Je Kipoozeo ni tiba ya kero katika ndoa au mahusiano?

Nadhani hapa BAK umegusia another dimension... "mambo ya kuambiwa"..kuna watu wanadhani ni vema kumtonya mtu pale Wanapojua habari za mhusika( nadhani mmenielewa hapa).
Je, ni vizuri wewe kuwa chanzo cha habari katika ndoa za watu? na je, wewe kama mwana ndoa utapenda kuletwa habari kumhusu mwenzi wako?
Binafsi sitapenda kuwa chanzo cha habari maana sitakuwa nawasaidia wana ndoa bali kuwafarakanisha.Vile vile sitapenda kuambiwa maana nisichokijua hakitanidhuru!
Nakuunga mkono 100% kuwa na principle ya kutosikia la mtu. Ndoa nyingi zimevunjwa kwa maneno ya pembeni haswa mnapokuwa ni wanandoa mnoishi mbali mbali.
Nilipoanza maisha ya ndoa, muda mfupi nikahamia London, then, DC, US, ambako wife alibaki mimi nikarejea Bongo.
Kila mwaka nilikuja DC for visit na mambo yalikuwa safi. Wakati fulani akaja mtu toka DC anatufahamu, akanieleza mambo ya wife huko DC na kusisitiza nisiulize kwenye simu maana wife atamhisi ni yeye maana ndio aliyekuja bongo. Japo nilinyamaza I was sudenly cold mpaka nilipokuja DC.
Ingawa wife alijitahidi kuwa as usual, mimi nilijikuta na kumuona cold mpaka nilipokuja kuuliza. Aliruka hatua mia na kudai huo ni umbeya wa wabongo wa DC. Naye akasema amesikia mengi juu yangu Bongo ila ameyapuuza. Japo hatimaye tuli compromise, life has never been the same.
Jamaa aliyeniletea habari akatangaza, 'nimetengenezwa'.
From there tukakubaliana hakuna kusikiliza lolote, hata akitokea msamaria mwema wa kuleta habari za bure, dawa ni kumwambia 'ishia hapo hapo' tuendelee na habari nyingine.
 
Japo nilinyamaza I was sudenly cold mpaka nilipokuja DC.
Ingawa wife alijitahidi kuwa as usual, mimi nilijikuta na kumuona cold mpaka nilipokuja kuuliza. Aliruka hatua mia na kudai huo ni umbeya wa wabongo wa DC. Naye akasema amesikia mengi juu yangu Bongo ila ameyapuuza. Japo hatimaye tuli compromise, life has never been the same.Jamaa aliyeniletea habari akatangaza, 'nimetengenezwa'.
From there tukakubaliana hakuna kusikiliza lolote, hata akitokea msamaria mwema wa kuleta habari za bure, dawa ni kumwambia 'ishia hapo hapo' tuendelee na habari nyingine.

Compromise hii haikuwa genuine au??
Why do u say that life has never been the same again? Nani alikuwa na kinyongo na mwenzie? na je hali hiyo ilipelekea kurekebisha mambo to the better au worse?
 
Compromise hii haikuwa genuine au??
Why do u say that life has never been the same again? Nani alikuwa na kinyongo na mwenzie? na je hali hiyo ilipelekea kurekebisha mambo to the better au worse?

Hivi ni kitu gani kitakachokuwepo kati ya wawili ambao kwa nmna moja au nyingine wamehakikisha au kupata habari za uhakikika kuwa mwenzi wake ana mpenzi au anatembea nje ya ndoa?. Mimi sina uzoefu lakini naamini life can't be the same again. Hata mngesameheana lakini we are all human beings and bad memories never fade away completely.
 
naamini life can't be the same again. Hata mngesameheana lakini we are all human beings and bad memories never fade away completely.

Nimekupata vizuri...
with this in mind, we can imagine how many couples are forced to live together physically while their hearts are somewhere else.Ni wangapi wanaishi na machungu tele moyoni miaka nenda rudi only God knows!

Kwa maana hii je ni vema watu kujifanya wanaendelea na maisha regardless of what had happened au ni vema kuachana kila mmoja atafute maisha mapya?
 
...Aliruka hatua mia na kudai huo ni umbeya wa wabongo wa DC. Naye akasema amesikia mengi juu yangu Bongo ila ameyapuuza.

...Pasco shukran kwa kushare (long distance) relationship experience yako. Kama inavyowakumba wengi, inaonekana nanyi mlipitikiwa na shetani hapo.

