Mama Amon
JF-Expert Member
- Mar 30, 2018
- 2,021
- 2,478
Picha ya antena za Vodacom, Tigo, Airtel na TTCL zikiwa zimesimikwa kwenye mnara wa Helios baada ya makampuni haya kusaini mkataba wa upangishaji na Helios
I. Utangulizi
Makubaliano ya Kiserikali kati ya Tanzania na Dubai kuhusu uwekezaji kwenye bandari za Tanzania yanaongozwa na Sheria za Kimataifa, Katiba ya Taifa la Tanzania, Sheria za Kitaifa zilizotungwa na Bunge la Tanzania, na mikataba mbalimbali inayoongozwa na sheria hizi.
Mikataba muhimu ni pamoja na mkataba wa IGA, mkataba wa HGA, mikataba ya wakandarasi, mikataba ya mikopo ya mabenki, na kadhalika, kama mchoro ufuatao unavyoonyesha:
Mchoro: Uhusiano kati ya Tanzania, Dubai, Kampuni zitakazotekeza miradi, na mikataba husika
Katika mazingira haya, kuna mtu, Lord Denning, ameuliza swali lifuatalo: Je, kuna mkataba wa IGA ambao uliwahi kusainiwa kati ya pande bili wnye kutaja gharama halisi za miradi kama vile bei ya huduma na kodi ya pango?
Jawabu kwa swali hili ni "ndiyo," na ufafanuzi ufuatao ni kwa ajili ya kuthibitisha hilo.
II. IGA na HGA ni mikataba mtambuka (framework contracts)
Mikataba ya IGA na HGA ni mikataba mtambuka, yaani "framework contracts." Kimsingi, mkataba mtambuka unaweza kuwa na sura mbili.
Kwanza, mkataba mtambuka unaweza kuwa mtambuka kwa sababu unahusu mradi unaotambuka nchi nyingi katika utekelezwaji wake na utekelezwaji wake unahitaji maamuzi ya kiserikali na kibunge kwa kufanya mabadiliko ya sheria kadhaa katika nchi zote husika, ambapo wigo wa mradi unafahamika, kiasi kwamba ikishasainiwa HGA hakuna haja ya mikataba mingine.
Mfano mzuri ni ule mradi wa bomba la mafuta linalounganisha Tanzania na Uganda, yaani mradi wa EACOP.
Pili, mkataba mtambuka unaweza kuwa mtambuka kwa sababu unahusu mradi unaotambuka nchi nyingi katika utekelezwaji wake na utekelezwaji wake unahitaji maamuzi ya kiserikali na kibunge kwa kufanya mabadiliko ya sheria kadhaa katika nchi zote husika, ambapo wigo wa mradi haufahamiki kikamilifu, kiasi kwamba, kushasainiwa kwa HGA hakuondoi haja ya mikataba mingine. Mchoro ufuatao unatoa picha kubwa kuhusu aina hii ya mikataba mtambuka:
Na tatu, mkataba mtambuka unaweza kuwa mtambuka kwa sababu unatambuka miradi tofauti inayotekelezwa ndani ya nchi ile ile moja, lakini miradi hiyo inatekelezwa kwa nyakati tofauti, katika maeneo tofauti na watekelezaji tofauti, lakini pasipo ulazimma wa kubadilisha sheria za nchi husika, kiasi kwamba kusainiwa kwa "Framework Contract" pamoja na "Project Contracts" kunaondoa mahitaji ya mikataba mingine, na hivyo kuondoa sababu ya uwepo wa IGA na HGA. Mchoro ufuatao unafafanua zaidi.
Kwa kifupi, tunaweza kusanifu hoja ifuatayo juu ya uhusiano uliopo kati ya "mkataba mtambuka," unaoitwa IGA" na "mkataba wa HGA"
Mosi, mkataba mtambuka (framework contract) ni mkabata wa jumla kati ya pande mbili, mfano, kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya Uganda; kati ya serikali ya Tanzania na taasisi ya kimataifa isiyo nchi kama vile Benki ya Dunia; au kati ya kampuni ya usafirishaji na kampuni ya mafuta.
Pili, mkataba mtambuka (framework contract) kati ya serikali na serikali, unaitwa "Intergovernmental agreement (IGA)" au "Heads of States Agreement (HSA)" au "Bilateral International Treaty (BIT)."
Tatu, na kwa hiyo, kimuundo, IGA, HGA na BIT zinafanana kwa sababu zote zinao muundo wa mkataba mtambuka (framework contract).
