Je, Makonda kavunja mwiko?

Je, Makonda kavunja mwiko?

Sina uhakika na undani wa sakata hili.
Ninachojua ni kwamba Makonda alikuwa na nafasi (bado anayo) ya kushughulikia hili kwenye kamati ya ulinzi na usalama ambako yeye ni mwenyekiti na Sirro ni mjumbe.
Hivi halijajadiliwa huko?
Makonda anatafuta sifa za kisiasa mbele ya jamii. Kwa nini asiende kwa IGP Mangu kama kweli ana hoja ya msingi?
Anadai watu washisha walitaka kumpa rushwa. Kachukua hatua gani kama si fix za kutaka sifa?
 
Makonda anastahili pongezi tena hakuangalia ukubwa wa mtu na kitengo chake,
Lazima tuache unafiki
Penye ukweli pawekwe wazi
Tunahitaji Tanzania yenye viongozi wasio wanafiki
Wafanye kazi kulingana na kiapo chake ,
Umeapa kuwatumikia Watanzania sio vitu vingine.
 
CCM ndio chanzo cha yote hayo,wacha wafu wazikane.Kila siku wapinzani wanapiga kelele juu ya reform ya jeshi la polisi mnawaona wapuuzi.Leo Makonda kazungumza kidogo mnakimbilia Jf kumuita shujaa,shame.Hv mmerogwaa au?Hao polisi wameanza pigiwa kelele toka lini?Si ndio mkawapa kiburi cha "kupiga tu"?toeni upuuzi,mnatukumbusha machungu
Sasa wewe nawe sijui wa wapi? Hao wapinzani si ndio wanasema rais ni dikteta alafu hili tukio la makonda mmelikemea kana kwamba huyo Siro hawezi kupoke rushwa!
 
Kabla ya kumwita Makonda "shujaa" tungesubiri kwanza TAKUKURU wamalize kazi. Kwangu zile ni tuhuma tu, na duniani hakuna shujaa wa tuhuma, kuna shujaa wa kusema ukweli tena ukweli mtupu usio na shaka. Tusije kumwona hero sasa na baadaye tukamwona zero. Tusubiri TAKUKURU...!
 
Ni kama hivyo Makonda kuweza kuwa muwazi na kuuliza alichouliza, kinaga ubaga. Kumuuliza kamanda wa polisi swali hilo ni ushujaa mkubwa sana, nnakushauri kaisome tena post namba maoja.

sema ni shujaa ndani ya ccm maana jeshi la polisi mmeligeuza kitengo cha ccm. Hao mapolisi kila siku watu wanahoji weledi wao kasoro wanaccm, ila sasa ndio mnaamka
 
Lema ana ushujaa gani? Wa "kuota" wakati hajalala??
Shujaa anaeweza kusimama katikati ya dimbwi la wadhalimu na kusema hapana sasa tosha na kutete haki za wanyonge. Lema ataingia kwenye vitabu vya historia kama mbunge jasiri na hasie ba uoga kwa kusema kile anacho amini ni ukweli.
 
Wapinzani tunawasikia kelele zao lakini hapa mada si upinzani. Mada ni Mkuu wa Mkoa wa Serikali inayotawala.

Siku mpinzani akiacha kupinga itabidi tubaki na chama kimoja tu.
kwahiyo unachojaribu kusema ni kuwa sasa mmoja wa watawala has come to his senses,kumbe mpaka wapigiwe kelele hivi ndio wasikie.Bado mkubwa wake naye,atasikia tu.
 
Sasa wewe nawe sijui wa wapi? Hao wapinzani si ndio wanasema rais ni dikteta alafu hili tukio la makonda mmelikemea kana kwamba huyo Siro hawezi kupoke rushwa!
unachangia utafikiri uko kwenye taarabu!Tumelikemea mimi na nani?Unaweza weka ushahidi hapa wa kiongozi yeyote aliyesema kwa niaba ya upinzani kuwa wamelikemea?sio lazima uchangie,jipe muda uwe unasoma michango ya wenzako tu,ukiiva ndio nawe utie pua humu
 
Ajira ya Paul Makonda kwa sasa inamlinda... Polisi wanamuangalia tu...
Jeshi la polisi linadumu...
Ajira ya Makonda itakapoisha ndio tutajua kama Makonda kavunja mwiko au polisi wanasubiri muda ufike...

Ajira yake iishe afu aseme hadharani namna ileile kuwa Sirro kapewa Rushwa... hapo ndio tutalijua jeshi la polisi lina uvumilivu.
Ghafla nimejikuta nakumbuka tukio la kukamatwa kwa aliekua Boss wa jeshi bwana Laurent Masha.
Mara tu baada ya kutoka kwenye kiti ama cheo cha kupewa
 
unachangia utafikiri uko kwenye taarabu!Tumelikemea mimi na nani?Unaweza weka ushahidi hapa wa kiongozi yeyote aliyesema kwa niaba ya upinzani kuwa wamelikemea?sio lazima uchangie,jipe muda uwe unasoma michango ya wenzako tu,ukiiva ndio nawe utie pua humu
Tatizo lako una kimuhemuhe sijui unakimbizwa?

Chadema wote hapa wanaona Makonda anatafuta sifa, sasa wewe utaniambia nini?

Huyo Siro ni nani asipokee rushwa? Wewe mgeni nchi hii?
 
Kuwa na adabu bibi unawezaje kusema makonda ni shujaa wakati uchunguz wa vyombo husika haujaleta majibu kuwa tuhuma yake ina ukweli au la na hata ikiwa itaonekana kuna ukweli basi wa kuprove kuwa sirro na kaganda wanatuhuma ni mahakama na si vinginevyo.Unampaje mtu credit wkt ishu haijawa proved au huo udas uliopewa unakufanya uendelee kujipendekeza ww.
 
Tatizo lako una kimuhemuhe sijui unakimbizwa?

Chadema wote hapa wanaona Makonda anatafuta sifa, sasa wewe utaniambia nini?

Huyo Siro ni nani asipokee rushwa? Wewe mgeni nchi hii?
Mkuu mbona hizo ni tuhuma tu? Kuna ushahidi wowote mpaka sasa kwamba Siro kapokea rushwa?
 
Tatizo lako una kimuhemuhe sijui unakimbizwa?

Chadema wote hapa wanaona Makonda anatafuta sifa, sasa wewe utaniambia nini?

Huyo Siro ni nani asipokee rushwa? Wewe mgeni nchi hii?
Hivi CHADEMA ni nani?kwahiyo nami kwa uchangiaji wangu umeshaniita CDM?Jukwaa hili kuna kipengele cha kuweka status yako kichama?Unamjuaje mtu kama ni CDM?Amekupa kadi yake ya uanachama?Unajadili kitoto sana,toa hoja sio kupiga mipasho tu.Hii ni JF sio facebook
 
Back
Top Bottom