Je, huyu anafaa kuolewa

Je, huyu anafaa kuolewa

tafuta mwanamke huko huko ulipo achana na longdistance relationship utaja lea mtoto si wako
 
Kashapata bwana mwingine huyo kinacho mfanya asikuache ni kwasababu bwana yake Hana pesa labda ni mwanafunzi mwenzake kwahiyo anakutumia ww Kama accnt yake ya akiba
 
Habari wadau

Jamani naomba mnishauri kuhusiana na haya mahusiano yangu kwani ni zaidi ya mwaka sasa bila kuyaelewa. Binafsi Mimi naishi Kenya ila kwetu ni Tanzania.

Ilikuwa ni mwaka jana nilipokuwa nafanya kazi za tiba ya asili mkoani Simiyu ndipo nilikutana na binti mmoja hivi, nikamueleza yaliyopo moyoni mwangu nayeye akanielewa sana. Kwa vile yeye alikuwa ni Mwanafunzi wa chuo cha Kati hapa nchini tulikaa pamoja Kama miezi 2.

Alisafiri kwenda huko dodoma na Mimi nikaenda zangu huko Kenya baada ya kumaliza kazi iliyonileta. Mwanzani mawasiliano yakuwa bomba sana but baada ya muda yalianza kupungua.

Ila tatizi lake hawezi kunitafuta Kama hana shida ya hela. Wakati mwingine namtumia text hata WhatsApp namuona yupo Online lkn hajibu isipokuwa anaisoma tu na kupotezea. Kuna wakati napata hasira namtusi ndipo anaanza kujibu kwa kujitetea.

Jamani naumia sana nikifikiria namna nilivyowekeza pesa nyingi kwake kweli naishiwa nguvu kabsa. Mfano saivi nimetuma text WhatsApp ila hajajibu japo kaisoma. Hivi hapo kuna tumaini la ndoa kweli.

Mbaya zaidi nikilalamika ananiambia kuwa anaumia ninapolalamika nipeni ushauri ila tatizo kubwa lipo kwenye kuishi naye mbali na kutonitafuta mpaka nimtafute au awe na shida ya pesa
Hahitaji uwe lofa kiwango cha standard gauge kujua kwamba hakupendi anakutumia. Vibinti vya chuo na long distance relationship wapi na wapi? We unatoa pesa wengine wanajimegea tu ndo ukweli mchungu.
Achana naye utawekeza sana na utalia ishia uwekezaji wako hapo, kwani mbona serikali imetosa miradi mingapi we unafail wapi
 
Hahitaji uwe lofa kiwango cha standard gauge kujua kwamba hakupendi anakutumia. Vibinti vya chuo na long distance relationship wapi na wapi? We unatoa pesa wengine wanajimegea tu ndo ukweli mchungu.
Achana naye utawekeza sana na utalia ishia uwekezaji wako hapo, kwani mbona serikali imetosa miradi mingapi we unafail wapi
Kashapata bwana mwingine huyo kinacho mfanya asikuache ni kwasababu bwana yake Hana pesa labda ni mwanafunzi mwenzake kwahiyo anakutumia ww Kama accnt yake ya akiba
Take this piece of advice and work on it.
Inauma sana kumuacha sijui naanzaje sasa
 
Inauma sana kumuacha sijui naanzaje sasa
Najua ni ngumu lakini yanini kuendelea na biashara yenye hasara.

Ninaandika kwa herufi kubwa, ACHANA NAYE ANAKUCHUNA TU HAKUPENDI NA ANAONA UNAMBOA NA MIMESEJI YAKO ANAKULILIA KWASABABU ANAONA ATAKOSA PESA ZAKO
 
Asanteee! Ila kwani siwezi kumroga na akanipenda?
Unaenda kuuza future yako, roho yako, sadaka zako, future ya watoto wako, ukoo wako kwa mganga kisa demu, by the way penzi la kuroga halina raha, kuna siku utatatakiwa kwenda ku update uchawi wako huko, ili penzi lianze kunoga tena.

Mbona wanawake ni wapo wengi kuliko wanaume? Au unajiweka sehem moja ndio maana huwaoni.

Acha mentality ya kuku, akikuta mchele au pumba akala hata zikiisha atachimba chimba hapo hapo, akidhani ndio sehemu pekee kwenye chakula.kumbe kuna shamba lina mahindi tele,na ghala lenye pumba tele.

