Jamii Forums inakutanisha wapenzi hadi kwenye ndoa

Jamii Forums inakutanisha wapenzi hadi kwenye ndoa

SOCIOLOGISTTZ

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2013
Posts
2,615
Reaction score
929
Jamii forums ni jukwaa kubwa sana na maarufu hapa Tanzania.

Linakutanisha watu wa kila namna kwenye eneo wanalolipenda. Natoa ushuhuda wa watu waliokutana huku JF kwa muda wa mwaka mmoja uliopita na sasa wanapanga mipango ya ndoa yao na jinsi itakavyokuwa.

Taarifa walizonipatia ni kwamba wameshakutana mara kadhaa ijapokuwa yale mambo mengine wameniambia hawajafanya kabisa. (hapa sijui kama ni kweli au wamenidanganya) walishatembeleana mara kadhaa huku wakinywa na kula nyama za mifugo mbalimbali.

Sasa wanamsubiri huyu Bwana amalize masters yake ili waoane kabisa. Nilimsikia huyu jamaa akimwambia bibiye kuwa angependa apate kwanza ujauzito kabla ya ndoa ili asiuziwe mbuzi kwenye gunia.

Nilicheka kwani sikujua kama ndiyo anomba vitu au anamaanisha alichokisema. Jumamosi yaa niKesho walinialika kwenye kikao chao (bwana na bibi huyo), lakini kwa ajili ya shughuli za kijamii sitakuwepo labda mpaka Jumamosi ijayo niliwaambia hivyo.

Nachotaka kusema hapa ni kwamba kweli nimeamini Jamii Forums inakutanisha watu mbalimbali ambao kabla walikuwa hawajuani na wengine hadi kwenye maisha ya ndoa.

Big up JF especially MMU
 
Hahahaaa..,,Weweee...Yaani kumbe umekuja kusema huku..!!
 
sociology haipo mbali saaaaaaaana na mascomu khakhaa!
 
Mkuu kama umefikia hatua ya kutoa taarifa hapa sidhani kama kuna ulazima wa kuficha majina..ukiona mko kwenye mahusiano na mnakaribia ndoa ila still mahusiano yenu ni ya kujifichaficha hapo kuna walakini
 
jf hii ninayoijua mm au?? tho ndege wafananao huruka wote. may be.
 
Mkuu kama umefikia hatua ya kutoa taarifa hapa sidhani kama kuna ulazima wa kuficha majina..ukiona mko kwenye mahusiano na mnakaribia ndoa ila still mahusiano yenu ni ya kujifichaficha hapo kuna walakini

Kuumbeee eeh!!! SOCIOLOGISTTZ njoo uweke wazi mambo.!!
 
Last edited by a moderator:
Wahusika wana haki pia ya kutaka majina yao ya humu yawekwe hadharani au la.

Mkuu kama umefikia hatua ya kutoa taarifa hapa sidhani kama kuna ulazima wa kuficha majina..ukiona mko kwenye mahusiano na mnakaribia ndoa ila still mahusiano yenu ni ya kujifichaficha hapo kuna walakini
 
Sasa tunaanza vikao ama bwa shee anamalizia masters yake kwanza? Na hawajafanya zile mambo huku jamaa anataka ujauzito kwanza? Inabidi upande mbegu kwa niaba ya shost wako
 
Wahusika wana haki pia ya kutaka majina yao ya humu yawekwe hadharani au la.

Ni sawa mkuu...ila unahisi wahusika ndo waliomtuma kupost huo uzi??
 
Back
Top Bottom