...hatimaye tuli compromise, life has never been the same. From there tukakubaliana hakuna kusikiliza lolote, hata akitokea msamaria mwema wa kuleta habari za bure, dawa ni kumwambia 'ishia hapo hapo' tuendelee na habari nyingine.

...na kweli, maana kunguru hafugiki. I hope compromise yenu haikuwa based kwakuwa watoto wapo involved! ...ndio maana "...lifunikwe kombe mwanaharamu apite," ...Jaribuni kuondoa huo umbali, kujinusuru na mengine mengi.
 
Jamani ukimpenda mke/mume fanya ni from your heart and you mean and stand for it the rest of your life. Tusitake sana kuwa na short cut za kumaliza matatizo yetu, yawe ya kifamilia, kazini na mengineyo. Hapa bwana ukioa/olewa fanya kweli na achana na lovers katika hali zote kama ulikuwa nao awali. Au kama umepata hitilafu katika ndoa, suluhisho si kwa kipoozeo. Hiyo ni short term and destructive solution. Mwenzio anapopata ukweli kuwa unatembea nje ya ndoa au mahusiano fulani ya kudumu, huwa kovu la kidonda hicho haliishi hata kama utaombwa msamaha. Jua kutembea nje si kama kumpiga mtu kofi au kusengenya, maana haya unaweza mumwomba mwenzio msamaha akasamehe na mkaendelea na maisha na kusahau. Ni vigumu kusahau cheating na maisha yakasonga kama awali.

Kwa wengi niliowaona, msamaha unakuwa temporary tu lakini baada ya muda inakuwa ni kukumbushiana tu hasa pale penzi linapoonekana linapungua hata kwa bahati mbaya pengine uko ofisini umebanwa na majukumu lakini mwenzio haamini, so ni kwamba trust inatoweka au kupungua sana. Ushauri ni vema tubadilike tuamue kuishi na wenzi wetu kwa uaminifu na relatioship utaifurahia. Tusipende kuwa wanyama kwani binadamu tuna utashi wetu. Heshimu mwili wako, na thamini mwenzi wako. Mkeo/mumeo ni mzuri kuliko wanawake/wanaume wote na kipoozeo ni hatari siku zote kwa wanawake na kwa wanaume pia.
 
Ni vigumu kusahau cheating na maisha yakasonga kama awali.

Kwa wengi niliowaona, msamaha unakuwa temporary tu lakini baada ya muda inakuwa ni kukumbushiana tu hasa pale penzi linapoonekana linapungua hata kwa bahati mbaya pengine uko ofisini umebanwa na majukumu lakini mwenzio haamini, so ni kwamba trust inatoweka au kupungua sana. .

Je huu ugumu wa moyo ni kwa wote wanawake na wanaume? Inakuwaje basi mwanaume anaweza hata kuzaa nje na kujaribu kuleta mtoto nyumbani kwa mkewe wa ndoa.. hii si ni kumbukumbu ya kudumu ya usaliti?
 
Human body is full of desires. Just control your desires. I concur with you Maane. Nachukizwa sana na watu kuifanya hii tabia ya aibu kama kawaida tu. I hate that.
 
Let me derive my theory...