Wadada wenye kazi zao wazuri wapo wengi, wanaohitaji mwenza, utakuta huyo hana ishu na anakupeleka.
 
Falsafa ya mahusiano usipofata kanuni za kiungu lazima zikutoe damu.
Mwanaume ni mpango wa Mungu kutawala dunia mwanaume ni ufunguo wa maisha kwa mwanamke.
Mwanaume ni baba kwa mke wake usipoonesha hizo tabia za kibaba kwa mke/mpenzi wako lazima ulie tuu.
Muoneshe njia,muoneshe upendo, mfunze maisha, mfunze heshima lazima akiwa na wewe ajifeel yuko chini ya himaya fulani laa ya sivyo.
Hayo yote yanafanywa ukiwa unalifahamu neno na neno ndio muongozo wako.
Mwanaume ni msingi ukitetereka hakuna jengo yeye ni pambo lako jitahidi mara zote ajihisi yuko salama.
Jamaa hamuwezi huyo demu kwanza hajiamini kabisa ndio maana anapelekeshwa hata akibahatika kumuoa huyo demu bado hatamuweza, sisi wanaume tupo duniani kumiliki kila kilichomo humu na kijione kipo Salama chini yetu ,jamaa ameyumba since day one yaelekea alimtongoza kiuwogauwoga demu akaona huyu mwamba hajiamini.
 
Habari wadau

Jamani naomba mnishauri kuhusiana na haya mahusiano yangu kwani ni zaidi ya mwaka sasa bila kuyaelewa. Binafsi Mimi naishi Kenya ila kwetu ni Tanzania.

Ilikuwa ni mwaka jana nilipokuwa nafanya kazi za tiba ya asili mkoani Simiyu ndipo nilikutana na binti mmoja hivi, nikamueleza yaliyopo moyoni mwangu nayeye akanielewa sana. Kwa vile yeye alikuwa ni Mwanafunzi wa chuo cha Kati hapa nchini tulikaa pamoja Kama miezi 2.

Alisafiri kwenda huko dodoma na Mimi nikaenda zangu huko Kenya baada ya kumaliza kazi iliyonileta. Mwanzani mawasiliano yakuwa bomba sana but baada ya muda yalianza kupungua.

Ila tatizi lake hawezi kunitafuta Kama hana shida ya hela. Wakati mwingine namtumia text hata WhatsApp namuona yupo Online lkn hajibu isipokuwa anaisoma tu na kupotezea. Kuna wakati napata hasira namtusi ndipo anaanza kujibu kwa kujitetea.

Jamani naumia sana nikifikiria namna nilivyowekeza pesa nyingi kwake kweli naishiwa nguvu kabsa. Mfano saivi nimetuma text WhatsApp ila hajajibu japo kaisoma. Hivi hapo kuna tumaini la ndoa kweli.

Mbaya zaidi nikilalamika ananiambia kuwa anaumia ninapolalamika nipeni ushauri ila tatizo kubwa lipo kwenye kuishi naye mbali na kutonitafuta mpaka nimtafute au awe na shida ya pesa
Mtreat mtu namna anavyotaka au kupenda. Sasa mtu hajibu ujumbe wako it means hapendi kuwasiliana na wewe, sasa kwann usimpe anachotaka...?!

Mkalie kimya, wacha apambane na habari zake...... Wewe tafuta ambaye usipomtext anakosa hamu ya kula na anasikia kama figo zinataka kutoka........

Mapenzi ni two way street. Ukiona unalazimisha penzi, basi jitafakari sana.
 
Inauma sana kumuacha sijui naanzaje sasa
Ebu tuondolee ujinga hapa
1. Uliwezaje kuacha ziwa la mama yako?
2. Uliwezaje kuiacha nchi ya Tanzania na kwenda kuishi Kenya?
3. Uliwezaje kuwaacha baba na mama yako na kwenda kujitegemea?

Tumia njia hizo hizo kumsahau huyo demu ambaye ameshakuacha ila wewe ndio unashindwa kukubali matokeo
 
Habari wadau

Jamani naomba mnishauri kuhusiana na haya mahusiano yangu kwani ni zaidi ya mwaka sasa bila kuyaelewa. Binafsi Mimi naishi Kenya ila kwetu ni Tanzania.

