Je, kuna maisha mengine baada ya hapa duniani?

Je, kuna maisha mengine baada ya hapa duniani?

Siyo kweli. Akiolojia na sayansi vinathibitisha juu ya ukweli na usahihi wa Biblia.

Habari zilizoandikwa kwenye Biblia ni mambo halisi, kama tusomavyo kuhusu matukio ya vita vya dunia, au hata migogoro ya sasa baina ya Palestina na Israeli.

Mungu alimuumba Mariam , halafu Mariam akamzaa huyo mungu ( Yesu) ... Ni kichaa pekee ndio anaweza kuamini hii contradictory logic

Yaliyomo kwenye Biblia, siyo tu kwamba ni habari za kihistoria, bali pia ni uvuvio mtakatifu ulioandikwa na watu halisi wakiomcha Mungu, mfano Musa, Daudi, Sulemani, Daniel.

Kumcha mungu ni nini ? Kwanini huyo mungu kaumba watu Dunia nzima ila hao watu wa middle east ndio waonekane ndio waliomcha! Kwanini hatuoni wazaramo au warangi kwenye hivyo vitabu kati ya watu waliomcha huyo mungu



Watu hawa wote ni wahusika halisi katika historia, wala si wahusika dhahania (fictional characters).

Ujumbe wao mahususi wa uvuvio kutoka kwa Mungu umetufikia sisi kupitia Biblia.

Viumbe vinakufa kwa sababu ya dhambi, kwa sababu ya uchaguzi mbaya wa Lusifa ama Shetani, kwa sababu mwanadamu alikubali naye kufuata njia ya Lusifa, akamwasi Mungu.
Kama sababu za binadamu kutenda dhambi ni Shetani kwanini mungu anaeijua kesho hakuacha kumuumba Shetani? Aliumbaje kiumbe alichojua kinaenda kumfanya binadamu atende dhambi halafu anahukumiwa na mungu Kwa kutenda dhambi Shetani ?

Lusifa alitumia uhuru wake vibaya. Mwanadamu naye alitumia uhuru wake vibaya.

Mungu muweza wa yote kwanini hakuumba binadamu wakamilifu wanaoweza kutumia uhuru wao vizuri

Kufa kwa viumbe haina maana kwamba mpango wa kuishi milele umetoweka. Kifo kimekuja kwa sababu ya dhambi.
Watoto wadogo wanaokufa na wao wametenda dhambi Gani ? Halafu kwanini dhambi za watu wachache waje wabebe watu wengine. Huyo mungu anaesema Kila mtu atabeba mzigo wake kwanini wale waliovunja Sheria za bustani ya eden wasibebe dhambi zao halafu wengine tuendelee kuishi milele!
Lakini pia mauti siyo mwisho wa mambo. Kuna maisha baada ya mauti, kwa wale ambao wamechagua kuufuata mpango wa Mungu wa wokovu kupitia Yesu Kristu.

Alijua. Mungu anajua mwisho toka mwanzo. Anajua yote. Isaya 46: 9, 10. Kila kitu ki wazi mbele Yake. Ebrania 4:13.

UPUMBAVU

Hii ndiyo maana Biblia inasema mpango huo uliandaliwa muda mrefu tangu kuwekwa misingi ya dunia. Ufunuo 13:8

Kutokea kwa dhambi haina maana kwamba mpango Wake umezuiwa. Dhambi katika mpango wa Mungu, ni sawa mfano wa njia mbovu kwa msafiri.

Mungu hakushtukizwa na dhambi wakati akimuumba Lusifa, malaika walioasi na hata mwanadamu ambaye ameanguka.

Alijua na aliliona hilo mapema, ndiyo maana akaandaa mpango mahususi, mkamilifu ili kukidhi hali hiyo ya dharura kabla ya kutimia kwa mpango Wake.

Ukamilifu wa mpango huo uko katika makusudi husika, namna ya utekelezaji na hatimaye matokeo yake.

Mungu angeweza kutumia njia nyingineyo, lakini uchaguzi Wake wa kuanza kushughulikia dharura ya dhambi ndilo jambo bora zaidi ambalo lingekuwa na manufaa kwa viumbe Wake wanadamu kwa malaika, milele na milele.

Kuasi kwa Lusifa kuliambatana na hoja zake mahususi (incendiary postulations) dhidi ya Mungu ambazo pekee zingeweza kujibika kikamilifu mazima milele (completely & finally forever), kwa mujibu wa silika takatifu na yenye upendo ya Mungu, kwa kuwaruhusu viumbe Wake wenye utashi huru japo ^wachungulie^ ng'ambo ya pili na kuhabiri maisha nje ya Mungu.

Kwa maneno mengine, kuasi kwa Lusifa ilikuwa fursa ya Mungu kumthibitishia vinginevyo dhidi ya fikra zake kinyume na Muumbaji.

