Jambo Usilolijua: Nyerere alipokea Taifa la namna gani? Mpango wa Kwanza wa Maendeleo 1961

Tatizo ni pale wanaosema alifeli wanaposhindwa kukubali kuwa kuna vitu unaweza kuvipima 'quantitatively' na vingine 'qualitatively.
Qualitatively ni pmoja na ethics(maadilli). Kwanfano Nyerere angeweza kuuza kipande cha nchi bila mtu kuhoji. Angeweza kuuza migodi bila sisi kujua wakati huo, lakini kuunganisha makabila 120 ili tuishi kwa utengamano sijui unapima kwa kuangalia nini.
Ngeria ilianza kama sisi na akina Nnandi Azikiwe, chief Obafemi Awolowo, kilichofuata ni mapinduzi moja baada ya jingine. Je wamefanikiwa zaidi ya kusikia North na South, Islam and Chrsitian wakikwaruzana kila siku licha ya utajiri wa mafuata walionano!!..
Mgodi mkubwa kabisa wa Almasi kule mwadui hivi unamilikiwa na nani na Tanzania inamiliki asilimia ngapi za mapato yote nasiki 25% tuliutaifisha ukatushinda, kisha ukarudishwa kwa wenyewe.

Tulitaifisha na tukawa tunawauzia hao hao tulio wanyanganya (Nadhani tulitaifisha management tu).

Tumbaku, tulikuwa tukiwauzia Afrika kusini na Zimbambwe na tukiagiza Landrover kutoka kwao, upande wa pili akiwasema kuwa ni makaburu.

Makabila 120 ya Tanganyika Nyerere akuyaunganisha, Nyerere alikuta tayari tuna utamaduni wa kutembeleana na kuchangayika, tofauti na nchi zenye makabila machache, uko kenya, Rwanda, burundi na Uganda yanawashinda kwa sababu makabila makubwa yapo machache na inakuwa rahisi kwa kabila moja kutawala nchi, sasa kwa nchi kama tanzania ni kabila gani lenye uwezo wa kupata kura za kuongoza nchi?
 
Mgodi mkubwa kabisa wa Almasi kule mwadui hivi unamilikiwa na nani na Tanzania inamiliki asilimia ngapi za mapato yote nasiki 25% tuliutaifisha ukatushinda, kisha ukarudishwa kwa wenyewe.
Tulitaifisha na tukawa tunawauzia hao hao tulio wanyanganya (Nadhani tulitaifisha management tu).
Tumbaku, tulikuwa tukiwauzia Afrika kusini na Zimbambwe na tukiagiza Landrover kutoka kwao, upande wa pili akiwasema kuwa ni makaburu.
Makabila 120 ya Tanganyika Nyerere akuyaunganisha, Nyerere alikuta tayari tuna utamaduni wa kutembeleana na kuchangayika, tofauti na nchi zenye makabila machache, uko kenya, Rwanda, burundi na Uganda yanawashinda kwa sababu makabila makubwa yapo machache na inakuwa rahisi kwa kabila moja kutawala nchi, sasa kwa nchi kama tanzania ni kabila gani lenye uwezo wa kupata kura za kuongoza nchi?

Labda umineelewa vibaya, niliposema Nyerere angeweza kuuza nina maana wakati huo akitafuta makarani hakuna ambaye angehoji endapo angeamua kuuza maeneo ya migodi au kuruhusu uchimbaji bila kuwafaidisha watanzania kama tunavyoona sasa.
Kasi iliyopo endapo Nyerere angeitumia kila kitu leo kingekuwa historia upande wa madini. Aliwahi kuulizwa kwanini kuna madini na nchi haitaki yachimbwe, akajibu madini hayaozi watakapokuwa tayari watanzania watayachimba. Tumekuwa tayari lakini udongo unapelekwa nje tunaachiwa mashimo. Kila tukuhoji zinaundwa tume na hatujui matokeo yake.

Kuhusu makabila, ni kweli yalikuwepo na yalikuwa yanashirikiana, lakini kumbuka baada ya uhuru kungetokea vurugu kubwa kutokana na kutaka nguvu za kiutawala. Nimetoa mfano wa Nigeria ambayo ina makabila kama sisi na wameishia kwenye vita, hii haina maana kuwa Wanigeria walikuwa hawashirikiani kama sisi kabla ya uhuru, hapana walikuwa kama sisi.

Sababu ya 1964 mutiny ilikuwa ni kutaka Africanization na hiyo isingepata mtu mahiri ingekwenda kwenye tribalization n.k
Kuunganisha makabila haina maana yalikuwa tofauti bali kuyaleta pamoja yaone ni sehehmu ya taifa moja.
Moja ya mpango ilikuwa kuwatawanya wafanyakazi na wanafunzi bila kujali maeneo yao, kuchgaua viongozi wa serikali bila kujali makabila yao n.k na ndio msingi mkubwa wa maelewano kati yetu, tofauti na nchi kama Kenya ambayo Waluo walikuwa waluo na wakikuyu ni kikuyu.

Ama Tanzania inakabila kubwa linaloweza kumchagua kiongozi, nakuhakikishia kuwa Wasukuma na binamu zao Wanyamwezi wanauwezo wa kumchagua kiongozi wa nchi kwa njia halali ya kura bila ubishi. Wao ni zaidi ya nusu ya wapiga kura.

Tunaposema makabila madogo ni kama wazanaki ambao si zaidi ya 50,000 lakini yapo makabila yenye watu zaidi ya milioni kwahiyo ni muhimu kuangalia neno udogo na uhalisia wake.
 
Labda umineelewa vibaya, niliposema Nyerere angeweza kuuza nina maana wakati huo akitafuta makarani hakuna ambaye angehoji endapo angeamua kuuza maeneo ya migodi au kuruhusu uchimbaji bila kuwafaidisha watanzania kama tunavyoona sasa.
Kasi iliyopo endapo Nyerere angeitumia kila kitu leo kingekuwa historia upande wa madini. Aliwahi kuulizwa kwanini kuna madini na nchi haitaki yachimbwe, akajibu madini hayaozi watakapokuwa tayari watanzania watayachimba. Tumekuwa tayari lakini udongo unapelekwa nje tunaachiwa mashimo. Kila tukuhoji zinaundwa tume na hatujui matokeo yake.

Kuhusu makabila, ni kweli yalikuwepo na yalikuwa yanashirikiana, lakini kumbuka baada ya uhuru kungetokea vurugu kubwa kutokana na kutaka nguvu za kiutawala. Nimetoa mfano wa Nigeria ambayo ina makabila kama sisi na wameishia kwenye vita, hii haina maana kuwa Wanigeria walikuwa hawashirikiani kama sisi kabla ya uhuru, hapana walikuwa kama sisi.

Sababu ya 1964 mutiny ilikuwa ni kutaka Africanization na hiyo isingepata mtu mahiri ingekwenda kwenye tribalization n.k
Kuunganisha makabila haina maana yalikuwa tofauti bali kuyaleta pamoja yaone ni sehehmu ya taifa moja.
Moja ya mpango ilikuwa kuwatawanya wafanyakazi na wanafunzi bila kujali maeneo yao, kuchgaua viongozi wa serikali bila kujali makabila yao n.k na ndio msingi mkubwa wa maelewano kati yetu, tofauti na nchi kama Kenya ambayo Waluo walikuwa waluo na wakikuyu ni kikuyu.

Ama Tanzania inakabila kubwa linaloweza kumchagua kiongozi, nakuhakikishia kuwa Wasukuma na binamu zao Wanyamwezi wanauwezo wa kumchagua kiongozi wa nchi kwa njia halali ya kura bila ubishi. Wao ni zaidi ya nusu ya wapiga kura.