Uhusiano / mahusiano ni kitu chenye tabia kama za viumbe hai, Uhusiano huzaliwa, hukua na hatimaye hufa. Katika kipindi chote cha maisha ya uhusiano / mahusiano ni lazima yawe na afya njema na maendeleo ukuaji huo yaangaliwe kwa maana ya kupewa virutubisho vinavyofaa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa kila mtu anasamehe yale ambayo yana maslahi yake mwenyewe binafsi na kuchukua yale ya pamoja. Lakini hata hivyo kwa vile Uhusiano / mahusiano yamebeba sifa za kiumbe hai basi iko siku mahusiano hayo ni lazima yatakufa kwa njia moja au nyingine moja katika njia kubwa ambayo haiepukiki ni pale mmoja kati ya wahusianaji anapofariki dunia. Ni wazi kuwa mahusiano kuanzia pale nayo yamekufa zinabaki ni kumbukumbu tu.
Namna nyingne ni kwamba uhusiano unaweza kupatwa na magonjwa kama kutoaminiana na huu ndiyo ugonjwa mkubwa kabisa kwani hauna tiba katika mahusiano, mahusiano yakipatwa na ugonjwa huu hudhoofika na hatimaye huenda kufikia kifo au kuishi na ugonjwa huo kwa muda mrefu kabla ya kifo.
Kuna matatizo ya madogomadogo ambayo huyakumba mahusiano nayo yana kuweza kutibika hapa kama vile wivu, kijicho nk
Lakini hata hivyo mahusiano hayawezi kuwa mazuri kama hayajengwi katika misingi iliyo imara. Siku zote huwa tunaamini kuwa ndoa ndiyo kipimo cha juu cha mahusiano, jambo hili limeendelea kuonesha kuwa siyo kweli. Watu wengine huingia kwenye ndoa wakiwa na sababu tofauti na zile ambazo zinajenga misingi ya kweli ya ndoa. Matokeo yake ni kwamba tunaona ndoa nyingi zinayumba na kukosa mwelekeo. Aidha tumeona kuwa wanandoa wanaishi pamoja na wanashirikiana katika mambo kadhaa lakini katika uhusiano uliodhofika. Ni vema wanamahusiano wakaweza kutambua kuwa mahusiano hayawezi kuwa sawa siku zote kuna up and down za hapa na pale.
Mwisho mahusiano yanaweza pia kutawaliwa na tabia za mmoja kati ya wanaohusiana, kwa vile tabia haina dawa basi ni vema kabla hujaingia katika mahusiano ya muda mrefu na mtu uwe umeridhika na tabia yake na endepo utagundua tabia yake ilikuwa imejificha hapo basi umeumia na unaweza kutafuta njia ambazo unadhani zinafaa kujitoa kwani tabia huwa haibadiliki.
Mwisho pia ni vema watu wakaangalia suala la flexibilty katika mahusiano kwani endapo utajenga dhana kuwa ni lazima niendelee na mahusiano na mtu hata kama anaonesha kuwa hayuko tayari kuendelea na mahusiano yenu hapo ni kujidanganya na utaendelea kujiletea matatizo yasiyokuwa ya kazima. Ni vizuri mkavunja mahusiano hayo ili pande mbili zinazohusika zisiendelee kukaa katika maumivu ambayo si ya lazima.

Mweleze mwenzio kuwa uko tayari ikibidi kuvunja mahusiano yenu kuonesha kuwa uko serious na unachokisema. Haya niliyoyaandika naamini kila ambaye yuko katika mahusiano inabidi wayaongee kwa kinaga ubaga bila ya kufichana. Kila mmoja wao aelewe nini faida na hasara za mahusiano yao.

unaweza ukaamua kuwa ndoa lakini katika uhusiano uliokufa...hili ni suala la kiimani zaidi sitapenda kuliongelea, lina wataalam wake.

Huu ni mtazamo wangu...
 
nilishafikia msukosuko huo wa swali la tatu, mie hiyo ctuation nilipambana nayo kwa kuwa busy na wanangu, kutoka nao kwa matembezi ya hapa na pale, jioni nikitoka ofcn ni kuwa nao busy na hiki na kile, weekend ndio hivyo tena matembezi ya kutoka asubuhi kurudi nao jioni! walinifariji sana wanangu, mpaka mr alikuja kujishtukia ananichezea rafu nilikuwa nimeshatakasika moyo kabisa mana nikaona ngoja afanye akizinduka kwamba ananichezea rafu akiwa na akili timamu atajirudi tu, na kweli alijirudi sana tena sana kupitiliza, kipoozeo kwa wakati kama huu kwa mawazo yangu hakisaidii chochote sana sana kitakubomolea/kuharibia tu.
 
Jamani kwenye huu mjadala tusizungumzie tu wale wanaotembea nje kwa kisingizio cha matatizo nyumbani bali pia tujadili wale ambao hutembea nje pamoja na kuwa ndani ya ndoa zao kila kitu ni shwari kabisa. Je, kulikoni hawa ambao ndoa zao hazina kasoro yoyote bado wanatembea nje?


nilijibiwa "mami shetani alinipitia"
 
nilishafikia msukosuko huo wa swali la tatu, mie hiyo ctuation nilipambana nayo kwa kuwa busy na wanangu, kutoka nao kwa matembezi ya hapa na pale, jioni nikitoka ofcn ni kuwa nao busy na hiki na kile, weekend ndio hivyo tena matembezi ya kutoka asubuhi kurudi nao jioni! walinifariji sana wanangu, mpaka mr alikuja kujishtukia ananichezea rafu nilikuwa nimeshatakasika moyo kabisa mana nikaona ngoja afanye akizinduka kwamba ananichezea rafu akiwa na akili timamu atajirudi tu, na kweli alijirudi sana tena sana kupitiliza, kipoozeo kwa wakati kama huu kwa mawazo yangu hakisaidii chochote sana sana kitakubomolea/kuharibia tu.

