passion_amo1
JF-Expert Member
- Dec 3, 2023
- 1,578
- 3,148
Wakuu habari za uzima?
Nikiwa zangu hapa sandaland na bro joh napitia stori za wana JF. Nikaona wimbi kubwa la wanawake wakilalamikiwa ni matapeli, kausha damu na maneno mengine mabaya
Leo nitaongea na KATAA NDOA mimi hawa sijawahi kuona sababu yao kimantiki na wengi ni fata mkumbo tu wasijue nini wanachoongelea.
Mosi, kukataa ndoa ni kuhalalisha uasherati na uzinzi. Mwanaume rijali lazima awe na mke ndani.
Wengi wanakataa ndoa kwa madai ya kwamba Ati mkiachana lazima mgawane pasu kwa pasu! Hilo linaweza kuwa kweli na lisiwe kweli vilevile. Kama ulichukua mtoto wa watu mkaanza kulala kwenye maboksi bila neti, godoro, kitanda na samani zingine na kakuvumilia. Iweje tayari umeshajipata Ati useme wewe nenda na hapa huna chako?
Kipindi unaondoka kazini anamuangalia mtoto kuanzia akiwa mdogo mpaka anaenda shule anafatilia maendeleo yake, na suala la kufatilia maendeleo ya watoto wanaume tupo nyuma sana na huo muda hatuna. Amekupikia, alikuwa anakufulia nguo na unaonekana mtanashati huko unapokwenda kwanini ukimuacha unataka aondoke bila kitu? Huo ni ukatili mkubwa sana.
Kama mwanaume anapaswa kukataa ndoa, let’s say sawa tukatae ndoa for the sake of argument. Ni mwanaume gani yupo radhi mtoto wake wakike achukuliwe bila utaratibu na aende kuishi na mwanaume mwingine? Kama huyo baba yupo hapa aseme?
Ndoa si lazima uende kanisani gharama za suti, shera, ukumbi na mengineyo. Hata kwenda kwa wazazi wa binti wakakupa baraka za kuishi na mtoto wao hiyo ni ndoa.
Kama hutaki kugawana mali na mwanamke ipo sheria ya kuandikisha mali zako ambazo tayari unazo wanasheria watanikumbusha sheria hiyo. Kwa maana hiyo Mke wako atajua kabisa kwamba mali fulani ni za kwangu. Na katika mgawanyo ataangaliwa mchango wake katika ndoa hiyo.
kuishi na mwanamke kwa kipindi cha miaka miwili hiyo ni ndoa (rebuttable presumption). Kwa maana kuwa kama umekuwa na mwanamke kwa kipindi hicho hio inatambulika ni ndoa kisheria.
Kama wanaopinga ndoa ni ile kwamba kila mtu akae kivyake je watoto mtakaowapata watapata wapi malezi ya baba na mama? Mtoto anahitaji malezi ya pande zote hivyo lazima muwepo pamoja na kukaa pamoja kwa miaka miwili na zaidi na ikathibitika hivyo hio ni ndoa.
Nataka niwaulize hao wanaopinga ndoa wanaelewa hata wanachoongelea?
Ndoa za kimila zinaweza kuwa hazina gharama kubwa, katibu tarafa lazima awepo katika ndoa hizi sababu yeye ndio anahusika kufatilia vyeti vya usajili.
Kukataa ndoa ni kuhalalisha uasherati na uzinzi.
Matatizo ya kwenye ndoa wanaume tunachangia 80% .
Embu fikiri, mtu anafahamu huyu ni Mke wa mtu na bado anaendelea kumtongoza na kumshawishi mpaka anafanikiwa. Unafikiria mume wake akifahamu hiyo ndoa itaendelea ku survive?
Kuna Hawa wanaopinga wanawake wawe watu wa nyumbani. sawa ngoja nikubaliane naye.
Baba mmoja alikuwa ni dereva bajaji posta alipata ajali akagongwa na kufa, ameacha watoto watano na kama alikuwa ni mama wa nyumbani. Embu fikiria mama huyu yupo katika kipindi gani katika kulea hao watoto?
Boss anafahamu huyu ni Mke wa mtu lakini anafanya visa kumpa kazi nyingi na kumtishia atamuachisha kazi. Hafikirii kwamba anaumiza watoto na mwanaume mwenzake ambaye yupo nyumbani kwa muda huo akimsubiri Mkewe. Tatizo ni mwanaume au kupata kazi mwanamke?
Kama yupo mwanaume ambaye mtoto wake wakike kamlea tangu udogoni mpaka anakuwa mtu mzima na anaona kijana anakaa na binti yake bila utaratibu maalumu na akaridhika ajitokeze aseme?
Kukataa ndoa kunasabbisha:
• Watoto kukosa upendo wa wazazi wote.
• Ongezeko la masingo maza
• Kama mtoto atalelewa na mama kuna hatihati aka adapt tabia za kike na kuingia katia ushoga.
• Mtoto kupitia manyanyaso Iwapo mwanamke huyo ataolewa na mwanaume mwingine, au mwanaume huyo atakaa na mwanamke mwingine hivyo mtoto huyo kupitia manyanyaso (si wote lakini.
Kuna wanaume waliotendwa kama mimi kabla sijapata Mke wangu wa sasa nikasema sitaoa. Kama ulitendwa tambua ni mwanaume mwenzako mwenye tamaa ya ngono ndio alikusabaishia.
Mwenye kupangua hoja karibu hapa.
Karibuni kwa wenye kuhitaji nguo quality tunatuma mikoani na nje ya nchi.