Nne, kuna mkataba mtambuka (framework contract) kati ya kapuni ya Vodacom inayotoa huduma za simu and kampuni ya HELIOS inayojenga na kukodisha minara ya masafa,
Na tano, tukipata mkataba mtambuka (framework contract) kati ya Vodacom na Helios, tunakuwa tumepata mfano hai wenye kuonyesha muundo wa mkataba wa IGA, unavyopaswa kuwa.
III. Mkataba kati ya Helios na Vodaco ni mifano hai wa mikataba mtambuka isiyohitaji IGA wala HGA
Hapa nchini, kuna mifano mingi ya "mikataba mtambuka" ya aina hii ya pili. Mikataba hii inaonyesha gharama halisi za miradi husika, hata kabla mikataba ya miradi husika kusainiwa. Mifano mizuri hapa Tanzania ni kama ifuatavyo:
- Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na kampuni ya Vodacom,
- Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya Tigo,
- Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya Airtel,
- Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya TTCL.
- Kuna "mkataba mtambuka" (framework contract) kati ya kampuni ya HELIOS na na kampuni ya Halotel.
Lakini makapuni haya hayana mitaji ya kutosha kwa ajili ya kujenga minara nchi nzima.
MInara ya kurusha mawimbi ya sauti (signal relay stations) huhitajika kwa ajili ya kusimika antena za kupokea na kurusha upya mawimbi ya sauti kutoka kwa mpigaji hadi kwa mpokeaji.
Lakini, Helios ni kampuni ya Uingereza yenye mtaji wa kujenga na kukodisha minara kwa makapuni mbalimbali.
Helios wanamiliki minara zaidi ya 1000, katika Afrika mashariki na Kati. Hivyo, haya makampuni yetu yanakodisha nafasi kwenye minara ya Helios ili yaweze kuweka antena zao kwenye minara hiyo, na kuwahudumia wateja wake.
Kampuni inapoanza kukodisha nafasi kwenye minara ya Helios inakuwa haijui kwa uhakika inahitaji minara mingapi na iliyo wapi.
Kwa hiyo, busara ni kukodisha minara ya Helios kwa awamu, kulingana na wateja wanavyopatikana na wanakopatikana.
Hivyo, mchakato wa kuingia mkataba kati ya kampuni ya Helios na kampuni kama vile Vodacom inachukua hatua nne. Yaani:
- Kusainiwa kwa mkataba mtambuka mmoja (framework contract) wenye kutaja taarifa chache za jumla, zitakazoweka singi wa mikataba ya saiti moja moja katika siku za usoni.
- Kampuni yenye mahitaji kuiandikia Helios ikiomba huduma ya kukodishwa mnara kwenye site mpya.
- Kusainiwa kwa mikataba ya saiti maalum (site cocntract), na hivyo kuongeza idadi ya minara ya Helios iliyokodishwa kwa kampuni pale tu mahitaji ya kampuni yanapoongezeka kwa sababu wateja wapya wamepatikana.
- Helios kuandaa mnara kwenye saiti kulingana na mahitaji, na hatimaye kampuni kukabidhiwa saiti hiyo.
KImsingi, kila "mkataba mtambuka" kati ya Helio na kampuni yoyote hapo juu, una sehemu zifuatazo:
- Maelezo ya msingi kuhusu makubaliano: Sehemu hii inaongelea wahusika katika mkataba, malengo ya wahusika, na mwongozo wa jumla kuhusu mahusiano ya siku za usoni.
- Kiammbatanisho cha kwanza ("schedule 1"): Kinaongelea "configuration", yaani aina ya huduma ambazo Helios anapaswa kuhakikisha zinapatikana kwenye kila saiti. Mfano:-- kuna sharti kwamba, kama mnara unaotaka kukidishwa uko sehemu ambako hakuna umeme wa gridi ya Taifa, basi Helios aweke jenereta; -- kuna sharti kwamba, kampuni itapewa ukubwa wa eneo la meta moja ya mmraba kwa ajili ya kusimika antena yake; -- kuna kifungu kinataja ukomo wa muda wa mkataba tambuka; -- kuna kifungu kinataja ukomo wa muda wa mkataba mahsusi utakaosainiwa katika siku za usoni; -- na kadhalika.
- Kiambatanisho cha pili ("schedule 2"): Kinaongelea kodi ya pango inayotajwa kwa kutumia kizio cha "TZS/site/month". Gharama hizi ziko katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni bei za kukodisha mnara ulioko kwenye maeneo yenye umeme wa gridi ya Taifa (bei nafuu). Na Kundi la pili ni bei za kukodisha mnara ulioko kwenye maeneo yasiyo na umeme wa gridi ya Taifa (bei kubwa).
