Jaribio la kugomea Sensa: Mwitikio wa Serikali

Serikali yawaangukia Waislamu
• Walimu 108 waenguliwa kwenye semina ya Sensa Dar

na Waandishi wetu
Tanzania Daima
WAKATI shinikizo la baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu kutaka kususia sensa likishika kasi, serikali imewaomba radhi Waislamu kutokana na matangazo yaliyorushwa na Kituo cha Televisheni ya Taifa (TBC), yaliyoonesha kwamba idadi ya Wakristo nchini ni kubwa kuliko Waislamu.

TBC ilirusha matangazo hayo siku ya Sikukuu ya Muungano (Aprili 26) mwaka huu na kuonesha idadi ya Wakristo ni asilimia 52, Waislamu asilimia 32 na madhehebu mengine asilimia 14.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa TBC, Clement Mshana alisema kuwa matangazo hayo yalitolewa kwenye mtandao wa Wikipedia na kurushwa hewani kimakosa.

Alisema baada ya kurushwa kwa matangazo hayo kimakosa, TBC walipokea barua nyingi kutoka Chama cha Wanataaluma wa Kiislamu Tanzania (Tanzania Muslim Professional Association) zikieleza kukerwa na taarifa hiyo.

Mshana Alisema katika barua hiyo, chama hicho kilitaka ufafanuzi jinsi takwimu hizo zilivyopatikana na TBC iwaombe radhi Watanzania.
Alisema Mei 15, TBC ilimwandikia barua Katibu Mkuu wa chama hicho cha Waislamu, Pazi Mwinyimvua na kuomba radhi kwa kasoro iliyotokea na kueleza kwamba shirika lake limemwonya mfanyakazi aliyerusha hewani takwimu hizo kimakosa.

“Nichukue fursa hii tena kuwaomba radhi ndugu zetu wa dini ya Kiislamu kutokana na maumivu waliyopata kutokana na takwimu hizo. Na kwa kuwa huu ni mwezi mtukufu wa Ramadhani na moja ya mahitaji wakati wa mfungo ni kusameheana, naomba waumini wote wa dini ya Kiislamu wapokee kwa moyo wa upendo ombi hili la kuwataka radhi,” alisema Mshana.

Aliongeza kwamba kwa kuwa suala hili limehusishwa na sensa ya watu na makazi, anawaomba waumini wa dini ya Kiislamu kusamehe kilichotokea na washiriki katika sensa ya watu na makazi itakayofanyika Agosti 26, mwaka huu.

Wakati serikali ikiendelea kuhimiza wananchi kushiriki sensa, kuna kundi la Waislamu limejitokeza kupinga tukio hilo.
Kundi hilo limekuwa likipita sehemu mbalimbali nchini kueneza sumu ya kuwataka Waislamu wasishiriki sensa kwa madai kuwa serikali imelenga kuwabagua kwa kutangaza takwimu zinazoonesha Wakristo ni wengi zaidi ya Waislamu.

Mmoja wa viongozi wa kundi hilo, Issa Sadick, hivi karibuni alizitaja baadhi ya sababu za kukataa kuhesabiwa kuwa ni serikali kuendelea kuwabagua Waislamu katika miradi mbalimbali ya maendeleo.

Hata hivyo Sheikh Mkuu Mufti Shabaan bin Simba hivi karibuni aliwataka Waislamu kushiriki sensa na walipuuze kundi la masheikh linalozunguka nchini kutaka wasusie.

Wakati huo huo, walimu 108 walioteuliwa kuhudhuria semina ya makarani wa sensa, wameenguliwa na nafasi zao kuzibwa na watu wengine.

Utafiti wa gazeti hili umebaini kuwa, walioenguliwa ni walimu wa Kituo cha Mafunzo cha Sekondari Tambaza jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa habari hizo, walimu hao wameenguliwa kutokana na kushindwa kufanya vizuri kwenye mtihani wa majaribio.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, baadhi ya walimu hao walisema wanapinga kuondolewa kwao kwani walikwishakubaliana katika mkataba wa malipo, na tayari walishaanza mafunzo kwa ajili ya kazi ya ukarani wa sensa.

Walisema kuwa wahusika wamekuwa wakiwaleta ndugu zao na kuwapunguza walimu ambao tayari walishaanza mafunzo kwa siku nne sasa.
Walimu hao walisema wanaitaka serikali iwalipe fedha zao za siku nne ambazo tangu waanze mafunzo hayo hawajalipwa.

Taarifa hii imeandaliwa na Zawadi Chogogwe, Agness Newa na Stella Mushi.


