James Orengo vs Tundu Lissu

James Orengo vs Tundu Lissu

Mungu Huwainua Wanyenyekevu Na Kuwapinga Wenye Kiburi
Sasa Hivi Tumeona Wazi
 
..lakini waandishi wanasema James Orengo wa kwenye majukwaa ya siasa ni tofauti na yule aliyeonekana mahakamani.

..mazingira ya mjadala, kuanzia na hoja iliyoko mezani, weledi wa wanaoshiriki mjadala husika, pamoja na busara na maadili ya muongoza mjadala, yana athari kubwa ktk jinsi ambavyo washiriki wa mjadala huo wata-behave.

..JAMES ORENGO ukimpeleka kwenye bunge la Tz linaloongozwa na SPIKA asiyetenda haki kama NDUGAI anaweza ku-behave tofauti kabisa na yule uliyemuona mahakamu kuu ya Kenya.

..Hata TL ukimuweka ktk mazingira ambayo HAKI inatendeka nina hakika atajenga hoja zake kwa utulivu.
Nawe mkuu sasa sijui ni mazingira gani Lissu anayataka ili atulie. Ni yeye anayeitisha Press conference, anasema anayotaka, maswali anaulizwa akitaka tena mwishoni, lakini bado ni kupayuka tuuu! Tone ya sauti siyo ya kushawishi, ni ya ugomvi, kwa ujumla hajui kuchagua maneo.
 
wapo sawa tu. Tundu lisu ashapangua kesi ya uchaguzi peke yake bila kuwakilishwa na wakili, nimesha appear na Tundu mara nyingi kama opponent wake, yupo vizuri sana na akili yake ni sharp...ujasiri anao sana, na anajua kufanay presentation na kukonvinsi mahakama jambo ambalo ni asset kubwa sana kwenye tasnia ya legal practice.
Mkuu nilimuuliza swali hilo yule mburula aliyekuwa anamkandia Lisu utafikiri anamjua mno Orengo wakati jina lenyewe la Orengo ameliona hapa JF!
 
Huyu bwana kajizolea sifa lukuki kwa wakenya na wapenda sheria wote duniani. Imefikia mpaka Watanzania wanamfananisha na Mwanasheria machachari Tundu Lissu..

Sijawahi kumshuhudia Lissu akiwa mahakamani, ila nimemwona Orengo, jamaa is very calm and calculated. Anaongea kwa tone ambayo kila mmoja atashawishika kumsikiliza, sijui Lissu akiwa mahakamani anakuaje, lakini kama anaongea kwa ile tone ya bungeni na kwenye mikutano ya kisiasa naona wazi Lissu atakuwa na weakness fulani.

Ningependa mpitie hili andiko ambalo limempa Orengo sifa lukuki na ni kwanini ameshinda hii kesi akiwagalagaza SC wengine wanne..

Five ways James Orengo has proved to be brilliant lawyer

JE NI HAKI KUMFANANISHA ORENGO NA LISSU? Naomba vijana wa siasa mkae pembeni ningependa kujibiwa na wanasheria na watu wenye uzoefu na mahakama..

Sent using Jamii Forums mobile app
Watu wengine mna akili mbovu. Sasa unataka lissu aongee kama Orengo kwanini? Kwani lissu ni Orengo? Kila mtu ni unique, amezaliwa na differences zake. Hata wangekuwa mapacha qasinfefanana kwa kilia kitu. Wote ni wazuri kitaaluma kwa namna tofauti. Wewe unachojaribu kuonyesha hapa, kama siyo ignorance bus ni ule uzumbukuku wa maccm kuchukia kila aliye wa upinzani. Badilika acha uzumbukuku.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tundu Antipas Lissu is "Eloquent"...he has legal language anapokuwa mahakamani,na anapokuwa bungeni,he has a "political Language".

Ubaya wa Lissu ni kuwa,maisha yake yote amechagua kuwa upande wa "kupinga" na si "kukubali"...Toka shule ya Msingi,Shule ya upili,chuo,JKT mpaka katika maisha yake ya kila siku,amechagua kuwa "upande wa wachache wasio na sauti"

Upande wa wachache huwa hauna sifa,ni upande wa kufitiniwa na kuhujumiwa...Zaidi ya lugha ya kimahakama,nje ya siasa na sheria,Tundu Lissu ni mtu muungwana sana,ana lugha nzuri na si mtu wa kisasi wala hasira za haraka!!

