Je, huyu anafaa kuolewa

Je, huyu anafaa kuolewa

Mwanafunzi wa chuo unahangaika nae,acha amalize chuo kwanza,hv unajua maisha ya wanawake wa chuo wew
 
Hawa ndio wale vijana wanao jiua kisa toto halimtaki halafu yeye ndio kakolea vibaya mno, ndio maana ana mtusi sometimes.
definitely hajiamini .
Afadhali unisaidie kumwambia huyu mvulana
 
Jamaa hamuwezi huyo demu kwanza hajiamini kabisa ndio maana anapelekeshwa hata akibahatika kumuoa huyo demu bado hatamuweza, sisi wanaume tupo duniani kumiliki kila kilichomo humu na kijione kipo Salama chini yetu ,jamaa ameyumba since day one yaelekea alimtongoza kiuwogauwoga demu akaona huyu mwamba hajiamini.
Mkuu umeona mbali
 
Habari wadau

Jamani naomba mnishauri kuhusiana na haya mahusiano yangu kwani ni zaidi ya mwaka sasa bila kuyaelewa. Binafsi Mimi naishi Kenya ila kwetu ni Tanzania.

Ilikuwa ni mwaka jana nilipokuwa nafanya kazi za tiba ya asili mkoani Simiyu ndipo nilikutana na binti mmoja hivi, nikamueleza yaliyopo moyoni mwangu na yeye akanielewa sana. Kwa vile yeye alikuwa ni mwanafunzi wa chuo cha Kati hapa nchini tulikaa pamoja Kama miezi 2.

Alisafiri kwenda huko Dodoma na mimi nikaenda zangu huko Kenya baada ya kumaliza kazi iliyonileta. Mwanzoni mawasiliano yakuwa bomba sana but baada ya muda yalianza kupungua.

Ila tatizo lake hawezi kunitafuta kama hana shida ya hela. Wakati mwingine namtumia text hata WhatsApp namuona yupo Online lakini hajibu isipokuwa anaisoma tu na kupotezea. Kuna wakati napata hasira namtusi ndipo anaanza kujibu kwa kujitetea.

Jamani naumia sana nikifikiria namna nilivyowekeza pesa nyingi kwake kweli naishiwa nguvu kabsa. Mfano sasa hivi nimetuma text WhatsApp ila hajajibu japo kaisoma. Hivi hapo kuna tumaini la ndoa kweli.

Mbaya zaidi nikilalamika ananiambia kuwa anaumia ninapolalamika nipeni ushauri ila tatizo kubwa lipo kwenye kuishi naye mbali na kutonitafuta mpaka nimtafute au awe na shida ya pesa.
CHAGUA CHAUMA,
RAIA TULE WALI_KUKU!!!
 
Dah pole mkuu China ukimpa mtu Figo unalipwa million 200 lakin Tanzania unampa mtu moyo wako na bado anakuomba hela ya kusuka![emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom