Je, asili ya majini ni ipi?

OK nimekupata mkuu lakini pale kwenye waumini wa kwanza kuingia katika dini niandika kwa context ya jinsia kwa wanaume na wanawake ila in general natambua kuwa ni bi Aisha in concerning to majini sikumaanisha kuumbwa nilimaanisha kusilimu walisilimu baadae sana baada ya binadam kusilim hicho ndicho nilichomaanisha
Oh my goodness! Pumbaa tupu na uzezeta!!
 
Afu hawa watu sijui huwa wanataka nini tu yaan nabii wao anaitwa issa lakin kila saa yesu jaman wafuas wa lucifer nyie nabii wenu ni issa bin mariam yesu ni mungu achaneni naye hawahusu nyie bakini na issa wenu kwan shida iko wapi arifu
Iv nyie wafuas wa lucifer huwa mnashida gan mnatafutaga nini mbona mnatumia nguvu sana kulazimisha issa ni yesu

nyie mna nabii wenu anaitwa issa sawa sisi hatukatai huo issa ni wenu bakien naye sisi hatuna shida nae issa siyo yesu ,yesu ni masihi issa ni nabii ambaye hata kwenye biblia hayupo kwahiyo achane kulazimisha

uzuri mpango wa lucifer tunaujua na tumeshashutika shetan ana mpango wa kusimika dini moja kupitia mazingaombwe kama haya

tofaut za ukristo na uisilamu ni nyingi sana kwanza waisilamu muna mungu wenu allah kwa jina jingine anaitwa ibilis wakristo mungu wetu ni jehova muumba mbingu na dunia kwahiyo bakien na mungu wenu na sisi tuna mungu wetu

Issa bin mariam habali za kuzaliwa kwake zilitoka kuzimu hakuna asiyejua kuwa kuzimu ni makazi ya ibilisi
Yesu kristo mungu habali za kuzaliwa kwake zililetwa na malaika kutoka mbinguni

Issa alizaliwa chin ya mtende hakuna asiyejua kuwa mitende iko arabun
Yesu kristo mungu alizaliwa kwenye hori la kulishia ngo'mbe bethelehemu hakuna asiyejua kuwa bethelehemu uyauhidin

Issa bin mariam alipotea katika mazingira ya kutatanisha na hajulikan alipo

Yesu kristo mungu aliteswa ,akafa akazikwa na akafufuka akapaa mbinguni

Issa hakubatizwa
Yesu alibatizwa kwa maji mto yorodan na yohona mbatizaji

Sasa mimi nashangaa anakuja mtu mmoja mfuas wa shetan anataka kulazimisha issa ni yesu
Nyie waisilamu hamna kichwa kinachoitwa yesu na hamutakaa mpate
Nyie bakien na nabii wenu issa sisi hatuna shida naye huyo ni wa kwenu
Kitu gan kinawawasha hadi mnaanza kudandia tren kwa mbele

Link Halima Mdee amjibu Rais Magufuli kuhusu madawa ya kulevya

Link2 Je, asili ya majini ni ipi?

Link3. Was Jesus a Muslim?

Link4. Was Jesus a Muslim?
 
Soma upate faida
JINA JEHOVAH SI JINA LA MUNGU ISIPOKUWA KOSA BAYA

Leo nawaleteeni jibu la swali moja kati ya mengi mliyoniuliza enyi vijana. JIbu ni refu lakini someni kwa utulivu. Ni juu ya jina JEHOVAH. Hali halisi ni kwamba kuna watu tunasadiki kuwa jina ‘JEHOVAH’ ni jina pekee la Mungu kwa vile linatokea mara 6832 katika Biblia zetu za Kiswahili au Kiingereza. Ndipo tunatamka kwa mbwembwe jina hilo na kuendeshea makongamano na sala kwa sauti za juu kabisa. Lakini nawataarifuni kwamba tumedanganyika na tumepotea kwa sababu hatujui jina hilo lilikotokea na hata watafsiri wa Biblia hawajachukua hatua ya kuondokana nalo. Kifupi, jina “Jehovah” ni mapato ya kosa la usomaji Kiebrania kimbumbumbu lililofanywa na Padre Peter Galantin, muungamishi wa Baba Mtakatifu Leo X na labda kabla yake kama inavyosomeka pia katika maandishi ya Raymond Martin (1270 B.K. hivi). Unajua, usilolijua ni kama usiku wa giza.
Usishtuke, nitakuelezea sasa hivi kosa lilivyofanyika. Lugha ya Wayahudi au Waisraeli ni Kiebrania, kama ilivyo lugha ya Watanzania Kiswahili. Hivyo Wayahudi wanazungumza Kiebrania. Ndiyo lugha waliyozungumza kabla ya kuchukuliwa utumwani Babeli. Lakini wakati wa utumwa wa Babeli hadi waliporudi kutoka utumwani na kisha kuendelea hadi wakati wa Yesu lugha yao ya siku kwa siku ilikuwa Kiaramayo, ijapokuwa Biblia yao, ndiyo Agano la Kale, kwa ujumla wake, iliendelea bado kusomwa katika Kiebrania chao cha zamani. Baadaye walipotawaliwa na Wagiriki (Waseleusidi), Wayahudi wakapaswa wajifunze Kigiriki (Kiyunani). Tangu mwaka 63 K.K., wakoloni wapya Warumi walipowafurusha Wagiriki wakaishika pia Israeli (Uyahudi), Wayahudi wakalazimika kujifunza Kilatini pia. Kumbuka, Kilatini ilikuwa lugha ya watu wa Dola ya Kirumi (ndio tunaowaita Warumi).
Ndiyo kisa wakati ule wa Yesu, nchini Israeli (Uyahudi) kulikuwa na lugha nne: Kiebrania, Kiaramayo, Kigiriki na Kilatini. Lugha hizo zilitumika ifuatavyo. Walisoma Maandiko Mtakatifu hekaluni na katika sinagogi katika Kiebrania; mitaani walizungumza Kiaramayo; askari wa Kirumi na wengine waliojifunza kwa wepesi walizungumza Kilatini na wasomi waliandika na kuzungumza Kigiriki. Ndiyo maana kibao cha mashtaka ya Yesu kiliandikwa katika lugha tatu: Kiebrania (kwa kweli kwa maana ya Kiaramayo) kwa ajili ya Wayahudi kusoma, Kilatini kwa ajili ya askari wa kigeni na wengineo na Kigiriki kwa ajili ya wasomi (rej. Yn 19:20).
Baada ya nchi ya Uyahudi kuanguka na Wayahudi kutawanyika (mwaka 70 B.K), kokote walikotawanyikia walijitahidi kurudi kwenye Kiebrania chao. Madhulumu na mateso waliyopewa na Adolf Hilter, kule Ujerumani, kabla na wakati wa vita kuu ya pili ya dunia (1939-1945) yaliutia ulimwengu zimanzi na wazo la kurudi Israeli na kujenga tena taifa lao likazaliwa.
Ndipo tangu mwaka 1948, kwa msaada wa Umoja wa Mataifa (wa wakati ule) na wa mataifa makubwa ya Marekani na Uingereza, Wayahudi walisaidiwa kurudi nyumbani kusudi wakalijenga upya taifa lao. Tangu taifa la Israeli lilipozaliwa (mwaka 1948), Kiebrania kikashika kasi, lakini Kiebrania kilichobadilika katika mengi. Hata hivyo, katika Biblia yao (ndiyo Agano la Kale), Kiebrania kimetunzwa kile kile cha zamani kwa maana wanaamini hakuna ruhusa kubadili neno la Mungu.
Ndiyo kisa Kiebrania kinachozungumzwa siku kwa siku siku hizi kimekuwa kipya, yaani kinatofautiana kwa namna fulani na Kiebrania cha kwenye Biblia yao. Tofauti hiyo ni kama iliyopo kati ya Kilatini na Kiitaliano, au kati ya Kilatini na Kireno au kati ya Kilatini na Kihispania. Usihangaike. Hatujapotea njia, nilitaka kukujuza japo kidogo historia ya Wayahudi. Sasa turudi kwenye neno letu la “JEHOVAH”.
Katika Kiebrania chao, Wayahudi huandika jina la Mungu wao kwa herufi nne YHWH. Hiyo herufi ya kwanza “Y” unaweza pia kuiandika na kuitamka kama “J” na hivi kuwa JHWH. Halafu hiyo herufi ya tatu “W” unaweza pia kuiandika na kuitamka kama “V” na hivi kuwa JHVH. Herufi hizi ndizo zinazofumbata lile jina aliloambiwa Musa katika Kut 3:14.
Basi, herufi za jina la Mungu wa Wayahudi huandikwa kwa herufi hizo nne YHWH au JHVH. Kwa Wayahudi hizo ni herufi takatifu kabisa, tena takatifu bin mno. Katika ulimwengu wa taaluma ya Biblia ni herufi zinazojulikana kwa istilahi maarufu “tetragrammaton”. Hebu nirudie na kusisitiza, herufi hizo ni herufi takatifu kabisa kabisa.
Sasa tuje kwenye uandikaji na usomaji wake. Herufi hizo zinapoandikwa katika Kiebrania huandikwa kwa kupindua, yaani herufi inayosomeka katika nafasi ya kwanza katika Kiswahili chetu, ndiyo ya mwisho katika uandishi wa Kiebrania. Kwa nini? Kwa sababu Wayahudi huandika na kusoma lugha yao ya Kiebrania kwa kuanzia kulia kwenda kushoto, yaani hivi HWHY. Uandikaji na usomaji huu wa kutoka kulia kwenda kushoto unalingana na uandikaji na usomaji wa lugha nyingine za Kisemiti, hususan, Kiaramayo na Kiarabu.
Nifuatilie vyema. Nimeshadokeza hapo juu kwamba herufi hizo nne (ndiyo tetragrammaton) zinatokea mara 6832 katika Biblia ya Wayahudi, ndiyo tunaloita sisi Agano la Kale. Sasa sikiliza kiroja hiki. Ijapokuwa herufi hizo zinatokea mara nyingi hivyo kwenye Biblia yao, Wayahudi wote wa kawaida walikuwa na bado hawaruhusiwi kuzisoma, si kwa sauti wala kwa kimya kimya kwa sababu ya utakatifu wa jina la Mungu wao. Kwa nini? Kwa sababu kuzisoma bure bure kungelingana na utovu wa heshima kwa Mungu mkuu na kuivunja amri ya Mungu ya kutolitaja bure jina lake.
Ndipo ilikuwa marufuku na bado ni marufuku kabisa Myahudi wa kawaida kuzisoma na kuzitamka herufi hizo. Hapo ndipo utakaponiuliza: Sasa walifanyaje walipokumbana na herufi hizo mara 6832 katika Maandiko yao matakatifu? Tulia nikueleze sasa hivi. Ni hivi, kusudi watu wasizisome wala kuzitamka, hususan watoto, Wayahudi walifundishana kuziruka kwa kutamka mojawapo ya maneno manne ya mbadala ‘ADONAI’ (Bwana wangu), au MAQOM (Mahali), au SHEM (Jina) au SHAMAIM (Mbingu). Hata hivyo, kati ya mibadala hii minne, wengi walipendelea sana kutumia mbadala wa ‘ADONAI’.
Ndipo kwa mibadala yao hiyo minne, hakukuwa na taabu ya kuzidi kwa Wayahudi wenyewe, maana kila walipokumbana na herufi hizo walisoma “kwa raha zao” ‘ADONAI’, au MAQOM, au SHEM au SHAMAIM. Lakini hatari ya watoto kuzisoma herufi zile kwa kukosa kuzoea mibadala iliyokuwa ikijulikana na wakubwa wote iliendelea pale pale.
Hebu sikiliza kitu kingine. Kabla ya karne ya 11 K.K., maneno yote ya Biblia ya Wayahudi yalikuwa yameandikwa kwa konsonanti tu. Yaani kama katika Kiswahili chetu, kwa neno “mama”, tungeliandika “mm” tu, kwa neno “baba” tungeliandika “bb” tu, kwa neno “kuku” tungeliandika “kk” tu, kwa neno “mimi” tungeliandika “mm” tu, kwa neno “kiko” tungeliandika “kk” tu, kwa neno “bibi” tungeliandika “bb” tu, kwa neno “korokoroni” tungeliandika “krkrn” tu na kadhalika. Kutofautisha kati ya “kk” ya “kuku” na “kk” ya “kiko” ingelitegemea mazoea na muktadha tu.