Asante ndugu yangu...
una bahati kuwa una watoto wanaoweza kukupa faraja kipindi kigumu kama hicho.Sasa fikiria kuwa huna watoto au kama unao wako shule ya bweni au ni wakubwa na hawapendi kukusindikiza matembezini.Ukianza kutoka na mashosti ndiyo mwanzo wa kuanza kumwaga mtama kwenye kuku wengi na kuanza kupewa ushauri potofu....utafanyaje?
 
Nadhani hapa BAK umegusia another dimension... "mambo ya kuambiwa"..kuna watu wanadhani ni vema kumtonya mtu pale Wanapojua habari za mhusika( nadhani mmenielewa hapa).
Je, ni vizuri wewe kuwa chanzo cha habari katika ndoa za watu? na je, wewe kama mwana ndoa utapenda kuletwa habari kumhusu mwenzi wako?
Binafsi sitapenda kuwa chanzo cha habari maana sitakuwa nawasaidia wana ndoa bali kuwafarakanisha.Vile vile sitapenda kuambiwa maana nisichokijua hakitanidhuru!


mie hapo ndio panaponishangaza binadamu tulivyo, huwezi kwenda kumwambia mtu mambo kama hayo coz wakiyaweka sawa mambo yao wewe utaonekana mchochezi tu, nilikuja kuambiwa kuhusu mr na nikamweleza huyo aliekuja kwamba cku nyingine plz ctaki uje unieleze mambo kama haya! tayari alishanitia cmanzi na hapo ndio nikaanza kuona cmu ya mr inakuwa busy kila wakati kitu ambacho awali niliuona huo u busy na kuona its non of ma biznes lakini alivyoniambia hivyo alinifanya nifatilie mwishowe nikajua ni kweli! haikunisaidia zaidi ya kuumia tu but nashukuru nilifanikiwa kuvuka hicho kikwazo.
 
Jamani naomba mnikumbushe mliko anzia nashindwa kudandia train kwa mbele.
 
Hivi ni kitu gani kitakachokuwepo kati ya wawili ambao kwa nmna moja au nyingine wamehakikisha au kupata habari za uhakikika kuwa mwenzi wake ana mpenzi au anatembea nje ya ndoa?. Mimi sina uzoefu lakini naamini life can't be the same again. Hata mngesameheana lakini we are all human beings and bad memories never fade away completely.


kuna wakati mambo yanaenda sawa kuna wakati akikukosea unaanza kufikiria mbali kule mlikotoka/sameheana.
 
mie hapo ndio panaponishangaza binadamu tulivyo, huwezi kwenda kumwambia mtu mambo kama hayo coz wakiyaweka sawa mambo yao wewe utaonekana mchochezi tu, nilikuja kuambiwa kuhusu mr na nikamweleza huyo aliekuja kwamba cku nyingine plz ctaki uje unieleze mambo kama haya! tayari alishanitia cmanzi na hapo ndio nikaanza kuona cmu ya mr inakuwa busy kila wakati kitu ambacho awali niliuona huo u busy na kuona its non of ma biznes lakini alivyoniambia hivyo alinifanya nifatilie mwishowe nikajua ni kweli! haikunisaidia zaidi ya kuumia tu but nashukuru nilifanikiwa kuvuka hicho kikwazo.

haya ya kuambiwa...
nadhani inabidi mtu ajiulize kwanza...kwa kutoa taarifa kwa mwanandoa kuhusu mienendo isiyofaa itasaidia kujenga au kuharibu.Kwa mwenye mapenzi mema nadhani hatathubutu kwenda kusema lakini mwenye nia mbaya ya kubomoa basi hiyo ndiyo njia rahisi.

Mwanandoa anayeletewa habari ajue kabisa kuwa mleta habari ni mchonganishi hivyo ajihadhari.
Kitu kingine ni kwamba hizi ndoa au ndoano zina mambo yake.Nadhani ni vema wahusika mke na mume kupambana wenyewe bila kuingiza mamluki wajekusaidia. Mamluki wa aina yeyote ile hawatatoa suluhisho la kudumu na wakitoka hapo ndo wa kwanza kwenda kutangaza mambo ya watu hata pale wenyewe wameshaelewana na kupatana.
 
