Je, CHADEMA wakiamdamana kwa Kikokotoo Uchwara, wafanyakazi mtaunga mkono?

Naona sasa maandamano yameshika kasi na kila mtu anayataka. Watu wa Arusha wametutamanisha.

Maandamano ni haki ya kila mtu, ikiwemo wafanyakazi wa umma na sekta binafsi.

Kuna hili la hovyo kabisa kuhusu kikokotoo cha kitapeli cha Rais Samia na CCM. Hakuna mtu anakikubali, sasa sijui kilitokea wapi. Hata wabunge wenyewe hawakikubali ndio maana wao wanavuta mpunga wote.

Na nyinyi wafanyakazi mnatafuta mtu wa kuliamsha baada ya vyana vyenu kuwasaliti. Sasa tunaweza kuongea na Mbowe na Lissu maandamano yakaelekezwa huko. Lakini swali ni Je, mnataunga mkono?
Wafanyakazi wengine wataunga mkono isipokuwa wafanyakazi wafu, yaani walimu. CC Mpwayungu Village
 
Back
Top Bottom