Gsana
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 4,383
- 1,340
Mods, na wana JF,
Haitakuwa busara kwa thread hii kuipeleka sehemu ya dini, inajulikana sehemu hiyo haifikiwi na watu wengi hapa JF ikiwa mimi mmoja wapo.
Ni matumaini yangu kuweza kuiaccess hii thread na kuona mijadala ikichangiwa ili kuweza kujua ukweli.
Sitegemei kuwa JF/Mods wapo kwa ajili ya kuchochea chuki dhidi ya Serikali iliyopo madarakani kwani kama itakuwa ni hivyo basi wanafanya jambo la hatari sana linaloweza kutugharimu. Tumeona ile thread ya OIC ikiachiwa kuchangiwa na kila mtu na mwenye kila tusi dhidi ya dini ya kiisamu na kejeli akiachiwa kwa marefu na mapana. Kwahiyo sioni sababu ya hii thread ya kisiasa zaidi kutupiwa huko kusikojulikana.
Mwisho napenda kutoa angalizo:
Sio haki kuhamisha thread ya mtu na kuipeleka sehemu asiyokuwa na access nayo. Hapa JF ni sehemu ya kutoa mawazo na kila mmoja aheshimiwe mawazo yake na sio kufungwa na kutupwa kapuni.
Kuna tetesi Zimeenea mtaani kuwa baada ya JK kuingia madarakani aligomea ruzuku iliyokuwa ikitolewa na Serikali kuendesha makanisa pamoja na taasisi zinazoendeshwa na makanisa katoliki nchini kama shule, hospitali na vyuo. "The Government shall provide financial assistance to Church institutions and shall seek financial assistance to Church run social services in its bilateral negotiations with foreign governments"
source :The Memorandum of Understanding between the Government of the United Republic of Tanzania and the Tanzania Episcopal Council (TEC) and the Christian Council of Tanzania-page 3 (attached herewith)
Nasikia JK aliwaambia kuwa nchi hii haina dini na itakuwa ubaguzi kuwapa ruzuku watu wa dini moja na kuwaacha wa dini nyinginezo akatolea mfano kuna waislam, wabudda, masingasinga, wahindu na wasiokuwa na dini je hao hawana haki ya kupewa ruzuku? na serikali ikitoa ruzuku kwa hawa wote itawezaje kujiendesha? Basi bora mkose wote. Hapo naona JK aliona mbali sana ila hakujua kama anajiharibia yeye na chama chake. Na ndio maana kwa kutumia mlango wa nyuma kuna chama kikasimamisha watumishi wa Mungu kwa wingi na kufanikiwa kupenya kila pembe ya Tanzania. Inasemekana Kanisa liliplay part kubwa kwa mafanikio ya chama fulani. Na hizo zilikuwa ni hasira za watumishi wa kanisa.
KUNA TETESI KUWA WAFUATILIAJI WA MAMBO WAMEITHIBITISHIA SERIKALI UBADHIRIFU MKUBWA WA RUZUKU ILIYOKUWA INATOLEWA NA SERIKALI SAMBAMBA NA MISAMAHA YA KODI. MISAMAHA HII YA KODI NI ILE YA UAGIZWAJI MAGARI NA VITU MBALIMBALI KUPITIA TRUSTEES ZA MAKANISA. NA TANGU KUANZA KUBANWA KUMEKUWA NA UAIGIZAJI WA VITU MDOGO TOFAUTI NA HAPO MWANZO, MAANA INASEMEKANA WAJANJA WALIKUWA WANATUMIA MWANYA HUO KUJINUFAISHA.
Ukiunganisha picha itaona hapo ndio chanzo hasa cha timbwili hili mnaloliona leo lililo vikwa ngozi ya vyama vya siasa ( upinzani ). Hapo awali Wakristo na CCM walikuwa chanda na pete. Ilikuwa ni kosa la jinai kwa mkristo mwenye imani kuwa upinzani ndio maana hata viongozi wao wengi mwaka 2005 walisema JK "chaguo la Mungu"
Leo hii ukitia pua tu JF na maeneo mengi kwenye mitandao na mitaani utakutana na shutuma kuwa JK ni Mdini, lakini hawatoi facts za udini wake.
Je, JK ni mdini?
Orodha ya Baraza la Mawaziri na Manaibu wa Wizara 26 za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2010 - 2015
- Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora etc,etc,etc... Nakushukuru kwa kuonesha kuwa jeykey ni mdini,ni mdini kweli kweli. Kumbuka Tanzania ina madhehebu ya dini mengi sana sina kumbuka ya jumla ila ni zaidi ya 25+,kama 32% ya utawala ni dini moja na 68% ni dini zilizobaki si unaona walioiteka nchi ni akina nani? Je hata tukisema iyo 68% ni protestant,TAG ,KATHOLIKI, INDUISM,AGAPE,MWINGIRA,Etc,yani madhehebu atleast 10, tayari 68/10 utapata 6.8% kila dini itakuwa chini ya 32% it means chini ya uislam mara 5 ivi! Kweli jeykey ni mdini! Kumbuka makanisa ya Tz sio moja na utawala wake uko tofauti kabisa kwa iyo mtoa hoja onesha ile dini inayotuumiwa kuwa favoured ina waziri wangapi? Acha kuupotoa umma,jadili kwa umakini zaidi! Lete hoja ya msingi kama ipo tujadili. Jk ni mdini kwa sababu yeye anauona udini nchini Tanzania!