Kuna wakati ukikaa na Lissu kuongelea maisha na familia,unaweza kujiuliza,hivi huyu ndio Lissu wa Bungeni?
Hii biography unayotoa umeipata wapi? Sisi tusiokuwa naye bedroom tutayajuaje hayo au tukuamini vipi wakati siku zote tunamuona akipayuka na mitusi hadi kwenye press conferences!
Kila mTZ anaeleweka kwa jinsi anavyoonekana na kueleweka hadaharani. Siyo mambo ya familia sijui misibani anafanya hivi! Oooh michango ya harusi anatoa, akilia machozi yanatoka, bhla-bhla.......!
 
Lissu anachokosea ni kutojua wapi pa kupigania. Anawafundisha watu kuopambana na Magu badala na mfumo wa siasa zetu.

Unalinganisha damu na tui hapa.
Sasa unaposema lissu anspigana na magu badala ya siasa unamaanisha nini? Kuna siasa bila watu? Nani msimamizi wabhuza siasa? Unapopigsna vita unapinga watu au kitu gani? Siasa ni watu na nilazima lissu apambane nao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwezi katu kumfananisha Lissu, anayetumia maneno na lugha ya mitaani na kijiweni kuwasilisha hoja zake, hata kama ni za msingi, na Orengo mtu mwungwana, mnyenyekevu, mstaarabu na makini katika matumizi ya maneno na lugha.

Katika muda mfupi, nimejifunza kwamba Lissu, anajaribu kujipambanua kama mwanaharakati, akijificha nyuma ya taaluma yake ya sheria, lakini ukweli unaanza kuonekana kwamba ni mtu hatari, mzandiki, kigeugeu na mwenye visasi na wakati huo huo akijipendekeza kwa maslahi yake, ambayo ni misifa na umaarufu. Hii imejitokeza tangu ashiriki kikamilifu kuwaondoa CHADEMA aliowaona wanatishia nafasi yake ya kutukuzwa.
 
Acha kumwaga sifa kwa wasiostahili. Umezaliwa lini? Nchi hii kuna watu walijitoa muhanga hata kutumia nguvu. Wengine kwa hoja ktk mazingira magumu ya kisiasa kuliko leo hii. Huyu Lissu bila ushabiki, siyo wa maana kiasi hicho! Unaweza kusoma? Tafuta majina haya: Che Mponda, Marando, Mtikila, Farther Tom, Hatty McGhee ...
Che mponda alifanya nini?!!
 
Tundu Antipas Lissu is "Eloquent"...he has legal language anapokuwa mahakamani,na anapokuwa bungeni,he has a "political Language".

Ubaya wa Lissu ni kuwa,maisha yake yote amechagua kuwa upande wa "kupinga" na si "kukubali"...Toka shule ya Msingi,Shule ya upili,chuo,JKT mpaka katika maisha yake ya kila siku,amechagua kuwa "upande wa wachache wasio na sauti"

Upande wa wachache huwa hauna sifa,ni upande wa kufitiniwa na kuhujumiwa...Zaidi ya lugha ya kimahakama,nje ya siasa na sheria,Tundu Lissu ni mtu muungwana sana,ana lugha nzuri na si mtu wa kisasi wala hasira za haraka!!

Kuna wakati ukikaa na Lissu kuongelea maisha na familia,unaweza kujiuliza,hivi huyu ndio Lissu wa Bungeni?
its seems ur very intellegent chief. salute kwako
 
Acha kumwaga sifa kwa wasiostahili. Umezaliwa lini? Nchi hii kuna watu walijitoa muhanga hata kutumia nguvu. Wengine kwa hoja ktk mazingira magumu ya kisiasa kuliko leo hii. Huyu Lissu bila ushabiki, siyo wa maana kiasi hicho! Unaweza kusoma? Tafuta majina haya: Che Mponda, Marando, Mtikila, Farther Tom, Hatty McGhee ...
Nawewe unaweza kuwazungumzia hao Maana yeye kachagua LISU...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani tofauti iko wazi. Ukisoma maelezo hayo, Orengo aliweza kutofautisha jukwaa la siasa na chumba cha mahakama. Jambo ambalo mwenzetu huyu anayeitwa machachari, hana kabisa! NImeona anavyoshindwa kutofautisha Bunge na mikutano ya mitaani. Nadhani Orengo ni mtu mwenye sifa za pekee. Ni mtu anayeweza kujua uso wa mwenzake unasema nini. Tatizo la Lissu anataka kila mtu amsikilize yeye anasema nini bila kujali msikilizaji ni nani.
Nabii hakubaliki nyumbani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Eloquent PLO credebility plunges to zero. Eti petition dead on arrival.
 