Ilikuwa ni mwaka jana nilipokuwa nafanya kazi za tiba ya asili mkoani Simiyu ndipo nilikutana na binti mmoja hivi, nikamueleza yaliyopo moyoni mwangu nayeye akanielewa sana. Kwa vile yeye alikuwa ni Mwanafunzi wa chuo cha Kati hapa nchini tulikaa pamoja Kama miezi 2.

Alisafiri kwenda huko dodoma na Mimi nikaenda zangu huko Kenya baada ya kumaliza kazi iliyonileta. Mwanzani mawasiliano yakuwa bomba sana but baada ya muda yalianza kupungua.

Ila tatizi lake hawezi kunitafuta Kama hana shida ya hela. Wakati mwingine namtumia text hata WhatsApp namuona yupo Online lkn hajibu isipokuwa anaisoma tu na kupotezea. Kuna wakati napata hasira namtusi ndipo anaanza kujibu kwa kujitetea.

Jamani naumia sana nikifikiria namna nilivyowekeza pesa nyingi kwake kweli naishiwa nguvu kabsa. Mfano saivi nimetuma text WhatsApp ila hajajibu japo kaisoma. Hivi hapo kuna tumaini la ndoa kweli.

Mbaya zaidi nikilalamika ananiambia kuwa anaumia ninapolalamika nipeni ushauri ila tatizo kubwa lipo kwenye kuishi naye mbali na kutonitafuta mpaka nimtafute au awe na shida ya pesa
Kitu nilichojifunza ni kuwa wanawake wengi ukianza naye tu mahusiano anabadili tabia yake ya asili,inawezekana ulipomuona mwanzoni hakuwa hivyo,ila pindi mkianzisha anakuwa tofauti,sasa sijajua inakuwa ni ushauri anaopewa na marafiki au ni nature yao,utakuta anaanza katabia ka kununa,au kutopokea simu mara moja ni mpaka urudie,au tabia ya kuzila/kususa,au kuomba hela kwenye kila kitu hata vile ambavyo mwanzoni aliweza kujimudu,inakuwa ni kama amepata benki ya kujipatia pesa ya kutatua kila shida yake,au kukufokea hata mbele za watu n.k. n.k....
 
Ebu tuondolee ujinga hapa
1. Uliwezaje kuacha ziwa la mama yako?
2. Uliwezaje kuiacha nchi ya Tanzania na kwenda kuishi Kenya?
3. Uliwezaje kuwaacha baba na mama yako na kwenda kujitegemea?

Tumia njia hizo hizo kumsahau huyo demu ambaye ameshakuacha ila wewe ndio unashindwa kukubali matokeo
Mtreat mtu namna anavyotaka au kupenda. Sasa mtu hajibu ujumbe wako it means hapendi kuwasiliana na wewe, sasa kwann usimpe anachotaka...?!

Mkalie kimya, wacha apambane na habari zake...... Wewe tafuta ambaye usipomtext anakosa hamu ya kula na anasikia kama figo zinataka kutoka........

Mapenzi ni two way street. Ukiona unalazimisha penzi, basi jitafakari sana.
Hawa ndio wale vijana wanao jiua kisa toto halimtaki halafu yeye ndio kakolea vibaya mno, ndio maana ana mtusi sometimes.
definitely hajiamini .
Kwa post hii nina mashaka na umri wako na kama umeshapevuka basi nina mashaka na akili zako
Nashukuru kwa ushauri wenu
 
pole sana kiongozi
hapo kuna weza kuwa na mambo kadhaa ya kuhisi ILA
1. Lenye uzito zaidi kwangu ni kuwa mbali na mpenzi wako
2. kama ameshamaliza chuo anapenda kusikia mipango ya kupeleka mapenzi yenu mbele; mfano lini mngependa kuoana/mtaishi wapi mkioana na yeye atoe mawazo yake nk
3. Sitaki kuwalaumu sana dada zetu kwani wakati mwingine wanapata changamoto kubwa sana; fikiria mtu uko huko Kenya yeye yupo Dodoma, na vijana wanamfuata pengine kutaka kumuoa na hana hakika uko ulipo ukoje mf; kama uliweza kuishi naye kwa miezi mbili pengine unaweza kuishi na mwingine tena; Je akikusubiri ukabadili mawazo na yeye amesha achia fursa zinazojitokeza nk; Wanapata changamoto sana. Nionavyo mimi changamoto KUBWA kuliko zote ni umbali...
Dada anahofu yasije mkuta kama ya shishimbi akakosa pote
 
Back
Top Bottom