Baadaye, Wayahudi waliamua kurahisisha usomaji wa lugha yao kwa kuzitia vokali. Basi, waandishi wao walioitwa Masoreti walifanya kazi kubwa ya kutia vokali maneno yote ya Biblia yao katika karne ya 11 K.K.
Lakini sikiliza jambo lingine, vokali za Kiebrania huandikwa chini ya konsonanti (isipokuwa katika maneno machache sana mbele ya konsonanti). Hivi katika usomaji, unaanzia kulia, unachukua konsonanti juu na kuokotea vokali yake chini (au katika maneno machache mbele yake) ili kujenga silabi na hivyo hivyo kuendelea kushoto hadi unamaliza neno na mstari wako unaosoma.
Sasa waandishi hao kwa kukinga hatari ya watoto na hata wakubwa wengine wenye papara, wasisome herufi takatifu “YHWH” au “JHVH” waliandika vokali za mbadala wao maarufu “ADONAI” chini ya herufi hizo takatifu. Vokali za jina “ADONAI” ni e, o na a zilizoandika pia kutoka kulia kwenda kushoto kadiri ya herufi “YHWH” au “JHVH” zilizoandikwa vile vile kutoka kulia kwenda kushoto. Hivi wakaandika e, o na a chini ya herufi “HWHY” au “HVHJ”. Ndipo ikawa imefanana na hivi, “HaWoHeY” na “HaVoHeJ” ila soma kwa kujipindua, yaani kutoka kulia kwenda kushoto. Sasa angali hatari. Hapo haikutakiwa kuziunganisha konsonanti na vokali hivyo, kwani hizo konsonanti zilikuwa za jina takatifu lisilopaswa kutamkwa na hizo vokali zilikuwa za jina “ADONAI” lililoruhusiwa na kutakiwa kutamkwa.
Sasa Padre Peter Galantin alifanyaje kosa lake la kiusomaji? Alifanya ifuatavyo. Katika kutokujua kwake kwamba konsonti “HWHY” au “HVHJ” zilikuwa za jina takatifu lisilopaswa kusomwa wala kutamkwa na Myahudi wa kawaida na vokali e, o na a zilikuwa vokali za jina mbadala “ADONA” akasoma kwa kuunganisha kila kitu kama nilivyoonesha hapo juu. Yaani akachanganya mambo, konsonanti HWHY au HVHJ ambazo zilikuwa ni jina la Mungu lisilotamkwa na Wayahudi wa kawaida na vokali e, o na a za jina la mbadala ‘ADONAI’ (Bwana wangu) lililoruhusiwa kutamkwa na mtu yeyote yule kama mbadala wake.
Ndipo katika kosa hilo, akasoma kimbumbumbu kutoka kulia kwenda kushoto na kupata HaWoHeY au HaVoHeJ yaani YeHoWaH au JeHoVaH ndiyo YEHOWAH au JEHOVAH. Kumbe, hili kosa la mwaka.
Nadhani sasa unaelewa na wala hujalewa. Kumbe alichokifanya Padre Peter Galantin siyo tu kilikuwa hakikubaliki kati ya Wayahudi wenyewe bali ilikuwa pia kufuru kubwa. Kwa nini? Kwa sababu usomaji wa herufi zile nne (tetragrammaton) ulikuwa mtakatifu sana na wa pekee sana. Nimeshasema konsonanti hizo zilikuwa zimekatazwa kutamkwa na watu wa kawaida. Niulize tu wala usisite: Sasa zilikuwa zinasomwaje au lini?
Nisikilize vyema. Herufi hizo zilikuwa zinasomwa NA KUHANI MKUU PEKE YAKE, TENA SIKU MOJA TU KATIKA MWAKA PALE ALIPOINGIA PEKE YAKE PATAKATIFU PA PATAKATIFU. Hiyo ilikuwa katika siku ile ya toba ya taifa (ndiyo Yom Kippur).
Basi, kwa jinsi hii, waamini wa kawaida hawakuwa hata na picha ya matamshi yake. Sasa kama Wayahudi wa kawaida hawakujua na hawajui hata leo hii namna ya herufi zile zinavyotamkwa wewe na mimi watu wa Bongo hii tunajinasibu vipi kujua zinavyotamkwa? Eti, tujue sisi wakati Wayahudi wenye Biblia yao hawajui? Lazima sisi tuwe waongo wa kutupwa. Kumbe, tunasema uongo mubashara!
Naongeza kusema. Nakwambia hivi, hata matamshi ya “YAHWEH” ni matamshi ya kusadifisha tu. Wote sisi hatujui jinsi herufi “YHWH” au “JHVH” zilivyotamkwa. Usinikaidi. Watafute hata Wayahudi wenyewe popote pale walipo, kwa karibu zaidi hapo jijini Dar es Salaam, uwaulize, watakwambia hawajui, sasa wewe na mimi ni nani katika suala hili hata tujidai na jina YEHOVAH? Basi, ni uongo wetu na aibu yetu. Nawasihini tuachane na jina YEHOVAH. Sisi Waafrika na Waswahili, jina MUNGU linatutosha kabisa. Tusiyatake makubwa tusiyoyaweza wala kuyajua.
Acha niongeze kusema tena. Tena siku hizi matamshi ya herufi hizo takatifu yametatizika zaidi na zaidi kwa sababu, kwa vile Wayahudi hawana tena Makuhani Wakuu na wala hekalu lao halipo tena, siyo tu hawana mtu wa kuzitamka bali hawana pia hata mahali pa kuzitamkia hata kama ni hiyo mara moja kwa mwaka. Hii maana yake hata namna ya kuzitamka herufi hizo kunapotelea kabisa angani.
Sasa namaliza somo langu. Nakupeni mfano wa kosa lilozaa matamshi yasiyojuzu ya YEHOWAH au JEHOVAH. Kosa hili tukilieleza kwa mfano wa Kiswahili ni hivi ifuatavyo. Waswahili tunamwita Muumba mbingu na nchi “MUNGU”. Sasa ingelikuwa kwamba jina hilo haliandikwi kwa herufi zote isipokuwa konsonanti MNG tu na kisha Waswahili wa kawaida tungelikuwa tunakazana na kuzitamka isipokuwa Askofu Mkuu tu, tena mara moja tu kwa mwaka pale angalipojificha nyuma ya altare peke yake. Na kwa watu wa kawaida tungelikuwa tunaruhusiwa kutamka jina “BWANA” kila herufi “MNG” zinapoonekana katika Biblia yetu. Baadaye upitishwe uamuzi wa kuandika vokali za jina BWANA yaani a na a chini ya konsonanti “MNG” kama hivi MANGA kwa kusudi la kuwasaidia wasomaji, hasa watoto, wasome neno BWANA bila kutamka herufi tukufu na takatifu “MNG”.
Halafu baada ya karne nyingi Biblia iwafikie labda Wachina ambao hawajui Kiswahili vizuri na halafu mmoja wao adhani kwamba kuandika MANGA ni sawa na yeye anyooshe usomaji wa jina MNG kwa kuunganishia vokali A na A za jina BWANA na hivyo ahitimishe kwa kusema jina la Muumba mbingu na nchi kwa Waswahili ni MANGA. Hapo Mchina huyo angelikuwa amewaingizwa wenzeke kwenye kosa la mwaka na ndipo jina MANGA lisingekuwa jina halisi la Muumba mbingu na nchi bali jina la utani mkubwa. Basi, ndivyo linavyofanana na kosa lililoibua matamshi ya YEHOWAH au JEHOVAH.
Kwa vyovyote iwavyo tumepotezwa na kosa la kiusomaji la Padre Peter Galantin na wote tunaotamba na matamshi hayo JEHOVAH hatujui tunachotamba nacho. Ni kama siku hizi sisi watu weusi tunavyotamba na jina baya kama “NIGGAZ” wakati ni tusi la Wamarekani weupe kuwatukania weusi wenzetu. Ni kama mtu asiyejua Kiingereza anavyoweza kuvaa T-shirt iliyoandikwa “MORTUARY ATTENDANT” (yaani mhudumu wa chumba cha maiti) kwenye sikukuu. Ni kama mkulima maskini anayetamba kijijini na T-shirt ya mtumba iliyoandikwa “SEX PISTON” na kadhalika. Maskini tuhurumiane! Lakini sasa kisomo kinatuwekea wazi kosa la matamshi ya JEHOVAH lilivyotokea, kumbe tuamue kukubali na kujinasua kutoka matamshi hayo batili. Wala si aibu kurudi nyuma na kuacha. Yeyote anayehusika, wakati ni leo.
Kumbe, basi, kati ya maneno ya kuondolewa kwenye Biblia zetu za Kiswahili na Kiingereza, pale zitakapofikia fursa zingine za kuboreshwa, ni neno JEHOVAH. Tulieni, nitawaonesheni maneno mengine katika nafasi zingine za usoni. Hiyo si kazi ya kila mtu, isipokuwa ni kazi ya watafsiri wa Biblia, yaani wale watu waliosomea Sayansi ya Biblia. Natumaini tumeelewana. Kwa herini, kwa leo! Fr. Amigu
 
Hivi kuna Binadamu yeyote ambaye ameshaenda Motoni,halafu akarudi Duniani kuelezea jinsi kulivyo? Au ni Imani tu za Binadamu kuwa ukifa unaenda Motoni au Peponi.
Swala la motoni au peponi si imani ya binadamu tu bali ni mafundisho ambayo yamo katika biblia na Quran.
Biblia ina mention juu ya moto, lakini sito kwenda kiundani sana juu ya hilo. Fundisho la moto katika biblia ni symbolical. Biblia inapo ongelea moto ina maanisha "kukatiliwa mbali" kwa maana ya kwamba Mungu akikuukumu kwa kutotii huto exist tena. That makes sense kwamba Mungu hawezi kukuchoma milele wakati umeishi miaka si zaidi ya 80 na kufanya dhambi baada kufika miaka 15 alafu uchomwe milele!? Kwa kweli hapo hamna haki! Lakini Quran inafundisha tofauti kwamba siku ya kiama mtenda dhambi anapata mateso milele!

Hii issue ya kuamini hivi vitabu vya imani inategemea na kitu gani ndani ya maandiko yamekusukuma kuamini. Binafsi baada ya kuisoma biblia nikaona kuna maandiko mengi ambayo si rahisi mwanadamu kujua pasipo taarifa kutoka kwa Mungu. Kwa mfano, biblia iliandika more than 4000 years ago kwamba dunia ni duara na hiko katika anga la mbingu pasipo kushikiliwa na kitu. Kwahiyo sasa kama biblia ingesema vingine nisinge kuwa na imani nayo.

