JamiiForums
JF Official Account
- Nov 9, 2006
- 6,202
- 5,014
Wakuu wana JamiiForums,
Tunatarajia kufanya mahojiano hivi karibuni na Mheshimiwa Khamis Kagasheki, Mbunge wa Bukoba Mjini ambaye alikuwa Waziri wa Maliasili na Utalii kabla ya kujiuzulu rasmi Bungeni na aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Switzerland.
Ndugu Kagasheki amekubali wito wa kushiriki mahojiano hayo yatakayolenga kujibu maswali yote yatakayotolewa na washiriki hapa JamiiForums.
Tunakaribisha washiriki wote wa JamiiForums kushiriki katika kufanikisha mahojiano hayo yatakayofanyika kwa njia ya video kwa kutoa maswali waliyo nayo.
Maswali yote yatakayowasilishwa hapa yakimlenga Mheshimiwa Kagasheki yatajibiwa na kurudishwa kwenu kwa njia ya video/audio na maandishi.
Maswali hayo yatakusanywa kwa muda wa siku tatu (leo April 17 - Aprili 19 saa sita kamili usiku).
Karibun
-----------
UFAFANUZI WA VIDEO
JamiiForums imeanzisha kitengo cha Video Production kitakachokuwa kinahoji watu mbalimbali (si wanasiasa tu) juu ya masuala mbalimbali katika Jamii.
Tumewahi kufanya mahojiano kama hayo (angalia - JamiiTalks - Mahojiano ya moja kwa moja na Mhe. Zitto Zuberi Kabwe katika JamiiForums ) kwa njia ya ki 'maandishi tu' ila sasa tumeboresha kwa kufanya iwe njia ya Video.
Mahojiano hayo baada ya kurekodiwa yatapandishsa humu JamiiForums ili kuweza kutazamwa jinsi mahojiano hayo yalivyokuwa na majibu ya maswali yenu/yetu toka kwa mhusika.
Asanteni.
Tunatarajia kufanya mahojiano hivi karibuni na Mheshimiwa Khamis Kagasheki, Mbunge wa Bukoba Mjini ambaye alikuwa Waziri wa Maliasili na Utalii kabla ya kujiuzulu rasmi Bungeni na aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Switzerland.
Ndugu Kagasheki amekubali wito wa kushiriki mahojiano hayo yatakayolenga kujibu maswali yote yatakayotolewa na washiriki hapa JamiiForums.
Tunakaribisha washiriki wote wa JamiiForums kushiriki katika kufanikisha mahojiano hayo yatakayofanyika kwa njia ya video kwa kutoa maswali waliyo nayo.
Maswali yote yatakayowasilishwa hapa yakimlenga Mheshimiwa Kagasheki yatajibiwa na kurudishwa kwenu kwa njia ya video/audio na maandishi.
Maswali hayo yatakusanywa kwa muda wa siku tatu (leo April 17 - Aprili 19 saa sita kamili usiku).
Karibun
-----------
UFAFANUZI WA VIDEO
JamiiForums imeanzisha kitengo cha Video Production kitakachokuwa kinahoji watu mbalimbali (si wanasiasa tu) juu ya masuala mbalimbali katika Jamii.
Tumewahi kufanya mahojiano kama hayo (angalia - JamiiTalks - Mahojiano ya moja kwa moja na Mhe. Zitto Zuberi Kabwe katika JamiiForums ) kwa njia ya ki 'maandishi tu' ila sasa tumeboresha kwa kufanya iwe njia ya Video.
Mahojiano hayo baada ya kurekodiwa yatapandishsa humu JamiiForums ili kuweza kutazamwa jinsi mahojiano hayo yalivyokuwa na majibu ya maswali yenu/yetu toka kwa mhusika.
Asanteni.