Wewe kawapelekee injili nyoka, Fisi, Chatu na viumbe vyote kama alivyokuagiza Yesu kumbe wote ni ndugu zako hao
Angalia pia Mark 16:9 Pia rejea Genesis 6:2&4, Job 1: 6 na Job 2:1 kumb 18:10-11
Kwa mujibu wa biblia bwana yesu anawaagiza wanafunzi wake watawanyike ulimwenguni wakahubiri Injili kwa viumbe wote.
Kwa matumaini kwamba na mapepo wamo, maana nao ni viumbe. Mark16:15-16
Ahaa
Kumbe umekubali kuwa Majini ni Waislamu na mnajumuika nayo katika ibada za Kiislamu.
Ndio unijibu sasa.
Ni wapi Muhammadi aliamriwa Kuyahubiria Majini.
Yaani awe Mtume wa Majini ?
Sasa ndugu yangu upo radhi kabisa kuchanganyika na Majini katika ibada zote za Kiislamu ?
Yesu alisema Injiri ihubiriwe kwa viumbe vyote lakini sio Majini.
Yakijiingiza Kanisani tuyatoe mara moja kwa kuyakemea.
Sijawahi kuona ndani ya Msikiti mnakemea Mapepo kwakuwa ni nyumba yao ya ibada.
Pale pale kwenye Marko ungesoma kidogo mstari wa mbele unge ona Yesu alivyo waagiza wafuasi wake kuyakemea Mapepo yote.
Marko 16:15
Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
Marko 16:16
Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
Marko 16:17
Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa [emoji117]pepo; watasema kwa lugha mpya.
Inapofikia Swala la Majini, Waislamu mnayatetea sana. Ati ni ndugu zenu wa kushirikiana nao.
Ona Yesu mwenyewe alivyokuwa anayakemea Majini.
Mathayo 8:28
Naye alipofika ng'ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile.
Mathayo 8:29
Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Mathayo 8:30
Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha.
Mathayo 8:31
Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe.
Mathayo 8:32
Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini.
Marko 1:23
Na mara palikuwapo ndani ya sinagogi lao mtu mwenye pepo mchafu; akapaza sauti,
Marko 1:24
akisema, Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je! Umekuja kutuangamiza?
Marko 1:25
Nakutambua u nani, Mtakatifu wa Mungu. Yesu akamkemea, akisema, Fumba kinywa, umtoke.
Marko 1:26
Yule pepo mchafu akamtia kifafa, akalia kwa sauti kuu, akamtoka.
[emoji117]Agano la Kale pia Mungu anawakataza watu kuwa shirika na Majini.
Mambo ya Walawi 17:7
Wala hawatatoa tena sadaka zao kwa wale majini, ambao huwafuata ili wafanye uasherati nao. Sheria hii itakuwa sheria ya milele kwao, kizazi baada ya kizazi.
Mitume na Manabii wote hakuna aliyewahi kufanya shirika na Majini iwe katika Ibada au kawaida.
Muhammadi aliruhusiwa na nani kuyashirikisha Majini katika Dini ya Kiislamu ?
Waislamu ni kweli bado mpo radhi kushirikiana na Majini katika Dini ?
Wakati wa ibada Msikitini kunakuwa na Mapepo mengi sana eti wanakuja kutubu kwa [emoji117]Mola wao Mlezi,
ha...ha..ha..[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mola wao Mlezi sijui ndio nani, ambaye hana mke wala mwana
72:1 - Sema: Imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi moja la majini lilisikiliza, na likasema: Hakika sisi tumeisikia Qur'ani ya ajabu!
72:2 - Inaongoza kwenye uwongofu, kwa hivyo tumeiamini, wala hatutamshirikisha yeyote na Mola wetu Mlezi.
72:3 - Na kwa hakika utukufu wa Mola wetu Mlezi umetukuka kabisa; hana mke wala mwana.
72:4 - Na kwa hakika wapumbavu miongoni mwetu walikuwa wakisema uwongo ulio pindukia mipaka juu ya Mwenyezi Mungu.
72:5 - Nasi tulidhani kuwa watu na majini hawamzulii uwongo Mwenyezi Mungu.
72:6 - Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa wanaume wa kijini;
Poleni sana, mmeingizwa chaka na Muhammadi.
Ukweli ni kwamba Majini ndiyo yaliyo mtumbukiza Muhammadi kwenye Dini yao ya Kiislamu.
Ungekuwa peke yako unayesoma hapa ningekupa ushahidi ungebaki na Butwaa na kuondoka haraka huko kwenye Kilinge cha Majini.