Kwa mfano, unajua mtu una amini kwamba mtu fulani ni baba yako kutokana na ushaidi fulani uliyo kuwapo ingawa hukushuhudia wao wakifanya matendo ya procreation! Bali imani inakuwepo kutokana na baadhi ya evidence zilizokuwepo kama kufanana, DNA, upendo wa wazazi na kadhalika. Haiwezekani mtu ufanane na baba yako alafu ukatae kwamba siyo baba yako hata kama hukushuhudia kile kitendo.
Ni sawa sawa na Biblia kuna mambo mengi yamethibitishwa kuwa kweli na binadamu kwa hivi sasa, na yaliongelewa siku nyingi kabla ya advances technology kuwepo.
 
uzuri mpango wa lucifer tunaujua na tumeshashutika shetan ana mpango wa kusimika dini moja kupitia mazingaombwe kama haya

tofaut za ukristo na uisilamu ni nyingi sana kwanza waisilamu muna mungu wenu allah kwa jina jingine anaitwa ibilis wakristo mungu wetu ni jehova muumba mbingu na dunia kwahiyo bakien na mungu wenu na sisi tuna mungu wetu

Issa bin mariam habali za kuzaliwa kwake zilitoka kuzimu hakuna asiyejua kuwa kuzimu ni makazi ya ibilisi
Yesu kristo mungu habali za kuzaliwa kwake zililetwa na malaika kutoka mbinguni

Issa alizaliwa chin ya mtende hakuna asiyejua kuwa mitende iko arabun
Yesu kristo mungu alizaliwa kwenye hori la kulishia ngo'mbe bethelehemu hakuna asiyejua kuwa bethelehemu uyauhidin

Issa bin mariam alipotea katika mazingira ya kutatanisha na hajulikan alipo

Yesu kristo mungu aliteswa ,akafa akazikwa na akafufuka akapaa mbinguni

Issa hakubatizwa
Yesu alibatizwa kwa maji mto yorodan na yohona mbatizaji

Sasa mimi nashangaa anakuja mtu mmoja mfuas wa shetan anataka kulazimisha issa ni yesu
Nyie waisilamu hamna kichwa kinachoitwa yesu na hamutakaa mpate
Nyie bakien na nabii wenu issa sisi hatuna shida naye huyo ni wa kwenu
Kitu gan kinawawasha hadi mnaanza kudandia tren kwa mbele

Link Halima Mdee amjibu Rais Magufuli kuhusu madawa ya kulevya

Link2 Je, asili ya majini ni ipi?

Link3. Was Jesus a Muslim?

Link4. Was Jesus a Muslim?[/QUOTE]
Mmmhhh toa ushahid
 
Nachangia tu.

Waislamu wanakitabu chao ambacho ndo mwongozo wao na kina mafundisho yake
Kwa hiyo wako sahihi wanachosema kama Qurani inavyosema.

Wakristo nao wana vitabu vyao wanavyo viamini, kama vile Torati, Manabii, Wafalme, Zaburi, Injili, ambavyo wameviweka pamoja na kuviita Biblia, vinatoa mwongozo na mafundisho ambayo wanapo yasema wako sahihi.

Kila dini iko sahihi kutokana na mwongozo wake.
Ziko imani nyingine nyingi tu kama Wabudha, Wahindu, Wa rastafari nk.
Nao wana vitabu vyao na wako sahihi wanapofata mafundisho yake.

Tatizo

Linatokana na swali

Je imani gani au dini gani ndiyo inayofuata maagizo ya Mungu aliyeumba mbingu na nchi na inatumia kitabu gani ?

Hapo kila dini au imani inasisitiza kuwa wao ndo wako sahihi

Kama ndo hivyo basi kila watu wabaki na imani yao au dini yao kwani wameisoma na kuielewa na wako tayari kupewa zawadi waliyo ahidiwa na Mungu wao.

Kama kutatokea wadadisi watakaotaka kuzisoma imani zote kwa hekima ili wamtafute Mungu wa kweli yupo katika imani au dini gani, basi wanaweza kubadilisha imani zao na kujiunga kwenye imani watayoiona ni sahihi

Hapo ndipo tunaposikia, Bwana Josefu amesilimu na kuwa Muislamu, au ustadh kilemile sasa ni Mkristo nk.

Bila hivyo kila mtu aheshimu imani ya mwenzake na ndo anavyoamini.

Huwezi kumbadilisha mtu ghafla katika imani yake au kumwaminisha mtu haraka juu ya imani nyingine na wengine hawako tayari kujaribu kuisoma kwa umakini imani nyingine ili kujua kuwa wapo sahihi au la.

Lazima mjue ukweli huu la sivyo
Mtabishana kutwakuchakuchakutwa, msifikie muafaka

Nasilisha.
 
Hivi kuna Binadamu yeyote ambaye ameshaenda Motoni,halafu akarudi Duniani kuelezea jinsi kulivyo? Au ni Imani tu za Binadamu kuwa ukifa unaenda Motoni au Peponi.
Ili kupata jibu la swali lako ni wewe mwenyewe unatakiwa kujiuliza je una akili? Je doctor gani alishawah kukufanyia operation ya kichwa kisha akathibitisha kuwa unazo au hauna??

Je unaweza kututhibitishia kuwa wewe una akili?

Utakapo tafakari jibu la haya maswali ndipo utakapo pata jibu la hilo swali lako!!

Sio kila kitu huthibitishwa kwa kuona
 
Naombeni kusadiwa kujua kuhusu majini. Nina imani watu wengi huwa tunatishwa sana..

Nina maswali naombeni kupewa msaada..

Nani aliwaumba majini?

Majini wameumbwaje na kwanini waliumbwa kwa kazi gani?

