Je, Makonda kavunja mwiko?

Je, Makonda kavunja mwiko?

Ufinyu wa akili ni pale unapolalamika kuwa kitu hakiko sawa ila haupendekezi kirelebishwe vipi.
Ebu tupia hiyo reform ya polisi ifanyikaje?
sina muda wa kurudia hapa,rejea hotuba za upinzani wizara ya mambo ya ndani kuanzia mwaka 2011-2014
 
mimi ningemwona shujaa kama angewakamata wale waliokuja mpaka ofcn na kujitambulisha kama wauza shisha.

Na wakataka kumwonga kiasi cha fedha ili awalinde wasidhurike na maamuzi ya serikali.

Lakini yeye akawachekea na kuwaambia yeye ni Mtakatifu sana hapokei rushwa na kuwaacha jamaa wakaondoka!

Sasa hapo ushujaa wake upo kwenye matamko? Au angekuwa shujaa kwa kuwachukulia hatua watuumiwa jibu mzee mwenzangu.

Wewe unaonaje?
 
"Ushujaa" nadhani hata Makonda alidhani hivyo..,,anzia kwa Kabwe.....ngoja nikueleze Makonda angekuwa shujaa Kama angesema hayo katika hali gani...
1. Mpinzani wa serikali.
2. Angekuwa Na cheo cha chini kabisa nje ya kamati ya ulinzi Na Usalama.
3. Angekuwa yeye Mwenyewe Ni polisi...
Neno "Shujaa" lingefi"t Sana hapo

Kwa ujumla, Makonda sio "Shujaa" na huwezi kuwa "shujaa" kwa kusema Tu, Na kitafuta umaarufu hewa.....
Ngoja nikwambie baadhi ya mashujaa WA siasa za Bongo baada ya uchaguzi mkuu hadi Leo Nov. 2016.
1.Bashe
2.Lema
3.Lissu
4.NA wengine wengi...


Ukiwa mpinzani unakuwa si shujaa, ni kituko ikiwa mpinzani hapingi.

Ushujaa ni kama alioufanya Makonda, yupo ndani ya "system" na ameweza kukisema chombo hicho hicho ambacho kinaogopewa na waliopo ndani ya "system".

Amma Makonda kavunja mwiko, amma amejitowa mhanga, amma haya ni mabadiliko ya kweli. Lolote linawezekana.
 
Hebu kwanza leta maana ya Neno "USHUJAA" kama ulivyolitumia katika uzi wako kisha tutatoa maoni. Huenda una maana tofauti.
 
Viongozi wa upinzani hasa mh Lema mbunge wa arusha amezungumza mara nyingi zaidi kuhusu udhalimu na uhafidhina wa polisi hapa Tanzania, napata faraja kama na watawala wanaanza kuyaona makosa ya polisi Tanzania, hiki siyo kilio kipya juu ya polisi wetu,
Makonda hajavunja mwiko wowote ila tu maslahi yake yameguswa amejikuta tu analiongea hilo hadharani kwa sababu ya maslahi binafsi, (hajui kwamba anamsaidia mh lema na upinzani kwa ujumla kupaza sauti dhidi ya udhalimu wa polisi wet) nina UHAKIKA waziri mkuu asingezungumza makonda naye asingezumza hayo,

Nina mengi naomba kuhitimisha
 
Hebu kwanza leta maana ya Neno "JASIRI" kama ulivyolitumia katika uzi wako kisha tutatoa maoni. Huenda una maana tofauti.


Sijaona ni wapi nimetumia neno "jasiri" kabla ya post hii katika post zangu za uzi huu.

Hivi huwa mnasoma vitu vilivyomo vichwani mwenu na si vilivyoandikwa au vipi?
 
mimi ningemwona shujaa kama angewakamata wale waliokuja mpaka ofcn na kujitambulisha kama wauza shisha.

Na wakataka kumwonga kiasi cha fedha ili awalinde wasidhurike na maamuzi ya serikali.

Lakini yeye akawachekea na kuwaambia yeye ni Mtakatifu sana hapokei rushwa na kuwaacha jamaa wakaondoka!

Sasa hapo ushujaa wake upo kwenye matamko? Au angekuwa shujaa kwa kuwachukulia hatua watuumiwa jibu mzee mwenzangu.

Wewe unaonaje?
Samahani Mkuu,nilikua naanisha "Shujaa"
 
Kama mkuu wa nchi , alitoa tamko kwamba polisi hatakiwi kuwa karibu na raia, maana yake alikuwa anaimarisha utengano kati uliokuwapo kabla.
 
CCM ndio chanzo cha yote hayo,wacha wafu wazikane.Kila siku wapinzani wanapiga kelele juu ya reform ya jeshi la polisi mnawaona wapuuzi.Leo Makonda kazungumza kidogo mnakimbilia Jf kumuita shujaa,shame.Hv mmerogwaa au?Hao polisi wameanza pigiwa kelele toka lini?Si ndio mkawapa kiburi cha "kupiga tu"?toeni upuuzi,mnatukumbusha machungu


Wapinzani tunawasikia kelele zao lakini hapa mada si upinzani. Mada ni Mkuu wa Mkoa wa Serikali inayotawala.

Siku mpinzani akiacha kupinga itabidi tubaki na chama kimoja tu.
 
Ukiwa mpinzani unakuwa si shujaa, ni kituko ikiwa mpinzani hapingi.

