwa wachache sana), ilikuwa siku zote nikiwaona polisi amma njiani amma wakija mashuleni walikuwa na tabasamu lisilokwisha na wenye nyuso za furaha kiasi cha kukufanya uliye karibu nao uwe na amani.

Hayo yaliisha mara tu baada ya kutangazwa azimio la Arusha.

Baada ya hapo mpaka hii leo, Polisi wamekuwa ni watu wasiocheka na watu, polisi imekuwa ndiyo tishio kwa watoto, mtoto wako akikosa ukimtajia polisi basi anaingiwa na uoga.

Jee, tumejiuliza kwanini? Mimi nna-majibu mengi sana kuhusu hilo lakini nnawaachia wachangia mada nanyi mjinafasi na kutoa dukuduku lenu kwa mtazamo wenu.

Paul Makonda, ameweza kuwasema polisi hadharani, tena kinaga ubaga. Mwiko ambao hata wakubwa zaidi ya Makonda kwenye uongozi wameshindwa kuuvunja kwa hapa kwetu Tanzania na nchi nyingi za Kiafrika kwa ujumla. Jee, kwanini?

Binafsi nnaona kitendo cha Makonda ni cha kishujaa sana. Wewe jee?

Nnaomba tuchangie hii mada huku tukielekeza maoni yetu kwa viongozi wa nchi pamoja na viongozi wa majeshi ya polisi kwa nia ya kuitaka polisi iwe rafiki zaidi wa wananchi na iwe ni kwa ajili ya wananchi na si kwa ajili ya viongozi wa nchi au watawala wa nchi pekee.

Ungeongezea kidogo namna Azimio la Arusha lilivyobadilisha hali ile. Au unachanganya na uamuzi wa kuingia mfumo wa chama kimoja?
 
Salaam.

Hapa hatuongeleai wala hatuchambui kama kuna ukweli au uongo kwa aliyosema Makonda, hapa tunaongelea ile kuweza kutamka tu aliyoyatamka, kwangu mimi ni ushujaa tosha.
Zilizotolewa ni tuhuma tu na tayari uchunguzi umeshaanza tusubiri taarifa kamili na sio kuanza kuwapa sifa na kuwavimbisha mabichwa wahusika wakati ukweli bado haujabainika.

Je kama mtu alitaka kiki tu ili aonekane anakwamishwa kumbe kashindwa kazi mwenyewe.
 
Hapana, haukuwepo ukoloni, nami nimeongelea polisi hata baada ya ukoloni, from experience au unachokisoma hukielewi?

US nimefika mara kadhaa, si mara moja wala mbili na huwezi nidanganya kuhusu Police wa US. Police wa US hajawahi kuogopwa na wasiovunja sheria.

Police wa Tanzania unaweza mfanyia hivi, hususan FFU?:

2016-10-25T213202Z_1_LYNXNPEC9O1LJ_RTROPTP_0_USA-POLICE_1.jpg


a-football-fan-greets-police-in-riot-gear-as-she-leaves-the.jpg
Mweeeh kipigo utakachokula hutasahau maisha yako yote.
 
tatizo ni lile lile la viongoz wa kipind hiki kutaka kufanya kazi ili waonekane na watu kwe media kwamba wanafanya kazi..hamna lolote....kama waziri mkuu asingekuwa na ratiba ya kuwepo pale cku ile ina maana hizo tuhuma zisngetolewa na kusingekuwa na uchunguz wowote kumhusu kamanda cro..watu waache kufanya kazi ili kuonekana kwe vyombo vya habari
 
Robo shujaa...Angewataja wale wote waliokua wanataka kumuonga angewafikisha Police na baadae Takukuru kwakua Mamlaka alikua nayo ila aliufyata
 
Ushujaa wa Makonda upo wapi kama ameshindwa Kuwakamata hao waliotaka kumpa hizo Ela??

Ushujaa wake upo wapi kama ameshindwa kuwasiliana na PCCB na kuwataarifu kuwa kunawatu wanataka kutoa rushwa??

Ushujaa wake uko wapi kama ameshindwa kuwataarifu police wawakamete hao watu maana yeye anawajua kwa sura na majina??

Ushujaa wake uko wapi kama yeye akiwa mkuu kamati ya ulinzi ya mkoa, anashindwa kuorganise mambo anaishia kuwalaumu watendaji wake wa chini??

MAISHA YA MAIGIZO NA SANAA SIO MAZURI, YANA MWISHO.

MASHUJAA WA KWELI WANATEKELEZA KWA VITENDO.
 
Back
Top Bottom