Mimi najiuliza na "umahiri " wangu wote wa sheria pamoja na wengine mbona mleta uzi kachagua kumlinganisha TL na Orengo? Tafakari!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NIMEKAA KENYA KWA MDA MREFU, NIMEHUDHURIA MIKUTANO YA KISIASA YA JAMES ORENGO, NAMWELEWA SANA. MAHAKAMANI ALITUMIA LUGHA YA MAHAKAMA, ILA JUKWANI HUTUMIA LUGHA YA SIASA AMBAYO SIO LEGAL LANGUAGE WALA HAIKUHITAJI KUWA SAHIHI ASILIMIA HATA 10%.

LISU BUNGENI HUTUMIA LUGHA YA BUNGE. JUKWANI HUTUMIA LUGHA YA JUKWAANI. MAHAKAMANI HUTUMIA LUGHA STAHA NA WELEDI WA HALI YA JUU (LEGAL LANGUAGE). ANACHEZA NA SHERIA VIZURI TENA MARA NYINGI SHERIA DHAIFU ANARUDI KWENYE KATIBA AMBAYO NDO MSIKNGIK EWA SHERIA NA KANUNU ZILIZOTENGENEZWA N A BBUNGE. KESI YA ESTER BULAYA NILIMPENDA. HE IS A MAN OF THE COURT. NA MARA NYINGI KINACHOMFANYA LISU KUSHIKNDA NI PALE AMBAPO ANATUMIA MDA MWINGI KUWA (AMICUS) KUISHAURI MAHAKAMA.

USIWADANGANYE WATU KUWA LISU SIO JEMBE. HE IS. I SAY HE IS.
 
Hakusema kuwa wachache wapo sahihi, bali huwatetea wanyonge hata katika mazingira ya kunyanyapaliwa.
Mara zote ameibuka kidedea.

Kwa kesi ya kupinga matokeo aliyoisimamia Orengo, ushahidi ulikuwa wazi mno kiasi hata Nimrod mkono angeshinda kesi hiyo.
Maana ilikuwa rahisi kuthibitisha irregularities kwenye uchaguzi na kuishawishi mahakama kuwa fairness haikuwepo.

TUNDU LISU KITU INGINE. Orengo nae ako poa.
Nimesoma michango mingi humu kuhusu hii mada, wachangiaji wa Tanzania wengi wamejaa chuki. Wewe umeeleza mchango bora na kweli maana kulinganisha watu na kazi zao hatupaswi kufanya kwa tukio la mmoja na mwingine sjfa na Tabia. Kwanza kulipaswa kuwe na kesi kadhaa zilizochukuliwa kila upande na tuchambue zilivyoendeshwa, mazingira yake na walioziongoza.. Kimsingi, Kenya wao kila kitu wako na taratibu nzuri za kufanya kuliko Tanzania ambapo mambo mengi utaratibu si wa sawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesoma michango mingi humu kuhusu hii mada, wachangiaji wa Tanzania wengi wamejaa chuki. Wewe umeeleza mchango bora na kweli maana kulinganisha watu na kazi zao hatupaswi kufanya kwa tukio la mmoja na mwingine sjfa na Tabia. Kwanza kulipaswa kuwe na kesi kadhaa zilizochukuliwa kila upande na tuchambue zilivyoendeshwa, mazingira yake na walioziongoza.. Kimsingi, Kenya wao kila kitu wako na taratibu nzuri za kufanya kuliko Tanzania ambapo mambo mengi utaratibu si wa sawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Thanks.
 
Acha dharau. Unamfananisha Orengo na huyo Mhemko anayekula matapishi hadharani?
You are nothing upstairs just calling lissu "mhemko" he is a man of action. The problem you are affected and infected partisan.!!! Pole utabakia mchumia tumbo kwa kuogopa ukweli eti umfurahishe banako. ?!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom