Je, hii 'Media Blackout' ya leo juu ya tukio zima la uchukuaji fomu wa Tundu Lissu ndiko kumuenzi vyema Mwanahabari Hayati Rais Mkapa?

Genta my brother, I’m sorry to tell you that this year is the LAST YEAR FOR CCM to lead Tanzania.

Mark my words. Huu ndo mwaka wa mwisho kuongoza Tanzania. From October nchi inaenda kuwa chini ya Chadema.

Nimesikiliza kwa Makini sana hotuba ya Mzee Butiku jana kwenye mkutano wa CCM. Kuna ujumbe aliutuma kwa TISS, Polisi, JWTZ na NEC . Kwa nilivyomsikia nimejiridhisha kuwa wazee wenye maamuzi yao waneridhia nchi kwenda upinzani mwaka huu.

Tukutane October ndugu yangu Genta!!

Na kwa Kuongezea tu ukiona Mzee Joseph Butiku anaongea na kutoa 'Observations' zake jua kwa 99.9% hayo pia yangekuwa Mawazo ya Nyerere.
 
Na kwa Kuongezea tu ukiona Mzee Joseph Butiku anaongea na kutoa 'Observations' zake jua kwa 99.9% hayo pia yangekuwa Mawazo ya Nyerere.
Swadakta my brother. Jana kwa maneno na body language ya mzee Butiku nina uhakika asilimia 100 kuwa Chadema wanachukua nchi October 2020.
 
Yaani hawako serious. Yaani kununua vifaa wameshindwa?
Vifaa vinavyohitajika ni
-camera yenye sdi out
-wireless microphone ya camera
-sdi cable
-liveUsolo
-modem ya 4G
-line ya 4g yenye bando.

Wakipata hiyo setup wanaweza kuenda live wakiwa popote kwenye mtandao kupitia youtube, facebook. Inabidi wanunue haraka kabla ya kampeni kuanza. Hakuna chombo chochote cha habari kitakacho onesha hata picha ya wapinzani.

NB: wale wazoefu wa kuagiza vitu mtafanya bajeti ya vifaa.

Na kwanini iwe hivi Kwao hadi wapitie 'Mateso' haya yote na kwanini kwa CCM iliwezekana na hawakuyapitia haya? Tuacheni 'Unafiki' sometimes.
 
Swadakta my brother. Jana kwa maneno na body language ya mzee Butiku nina uhakika asilimia 100 kuwa Chadema wanachukua nchi October 2020.

Nakubaliana nawe sehemu fulani ila hilo la CHADEMA kuchukua nchi kwa sasa 'nakukatalia' kwani hata Wao kuna mahala 'walijichanganya' sana tu.
 
Ninaanza kuamini taratibu kuwa yawezekana kuna 'Wanafiki' na 'Wapumbavu' fulani 'wanamshauri' vibaya na 'Kumponza' Kisiasa Rais wangu JPM.
Sio kwamba yeye ndo "pioneer" anatoa maelekezo kwa washauri wake maarufu kama "amri toka juu"?
 
Nichukieni mtakavyonichukia GENTAMYCINE ila pamoja na kwamba nakipenda Chama changu Tawala ambacho ndicho Kimeshika Dola ya Kiserikali cha CCM, ila kama 'Mwanataaluma' kitendo kilichofanyika leo hasa cha 'Media Blackout' dhidi ya Tukio zima la Uchukuaji Fomu wa Tundu Lissu wa CHADEMA na ambayo nayasikia yameendelea huko katika Newsrooms ni 'Upumbavu' mtupu.

Sijaona sababu yoyote ile ya Vyombo Vikubwa vya Habari nchini Kupigiwa Simu na hata Waandishi wake 'Kutishwa' hasa kama wakipeleka Hewani ( kama haya Madai ni ya kweli kwani sijayathibitisha bado ) Habari za hili Tukio zima, lakini kinachonisikitisha tu ni kwamba Serikali yangu ya CCM imefanya mengi na makubwa kwa miaka hii Mitano sasa iweje leo hii imuogope Tundu Lissu hivi?

Najua kuwa Tundu Lissu ( Mtani wangu huyu kutoka Mkoani Singida nae ana Changamoto zake ) ila binafsi nilidhani njia pekee ya 'Kummaliza' Kisiasa ni Sisi wana CCM na Serikali yetu Kumuonyesha kwa Vitendo 'Maendeleo' tuliyoyafanya na siyo 'Kumuogopa' hivi hadi kumfanyia 'Mizengwe' ili Tukio zima la leo lisiwe Masikioni mwa Watu ( Watanzania ) tukidhani kuwa labda ndiyo tutamuweza.

Wala haiitaji 'Akili' kubwa kujua ya kwamba kadri Mamlaka husika iliyo chini ya Chama changu Tawala cha CCM kinavyopambana kutaka 'Kumzima' Kisiasa na Kiumaarufu hivi Tundu Lissu kwa 'Kuwatishia' Wanahabari na Vyombo vyao basi ijue ya kwamba ndiyo inasaidia mno Kumuongezea 'Umaarufu' wako na hapa kuna 'Athari' nyingi tu kwa upande wa Kura CCM yangu itazipata.