Unapozungumzia Mungu mwenye upendo timilifu na mwanadamu (au hata malaika) mwenye utashi huru, ni rahisi kutambua kwa nini viumbe wenye uwezekano wa kutenda dhambi waliumbwa.

Ni kana kwamba Mungu, ili kudhihirisha upendo Wake wa juu zaidi kwa mwanadamu na malaika na viumbe Wake wengine wenye nadhari za juu za maarifa, aliamua kuumba nafsi zenye utashi huru zikiakisi utashi Wake Mwenyewe.

Mwanadamu ameumbwa katika sura na mfano wa Mungu. Huo ndio upeo wa upendo wa Mungu.

Kudai kwamba Mungu alishindwaje kuumba dunia isiyo na uwezekano wa kufikwa umauti ni kutotambua silika na baraka kuu ya Mungu kwa viumbe Wake -- upendo.

Pia, kudai kwamba Mungu alishindwaje kuumba dunia isiyo na uwezekano wa kufikwa na dhambi na mauti ni sawa na kudai kwamba kwa nini Mungu asingetuumba tukiwa watii tarasili (automatic obedients), tulio radhi wakati wote, na tusio tayari katu wala wenye uwezekano wowote kabisa wa kubadili msimamo huo -- watii halaki (blind obedients), unaweza kusema.

Kama hilo angelifanya Mungu, basi tusingekuwa tumeumbwa katika ^sura na mfano Wake.^

Kwa namna hiyo, tusingekuwa tunamtumikia kutokana na moyo wa upendo, bali kwa kusukumwa na hulka asili ndani yetu iliyotarakibiwa awali (intrinsically preprogrammed nature) -- tungekuwa mithili ya roboti.

Matokeo yake, tungekosa utashi huru, ambayo ni tunu bora zaidi miongoni mwa amana alizotubarikia Maulana.

Pamoja na tunu hii kuu, ukaja pia uwajibikaji kwa upande wa mwanadamu kuhusu matumizi husika. Na ndipo hatari kuu ikafuatia. Lakini huo haukuwa mwisho wa mambo.

^Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.^ ~ 1 Korintho 15:22

Mungu hajashindwa kitu, na wala kushindwa hakupo katika asili Yake takatifu.

Ubongo wa mwanadamu ndio unakataa kukubali mambo jahara aliyoyafunua Mungu kuhusu mpango Wake kwetu.

Hivi inawezekanaje Mungu wa milele, aliyeumba vitu vyote, hata ahusishwe na msamiata wa kushindwa?

Ni wazi kwamba kudai Mungu ameshindwa, hilo tu kwa lenyewe ni kumkufuru.

Kila jambo analotenda Mungu, kila kitu anachoruhusu kitendeke, huwa kina kusudi maalumu.

Na ndiyo maana dunia, baada ya dhambi, wadhambi, Shetani na malaika zake kutokomezwa milele, bado itakuwa sehemu ya kutimizia lengo hilo la awali la Mungu

^1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.

3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, Naye atafanya maskani Yake pamoja nao, nao watakuwa watu Wake. Naye Mungu Mwenyewe atakuwa pamoja nao.

4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.

5 Na Yule aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.

6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yule mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.

7 Yule ashindaye atayarithi haya, Nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

27 Na ndani yake hakitaingia kamwe chochote kilicho kinyonge, wala yule afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo.^ ~Ufunuo 21
 
Kim Jong Jr hapo juu uliponinukuu ungepaswa kutenganisha maoni yako, na yale ambayo mimi nimeandika.

Kitendo cha kufanya nisomeke kana kwamba nimeandika maoni yako, ambayo ni potofu, siyo cha kiungwana hata kidogo.

Naomba Moderator liangalieni hili maana ni kasoro ya App yenu.
 
Well huo ni mtazamo wa kibinadamu,
Lakini hata Sisi binadamu, hatukutokea tu, kuna master planner alituweka hapa.
Na yeye kupitia vitabu vyake(wengine hawaviamini) kasema kuna maisha baada ya kifo,
Ukiona mtu ana simu ya tekno au I phone, moja kwa moja unaamini imetoka china, au USA, na, samsung imetoka Korea, na unanunua unatumia,ukiamini kabisa ma designer wa USA wapo vzr kuliko china, na unaona ufahari kuwa na Iphone kuliko Tecno! Richa ya kwamba hujawahi, hata kuvuka chalinze achilia mbali kuona hiyo Iphone ikitengenezwa!
Ni logic ndogo tu, na wengi wa wale wanaodai hakuna maisha baada ya kifo, hata elimu ya dini kidogo hawana, hawawezi hata kukupa Historia ya vitabu vitakatifu, ka elimu kadogo, kasoma vijarida na kusikiliza upuuzi wa story book, anakuja hapa mishipa ya shingo imemsimama,
Kuna vitu vingi watu wa kawaida hawajuhi, chukua muda uwasome uwasikilize viongozi, wa dini(sio mwamposa, wale wenye PHD za theology), mapadre, Mashekh kama Dr Naik wa peace TV, Myles Munroe, TD Jakes, John hagee,na wasomi wengine kama Chris Mauki,Vusi Thembekwayo, Bagonza nk,
Sikiliza waliobobea kwenye maswala ya dini, kuna kitu utajifunza.
Sio una sikiliza story book, kutoka kwa form 4 leaver, then unajiona umebokuuuuuuaaaaaa!
 