Mimi binafsi sioni SABABU ya kuwaomba radhi hawa ndugu zetu Waislam. Wanachotaka wao wambiwe Tanzania kuna Waislam wengi kuliko Wakristo na sijui itawasaidia nini katika Uislam wao. Kitendo tu cha kusema Wakristo ni 52% na Waislam ni 32% na DINI zingine ni 14% kwao inawasumbua sana. Kwamtazamo wao kipengere cha DINI kikiwekwa kwenye dodosa la sensa; haitamaliza matatizo yao. Lazima watakuja na lingine.

Kuondoa ubishi wakijinga basi tuseme hivi NCHI YA TANZANIA INA WAISLAM 100% WAKRISTO 0% na DINI ni 0%. Hapo sasa mmeridhika? Au bado mnalialia tena? Acheni jamani wakubwa nyinyi.
 

Mimi binafsi sioni SABABU ya kuwaomba radhi hawa ndugu zetu Waislam. Wanachotaka wao wambiwe Tanzania kuna Waislam wengi kuliko Wakristo na sijui itawasaidia nini katika Uislam wao. Kitendo tu cha kusema Wakristo ni 52% na Waislam ni 32% na DINI zingine ni 14% kwao inawasumbua sana. Kwamtazamo wao kipengere cha DINI kikiwekwa kwenye dodosa la sensa; haitamaliza matatizo yao. Lazima watakuja na lingine.

Kuondoa ubishi wakijinga basi tuseme hivi NCHI YA TANZANIA INA WAISLAM 100% WAKRISTO 0% na DINI ni 0%. Hapo sasa mmeridhika? Au bado mnalialia tena? Acheni jamani wakubwa nyinyi.

Mzee MsemKweli, Una onekana upo misinformed. Kuna ubaya gani kujua idadi ya Watanzania kwa kabila zao, dini zao, asili zao au tofauti zao. MIMI NADHANI JAMII YOYOTE ILIO MAKINI HAIWEZI KUEPUKA HILI. SASA KAMA NIA NI NZURI, KWA NINI KUFICHA UKWELI? KWA NINI KUTOA TAKWIMU ZA UONGO?. ILI AFAIDIKE NANI?. JE NI KOSA KWA MUJIBU WA SHERIA ZA KIMATAIFA KUJUA IDADI YA WATU KATIKA NCHI ZAO KWA MUJIBU WA DINI ZAO?. VIPI KIPENGELE HIKI KIONDELEWE KINYEMELA HALAFU ZICHOMEKWE TWAKIMU ZA WIKIPEDIA?. SASA KAKA HATA HILI LINAHITAJI PHD KULIANALYSE?

SASA KWA NINI WAWEKE KIPENGELE CHA KUJUA IDADI YA MAKANISA, MISIKITI NA NYUMBA NYINGINE ZA IBADA KATIKA SENSA NA IWE HARAMU KUJUA IDADI YA WANAO TUMIA MAJUMBA HAYO? WEWE UNAJUA LENGO LAO NINI?.


AU NDIO WALE WALE WA 1+1+1 = 1 ??
 
  • Thanks
Reactions: BAK
jaman jaman jaman!!!!! tuwasikilize na tuingize icho kipengele,kwani hata cc kaskazini tuko wengi kuliko wao na hakuna vita!!
 
Sensa ni haki kwa kila Mtanzania.
Haitapendeza ikidoda.

ipendeze kwani imekuwa keki hiyo,wacha idode wenyewe wametaka hivo toka mwanzo hao walioteuliwa kuwa makarani wengine hawajui kusoma wala kuandika unategemea atajaza nini kwenye hayo madodoso?lakini ndicho serikali wametaka!walifikiri wanawakomoa walimu kwa kuwaengua kwenye hilo zoezi lakini nchi ndo inapata hasara,sensa ni jambo zuri likiendeshwa ka utaratibu unaoleweka lakini hili la sasa JK na wenzie wamechemsha,mkapa alifanya mpaka sensa ya ng;ombe na wala hakukuwa na shida. wao wanjua ni mwaka wa sensa wanaanza na kupandikiza udini.Wamewaprovoke waislamu bure kabisa na makusudi kabisa ili wafanye justification kuwa kuna udini na sensa imekwama kutokana na waislamu kugoma kuhesabiwa,HAPANA SENSA WAMEIVURUGA WENYEWE NA HAKIKA HAKUNA TAKWIMU YOYOTE RELIABLE ITAKAYOPATIKANA.tumeshindwa katika mengi jamani hata la kujua tuko wangapi?lakini sishangai,naibu spika mwenyewe aliwahi kuulizwa na star tv ana watoto wangapi akasema hajui idadi so nafikiri idadi yetu sio muhimu sana jamani TWENDE TU!
 