Tunaposema makabila madogo ni kama wazanaki ambao si zaidi ya 50,000 lakini yapo makabila yenye watu zaidi ya milioni kwahiyo ni muhimu kuangalia neno udogo na uhalisia wake.
Kwa hiyo Wanyamwezi na Wasukuma kwa ujumla wao wanafika robo tatu au zaidi ya theruthi mbili (2/3) ya Watanzania wote! Yaani wapo zaidi ya Milioni thelathini. Dah! Haya!
 
sundi;2148505]Mdau, I appreciate your analysis. But this does not mean I should discredit your analysis simply bse I have read it here in JF. Is JF a better forum than Wikipedia, New York Times or Raia Mwema?
Sundi, tukiweka mawazo hapa yanakuwa subjected to criticism, hata unapo discredit ni sehemu muhimu sana kwasababu hatuwezi kuwa na mtazamo mmoja na wala hakuna mwenye mawazo sahihi.

Nilposema columnist wa New York time au Raia mwema simaanishi gazeti lote nina maana kuna maeneo ya watu kutoa mawazo yao kwa uchambuzi na uelewa wao, lakini sehemu hiyo isichukuliwe kama sahihi au hitimisho kwasababu mawazo ya jenerali au Mbwambo ni mitazamao yao, na vile vile katika New york times. Kuna habari (news) ambazo zipo authenticated na makala za watu kama akina Fareed Zacharia ambazo ni maoni n.k

Sio kila habari ni sahihi ndani ya mtandao ikiwemo JF, hizi ni sehemu zinazotupa mwanga wa kwenda kutafuta authenticated source ambazo zipo verified na trusted. Wikipedia sidhani unaweza kuifanyia reference bila kuwa na support ya relieable source nyingine.

Niliposema tuangangalie hoja ya Nyerere JF nina maana ya kuwa tujadili offiicial, authenticated and verified source iliyowekwa hapa ambayo ni maneno au mtazamo wa Nyerere mwenyewe tunayemjadili bila kupitia sehemu au maoni ya watu wengine ambao watakuwa na mtazamo wao.
Nina maana document ndiyo Nyerere aliitumia, na ni wajibu wetu tuiangalie kwa macho na fikra zetu bila usaidizi wa jicho lingine linaloweza kuwa linampendelea au linamchukia.

Hii itatusaidia kuondoa ile dhana ya kusikia au kusimuliwa ambayo inaleta maswali mengi yasiyothibitika na sasa kuanza kuivuruga jamii yetu.
Kwa kuiangalia document iliyopo mbele yetu tujiulize, wapi Nyerere alitumia ukabila, udini au ukanda, alionea makabila gani n.k!! bila kuhadithiwa au kusoma maoni ya watu wengine yanayoweza kuwa sahihi au la.
 
Kwa hiyo Wanyamwezi na Wasukuma kwa ujumla wao wanafika robo tatu au zaidi ya theruthi mbili (2/3) ya Watanzania wote! Yaani wapo zaidi ya Milioni thelathini. Dah! Haya!

Tanzania ina watu milioni 40, si wote wanaopiga kura kumbuka. Ninasema idadi ya wapiga kura, angalia statistics. Usibadilishe maana.
Pili, uchaguzi wetu hautegemei 1/2 au 2/3 ni 'winner takes all'. Kwa maana nyingine rais anaweza kuchaguliwa kwa tofauti ya kura 10.
 
Mdau, I appreciate your analysis. But this does not mean I should discredit your analysis simply bse I have read it here in JF. Is JF a better forum than Wikipedia, New York Times or Raia Mwema?

Mzee MM: Mwalimu ignored Kambona's advise not to take up the policy of 'Ujamaa' wholesale. He decided to copy the chinese ideology championed by Mao Zedong. What he didn't know is that behind closed doors theses communist policies where causing famine and starvation in China. Lookup the 'Great Chinese Famine ' this famine cuased the deaths of up to 45 Million people. Mao didn't know the extent of this mass extinction kwasababu alikuwa mkali hataki kuambiwa kwahiyo watu wa serikali yake walikuwa wanamficha kwa kupanda mazao ya bandia akitembelea mashamba yao.