Kim Jong Jr hapo juu uliponinukuu ungepaswa kutenganisha maoni yako, na yale ambayo mimi nimeandika.

Kitendo cha kufanya nisomeke kana kwamba nimeandika maoni yako, ambayo ni potofu, siyo cha kiungwana hata kidogo.

Naomba Moderator liangalieni hili maana ni kasoro ya App yenu.
Kwanini usimuombe mungu atenganishe nilichokichanganya kwenye andiko lako ?


Unakimbilia Kwa moderators , je wana nguvu kuliko mungu ?
 
Well huo ni mtazamo wa kibinadamu,
Lakini hata Sisi binadamu, hatukutokea tu, kuna master planner alituweka hapa.
Na yeye kupitia vitabu vyake(wengine hawaviamini) kasema kuna maisha baada ya kifo,
Ukiona mtu ana simu ya tekno au I phone, moja kwa moja unaamini imetoka china, au USA, na, samsung imetoka Korea, na unanunua unatumia,ukiamini kabisa ma designer wa USA wapo vzr kuliko china, na unaona ufahari kuwa na Iphone kuliko Tecno! Richa ya kwamba hujawahi, hata kuvuka chalinze achilia mbali kuona hiyo Iphone ikitengenezwa!
Ni logic ndogo tu, na wengi wa wale wanaodai hakuna maisha baada ya kifo, hata elimu ya dini kidogo hawana, hawawezi hata kukupa Historia ya vitabu vitakatifu, ka elimu kadogo, kasoma vijarida na kusikiliza upuuzi wa story book, anakuja hapa mishipa ya shingo imemsimama,
Kuna vitu vingi watu wa kawaida hawajuhi, chukua muda uwasome uwasikilize viongozi, wa dini(sio mwamposa, wale wenye PHD za theology), mapadre, Mashekh kama Dr Naik wa peace TV, Myles Munroe, TD Jakes, John hagee,na wasomi wengine kama Chris Mauki,Vusi Thembekwayo, Bagonza nk,
Sikiliza waliobobea kwenye maswala ya dini, kuna kitu utajifunza.
Sio una sikiliza story book, kutoka kwa form 4 leaver, then unajiona umebokuuuuuuaaaaaa!
kama binadamu alitokea Kwa master planner na huyo master planner alitokea wapi? Chanzo hakipaswi kuishia Kwa master planner lazima turudi nyuma tujue na huyo master planner alitokea wapi! By this logic Chenye chanzo kina chanzo.


Huyo mungu kwanini atumie watu wengine Ili yeye ajulikane ( hao uliowataja). Kwanini asiumbe binadamu awe anamjua mungu by default pale anapozaliwa ? Yeye mungu anaeijua kesho yetu kwanini aumbe binadamu anaemjua kesho atatenda matendo yasiyompendeza mungu na Kisha anamuhukumu huyo binadamu.

Hivi wewe unajua mtoto wako kesho atazini na nguvu za kumfanya asizini unazo ila unamuacha azini halafu unampa na adhabu! By the way hata hiyo dhambi ya kuzini muasisi wake sio yeye bali ameikuta!


Huyo mungu wenu ni muonezi na dictator! NDIO!

Hizi ni hadithi za uchwara
 
kama binadamu alitokea Kwa master planner na huyo master planner alitokea wapi? Chanzo hakipaswi kuishia Kwa master planner lazima turudi nyuma tujue na huyo master planner alitokea wapi! By this logic Chenye chanzo kina chanzo.


Huyo mungu kwanini atumie watu wengine Ili yeye ajulikane ( hao uliowataja). Kwanini asiumbe binadamu awe anamjua mungu by default pale anapozaliwa ? Yeye mungu anaeijua kesho yetu kwanini aumbe binadamu anaemjua kesho atatenda matendo yasiyompendeza mungu na Kisha anamuhukumu huyo binadamu.

Hivi wewe unajua mtoto wako kesho atazini na nguvu za kumfanya asizini unazo ila unamuacha azini halafu unampa na adhabu! By the way hata hiyo dhambi ya kuzini muasisi wake sio yeye bali ameikuta!