Gharama ya sensa Shilingi 140 Billioni matokeo ya sensa SIFURI, ZERO, NILCH...Nani wa kulaumiwa? Serikali DHAIFU.

ipendeze kwani imekuwa keki hiyo,wacha idode wenyewe wametaka hivo toka mwanzo hao walioteuliwa kuwa makarani wengine hawajui kusoma wala kuandika unategemea atajaza nini kwenye hayo amdodoso?lakini ndicho serikali wametaka!walifikiri wanawakomoa walimu kwa kuwaengua kwenye hilo zoezi lakini nchi ndo inapata hasara,sensa ni jambo zuri likiendeshawa ka utaratibu un aoleweka lakini hili la sasa JK na wenzie wamechemsha,mkapa alifanya mpka sensa ya ng;ombe na wala hakukuwa na shida wao wanjua ni mwaka wa sensa wanaanza na kupandikiza udini.Wamewaprovoke waislamu bure kabisa na makusudi kabisa ili wafanye justification kuwa kuna udini na sensa imekwama kutokana na waislamu kugoma kuhesabiwa,HAPANA SENSA WAMEIVURUGA WENYEWE NA HAKIKA HAKUNA TAKWIMU YOYOTE RELIABLE ITAKAYOPATIKANA.tumeshindwa katika mengi jamani hata la kujua tuko wangapi?lakini sishangai,naibu spika mwenyewe aliwahi kuulizwa na star tv ana watoto wangapia akasema hajui idadi so nafikiri idadi yetu sio muhimu sana jamani TWENDE TU!
 
Sensa itadoda, umati wa waislamu uliokuwepo mwembe yanga na vipeperushi na Elimu iliyotolewa achilia mbali harakati zilizoripotiwa kutoka mikoa yote Tanzania bara , na visiwani ndio kabisaaaaaaaaaaaaaaaaa inatosha zoezi kudoda, Watawahesabu bakwata na Wakristo wao, moja ya mbinu za kutaka move ya kususia sensa ifeli inafanywa humu JF ya kufuta Nyuzi zote zinazohusu mambo ya sensa mfano leo niliporusha uzi huu uliondolewa:-

How GoT underdeveloped Islam dominated places/regions through census data
Kwa muda sasa nilikuwa najua kuwa mikoa mingi ambayo waislamu ni wengi sana ukilinganisha na dini nyingine ilirudishwa nyuma kimaendeleo kwa makusudi na serikali kupitia kinachojulikana kwa sasa Mfumo Kristo(MK), Nilichokuwa sijui ni jinsi gani takwimu za sensa zilivyotumika kuchangia kudumaza maendeleo ya Mikoa hii ambayo ni Tanga,Pwani Kigoma Lindi Mtwara n.k, ni hadi jana nilipohudhuria baraza la Idd Mwembe Yanga nikakutana na kijitabu Chenye Title SABABU ZA WAISLAMU KUTOSHIRIKI SENSA YA MWAKA HUU (2012) nanukuu maneno yaliyoandikwa ukurasa wa 25, subtitle Kwa nini waislamu wanadai tume huru ya Sensa? Kama ifuatavyo:’Tume ya sensa ndio chombo rasmi kinachohusika na uratibu wa zoezi zima la sense mwaka huu. Sisi waiskamu hatuna imani hata kidogo na Idara ya Taifa ya takwimu na hiyo tume ya sens akwani kuna ushahidi wa kutosha hivyo mara zote hutoa takwimu za uongo kwa madhumuni ya kuukandamiza uislamu na kuunufaisha ukriso ili kuhalalisha dhulma kwa waislamu. Watumishi wengi sana wa hivyo vyombo ni wakristo na waislkamu ni wachache sana tena wenye nyadhifa za uongozi na kutoa maamuzi ni wakristo..Hatuna imani na idara ya taifa ya takwimu na tume yake kwani hushiriki katika propaganda ya kwamba katika nchi hii waislamu ni wachache ikilinganishwa na wakristo kwa kutoa matokeo Sensa katika maeneo na mikoa yenye waislamu wengi kwamba idadi ya watu huko ni ndogo, na ktika mikoa na maeneo yenye wakristo wengi idadi ya watu huko ni kubwa sana. Mfano katika sense iliyofanyika mwaka 1988 Idadi ya wakazi wa mkoa wa Tanga ilikuwa ni 1,500,000,na ilipofanika sensa ya mwaka 2002 idadi ya watu mkoani humo ilibaki kuwa 1,500,000.Maana yake ni kwamba katika kipindi cha miaka 12 (1988 hadi 2002) idadi ya watu mkoa wa Tanga haijaongezeka hata mtu 1!
Sababu ya kufanya hivyo ni kwamba katika mkoa wa Tanga kuna idadi kubwa sana ya waislamu ukilinganisha na Wakristo,hivyo kutoa Takwimu zinazoonesha kwamba Mkoa huo una idadi kubwa ya watu mantiki yake mkoa huo una idadi kubwa ya waislamu kitu ambachoidara ya takwimu na sensa hawawezi kufanya kwa sababu nia yao siku zote nimkuonesha idadi ya waislamu katika nchi hii ni wachache.
Athari ya takwimu izo ni kwamba serikali inapopanga mipango ya maendeleo na huduma za kijamii katika mkoa huo huzingatia takwimu hizo hivyo huukosesha mkoa huo miradi na fursa mbalimbali za kimaendeleo na huduma za jamii. Kama idadi ya watu ni ileile haijaongezeka kuna haja gani ya kupanua na kuongeza huduma za jamii kama vile Shule Hospitali Maji safi na Salam barabara n.k.,Maana yake mkoa wa Tanga baada ya matokeo ya sense ya mwaka 2002 haikupewa kipaumbele chochote katika miradi ya maendeleo na huduma za jamii na serikali kwani vilivyokuwepo mwaka 1988 vinatosheleza maana idadi ya watu ni ileile!
Mkoa wa Tanga tumetoa kama mfano lakini huo ndio mpango mzima na hali halisi ilivyo katika mikoa yote ya waislamu. Ukipitia takwimu zote za sensa katika nchi hii, mikoa yenye idadi ndogo ya watu ni mikoa inayokaliwa na waislamu wengi na mikoa yenye idadi kubwa ya watu ni mikoa iliyokaliwa na wakristo wengi!
Maana yake ni kuwa mikoa yenye waislamu wengi itapewa idadi ndogo ya miradi ya maendeleo ukilinganisa na mikoa yenye idadi kubwa ya wakristo ambayo itapewa miradi mingi ya maendeleo…..
Idara ya taifa ya Takwimu na tume ya sensa, sisi waislamu hatuna imani nazo kwani zote kwa pamoja hutoa takwimu za uongo zikiwepo za idadi ya watu kama tulivyoeleza hivyo bila tume huru ya sensa yenye uwiano sawa wa kidini baina ya waislamu na wakristo, sisi waislamu hatushiriki sensa ya mwaka huu na zingine zote zijazo. Mwisho wa kunukuu.
 
