Ishi Maisha Yako: Acha Kutafuta Kukubalika kwa Lazima
Mdau, usitafute kupendwa, kukubalika, au kuheshimiwa kwa nguvu. Kupendwa kwa kulazimisha au kutaka heshima ya lazima hakuna mvuto wowote, kwa sababu sio uhalisia (originality). Heshima na upendo wa kweli havihitaji nguvu kubwa kupatikana; vinakuja vyenyewe pale unapokuwa wewe.
1. Ishi Maisha Yako Bila "Kufake"
Fanya mambo yako bila kuhitaji uthibitisho au makofi (validation) kutoka kwa watu. Kuwa wewe kama wewe na usitake kujifanya mtu mwingine ili tu uonekane unafaa kwenye jamii. Be original always.
Mfano wa Maisha: Ukiwa una uwezo wa kununua simu ya Sh 300,000, inunue na uitumie kwa amani. Usikope au kujinyima chakula ili ununue simu ya Sh 1,500,000 kwa lengo la kuwavutia marafiki au kupata "Likes" mitandaoni. Ukweli ni kwamba, sifa za mtandaoni hazilipi kodi ya nyumba yako.
2. Upendo wa Lazima Haufai
Unapolazimisha watu wakupende au wakuone wewe ni wa maana, unajishusha thamani na unakuwa mtumwa wa hisia zao.
Mfano wa Mahusiano: Kumpigia mtu simu mara 20 kwa siku, au kumnunulia zawadi za gharama kubwa mtu ambaye hakuonyeshi ushirikiano, ni kupoteza muda. Badala ya kulazimisha upendo huo, wekeza nguvu zako kwa watu wanaothamini uwepo wako bila masharti.
3. Heshima Huletwa na Uhalisia, Sio "Kiki"
Huwezi kuamuru watu wakuheshimu kwa sababu tu una vyeo, fedha, au muonekano fulani. Heshima ya kweli inajengwa na tabia yako, misingi yako (principles), na jinsi unavyojichukulia.
Mfano wa Kazi/Biashara: Kwenye eneo la kazi, usiwaseme vibaya wenzako au kujipendekeza kwa bosi ili uonekane wewe ndiye mfanyakazi bora. Fanya kazi yako kwa weledi, heshimu kila mtu kuanzia mlinzi hadi mkurugenzi. Heshima yako itazungumza yenyewe kupitia matokeo ya kazi yako.
Neno la Mwisho
Kumbuka, ukiishi kwa kuwaridhisha watu, utakuwa unabadilika kila siku kama kinyonga kwa sababu binadamu hawana jopo la kuridhika. Kuwa wewe, simamia unachokiamini, na ishi kwa amani.
Alamsiki!