Je, kuna maisha mengine baada ya hapa duniani?

Shwain
 
Ukifa umekufa hakuna maisha baada ya hapo. Dini na vitabu vyake vimekuja ku regulate tabia za binadamu na kututawqla kutengeneza inferiority kwetu.
Waliokufa kabla ya hizi dini walienda wapi??
 
Ukifa umekufa hakuna maisha baada ya hapo.
Uthibitisho uko wapi?

Dini na vitabu vyake vimekuja ku regulate tabia za binadamu na kututawqla kutengeneza inferiority kwetu.
Unaweza kuweka mfano mmoja, labda? Jinsi ambavyo dini inajenga unakisihi changamani (inferiority complex)?

Waliokufa kabla ya hizi dini walienda wapi??
Tambua kwamba dini (kwa mantiki ya imani juu ya Mungu), ni ya kale kama ulivyo ubinadamu wenyewe.

Dini imekuwepo mara tu wanadamu walipoumbwa.

Unasomaje Maandiko? Wapi hapo imesema hakuna maisha baada ya kifo?

Maandiko ambayo umenukuu yanasema tu kwamba mtu afapo, anakoma kuishi kwa vyovyote vile -- kiroho, kimwili, kiakili.

Lakini kuhusu nini kitatokea baadaye, maandiko husika hayasemi chochote.

Ukisema:
Watu wa kizazi hiki hawalali kabisa.

Je, maana yake ni kwamba hawalali kabisa siku zote?

Hivi siyo kwamba kauli hiyo inazungumzia kipindi fulani mahususi?

Maandiko hayo pia yanapaswa kueleweka kwamba kwa kipindi mtu afapo, awapo kaburini, muda huo hakuna chembe yoyote iliyopo ya uhai wake, ama kiroho, kimwili, au kiakili.

Mtu huyo anakuwa amekoma kuwepo, kana kwamba hakuwahi kuzaliwa kamwe.

Lakini maandiko hayo hayasemi chochote kuhusu kudumu katika hali hiyo ya umauti milele.

Umewahi kusikia kuhusu habari ya ufufuo wa wafu?

The dead remain in their grave until resurrection -- when Jesus Christ will call them forth from their grave for judgment.
 
Uliza swali moja ueleweke na ujibiwe sio unaandika insha
 
Nice comment
 
YOLO! You only live once and die for such a long time
Everybody knows that ^a long time^ doesn't mean forever. Does it?

You really have some splanin' to do!
Uliza swali moja ueleweke na ujibiwe sio unaandika insha
Acha uvivu na ufinyu wa akili, wewe. Hoja na maswali yote yanategemea hoja na maswali yaliyopita.

Shule ulisomea wapi kwani?
 
Nafsi pekee inakiri hilo huku haijijui kama wewe ushahidi mwepesi kama mzee yule kaishi maisha ya kusema Mungu hayupo mpaka uzee wake aling'atwa na mbwa akabatizwa yote ni maandalizi ya aendako kingine usingizi nalo ni jawabu tosha
Tatizo unachanganya wanaoamini Mungu hayupo na wanaoamini dini za ukristo na uislam siyo dini za WAAFRIKA wamebambikizwa na wao kuzipokea pasipo kujiongeza.
 
Kama we hutaki kuamini vitabu vya dini Basi usiwahi kusema Kwamba hamna maisha baada kifo kwa sababu unaongea kitu usichokijua,
Ukiulizwa je Kuna maisha baada kifo sema sijui ,Kama vile ulikuwa hujui Kama utawahi kuishi duniani Ila umeishi ndo umejua Kuna maisha duniani.
Wanasayansi hamuamini msichokiona Wala kukiskia Sasa mbona unaamini kuwa hamna maisha wakati hujafa subiri ufe ndo upate jibu.
Kwa sisi tunaomini dini tunasema yapo kwa sababu tunaamini tusiyo yaskia Wala kuyaona Ila kwa elimu inyotoka kwa muumba ,
Imani inaambatana na elimu ,Soma ujue Kisha amini.
 
Hivi wakuu tukiacha hizi nadharia na dhana zingine za kufikirika kuhusu hatima yetu baada ya kifo.

Nataka tuongee kiume sasa.

Hivi ni kweli tukifa kuna mahali tunaenda au ni siasa na kufarijiana tu ilmradi maisha yasonge?
Mkuu cha kwanza kabisa amini kama Mungu yupo na siku ya mwisho siku ya kulipwa matendo yako yote uliyofanya Dunian ipo pia, so kuna maisha mengine baada ya kifo yapo na utayakuta...
 
Mungu ni nini? Na yuko wapi? Kazi yake katika maisha yako ni nini?

Unasemaje kuhusu mada iliyoandikwa humu siku za nyuma,ilikuwa inasema uingo mkubwa ulowahi kutokea duniani?! Unadhibitishaje kwamba kinachoongelewa si kweli?
Oya vitu vyengine mnakufuru wazee
 
Ndio kuna hali nyingine ingawa sio maisha kama haya.Yakoje..mimi sijui lkn niko na uhakika 100% yapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…