kabla ya hiyo nilituma hii ikaondolewa:

Ndugu wanajamvi, waislamu hawahesabiwi kwa sensa isiyo na kipengele cha dini, tunajua pia kuwa BAKWATA watahesabiwa. Ni wazi kuwa serikali inaweza kufanya chochote lakini haiwezi kuwalazimisha watu kufanya chochote, haikuwa hivyo tokea mamlaka zilipoanza kuwepo duniani. KWA HILI LA SENSA YA MWAKA HUU TUNASEMA, WAISLAMU HAWATAHESABIWA BAKWATA, WAKRISTO NA WAPAGANI WAMEKUBALI KUHESABIWA

  1. Kwa nini kipengele cha sensa kiliondolewa?
Inasadikika kuwa sensa ya mwisho kufanyika wakati wa ukoloni Tanzania ilikuwa na Waislamu asilimia 60, Tukisema kuwa serikali ilikiondoa kipengele hiki kwa sababu maalumu ikiwemo kuwa na nafasi ya kuendeleza na kusadikisha takwimu za uongo ili kushamirisha Mfumo Kristo (MK) Tanzania tunakosea?

  1. Kwa nini taasisi mbalimbali za serikali na binafsi zimekua zikitoa takwimu za watu na dini zao?
Mfano 0fisi ya waziri mkuu inadai wakristo ni 45%-waislamu 35%. TBC1, imetangaza wakristo ni 52%-waislamu 32%.Bodi ya watalii -Christianity and Islam are the predominant religions of Tanzania. About 40-45% of the population practice Christianity, about 35-40% practice Islam.,Tovuti kikatoliki (RCNet) waislamu 34%- na wakristo ni 44%
Na hapa kuna hoja mbili,
a) kwa nini takwimu zinatofautiana? na b)kwa nini pamoja na kutofautiana zote zinaonesha wakristo ni wengi kuliko waislamu?
Kwa kawaida jambo la uongo lazima hukwama, takwimu zinatofautiana kwa sababu ni za uongo, Zote zinaonesha wakristo ni wengi kwa sababu za kukidhi matakwa ya MK.
Mkurugenzi wa TBC alipoulizwa kuhusu takwimu katoa wapi aliishia kuomba radhi, kakosea, swali ni je kakosea nini? Amekuwa akikosea mambo mangapi ya kitaifa kwa ujumla wake kama lilivyo hili? Huu ndio MK
3.Kwa nini kiwepo kipengele cha kuhesabiwa kwa nyumba za ibada?
Waislamu wakisema kuwa kuhesabiwa kwa nyumba za ibada pekee kunaweza kutumiwa na wapotoshoshaji wa Umma kupitia MK, kuwa Wkristo ni wengi kwani siku hizi kuna utitiri wa madhehebu kikristo na makanisa binafsi hata kama yana waumini wachache achilia mbali uyoga wa makanisa yanojiita ya wokovu? Kwa nini nyumba za ibada na sio na wanaoabudu humo?, Serikali inataka kugawa misala misikitini na mabench kanisani?
Waislamu wa leo ni tofauti na wa enzi hizo, wanajua wanachokifanya na hili la sensa ni moja na mengine yatakuja,hatuhitaji kumtafuta kiongozi wala Sheikn Ponda kwa hili, elimu tulishapata , macho yalishafumbuliwa na Tunaelewa athari za mfumo Kristo katika jamii