Kariakoo kwa sasa.
Nikiwa zangu hapa sandaland na bro joh napitia stori za wana JF. Nikaona wimbi kubwa la wanawake wakilalamikiwa ni matapeli, kausha damu na maneno mengine mabaya
Leo nitaongea na KATAA NDOA mimi hawa sijawahi kuona sababu yao kimantiki na wengi ni fata mkumbo tu wasijue nini wanachoongelea.
Mosi, kukataa ndoa ni kuhalalisha uasherati na uzinzi. Mwanaume rijali lazima awe na mke ndani.
Wengi wanakataa ndoa kwa madai ya kwamba Ati mkiachana lazima mgawane pasu kwa pasu! Hilo linaweza kuwa kweli na lisiwe kweli vilevile. Kama ulichukua mtoto wa watu mkaanza kulala kwenye maboksi bila neti, godoro, kitanda na samani zingine na kakuvumilia. Iweje tayari umeshajipata Ati useme wewe nenda na hapa huna chako?
Kipindi unaondoka kazini anamuangalia mtoto kuanzia akiwa mdogo mpaka anaenda shule anafatilia maendeleo yake, na suala la kufatilia maendeleo ya watoto wanaume tupo nyuma sana na huo muda hatuna. Amekupikia, alikuwa anakufulia nguo na unaonekana mtanashati huko unapokwenda kwanini ukimuacha unataka aondoke bila kitu? Huo ni ukatili mkubwa sana.
Kama mwanaume anapaswa kukataa ndoa, let’s say sawa tukatae ndoa for the sake of argument. Ni mwanaume gani yupo radhi mtoto wake wakike achukuliwe bila utaratibu na aende kuishi na mwanaume mwingine? Kama huyo baba yupo hapa aseme?
Ndoa si lazima uende kanisani gharama za suti, shera, ukumbi na mengineyo. Hata kwenda kwa wazazi wa binti wakakupa baraka za kuishi na mtoto wao hiyo ni ndoa.
Kama hutaki kugawana mali na mwanamke ipo sheria ya kuandikisha mali zako ambazo tayari unazo wanasheria watanikumbusha sheria hiyo. Kwa maana hiyo Mke wako atajua kabisa kwamba mali fulani ni za kwangu. Na katika mgawanyo ataangaliwa mchango wake katika ndoa hiyo.
kuishi na mwanamke kwa kipindi cha miaka miwili hiyo ni ndoa (rebuttable presumption). Kwa maana kuwa kama umekuwa na mwanamke kwa kipindi hicho hio inatambulika ni ndoa kisheria.
Kama wanaopinga ndoa ni ile kwamba kila mtu akae kivyake je watoto mtakaowapata watapata wapi malezi ya baba na mama? Mtoto anahitaji malezi ya pande zote hivyo lazima muwepo pamoja na kukaa pamoja kwa miaka miwili na zaidi na ikathibitika hivyo hio ni ndoa.
Nataka niwaulize hao wanaopinga ndoa wanaelewa hata wanachoongelea?
Ndoa za kimila zinaweza kuwa hazina gharama kubwa, katibu tarafa lazima awepo katika ndoa hizi sababu yeye ndio anahusika kufatilia vyeti vya usajili.
Kukataa ndoa ni kuhalalisha uasherati na uzinzi.
Matatizo ya kwenye ndoa wanaume tunachangia 80% .
Embu fikiri, mtu anafahamu huyu ni Mke wa mtu na bado anaendelea kumtongoza na kumshawishi mpaka anafanikiwa. Unafikiria mume wake akifahamu hiyo ndoa itaendelea ku survive?
Kuna Hawa wanaopinga wanawake wawe watu wa nyumbani. sawa ngoja nikubaliane naye.
Baba mmoja alikuwa ni dereva bajaji posta alipata ajali akagongwa na kufa, ameacha watoto watano na kama alikuwa ni mama wa nyumbani. Embu fikiria mama huyu yupo katika kipindi gani katika kulea hao watoto?
Boss anafahamu huyu ni Mke wa mtu lakini anafanya visa kumpa kazi nyingi na kumtishia atamuachisha kazi. Hafikirii kwamba anaumiza watoto na mwanaume mwenzake ambaye yupo nyumbani kwa muda huo akimsubiri Mkewe. Tatizo ni mwanaume au kupata kazi mwanamke?
Kama yupo mwanaume ambaye mtoto wake wakike kamlea tangu udogoni mpaka anakuwa mtu mzima na anaona kijana anakaa na binti yake bila utaratibu maalumu na akaridhika ajitokeze aseme?
Kukataa ndoa kunasabbisha:
• Watoto kukosa upendo wa wazazi wote.
• Ongezeko la masingo maza
• Kama mtoto atalelewa na mama kuna hatihati aka adapt tabia za kike na kuingia katia ushoga.
• Mtoto kupitia manyanyaso Iwapo mwanamke huyo ataolewa na mwanaume mwingine, au mwanaume huyo atakaa na mwanamke mwingine hivyo mtoto huyo kupitia manyanyaso (si wote lakini.
Kuna wanaume waliotendwa kama mimi kabla sijapata Mke wangu wa sasa nikasema sitaoa. Kama ulitendwa tambua ni mwanaume mwenzako mwenye tamaa ya ngono ndio alikusabaishia.
Mwenye kupangua hoja karibu hapa.
Karibuni kwa wenye kuhitaji nguo quality tunatuma mikoani na nje ya nchi.
Kariakoo kwa sasa.