Kwanini hawaonekani nguvu gani au wao wapo ulimwengu gani hasa hadi tunashindwa kuwaona?

Je, vitabu vya dini vinasemaje kuhusu hawa viumbe ni sehemu gan majini watajwa na je mitume wa Mungu wamewahi kuwatumia hawa kwa kazi gani na kwanini?

Kwanini wanaonekana kuwa na nguvu zaid kuliko binadamu, mbinu ipi sahihi ya kuwadhibiti hao viumbe?

Je, maumbile yao halisi ni yapi na utawezaje kuwatambua?

Je, Mungu wanayemwamini ni huyu tunayemwamini sisi na huko watahesabiwa vipi haki siku ya mwisho na adhabu yao itakuwaje kwenye moto wa milele (nasikia wapo kama moto sina uhakika).

Je, wanaliana vip mimba zao hukaa muda gan na huishii miaka mingap tokea azaliwe yaani jin Mzee yupoje.

Mfumo wao wa utawala upoje na je kuna adhabu za kuwapatia endapo wanasumbua binadamu?

Je, wanaweza kuzaa na binadamu na mtoto akizaliwa huwaje?

Yaan dah yapo mengi maswali!
Naona wengi badala ya kukupa majibu wamehamia ktk malumbano ya kidini.

In shaa Allah nitajitahidi kukujibu walau kwa uchache Kama ifuatavyo : Swali lako la kwanza ni:

1)NANI ALIYE WAUMBA MAJINI?

Jibu: majini wameumbwa na Mwenyezi Mungu. Uthibitisho ni Qur 51:56 Allah aliposema:

"Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu mimi "

Pia 7:54 Qur an
" .... Fahamuni : kuumba (ni kwake tu Mwenyezi Mungu) na amri zote ni zake (Mwenyezi Mungu), ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu Mola wa walimwengu wote".

Pia Qur 30:26 inasema
"Na vyote vilivyopo mbinguni na ardhini humtii yeye.

Bila shaka huu ni ushahidi tosha kuwa Mwenyezi Mungu ndiye ALIYE WAUMBA MAJINI NA VITU VYOTE UVIONAVYO ULIMWENGUNI.

2)
umeuliza WAMEUMBWAJE?
Jibu: wameumbwa kwa Moto. Ushahidi: quran 7:12

".....Akasema (iblisi) : mimi ni bora kuliko yeye, (mimi) umeniumba kwa moto, naye umemuumba kwa udongo. "

Pia Qur 55:15
" Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto ".

Kwa hiyo MAJINI waliumbwa kwa moto.

3)
KWA NINI HAWAONEKANI
Jibu:
Ameitwa Jinni kwa sababu ya kutoonekana kwake na watu, hii ni kwa sababu kila kisichoonekana kwa jicho la binadamu ktk lugha ya kiarabu jina lake (hutoholewa) hutokana na herufi hizi (JIYM) na (NUUN).

Kwa mfano :bustani huitwa 'janna' kwa sababu ya kuzungukwa kwake na majani kila upande pasiweze kuonekana ndani.

Mfano wa pili. :Elimu ya uzazi huitwa 'Ilmul ajinna' kwa sababu ya kutoonekana kwake kile kilichokuwemo tumboni mwa mzazi.

Na majinni nao wamepewa hilo jina kwa sababu ya kutoonekana kwao kwa macho ya binadamu.

Ukichunguza hayo maneno 'JANNA' 'AJINNA ' na' JINNI' yana herufi ya JIYM na NUUN ndani yake.

4)
WANATAJWA WAPI KTK VITABU VYA DINI?

Jibu: Hawa majini wametajwa ktk Qur an na ktk biblia. Ktk Qur an wametajwa sehem tofaut tofaut na pia ipo sura inyowaelezea kwa kirefu, sura ya 72.

Pia ktk biblia wametajwa katika maeneo tofauti tofauti.
Mfano 1wafalme 13:17 walihusishwa na ujenzi wa nyumba ya nabii suleyman.

Pia ktk yuda 1:6-na 2kornto 11:14-15 biblia inawatambua majini km malaika waovu.
Ila ikumbukwe kuwa malaika waliumbwa kwa nuru na majinni kwa moto

Yuda 1:9 imemtaja kwa jina la "IBLIS" Kama alivyo tajwa ktk quran. Yuda 1:9 "lakini malaika mkuu alipo shindana na ibilisi na kuhojiana naye...."
Pia ufunuo 20:10 inasema ibilisi mwenye kuwadanganya watu atatupwa kwenye shimo la moto.
Hata ukisoma quran 6:128 inasema hao majini waovu na wafuasi wao wa kibinadamu wataingia Motoni.

(5)
NAMNA YA KUWADHIBITI
Jibu: kuwadhibiti kwake ni kwa kuisoma quran. Ukiisoma ayatul kursiy asubuh basi unajilinda nao tangu hiyo asubuh mpaka jioni yake.

Na pia Ukiisoma tena kwa hiyo jioni basi utajilinda dhidi yao mpaka asubuh yake.

kwa kifupi pendelea kuisoma hii ayatul kursiy In shaa Allah Mwenyezi Mungu atakuepusha nao.

(6)
MAUMBILE YAO HALISI
Jibu: Mtume (swalla Allahu 'Alayhi wa sallam) amesema:
"majini wako namna tatu, namna moja wana mabawa wanaruka na (namna) nyingine majoka na ng' e na hawapendi kuashiria mahala pamoja na hupenda kuhama".

Atw-twabraaniy na Al-haakim na Al-Bugharary.

(7)
WANAAMINI MUNGU GANI?
Jibu: miongoni mwao wapo walio silimu na walio Baki kwenye ukafiri ambao ndio huwapotosha binamu ili waende nao Motoni siku ya mwisho .