  1. Tulisadikishwa kuwa waislam hawakusoma, kumbe data zinaonesha NECTA inawapunguza
  2. Tukasadikishwa kwamba hawajengi Mashule na Hospitali ila wanajenga misikiti, kumbe wenzetu wanajenga kupitia fedha wanazopewa na serikali hii hii kupitia MoU
  3. Tukasadikishwa kuwa nchi hii haina dini , kumbe serikali yetu ina mfumo Kristo ambao haukuandikwa popote lakini unafanya kazi zake kwa siri na waziwazi
TUMEKATAA KWENDA KWA MATAKWA YA MK, NARUDIA WAISLAMU HATUHESABIWI.
 
Sensa itadoda, umati wa waislamu uliokuwepo mwembe yanga na vipeperushi na Elimu iliyotolewa achilia mbali harakati zilizoripotiwa kutoka mikoa yote Tanzania bara , na visiwani ndio kabisaaaaaaaaaaaaaaaaa inatosha zoezi kudoda, Watawahesabu bakwata na Wakristo wao, moja ya mbinu za kutaka move ya kususia sensa ifeli inafanywa humu JF ya kufuta Nyuzi zote zinazohusu mambo ya sensa mfano leo niliporusha uzi huu uliondolewa:-

How GoT underdeveloped Islam dominated places/regions through census data
Kwa muda sasa nilikuwa najua kuwa mikoa mingi ambayo waislamu ni wengi sana ukilinganisha na dini nyingine ilirudishwa nyuma kimaendeleo kwa makusudi na serikali kupitia kinachojulikana kwa sasa Mfumo Kristo(MK), Nilichokuwa sijui ni jinsi gani takwimu za sensa zilivyotumika kuchangia kudumaza maendeleo ya Mikoa hii ambayo ni Tanga,Pwani Kigoma Lindi Mtwara n.k, ni hadi jana nilipohudhuria baraza la Idd Mwembe Yanga nikakutana na kijitabu Chenye Title SABABU ZA WAISLAMU KUTOSHIRIKI SENSA YA MWAKA HUU (2012) nanukuu maneno yaliyoandikwa ukurasa wa 25, subtitle Kwa nini waislamu wanadai tume huru ya Sensa? Kama ifuatavyo:’Tume ya sensa ndio chombo rasmi kinachohusika na uratibu wa zoezi zima la sense mwaka huu. Sisi waiskamu hatuna imani hata kidogo na Idara ya Taifa ya takwimu na hiyo tume ya sens akwani kuna ushahidi wa kutosha hivyo mara zote hutoa takwimu za uongo kwa madhumuni ya kuukandamiza uislamu na kuunufaisha ukriso ili kuhalalisha dhulma kwa waislamu. Watumishi wengi sana wa hivyo vyombo ni wakristo na waislkamu ni wachache sana tena wenye nyadhifa za uongozi na kutoa maamuzi ni wakristo..Hatuna imani na idara ya taifa ya takwimu na tume yake kwani hushiriki katika propaganda ya kwamba katika nchi hii waislamu ni wachache ikilinganishwa na wakristo kwa kutoa matokeo Sensa katika maeneo na mikoa yenye waislamu wengi kwamba idadi ya watu huko ni ndogo, na ktika mikoa na maeneo yenye wakristo wengi idadi ya watu huko ni kubwa sana. Mfano katika sense iliyofanyika mwaka 1988 Idadi ya wakazi wa mkoa wa Tanga ilikuwa ni 1,500,000,na ilipofanika sensa ya mwaka 2002 idadi ya watu mkoani humo ilibaki kuwa 1,500,000.Maana yake ni kwamba katika kipindi cha miaka 12 (1988 hadi 2002) idadi ya watu mkoa wa Tanga haijaongezeka hata mtu 1!
Sababu ya kufanya hivyo ni kwamba katika mkoa wa Tanga kuna idadi kubwa sana ya waislamu ukilinganisha na Wakristo,hivyo kutoa Takwimu zinazoonesha kwamba Mkoa huo una idadi kubwa ya watu mantiki yake mkoa huo una idadi kubwa ya waislamu kitu ambachoidara ya takwimu na sensa hawawezi kufanya kwa sababu nia yao siku zote nimkuonesha idadi ya waislamu katika nchi hii ni wachache.
Athari ya takwimu izo ni kwamba serikali inapopanga mipango ya maendeleo na huduma za kijamii katika mkoa huo huzingatia takwimu hizo hivyo huukosesha mkoa huo miradi na fursa mbalimbali za kimaendeleo na huduma za jamii. Kama idadi ya watu ni ileile haijaongezeka kuna haja gani ya kupanua na kuongeza huduma za jamii kama vile Shule Hospitali Maji safi na Salam barabara n.k.,Maana yake mkoa wa Tanga baada ya matokeo ya sense ya mwaka 2002 haikupewa kipaumbele chochote katika miradi ya maendeleo na huduma za jamii na serikali kwani vilivyokuwepo mwaka 1988 vinatosheleza maana idadi ya watu ni ileile!
Mkoa wa Tanga tumetoa kama mfano lakini huo ndio mpango mzima na hali halisi ilivyo katika mikoa yote ya waislamu. Ukipitia takwimu zote za sensa katika nchi hii, mikoa yenye idadi ndogo ya watu ni mikoa inayokaliwa na waislamu wengi na mikoa yenye idadi kubwa ya watu ni mikoa iliyokaliwa na wakristo wengi!
Maana yake ni kuwa mikoa yenye waislamu wengi itapewa idadi ndogo ya miradi ya maendeleo ukilinganisa na mikoa yenye idadi kubwa ya wakristo ambayo itapewa miradi mingi ya maendeleo…..
Idara ya taifa ya Takwimu na tume ya sensa, sisi waislamu hatuna imani nazo kwani zote kwa pamoja hutoa takwimu za uongo zikiwepo za idadi ya watu kama tulivyoeleza hivyo bila tume huru ya sensa yenye uwiano sawa wa kidini baina ya waislamu na wakristo, sisi waislamu hatushiriki sensa ya mwaka huu na zingine zote zijazo. Mwisho wa kunukuu.
 
