Saint_Mwakyoma
JF-Expert Member
- Jun 8, 2019
- 865
- 1,205
Kumezuka wimbi kubwa la wanaume wengi wanaozama kwenye dimbwi la mahusiano ya kimapenzi na baadae sana wanagundua wapenzi wao wamewazidi umri kitu ambacho jamii ya kiTanzania inakichukulia kama kitu cha aibu na cha ajabu mno.
Kwenye kila taasisi kuanzia ya familia, makazini na nyumba za ibada uhukumu kwa ubaya sana wapenzi hawa na mala zote anayeonekana anamuonea mwenzake ni mwanamke kisa ni mkubwa kiumri.
Kitendo hiki kikitokea kwa mwanamke kuzidiwa umri na mwanaume kwenye mahusiano ya kimapenzi kinapokelewa kama kitu sahihi na kimekamilika , mwanamke anaweza zidiwa hata miaka 10-20 na mwanaume na jamii inaona ndio kitu sahihi na wengi wa wanawake hufurahia hili lakini punde tu !! Mwanamke anapomzidi umri yule mwanaume basi hao wapenzi husakamwa na kusimangwa kwa methali na nahau na vijembe kutwa kucha.
Jamii inabidi ibadilike sasa ....nawasilisha
Kwenye kila taasisi kuanzia ya familia, makazini na nyumba za ibada uhukumu kwa ubaya sana wapenzi hawa na mala zote anayeonekana anamuonea mwenzake ni mwanamke kisa ni mkubwa kiumri.
Kitendo hiki kikitokea kwa mwanamke kuzidiwa umri na mwanaume kwenye mahusiano ya kimapenzi kinapokelewa kama kitu sahihi na kimekamilika , mwanamke anaweza zidiwa hata miaka 10-20 na mwanaume na jamii inaona ndio kitu sahihi na wengi wa wanawake hufurahia hili lakini punde tu !! Mwanamke anapomzidi umri yule mwanaume basi hao wapenzi husakamwa na kusimangwa kwa methali na nahau na vijembe kutwa kucha.
Jamii inabidi ibadilike sasa ....nawasilisha