Quran 72:14 "nasi wapo miongoni mwetu walio silimu, na wamo miongoni mwetu walio kengeuka. Walio silimu hao ndio Walio tafuta uongofu

Kwa hiyo ktk wao majini wapo miongoni mwao walio silimu na waka mwamini Mwenyezi Mungu huyu tunaye mwamini wanadamu. Nao wakitenda mema basi watalipwa Kama watakavyo lipwa wanadamu watendao mema. Na wale waovu nao watalipwa Kama ilivyo kwa wanadamu watendao waovu.

(8)
WATAADHIBIWA ADHABU GANI?
Jibu: Majini waovu wataadhibiwa adhabu ya moto. Uthibitisho ni quran

6:128 "Na ile siku atapo wakusanya wote awaambie: Enyi makundi ya Majini! Hakika nyinyi mmechukua wafuasi wengi Katika wanadamu.

Na marafiki zao katika wanadamu waseme: Mola wetu! Tulinufaishana sisi na wao, na tumefikia ukomo wetu ulio tuwekea

Basi Mwenyezi Mungu atasema: moto ndio makaazi yenu, mtadumu humo ila apendavyo Mwenyezi Mungu. Hakika Mola wako niwenye hekma na mwenye kujua.

Pia rejea Ufunuo 20:10
"Na Yule ibilisi mwenye kuwadanganya akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti alimo Yule mnyama na Yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku Hata milele na milele "

(9)
JE WANAWEZA KUZAA NA BINADAMU
Jibu : Ndio quran 18:50 inaonyesha kuwa ana kizazi chake (generation) pia quran 17:64 yaonyesha kuwa anauwezo wa kuzaa na mwanadamu

Rejea visa vya majini mahaba
Utapata kuelewa zaidi Juu ya hili.
Yangu ni hayo, km kuna sehemu nimeenda wrong basi wataalam watanisahihisha
 
