James Millya chunga kauli zako

James Millya chunga kauli zako

Crucifix

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2011
Posts
1,655
Reaction score
593
"Ndugu zangu tunamleta kamanda msofe, mchagueni akawashughulikie panya kwenye halmashauri yetu."

Kauli kama hizi zikiendelea zitakuja kukugharimu wewe pamoja na chama chako ulichojiunga juzijuzi. Au na wewe ulikuwa panya kabla ya kujiondoa CCM?
 
Halmashauri ya jiji la Arusha ina Panya, mchwa, viwavijeshi, siafu, kenge, kunguru, nzige...kunaitajika pestcide itakayo ua bila kubakiza kitu hapo...

Safi sana Millya kauli ya Kimapinduzi hiyo...
 
Lugha za kistaarab ni muhimu. Lazima CDM wajitofautishe na wanaowapinga. i.e Lucinde!
 
Crucifix unamtisha Millya au ni mkwara tu? Yaani siku zote hujajua kuwa CCM hawana tofauti na mchwa, panya, mbwa hata viwavi? Hebu angalia nchi yetu inavyoliwa na kila mdudu huku ikidhalilika kuliko hata mbwa. Shame on you!
 
Halmashauri ya jiji la Arusha ina Panya, mchwa, viwavijeshi, siafu, kenge, kunguru, nzige...kunaitajika pestcide itakayo ua bila kubakiza kitu hapo...

Safi sana Millya kauli ya Kimapinduzi hiyo...

Mwisho wa siku mahakama zikitengua matokeo kutokana na lugha zisizofaa tusirudi tena kulalamika eti kuna shinikizo la kisiasa. Kumbuka kauli ziligharimu ubunge wa Lema
 
Mbona sioni ubaya hapo! Hivi hiyo kauli na zile kauli za lusinde ipi ni mbaya. Kwetu CDM hatuna ubaya na hiyo kitu au mnataka kumwambia Tendwa atoe tamko? Imewagusa.
 
Crucifix unamtisha Millya au ni mkwara tu? Yaani siku zote hujajua kuwa CCM hawana tofauti na mchwa, panya, mbwa hata viwavi? Hebu angalia nchi yetu inavyoliwa na kila mdudu huku ikidhalilika kuliko hata mbwa. Shame on you!

Simtishi Millya, lakini kuNa watu watakuja kuzitumia kauli hizo hizo na zitawanufaisha. NINAONA MBALI......
 
Mbona sioni ubaya hapo! Hivi hiyo kauli na zile kauli za lusinde ipi ni mbaya. Kwetu CDM hatuna ubaya na hiyo kitu au mnataka kumwambia Tendwa atoe tamko? Imewagusa.

Tuanataka staha. Kama Lusinde ni mwehu basi unataka Millya nae awe mwehu? Tunataka kampeni ya kistaarabu
 
Crucifix unamtisha Millya au ni mkwara tu? Yaani siku zote hujajua kuwa CCM hawana tofauti na mchwa, panya, mbwa hata viwavi? Hebu angalia nchi yetu inavyoliwa na kila mdudu huku ikidhalilika kuliko hata mbwa. Shame on you!
mleta uzi yuko kwenye hiyo network ya mapanya ndio maana imemuuma sana,na ukome!
 
haki ilibakwa,tunasubiri rufaa

Yawezekana kabisa haki ilibakwa, lakini aliyeibaka alipata kisingizio ambacho bado anacho - lugha chafu.
Je ni sahihi kuendelea kumpa kisingizio hicho?
 
mleta uzi yuko kwenye hiyo network ya mapanya ndio maana imemuuma sana,na ukome!

unajifaragua tu lakini moyoni mwako unajua wazi ustaarabu ndio tunu bora
 
Mnawaita wenzenu Panya nyie mkiambiwa mnavaa magwanda kama mmejinyea mnalalamika.
 
Back
Top Bottom