Halafu Wiki iliyoisha tulikuwa tunamsifu na kumpamba kweli kweli Nguli wa Habari nchini na Mwandamizi kabisa Rais wa Awamu ya Tatu Hayati Benjamin William Mkapa kwamba alipenda 'Demokrasia' na hakuwa na 'Mabavu' dhidi ya Wapinzani. Je, huu 'Upumbavu' uliofanywa leo wa 'Kuvitishia' Vyomba vya Habari Vikubwa nchini 'Visiripoti' Tukio la Lissu ndiyo Kumuenzi Mkapa?

CCM yangu naipenda, Rais na Mwenyekiti wangu Dkt. Magufuli namkubali sana hata Mwenyezi Mungu anajua ila huu 'Upuuzi' mkubwa sijaupenda.
Kama ni kweli media zimetishwa hakuna tatizo maana siku hizi utandawazi umetandaa mnahofia nini?

Kama kuna kilichozuiwa kuonekana si tumeona shida iko wapi?
 
Licha ya media kuzuiwa chadema ilishindwa Nini kuanzisha online media, page zao na kutoa habari, maana jinsi wanavobanwa na ccm kuachwa wanapigwa gape, atleast wangerusha tukio kwenye account za CDM kusubiria huruma tu watasanda, CCM imechokwa ni vile inajipa promo
Ukiuliza swali la namna hiyo lazima uje na jibu kwanza kama TBC ni mali ya CCM, C= Chama, C= Cha, M= Majang............a, huu ujasiri wa kujimilikisha chombo hiki cha umma wameupata wapi?
 
Genta my brother, I’m sorry to tell you that this year is the LAST YEAR FOR CCM to lead Tanzania.

Mark my words. Huu ndo mwaka wa mwisho kuongoza Tanzania. From October nchi inaenda kuwa chini ya Chadema.

Nimesikiliza kwa Makini sana hotuba ya Mzee Butiku jana kwenye mkutano wa NCCR. Kuna ujumbe aliutuma kwa TISS, Polisi, JWTZ na NEC . Kwa nilivyomsikia nimejiridhisha kuwa wazee wenye maamuzi yao waneridhia nchi kwenda upinzani mwaka huu.

Tukutane October ndugu yangu Genta!!
Kuota ni haki ya kila mmoja maana sio tendo la hiyari
 
Tatizo Tundulisu ni kiropo ropo anaweza tukana chombo cha habar na chenyewe kikahusika so anae wakimbiza waandish wa habar ni yeye mwenyewe
 
Nasubiri taarifa ya habari ya TBC leo saa moja usiku(wanaiita, Hadubini kwa siku ya jumamosi) Kama wataonyesha.
 
Uko sahihi Sasa kipindi kina ruzuku walishindwa kuwekexa Mambo muhimu ka haya, CDM inabidi kutafta vichwa vipya vya kuwapa ushauri, hii kulia Lia faulo za ccm hazisaidii

Ushauri wako ni mzuri, tatizo hapo ni zaidi ya cdm kukosa hizo online tv nk. Dhamira ya kiongozi wa nchi ndio tatizo. Hata hao wanaomzunguka na kuwaagiza watishie vyombo vya habari wanajua kabisa sio sawa anachofanya, ila wafanyeje wakati wanafamilia za kulisha. Hali hii ya mapenzi bandia,ndio inawafanya wanaccm waseme wao ni imara kuliko wakati mwingine wowote! Cha ajabu kuna watu wanaamini kuwa kwa sasa ccm ni imara.

Hakuna kitu kigumu dunia hii kama kulazimisha kupendwa. Siku za nyuma kidogo niliwahi kumpenda mrembo mmoja, nilikuwa nampenda kweli kweli. Lakini mrembo yule alikuwa na mpenzi wake. Kwakuwa nilikuwa na vinoti noti si haba, nilitumia umasikini wa mrembo yule kumpata. Baada ya kugundua kwamba ana mpenzi wake, nikaanza kutumia vinoti vyangu kumtengenezea mazingira hatarishi yule mpenzi wake mwingine, kwani nilijua nikikosa mshindani nitakalia kiti kwa raha. Yule mrembo alinisimulia, lakini kwa dhati ya moyo wangu nilikuwa najua fika mapenzi ya yule mwanadada ni kwa yule mshindani wangu. Yule mrembo nilifika mahali nikawa namfanyia undava ili anikubali mimi tu. Siku ya siku yule mrembo akapata ujasiri akaniambia ni kweli namsaidia, lakini hanipendi, bali ni shida tu, hivyo akasema tuachane. Na kweli akaenda kuolewa na mshindani wangu. Hali ile iliniacha na maumivu makubwa ya moyo. Ila hali ile iliniacha na fundisho la kuwa kama hupendwi hupendwi tu, hata utumie nguvu kubwa kiasi gani. Hali hii ndiyo inayokuta ccm kwa sasa.
 
Back
Top Bottom