Kweli nchi imeoza maana kama takwimu zilikosewa takwimu ambazo ziko accurate ni zipi kama zipo? Kama hakuna je Serikali ina mpango gani katika kuhakikisha inapata takwimu ambazo ziko accurate?

Mkuu, unazitaka hizo takwimu za dini za wa-Tz ili zitumike kwa lipi?
Ili serikali iwajengee misikiti na makanisa na kuwatafutia mibuyu ya kuabudia ka wale wasioamini dini za kigeni?

Sijajua kwa nini baadhi ya wa-Tz ni wagumu kuelewa kwa nini serikali haikitaki kipengele cha dini za watu wake katika sensa? Kwa ufupi ni kwamba, hakina umuhimu kwa mipango ya maendeleo ya nchi.

Huyo mkuu wa TBC naye kajichanganya katika kutapatapa kujibu au kujikosha. Hakutakiwa kusema kwamba takwimu zimekosewa kana kwamba anazo takwimu zingine ambazo ni sahihi.

Alitakiwa tu kusema, serikali haina takwimu rasmi za idadi ya watu kwa imani zao, full stop.
 
Sioni mantiki ya kuzuai kipengele cha dini ndani ya Sensa. Ukiangalia takwimu nyingi online zinaonyesha asilimia za dini. Dini haina madhala yeyote na wala haitapunguza au kuvunja kipengele chechoye cha katiba. Ni muhimu sana hasa kwa watalii wanapokuja nchini kuelewa sehemu na uwiano wa dini, hivyo waheshimu law of land. Mfano watalii toka meddle east wakienda sehemu kama Mbeya, watafahamu from online majority ni wakristo, kwa hiyo ni rahisi kujihadhari na Kiti moto. Sama wazungu wakitembelea Mafya.
Kipengele cha dini ni muhimu sana hasa ktk fani ya utalii .

Mkuu, binafsi sioni mantiki ya hoja zako, hususan unapoaonisha utalii na imani za dini za wakaazi wa eneo husika la utalii kwa TZ.

TZ haijagawanywa kikanda, kutegemeana na imani za watu. Hakuna pahala katika TZ ambako wapo aidha waislamu tu au wakristo tu au wanaoabudu dini za kimila tu! Nchi yote imejaa mchanganyiko wa watu wenye imani tofauti tofauti.

Hivyo kusema ukienda eneo fulani ndani ya TZ unatakiwa u-behave hivi au vile, ati kwa sababu tu wakaazi wengi wa eneo hilo ni wa imani fulani ni upuuzi na ujinga, ni namna ya kuanza kubaguana.

Ndicho kitakacholeta ubaguzi kwamba kwa kuwa waislamu ni wengi eneo fulani basi makanisa yasijengwe ili waislamu walio wengi wasibughudhiwe wakati wa ibada zao??!!!

The government of TZ is quite right, no need for the question of religious identification of its citizens in the census questionnaire.
 
kabla ya hiyo nilituma hii ikaondolewa:

Ndugu wanajamvi, waislamu hawahesabiwi kwa sensa isiyo na kipengele cha dini, tunajua pia kuwa BAKWATA watahesabiwa. Ni wazi kuwa serikali inaweza kufanya chochote lakini haiwezi kuwalazimisha watu kufanya chochote, haikuwa hivyo tokea mamlaka zilipoanza kuwepo duniani. KWA HILI LA SENSA YA MWAKA HUU TUNASEMA, WAISLAMU HAWATAHESABIWA BAKWATA, WAKRISTO NA WAPAGANI WAMEKUBALI KUHESABIWA

  1. Kwa nini kipengele cha sensa kiliondolewa?
Inasadikika kuwa sensa ya mwisho kufanyika wakati wa ukoloni Tanzania ilikuwa na Waislamu asilimia 60, Tukisema kuwa serikali ilikiondoa kipengele hiki kwa sababu maalumu ikiwemo kuwa na nafasi ya kuendeleza na kusadikisha takwimu za uongo ili kushamirisha Mfumo Kristo (MK) Tanzania tunakosea?

  1. Kwa nini taasisi mbalimbali za serikali na binafsi zimekua zikitoa takwimu za watu na dini zao?
Mfano 0fisi ya waziri mkuu inadai wakristo ni 45%-waislamu 35%. TBC1, imetangaza wakristo ni 52%-waislamu 32%.Bodi ya watalii -Christianity and Islam are the predominant religions of Tanzania. About 40-45% of the population practice Christianity, about 35-40% practice Islam.,Tovuti kikatoliki (RCNet) waislamu 34%- na wakristo ni 44%
Na hapa kuna hoja mbili,
a) kwa nini takwimu zinatofautiana? na b)kwa nini pamoja na kutofautiana zote zinaonesha wakristo ni wengi kuliko waislamu?
Kwa kawaida jambo la uongo lazima hukwama, takwimu zinatofautiana kwa sababu ni za uongo, Zote zinaonesha wakristo ni wengi kwa sababu za kukidhi matakwa ya MK.
Mkurugenzi wa TBC alipoulizwa kuhusu takwimu katoa wapi aliishia kuomba radhi, kakosea, swali ni je kakosea nini? Amekuwa akikosea mambo mangapi ya kitaifa kwa ujumla wake kama lilivyo hili? Huu ndio MK
3.Kwa nini kiwepo kipengele cha kuhesabiwa kwa nyumba za ibada?
Waislamu wakisema kuwa kuhesabiwa kwa nyumba za ibada pekee kunaweza kutumiwa na wapotoshoshaji wa Umma kupitia MK, kuwa Wkristo ni wengi kwani siku hizi kuna utitiri wa madhehebu kikristo na makanisa binafsi hata kama yana waumini wachache achilia mbali uyoga wa makanisa yanojiita ya wokovu? Kwa nini nyumba za ibada na sio na wanaoabudu humo?, Serikali inataka kugawa misala misikitini na mabench kanisani?
Waislamu wa leo ni tofauti na wa enzi hizo, wanajua wanachokifanya na hili la sensa ni moja na mengine yatakuja,hatuhitaji kumtafuta kiongozi wala Sheikn Ponda kwa hili, elimu tulishapata , macho yalishafumbuliwa na Tunaelewa athari za mfumo Kristo katika jamii


  1. Tulisadikishwa kuwa waislam hawakusoma, kumbe data zinaonesha NECTA inawapunguza
  2. Tukasadikishwa kwamba hawajengi Mashule na Hospitali ila wanajenga misikiti, kumbe wenzetu wanajenga kupitia fedha wanazopewa na serikali hii hii kupitia MoU
  3. Tukasadikishwa kuwa nchi hii haina dini , kumbe serikali yetu ina mfumo Kristo ambao haukuandikwa popote lakini unafanya kazi zake kwa siri na waziwazi
TUMEKATAA KWENDA KWA MATAKWA YA MK, NARUDIA WAISLAMU HATUHESABIWI.

Pole sana mkuu kwa mawazo hayo ya miaka ya kikoloni, wakati ambapo mababu na mabibi walikuwa wanawaficha watoto wao hususan wa kike wasiandikishwe shule ati wazungu watawaharibu, watawalisha nguruwe, watakuwa hawajui kazi za kuwatumikia waume zao nk.

Inasikitisha sana unaposema waislamu wamesoma sana kuliko wakristo halafu bado pamoja na elimu waliyokuwa nayo baadhi yao wanashindwa kuelewa umuhimu wa sensa.

Mkuu, na hapo Rais, makamu wa Rais, Waziri wa elimu, waziri wa ulinzi, waziri wa Afya na vitengo vingine nyeti ni waislamu. Je wangekuwa ni wakristo si ingekuwa balaa.

Yaani kwa akili yako na elimu yako viongozi wote hao niliowataja hapo juu ni mbumbumbu kwa uelewa wako kiasi cha kushindwa kuona ubaya wa hiyo unayiita MOU, na kukubaliana waendelee kuwakandamiza waislaamu wenzao na kuwapendelea wakristo?

Kama ndiyo basi wanatenda dhambi kubwa, kama sivyo basi uliyoyaandika ni uongo unaodhalilisha upeo wa elimu yako na ya wanaokuamini. Pole sana mkuu.
 
mimi bnafs naangalia wapi wanakosea na bado nafanya kazi kama mtumishi wa umma inapobidi nasaidia kwani semina zote zipo mashuleni ambako ndipo walimu tulipo.Madawati, viti vya kukalia huduma ya choo, breakfast, stionary na wanapogota inabidi waseme. Kwa ufupi mm naelewa mipaka ya siasa na kazi.Everythin is in good order na wala sio 'LOLOTE NA LIWE' Hizo pesa za sensa zimewafanya watu waangalie maslahi zaidi lakini hii ni kutojitambua na viongozi wengi kukosa hekima na busara ya kuamua mambo kwa ufasaha.
 
Hivi ina maana ni uongo kwamba wakristo sio wengi kuliko dini zingine?yaani hata kama swali hilo likiulizwa hio August 26 TBC watabaki kuwa sahihi milele hadi hapo dini zingine wakizidi kuzaliana kwa wingi.
 
Mkuu, binafsi sioni mantiki ya hoja zako, hususan unapoaonisha utalii na imani za dini za wakaazi wa eneo husika la utalii kwa TZ.

TZ haijagawanywa kikanda, kutegemeana na imani za watu. Hakuna pahala katika TZ ambako wapo aidha waislamu tu au wakristo tu au wanaoabudu dini za kimila tu! Nchi yote imejaa mchanganyiko wa watu wenye imani tofauti tofauti.

Hivyo kusema ukienda eneo fulani ndani ya TZ unatakiwa u-behave hivi au vile, ati kwa sababu tu wakaazi wengi wa eneo hilo ni wa imani fulani ni upuuzi na ujinga, ni namna ya kuanza kubaguana.

Ndicho kitakacholeta ubaguzi kwamba kwa kuwa waislamu ni wengi eneo fulani basi makanisa yasijengwe ili waislamu walio wengi wasibughudhiwe wakati wa ibada zao??!!!

The government of TZ is quite right, no need for the question of religious identification of its citizens in the census questionnaire.


Hili suala hakyanani tutavutana mpaka mwisho. kama wewe unadhani hizo takwimu hazina maana, waulize TBC, BODI YA UTALII na WAKATOLIKI. kwa nini wao wanazo na wanazitumia kwa faida gani??? NA WALIZIPATAJE??? ni bora wangekuwa nazo za wakatoliki peke yao, sasa wanazo mpaka na za waislamu, walituhesabu lini??? hii inashangaza sana, nashangaa watu wanawashangaa waislamu, ki-msingi tulitakiwa tuwashangae hao wenye takwimu haramu, walizipata wapi??? na wanazitumia kwa maslahi ya nani???
 
Kila muislamu atakayekubali mpango wa kugoma sensa ifikapo Agosti 26 atakuwa ameshiriki kuhujumu mipango ya maendeleo ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete.

serikali ikishindwa kufikia mipango yake ya maendeleo wapo watakaosema ni "mfumo kristo" au itaelezwa kwamba ni mkakati wa upinzani kwani tunapenda majibu mepesi/marahisi yasiyo na vielelezo.

Msukumo wa kugomea sensa una mantiki moja tu nzito, kumwangusha JK.
 
kwa hakika sensa ikisema tuko milioni 25 wakati tuko milioni 45 baada ya mkakati wa kugoma, Jk hataweza kufikia malengo yake kwa takwimu bandia
 
Back
Top Bottom