James Millya chunga kauli zako

James Millya chunga kauli zako

neno Panya limetumika kifasihi tu,kwa mtu aliemakini atapenda kujua tabia za panya na namna can reflect those rats behaviours to humans,nadhani kama kauli imekukwaza pole bt haikuwa na maana ya kutusi bali kuelezea the fact,thats politics mkuu.
 
Crucifix huwezi kuona mbali kwa vitisho bali hoja yenye mashiko. Kutishana ni mambo ya kizamani na isitoshe mtu mzima hatishiwi nyau so to speak.
 
Baraza la kiswahili Tanzania liko wapi maana wanatuaribia lugha yetu!
 
Mnawaita wenzenu Panya nyie mkiambiwa mnavaa magwanda kama mmejinyea mnalalamika.
kwenye halmashauri zetu zina Kunguru, paka shume, panya Viwavijeshi nk. Hivyo wote wanatakawa kushughulikie. Pia kuna mchwa na siafu, hawa tuwape ushirikiano! Haya si matusi kaka, kama unazijua tabia za wanyama hawa utabaini kwamba ni lugha ya picha tu imetumika. Tena hata kwenye kiswahili inaruhusiwa! Hujawahi sikia msemo huu "wanafanya kazi kama mchwa!"
 
hata kama unadhani kuwaita watu panya si matusi, lazima tujenge kizazi kinachotumia lugha safi

mkuu crucifix, arumeru mashariki wakati wa kampeni za ubunge, walahi kwenye mikutano ya ccm kizazi kizuri sana kimejengwa.
 
Mwisho wa siku mahakama zikitengua matokeo kutokana na lugha zisizofaa tusirudi tena kulalamika eti kuna shinikizo la kisiasa. Kumbuka kauli ziligharimu ubunge wa Lema

Kwani tafsiri yako ya neno panya nini? Kwani halimashauri kuna panya au kuna watu? unawezaje kumkamata mtu kauli kama hiyo? Jee kama alimaanisha panya buku ambao wako kwenye jengo la halimashauri je? Ha ha haaaa
 
nafikiri CRUCIFIX amechemsha,tumuombee arudi kuutambua ukweli kwamba Halmashauri nyingi ni balaa ni zaidi ya panya.
 
"Ndugu zangu tunamleta kamanda msofe, mchagueni akawashughulikie panya kwenye halmashauri yetu."

Kauli kama hizi zikiendelea zitakuja kukugharimu wewe pamoja na chama chako ulichojiunga juzijuzi. Au na wewe ulikuwa panya kabla ya kujiondoa CCM?

Panya ni wadudu wanaokula mazao ghalani.Wala rushwa au wafanya ufisadi hawana tofauti sana na hawa wadudu kabla ya kuonekan hadharani ndipo watu hupata kakika kuwa ni watu na si panya ndio wanakula hazina ya serikali.

Millya hawezijua kama hao waharibifu ni watu,kwani hata halamashauri nayo ina panya wengi tuu wanakula hadi mafaili.Takukuru ndio wanapaswa thibitisha kuwa ni watu na si panya.
 
Kwa njisi inchi hii inavyotafunwa na mafisadi ni jambo la busara kuifananisha ccm na fisi.!
 
Back
Top Bottom