Huyo mungu wenu ni muonezi na dictator! NDIO!

Hizi ni hadithi za uchwara
Bro kama Mungu anakuwa na chanzo huyo sio Mungu tena, Mungu hafungwi na muda,
Bro najua wewe una amini una akili, lakini bila Shaka, hujawahi kuziona akili, Ila unaamini unazo! Ni, logic ndogo tu, there is no way we just happened to be here! In our body, na mifumo yote ya kimwili, digestion system, nerve system nk, surely some baby designed it! He/she had to exist beyond matter, time, nk.
 
kama binadamu alitokea Kwa master planner na huyo master planner alitokea wapi? Chanzo hakipaswi kuishia Kwa master planner lazima turudi nyuma tujue na huyo master planner alitokea wapi! By this logic Chenye chanzo kina chanzo.


Huyo mungu kwanini atumie watu wengine Ili yeye ajulikane ( hao uliowataja). Kwanini asiumbe binadamu awe anamjua mungu by default pale anapozaliwa ? Yeye mungu anaeijua kesho yetu kwanini aumbe binadamu anaemjua kesho atatenda matendo yasiyompendeza mungu na Kisha anamuhukumu huyo binadamu.

Hivi wewe unajua mtoto wako kesho atazini na nguvu za kumfanya asizini unazo ila unamuacha azini halafu unampa na adhabu! By the way hata hiyo dhambi ya kuzini muasisi wake sio yeye bali ameikuta!


Huyo mungu wenu ni muonezi na dictator! NDIO!

Hizi ni hadithi za uchwara
Yes najua kesho mtoto atazini,na nitamuadhibu, lakini good news ni kuwa, ana free will, anaweza akakataa kuzini vile vile, na akizini, toba IPO, anapata msamaa
 
hapa DUNIANI SIO KWETU MAKAZI YETU YAPO MBINGUNI.
Tumekuja tutapita..
Tutakwenda kuhukumiwa kutokana na mate ndo yetu.
Umedhulumu mtu utakwenda kumlipa,umemuua mtu utakwenda kumlipa,umempiga utakwenda kumlipa n.k
Haiwezi KUPITA HIVI HIVI.

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
 
Imani kitu Cha ajabu sana watu mnaamini Kuna watakao kwenda kuchomwa moto mkali milele,wengine mnaamini Kuna watakao imba na malaika milele,wengine mnaamini Kuna mabikra wanawasubiria huko akhera kwenye mabwawa ya tungi ni kula starehe milele!!
Mi sielewi
Katika hayo kuna ya ukweli na uongo.
 
Hivi wakuu tukiacha hizi nadharia na dhana zingine za kufikirika kuhusu hatima yetu baada ya kifo.

Nataka tuongee kiume sasa.

Hivi ni kweli tukifa kuna mahali tunaenda au ni siasa na kufarijiana tu ilmradi maisha yasonge?
Subili wazungu waje wakupe ukweli sababu ndio unao waamini sidhani hapa kama kuna utakae muamini
 
Tahadhari tu kwamba hao wanaoharakisha kuwahakikishieni kwa ujasiri wote kwamba hakuna maisha baada ya mauti, hawajawahi kufa kamwe.
Kama ambayo hao wanaowaharakishieni kuwaambia kwamba Kuna maisha baada ya kifo hawajawahi kufa kamwe. The vice Versa is true chief.
 
hapa DUNIANI SIO KWETU MAKAZI YETU YAPO MBINGUNI.
Tumekuja tutapita..
Tutakwenda kuhukumiwa kutokana na mate ndo yetu.
Umedhulumu mtu utakwenda kumlipa,umemuua mtu utakwenda kumlipa,umempiga utakwenda kumlipa n.k
Haiwezi KUPITA HIVI HIVI.

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
umesema vema mkuu. lete proof tufunge huu uzi
 
Hivi wakuu tukiacha hizi nadharia na dhana zingine za kufikirika kuhusu hatima yetu baada ya kifo.

Nataka tuongee kiume sasa.

Hivi ni kweli tukifa kuna mahali tunaenda au ni siasa na kufarijiana tu ilmradi maisha yasonge?
Swali lako linaibua hisia za mimi kuuliza kama unaelewa maana ya kufa
 
Tahadhari tu kwamba hao wanaoharakisha kuwahakikishieni kwa ujasiri wote kwamba hakuna maisha baada ya mauti, hawajawahi kufa kamwe.
Hata wanaoeneza uongo huo kwamba kuna maisha Baada ya kifo nao hawajawahi kufa.

Uhakika kwamba hakuna maisha baada ya kifo unatokana na uelewa wa dhana yenyewe kama ilivyo.

Unaelewa maana ya kifo/kufa?
 
Back
Top Bottom