Ushujaa ni kama alioufanya Makonda, yupo ndani ya "system" na ameweza kukisema chombo hicho hicho ambacho kinaogopewa na waliopo ndani ya "system".

Amma Makonda kavunja mwiko, amma amejitowa mhanga, amma haya ni mabadiliko ya kweli. Lolote linawezekana.
Unawez ukawa sahihi, kwamba angekuea "mpinzani" asingeonekana "shujaa" lakini kwa mtu alie ndani ya "system" unadhani Ni dawa kuishia kwenye kutoa shutuma peke yake?

Ni kweli, "shutuma" na "ushujaa" wa Makonda pengine ukaeleta mabadiliko....
 
....
Hayo yaliisha mara tu baada ya kutangazwa azimio la Arusha.
....
Unataka kusema nini hapo? Kwamba nchi iliingia kwenye regime ya kijeshi au? Au kwamba mfumo wa kijamaa/komunisti ambao ndio ulikuwa vision ya Nyerere haukuwa rafiki kama ule kikoloni?
 
Hebu kwanza leta maana ya Neno "USHUJAA" kama ulivyolitumia katika uzi wako kisha tutatoa maoni. Huenda una maana tofauti.


Ni kama hivyo Makonda kuweza kuwa muwazi na kuuliza alichouliza, kinaga ubaga. Kumuuliza kamanda wa polisi swali hilo ni ushujaa mkubwa sana, nnakushauri kaisome tena post namba maoja.
 
Unataka kusema nini hapo? Kwamba nchi iliingia kwenye regime ya kijeshi au? Au kwamba mfumo wa kijamaa/komunisti ambao ndio ulikuwa vision ya Nyerere haukuwa rafiki kama ule kikoloni?


Nilikuwepo.
 
Ni shujaa kweli kweli mpaka kumtuhumu PM kuwa anatoa vibali vya shisha na mpaka leo hajaguswa.
 
Mimi naona kama ni utovu wa nidhamu, kimaadili ya kazi hakutakiwa kujimbizana na wakubwa zake hadharani.

PM na Sirro wana hadhi zao angewafuata ofisini au angesubiri vikao husika.

Sitetei upande kwa vile binafsi sina imani na jeshi la polisi wala Makonda mwenyewe kutokana na tabia zake.

Ila nachoweza kusema tabia hii ikiachwa isiendelee kuna siku atamtuhumu hadharani Mkuu wa Majeshi kuwa anashirikiana na nchi jirani kuhujumu nchi na kuleta taharuki.
 
Makonda oyeeeeeeee big up sana kwa ushujaa uliouonyesha nimekupenda sana waache hawa wakaanga sumu wakuone mjinga na unajipendekeza kwa mukulu lakini wanadaresalaam tunakusapot kwa kile unachofanya. NAKUHAKIKISHIA UTABAKIA KUA MKUU WA MKOA WA DARE SALAAM FOREVER NA HAKUNA WAKUKUTUMBUA KWANI HATA RAISI JPM ANAPENDA JUHUDI ZAKO KWAKUWA HAUOGOPI KITU KATIKA KUTAFUTA MASLAHI KWA AJIRI YA MKOA WAKO.
 
Tatizo si ushujaa wa Makonda. Tatizo ni kuweka mambo katika vyombo vya habari yeye akiwa ni RC hiyo si sawa.
Ni kama vile Mzazi watoto wamekuwa wakorofi halafu anaenda kuwashitaki kwa JIRANI yake, je atakuwa ni mzazi AINA gani?

Jeshi la Polisi kwa mtazamo wangu halihitajiki KUOGOPWA maana la MKOLONI lilikuwa na tabia hiyo. Ndo maana hata sasa jeshi la Polisi limebadili training manual yake na kuleta UHUSIANO WA JAMII na community policing -Polisi jamii!

Maana Polisi akiwa mbali na raia ATAPATA WAPI habari za KIHALIFU?
Wale wanaotisha wananchi ni kwa sababu wanaona wananchi hawajui SHERIA na HAKI zao. Una HAKI ya KUKATAA KUONEWA naPolisi sheria itakulinda!
Ndo maana Polisi wanaojichukulia sheria mikonono mwao WENGINE WAMEFUNGWA!

Kitendo cha Makonda si cha KISHUJAA bali ni KUTOJUA jukumu lake kama RC. Haitajiki kulia lia bali kutoa riport yake kwa mamlaka HUSIKA badala yakuifanya serikali ya Magufuli ionekane ni kama WANAPIGANA wao kwa wao.
Si picha nzuri kwa Kamanda Siro na Makonda pia!
 
Ni kitendo cha kishujaa sana. Jwtz nao wako kikaangoni, askari wake wengi wanajifanya wababe kwa raia na barabarani, ukiwahoji wanaweza kukuchangia kukupiga, wanajenga ukuta na raia! Nidhamu ya uoga dhidi yao ma wananchi ndo kilichopo katikati!

mmewatumia kama mpira wa kiume saa hii mnawananga. Kila siku wapinzani wamekuwa wakiwaambia ukweli hao polisi mkawa kimya. Sasa ndio mnawadhalilisha hapa. Ila ni afadhali ili polisi akili iwarudie watekeleze wajibu wao kwa mujibu wa sheria na sio kiwatii wanasiasa wa ccm.
 
Back
Top Bottom