Mjadala ulianzia kuangalia haya maswali matatu:
Suali langu ni hili:
1.Je, ( kipoozeo) hiki ni kitu kilichopo katika yale mambo yanayofundwa kimila au kwenye kitchen party au ni suala la mtu akili-kichwani mwake?

2.Hivi wanaume wanapowakosea akina mama na kuona wamesamehewa hudhani imeisha kweli au nao huwa na wasiwasi?

3. Akina mama mnadhani kuna njia mbadala ya kumaliza maumivu ya kero zinazowapata kwenye ndoa ( haswa suala la kuendewa kinyume - kukosekana uaminifu kunakofanywa na waume mara kwa mara) badala ya kipoozeo?

Naomba michango yenu.

Jamani naomba mnikumbushe mliko anzia nashindwa kudandia train kwa mbele.
haya changia Fidel
 
Nimekupata vizuri...
with this in mind, we can imagine how many couples are forced to live together physically while their hearts are somewhere else.Ni wangapi wanaishi na machungu tele moyoni miaka nenda rudi only God knows!

Kwa maana hii je ni vema watu kujifanya wanaendelea na maisha regardless of what had happened au ni vema kuachana kila mmoja atafute maisha mapya?[/QUOTE

wakati mie nipo kwenye prblm na mr kuna frnd wangu 1 akaniambia " hayo mambo mbona ni madogo sana nyamayao anayokufanyia mr? laiti ungefanyiwa ninayofanyiwa me cdhani kama unaweza kustahimili but 2tabanana pale pale aondoke yeye aniachie mie nyumba"...huyu frnd wangu alipitia misuko suko mingi sana mojawapo ni mr wake kuwa na uhusiano wa kimapenzi na dada yake walie share baba, na bado wanaendelea kuishi pamoja kama wanandoa, nadhani ukifikiria mlipotoka then ndoa ije ife kibudu inabidi tu mtu ugangamale na kilicho chako mana unaweza kuachia hapo kwenda kwingine ukakuta balaa zaidi, bora ulipopazoea kuliko utakapokwenda kupaanza.
 
Jamani naomba mnikumbushe mliko anzia nashindwa kudandia train kwa mbele.

Fidel,
unaweza kuanza kuchangia kwenye suali la pili hili hapa:
2. Hivi wanaume wanapowakosea wake/magirlfriends zao na kuona wamesamehewa hudhani imeisha kweli au nao huwa na wasiwasi?

Hili swali nadhani ni muhimu kulijadili ka maana inaelekea wanaume wengi wanadhana potofu kuwa mwanamke siku zote atasamehe tu, ila mwanaume akikosewa ( kusalitiwa) ni mwisho wa uhusiano na hakuna kusamehe.
Nimekumbuka kisa kimoja niliwahi kusoma zamani kwenye literature class..(nimesahau title ya kitabu mniwie radhi)..Setting ya story ni South Africa wakati wa ubaguzi wa rangi ... main character ni mwanamke Matilda.Huyu alikuwa na bwana wa pembeni aliyekuwa na mazoea ya kumtembelea mara baada ya mume kutoka kwenda kazini.Siku ya siku mume karudi ghafla...doezi likamudu kutokomea lakini likasahau kofia.Mume alielewa kilichokuwa kinaendelea ila hakufanya fujo yoyote.Matilda kila akiandaa chakula - iwe ni chai asubuhi au chakula mchana au usiku, mumewe alikuwa anasisitiza kuwa mgeni yule ( kofia) aandaliwe naye sahani na kukaribishwa rasmi.Hii ilikuwa torture tosha kwa Matilda.Nadhani mwisho Matilda alikuja kujiua.Hii inaonyesha ni jinsi gani wenzetu hawamalizi ishu.
Sasa tukirudi kwenye topic yetu, enyi wanaume, kwanini mnajiaminisha sana kuwa mmesamehewa 100% na hata baada ya hapo mnaendeleza tabia ileile bila kujali mnawaumiza wake/galfriends wenu?
 
Binafsi naona jibu ni 'hapana'. Namaanisha Kipoozeo sio tiba ya kero katika ndoa au mahusiano. Ingekuwa vema kutatua tazizo na kuweka mazingira na mbinu ya kila mmoja katika hayo mahusiano kusimama katika zamu au jukumu lake. Mtu ukisema utaenda huko utapooza, ukirudi tatizo si linabaki palepale?
 
Back
Top Bottom