Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 60,816
- 100,481
Mgambo wa maadili wa Sharia katika Jimbo la Katsina, Nigeria wakiwa na viboko na marungu wamevamia lodge mojawapo jimboni humo na kuanza kutandika wateja.
Majimbo 12 kati ya 36 ya Nigeria yana utawala wa Sharia wa Kiislamu ambapo huwa na mgambo waitwao Hisba kuhakisha Sheria ya Kiislamu inafuatwa na waumini wa dini ya Kiislamu, huwa wanaweza kupita kwenye bar, lodges na hotel kutekeleza sharia za kuzuia uzinzi na unywaji pombe, pia huweza kuwaadabisha wanawake kwenye suala la mavazi na huakikisha waumini wanafunga wakati wa Ramadhani.
Huwa najiuliza kwenye utawala wa Sharia katika taifa la mchanganyiko kama Nigeria sasa wasimamizi wa sharia huwa wanatofautishaje kati ya Waislamu na Wakristo?!
Mfano wakikutwa lodge muislamu na mkristo wanazini sharia itatimizwaje hapo? Au akikutwa mtu anamuuzia kitimoto au pombe muislamu sharia itatekelezwaje hapo?!
Majimbo 12 kati ya 36 ya Nigeria yana utawala wa Sharia wa Kiislamu ambapo huwa na mgambo waitwao Hisba kuhakisha Sheria ya Kiislamu inafuatwa na waumini wa dini ya Kiislamu, huwa wanaweza kupita kwenye bar, lodges na hotel kutekeleza sharia za kuzuia uzinzi na unywaji pombe, pia huweza kuwaadabisha wanawake kwenye suala la mavazi na huakikisha waumini wanafunga wakati wa Ramadhani.
Huwa najiuliza kwenye utawala wa Sharia katika taifa la mchanganyiko kama Nigeria sasa wasimamizi wa sharia huwa wanatofautishaje kati ya Waislamu na Wakristo?!
Mfano wakikutwa lodge muislamu na mkristo wanazini sharia itatimizwaje hapo? Au akikutwa mtu anamuuzia kitimoto au pombe muislamu sharia itatekelezwaje hapo?!