pole sana! ila mimi naomba kuuliza kwanini waume zetu hawapendi tuingie JF? ukiwa bize na simu utasikia vipi,uko JF?kunani JF?
Hapa inatokana na aina ya mme au boyfriend uliye naye kwa upande wangu mwandani wangu Dinazarde simzuii kuingia JF tusichanganye habari. Kilichotokea siku mzima nilikuwa busy na kazi naye akaingia JF kwakuwa hakuwa na shughuli nyingi baadaye nikampigia simu Kisha tukaingia whatsapp cha kushangaza akawa anaandika anapotea anaandika swali anapotea nikamuuliza uko busy Sana au simu zinaingia? Akasema hapana basi nikahisi isije kuwa alikuwa naenda JF na kwa lugha nyingine JF kumegeuka pa maana anasahau na familia nilichofanya Ni kuangalia ule muda wa charting na aliokuwa anapotea kuangalia iwapo alienda kupost comment na kumbe nilikuwa sahihi kwa asilimia 100%
Mie siko controlling wala obsessed na yeye kwenda JF by the way ni mie nilimshauri aingie JF afanye comments zake kwa uhuru afurahie nafsi zamani alisoma tu kwa kufanya vile tunaopenda JF tusisahau familia na JF ikachukua nafasi yake tufurahie uhuru wa kutoa maoni pia tujue familia ni ya kwanza mengine yanafuata
Wanawake pia tuelewe jamaa yako akikupa uhuru wa kufanya upendalo bila kwenda kinyume cha maadili tusiabuse kwa maneno yake nimemkamata yule haendi popote mie nafanya nipendalo pia wanaume tusiwanyime wanawake uhuru love ni pamoja na kufeel matakwa ya mwenzio ili mradi hayako kinyume na maadili. Unaweza kumzuia kumbe anafanya kisiri nawe unaona kuwa mpenzi wangu Jamii haendi kabisa sijui ndo sita au la tubalance sehemu zote