- Kiambatanisho cha tatu ("schedule 3"): Kinaongelea muundo na maudhui ya mkataba utakaosainiwa kwa ajili ya kukidisha saiti moja tu, yaani kukodisha mnara mmoja pekee. Kwa hiyo, kama kampuni ya Vodacom itakodisha minara 100, kutasainiwa mikataba mahsusi 100.
- Kiambatanisho cha nne ("schedule 4"): Kinaongelea utaratibu wa kuongeza mnara mpya, yaani jinsi kampuni yenye mahitaji itakavyowasiliana na Helios na kuonyesha huduma ya mnara mpya ianze kutolewa lini.
- Kiambatanisho cha tano ("schedule 5"): Kinaongelea utaratibu wa kukabidhiana huduma kwenye saiti.
- Kiambatanisho cha sita ("schedule 6"): Kinaongelea protokali ya kutumia saiti, maana kwenye mnara mmoja kuna wakodishaji wengi. Yaani, unakuta kuna antena za Tigo, Airtel, Vodacom, na kadhalika.
Baada ya kusema hayo hapo juu sasa nafanya majumuisho muhimu kwa kuzingatia hoja yafuatayo:
Njia mojawapo ya kusanifu hoja, ni kuanzia kwenye ufanano wa vitu viwili (argument by analogy). Njia hii huzalisha hoja yenye muundo wa kimantiki ufuatao:
- Kitu X na kitu Y vinafanana kwa sababu kila kimoja kinazo sifa kadhaa zinazounda seti Z.
- Kitu X pia kinaonekana kuwa na sifa nyingine P.
- Kwa hiyo, kitu Y pia kinapaswa kuwa na sifa hiyo P.
Mosi, Kampuni ya HELIOS kutoka Uingereza na kammpuni ya DPW kutoka Dubai zinafanana katika sifa zifuatazo:
- zote ni Kampuni za wawekezaji wa Kigeni;
- zote zinaotaka mazingira yenye utulivu wa kisheria na kisiasa kwa ajili ya uwekezaji ili wafanikiwe kuwekeza, kuvuna na kuhamisha faida kutoka nchini Tanzania;
- zote zinahitaji kimilikishwa ardhi kwa ajili ya kuitumia kama saiti ya miradi yake;
- na zote zinajenga saiti zinazoitwa minara, kuziboresha na kisha kukodisha nafasi yenye eneo maaluma kwa muda fulani kwa makampuni kadhaa. Kwa upande mmoja, HELIOS wanasimika minara na kuikodisha kwa makampuni yanayosafirisha mawimbi ya simu hapa Tanzania. Kwa upande mwingine, DPW wanajenga saiti zinazoitwa bandari, kuziboresha na kuvikodisha kwa watu wanaosafirisha mizigo kwa kutumia meli.
Tatu, kwa hiyo, Kampuni ya DPW kutoka Dubai inapaswa kuwa na uwezo wa kuendesha biashara zake kwa kutummia "mkabata mtambuka" (framework agreement) pamoja na "mikataba ya miradi mahsusi" (project site agreements), pasipo kuhitaji mkataba wa IGA kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya Dubai wala mkataba wa HGA kati ya DPW na serikali ya Tanzania.
Nne, kuipa kampuni ya DPW unafuu unaotokana na mikataba ya IGA na HGA na kuzinyima unafuu huo kampuni baki za wawekezaji wa kigeni ni ubaguzi usio na sababu za msingi dhidi ya baadhi ya wawekezaji wa kigeni.
Na tano, kwa hiyo, kwa ajili ya kutenda haki sawa kwa wawekezaji wote wa kigeni, Tanzania inapaswa kuepuka mikataba ya IGA na HGA.
V. Hitimisho na mapendekezo
Mkataba mtambuka (framework contract) kati ya Helios na makampuni ya simu ni kama mkataba kati ya nchi na nchi (IGA). Na mkataba wa saiti kati ya Helios na makampuni ya simu ni kama mkataba wa ngazi ya miradi kati ya nchi mwenyeji na mwekezaji wa kigeni (HGA).
Kwa hiyo, inawezekana, na ni lazima, kutaja gharama za mradi kama vvile kodi ya pango na pia ukomo wa muda kwenye IGA.
Na kama ambavyo Helios na makampuni ya simu yanasaini "Framework Agreements" na baadaye "Project Site Agreements," vivyo hivyo DPW na TPA wanaweza na wanapaswa kusaini nyaraka za aina hii.
Hakuhitajiki IGA wala HGA kamwe ili kuiwezesha DPW au kampuni yoyote iwayo kuwekeza katika bandari za Tanzania!
Mama Amon Desk
"Summbawanga Town"
Sumbawanga.
30 Julai 2023.