Majini ni malaika walio muasi Mungu pamoja na Shetani ,Majini yanatumiwa na shetani kutumikisha watu. wakrito wanayaita mapepo .Hakuna ushirika wowote kati ya ukristo na majini au mapepo ,kiufupi hayataki jina la Yesu. Ila kuna ushirika mkubwa kati ya uislamu na Majini ,wanaswali nayo wanasema ni maislamu .Mimi hapo ndio napata mashaka makubwa juu ya Dini hii.
Kwa bahati mbaya sana mambo yahusuyo majini katika imani ya Kiislamu ni tofauti sana na vile tulivyosoma katika Biblia. Ingawa Quran na Hadithi za Muhammed, Mtume wa Waislamu, Vinatutaka sisi wakristo tumwamini allah S.W. mungu anayeabudiwa na Waislamu Misitikini.
Katika Suratul Waqia 51:56.
“ Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu” katika Quran Suratul Al- Ankabut (Buibui), 29:46-47) “ Wala msibishane na watu waliopewa kitabu (kabla yenu) ila kwa yale (majadiliano) yaliyo mazuri isipokuwa wale waliodhulumu miongoni mwao na semeni tunaamini yaliyoteremshwa kwetu na yaliyoteremshwa kwenu na Mungu wetu na Mungu wenu ni mmoja nasi ni wenye kunyenyekea kwake”.
Waliopewa kitabu kwa mujibu wa Quran ni Wayahudi na Wakristo. Je, hoja kuwa Mungu wetu na Mungu wao wanayemwabudu kuwa ni mmoja je ni sahihi?. Tuchunguze kuhusiana na mafundisho ya Allah S.W. wa misikitini kuhusu majini ndipo tutajua ni mmoja au la!.
Muislam yeyote ili imani yake ikamilike ni lazima aamini yanayoonekana na yasiyoonekana katika Suratul Al- Baqarah (Ng’ombe Jike la Njano), 2:1-3.
“ Alif Lam Mym. Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake ni uongozi kwa wamchao mwenyezi Mungu ambao huyaamini yasiyoonekana (maadaam) yamesemwa na mwenyezi Mungu na Mtume wake) husimamisha sala na hutoa katika yale tuliyowapa.
Quran peke yake ukiichunguza utaona kuwa majini yamechukuliwa kama ni viumbe tofauti na mashetani, wanasema hivyo kwa sababu katika uislamu majini yamepewa hadhi kubwa sana na ya kipekee. Hadhi hiyo ni kwa sababu majini waliamini Quaran.
Tusomapo katika Quran Suratul al- Ahqaf, (Kichuguu cha mchanga) 46:29
“ Na (wakumbushe) tulipokuletea kundi la majini (kuja kwako) kusikiliza Quran. Basi walipoihudhuria walisema (kuambiana):- “ Nyamazeni (msikilizeni maneno ya Mwenyezi Mungu)” Na ilipokwisha (Somwa) walirudi kwa jamaa zao wakiwaonya”.
Na ndani ya Quran kuna sura nzima inayoitwa sura ya majini (Mashetani) hiyo ni sura ya 72. katika sura hiyo inasema 72:1-3, 14. “ Sema: imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi moja la majini liliisikia (Qurani) likasema hakika tumesikia Qurani ya ajabu inaongoza katika uongofu. Kwa hivyo tumeiamini wala hatutamshirikisha yoyote tena na Mola wetu na kwa hakika utukufu wa Mola wetu umetukuka kabisa. Hakujifanyia mke wala mwana……………………. Nasi wamo miongoni mwetu na wamo miongoni mwetu waliokengeuka waliosilimu hao ndiyo waliotafuta uwongofu.
Kwa hiyo aya hizi zinaonyesha kuwa Quran ilipokuja ndipo majini waliposilimu. Kumbuka kuwa Quran imeanza mwaka 610 B.K kipindi ambacho Biblia tayari ili kuwepo kwa karibu karne 6.
Akifafanua asili ya majini Mwanazuoni mkubwa wa kiislamu aitwaye Abdalllah Saleh Farsy aliye kuwa Kadhi Mkuu Zanzibar, kisha akawa Kadhi Mkuu Kenya katika kitabu alichoandika kiitwacho “ Maisha ya Nabii Mohammad” ule Uk. 31 anasema “ Katika safari yake ya kurejea Taif ndipo walipomjia majini wakasilimu kama inavyoonesha haya katika Suratul Jinn. Majini ni viumbe vyepesi vinavyokaa angani. havina viwiliwili kwa hiyo haviwezi kuonekana na wanadamu ila vinapojibadili kwa umbo lenye kiwiliwili. Na vina uwezo huo wa kujibadili kwa sura ya kuweza kuonekana. WAO NA MASHETANI WANA ASILI MOJA. Kwa hiyo asili ya majini ni shetani.
Suala linalohusu malaika linawasumbua sana waislam hata hawana uhakika wake.
Tumesoma ndani ya Biblia kuwa kuna kundi la malaika waliokosa ambao ndiyo wanaoitwa majini lakini tusomapo Quran inatoa maelezo tofauti.
Quran suratul As- Sajdah, (kusujudu) , 32:13 “ Na tungelitaka tungempa kila mtu uwongofu wake (kwa lazima kama tulivyowapa malaika lakini binadamu amepewa huria ya kufanya alitakalo- lililo jema na baya).
Katika ulimwengu wa Kiislamu Malaika wote ni8 wema na wanamwabudu mungu.
Hapa ndiyo tatizo linapoanzia. Quran iliyokuja baadaye inasema malaika wote ni wema wakati biblia kitalu kilichoitangulia Quran kinasema kuna malaika walioasi na wakafukuzwa katika utukufu wa Mungu.
Katika Quran Suratul, al- Kahf, (Pango) 18:50 “ Na (Kumbukeni) tulipowaambia Malaika, Msujudieni Adamu. Basi wakamsujudia isipokuwa Ibilisi yeye alikuwa miongoni mwa majini na akavunja amri ya mola wake……..”
Katika aya hiyo tunaona ibilisi akilaumiwa kwa kutomsujudia Adamu ingawa amri ya kusujudu walipewa malaika kumbe kwa mujibu wa Quran Ibilisi alikuwa miongoni mwao hao malaika yaani na yeye akiwa malaika.
Kwa sababu Quran haina habari kuhusu malaika walioasi yaani majini ndiyo maana wanapata tabu kuhusu jambo hilo. Na ndiyo maana pamoja na kujua kuwa hayo majini ni mashetani, Muilsamu amehiari kushirikiana nayo kwa kuswali nayo msikitini. Na hata mwislamu huyu anapomaliza kusali husalimia kulia na kushoto akiwasalimia watu malaika na majini (mashetani) waliokuja kushiriki naye katika Ibada yake, soma katika (Irshadul Muslimiin, Sheikh Said Musa, Uk. 38).
Katika Tafsiri ya Quran ya Iman Jalalaini Uk. 6:151 anasema kuhusu majini “ Hao ni watoto wa Ibilisi”
Hii ndiyo sababu hata wanawake wa Kiislamu wakiwa katika kipindi cha hedhi hawaendi msikitini kwa sababu kuna majini na chakula cha majini ni damu. Tafakari kwa hiyo sifa ya hayo majini au mashetani kwa ujumla ni kuwa “ hujaribu kwa bidii sana kuwa karibu na waamini wale wanaosali, kufunga na kusoma Qurani “ (Asili ya majini, Dk. Ahmed H. Sakr Uk. 28) ndiyo maana baadhi ya waislam wao binafsi wasingependa kuwa waislamu lakini majini huwashurutisha kwenda kuswali.
Kwa sababu wao waislamu hawajui kupambanua kati ya majini ambayo ni roho chafu na wale malaika watakatifu wa Mungu Jehova, ndiyo maana hata akiwa katika sala yake hana uhakika kwa sababu huyo jinni (shetani) amemteka na anamfanyia atakavyo na yeye ni mtumwa wa huyo jinni (shetani)
Katika kitabu kiitwacho Mkweli Mwaminifu cha Sheikh Said Moosa Mohamed Al- Kindy wa Muscut Oman, juzuu 1-2 Uk 42 Hadithi Na. 74.
“ Anamwijia mmoja wenu shetani (Jini) katika sala basi anapuliza (anampuliza) katika matako yake, basi (yule mtu) inamuijia fikra ya kuwa umemtoka upepo (kafusa) naye haukumtoka, basi akiona namna hiyo asiondoke (kwenye sala}) mpaka asikie sauti ( ya kutoka upepo) au anuse harufu ( ya huo upepo uliyomtoka, ndio aondoke).

Katika kitabu kiitwacho Asili ya Majini, cha Sheikh Dr Ahmad H. Sakr Uk. 116 anasema “ Hadithi ya Mtume inathibitisha jambo hili kuwa majini (mashetani) na watu wanaweza kuoana aliposema kwamba iwapo mtu ataingia katika uhusiano wa kindoa na mkewe anatakiwa ataje jina la Mwenyezi Mungu ajilinde kwa Mwenyezi Mungu dhidi ya shetani aliyefukuzwa mbali na rehema. Vinginevyo shetani hujiviringisha katika dhakari (sehemu ya siri za mwanaume) ya mtu huyo na atashirikiana naye katika tendo hilo. Tafakari yetu kuwa hiyo jinni anayeshiriki naye tendo la ndoa pamoja naye kwa mkewe ametumwa na nani?

soma vizuri hayo uliyoandika ndipo utakapoona uijui elimu ya waislamu juu ya majini usitake kueleza kitu ambacho huna elimu nacho, waachie wenyewe waislamu wajieleze na nawe jielezee kwa upande wako ili sote tupate faida kwa swali hili zuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom