Sam Gidori
Senior Member
- Sep 7, 2020
- 165
- 414
Wachezaji wawili wa Afrika Kusini ambao wapo nchini Japan kushiriki mashindano ya Olimpiki wamethibitishwa kuwa na maambukizi ya virusi vya corona siku ya Jumamosi, wakitajwa kuwa washiriki wa kwanza wa mashindano hayo kupata maambukizi ya virusi vya corona wakiwa ndani ya Kijiji cha Olimpiki.
Washiriki wengine wawili, Kocha wa mchezo wa raga na mchambuzi wa video, wote raia wa Afrika Kusini wamepatikana pia na maambukizi ya virusi vya corona wakiwa nchini Japan, na kufanya idadi ya Waafrika Kusini walioambukizwa virusi hivyo kufikia wanne.
Mhudumu wa Afya wa msafara wa wachezaji wa mchezo wa raga amesema ameshangazwa na maambukizi kwani kigezo cha kuruhusiwa kutoka Afrika Kusini ni kutokuwa na maambukizi ya corona.
Mkuu wa Kamati ya Olimpiki amewahakikishia wananchi wa Japan kuwa uwezekano wa wao kupata maambukizi kutoka kwa washiriki wa mashindano ya Olimpiki ni ‘sifuri’ kutokana na tahadhari iliyowekwa.
Hata hivyo, bado kuna hali ya wasiwasi kutokana na kuongezeka kwa visa vya maambukizi mapya katika mji wa Tokyo, kuzidi watu 1,000 kila siku kwa siku nne mfululizo.
Chanzo: SkySports
Washiriki wengine wawili, Kocha wa mchezo wa raga na mchambuzi wa video, wote raia wa Afrika Kusini wamepatikana pia na maambukizi ya virusi vya corona wakiwa nchini Japan, na kufanya idadi ya Waafrika Kusini walioambukizwa virusi hivyo kufikia wanne.
Mhudumu wa Afya wa msafara wa wachezaji wa mchezo wa raga amesema ameshangazwa na maambukizi kwani kigezo cha kuruhusiwa kutoka Afrika Kusini ni kutokuwa na maambukizi ya corona.
Mkuu wa Kamati ya Olimpiki amewahakikishia wananchi wa Japan kuwa uwezekano wa wao kupata maambukizi kutoka kwa washiriki wa mashindano ya Olimpiki ni ‘sifuri’ kutokana na tahadhari iliyowekwa.
Hata hivyo, bado kuna hali ya wasiwasi kutokana na kuongezeka kwa visa vya maambukizi mapya katika mji wa Tokyo, kuzidi watu 1,000 kila siku kwa siku nne mfululizo.
Chanzo: SkySports