Pia serikali ya mwalimu ilitaifisha mashamba ya wakulima wakubwa wa kigeni wa wakati huo na kuwa beza kuwa ni ' Ma-Kabaila '. In the long run this was a bad decision. As your report indicates, we were not there technically. Hata leo baada ya SUA kuzalisha Ma-Gradute wote we still don't have the know-how.

Baada ya miaka karibu 50 we are back to square one. Multi-party democracy, Mkukuta and free enterprise. Advise given by Kambona nearly 50 years ago, ignored it, akamwita 'Bepari' / Mwizi na kumtimua.

I genuinely believe Mwalimu wanted to develop Tanzania but his ideas came short. Today's leaders are completely unpatriotic and look to leadership as a means to become Wealthy - easily.

Kama wahenga wasemavyo. Yaliyopita si ndwele, tugange yajayo. It is not enough for us to talk about the successes and failures of previous administrations. The real challenge is what are we as going to do about the current malaise.

Jamani kushindwa au kuendelea kwa Tanzania in 1963 kusingwe sababishwa na Ujamaa au Upepari. Hizi ideology zimewekwa kwenye vichwa vyetu na wachumi waliosoma chini ya World Bank Syllabus kwamba Free market does this and Ujamaa does that. Ukweli ni kwamba in 1985 tuliachana na ujamaa na tukaanza na free market. Miaka 26 badae over 50% ya uhuru wetu tumejaribu ubepari and the results ndio hii chaos ambayo tupo leo. Nimeshaandika article nikasema Tanzania ya 1970 is better than Tanzania ya Leo. If you're using skyscrapers kama ndio kipimo cha maendeleo bali leo kweli kuna maendeleo, lakini kama unatumia economical terms ambazo zinatumiwa na wachumi basi Tanzania is in bad shape. Na tumefuata mfumo wa kambona since 1985.

We applied everything kutoka IMF and World Bank, tume devaluate currency yetu ili kuboost trade, tume adopt ERP I wakasema no hii sio sawa wakaja na ERP II ambayo wakasema hii tunaita SAP tukafuta kila walichosema, then wakaja na MDGs tukafuata kila walichosema, wakasema kwamba Tanzania ni success story, tukake even one step further tukaandika MKUKUTA which is total Garbage, na leo tumeandika mpango wa miaka mitano which is another shameful story kwa Taifa. With all this plans bado, umeme unafikia 15% ya Watanzania nao wanaumia kwa miezi saba tuu na miezi 4 hawana umeme kabisa katika mwaka. Mpaka leo kujifungua mtoto ni sawa na kamali maana hujui kama atazaliwa au laa. Mpaka leo hatuna barabara ambayo inaunganisha west to east, mpaka leo HATUJAJENGA HATA BARABARA MOJA MPYA. so, spare that argument kwamba Kambona sijui all those are just plans no one knows zingeenda vipi.

On other side Mwalimu amejaribu, I don't support motive zake nyingi lakini you can see the results. Tanzania airport, Mtera, UDSM, SUA and the list goes on and on.... While JK, MKapa and mwinyi combine labda wamejenga uwanja wa mpira na daraja la mtwara ambalo tumekopa at 20% interest. Do you know that? au mnashangilia tuu.

Na huyu raisi mpya tuliyenaye yeye anakaribisha kila mtu ikulu, kuanzia V.P wa Symbion energy mpaka mkurugenzi wa peace corp. Don't make me even go kwenye swala la Symbion maana that is dowans with approval from Hillary Clinton. Same people who managed Dowans ndio wanao manage Symbion Power.

Tanzania inatatizo la ledership na sio idea.
 
On other side Mwalimu amejaribu, I don't support motive zake nyingi lakini you can see the results. Tanzania airport, Mtera, UDSM, SUA and the list goes on and on.... While JK, MKapa and mwinyi combine labda wamejenga uwanja wa mpira na daraja la mtwara ambalo tumekopa at 20% interest. Do you know that? au mnashangilia tuu.

Naomba ufafanue mifano michache ya motives za Nyerere ambazo zinakupa shida. Maana yake ni rahisi kuhukumu vitendo vya mtu kuliko motives zake kwani motives ni masuala ya moyo wa mtu.
 
Tunashukuru Mkuu Mwanakijiji kwa hii document kwa vile itatusaidia sana kufahamu mambo mengi hasa kile ambacho mwalimu alitaka kifanyike kuendeleza nchi yetu. Wengi wetu pia tutaelewa kilichomo ndani ya hii Devplan kama tutaendelea kuichambua kama alivyofanya Mkuu Nguruvi3 kwani anaichambua kwa lugha zote kiswahili na kingereza. Keep it up!
 
Jamani kushindwa au kuendelea kwa Tanzania in 1963 kusingwe sababishwa na Ujamaa au Upepari. Hizi ideology zimewekwa kwenye vichwa vyetu na wachumi waliosoma chini ya World Bank Syllabus kwamba Free market does this and Ujamaa does that. Ukweli ni kwamba in 1985 tuliachana na ujamaa na tukaanza na free market. Miaka 26 badae over 50% ya uhuru wetu tumejaribu ubepari and the results ndio hii chaos ambayo tupo leo. Nimeshaandika article nikasema Tanzania ya 1970 is better than Tanzania ya Leo. If you're using skyscrapers kama ndio kipimo cha maendeleo bali leo kweli kuna maendeleo, lakini kama unatumia economical terms ambazo zinatumiwa na wachumi basi Tanzania is in bad shape. Na tumefuata mfumo wa kambona since 1985.

We applied everything kutoka IMF and World Bank, tume devaluate currency yetu ili kuboost trade, tume adopt ERP I wakasema no hii sio sawa wakaja na ERP II ambayo wakasema hii tunaita SAP tukafuta kila walichosema, then wakaja na MDGs tukafuata kila walichosema, wakasema kwamba Tanzania ni success story, tukake even one step further tukaandika MKUKUTA which is total Garbage, na leo tumeandika mpango wa miaka mitano which is another shameful story kwa Taifa. With all this plans bado, umeme unafikia 15% ya Watanzania nao wanaumia kwa miezi saba tuu na miezi 4 hawana umeme kabisa katika mwaka. Mpaka leo kujifungua mtoto ni sawa na kamali maana hujui kama atazaliwa au laa. Mpaka leo hatuna barabara ambayo inaunganisha west to east, mpaka leo HATUJAJENGA HATA BARABARA MOJA MPYA. so, spare that argument kwamba Kambona sijui all those are just plans no one knows zingeenda vipi.

On other side Mwalimu amejaribu, I don't support motive zake nyingi lakini you can see the results. Tanzania airport, Mtera, UDSM, SUA and the list goes on and on.... While JK, MKapa and mwinyi combine labda wamejenga uwanja wa mpira na daraja la mtwara ambalo tumekopa at 20% interest. Do you know that? au mnashangilia tuu.

Na huyu raisi mpya tuliyenaye yeye anakaribisha kila mtu ikulu, kuanzia V.P wa Symbion energy mpaka mkurugenzi wa peace corp. Don't make me even go kwenye swala la Symbion maana that is dowans with approval from Hillary Clinton. Same people who managed Dowans ndio wanao manage Symbion Power.

Tanzania inatatizo la ledership na sio idea.

I hear you Mkuu. I think we all conclude there is little progress if any since independence:

- NO Roads
- NO Schools
- NO Hospitals
- NO Electricity
- NO Running Water
- High Un-employment
- De-motivated Doctors and Teachers

And much more. Would anyone know how and where to start solving the issues mentioned?
 
I hear you Mkuu. I think we all conclude there is little progress if any since independence:

- NO Roads
- NO Schools
- NO Hospitals
- NO Electricity
- NO Running Water
- High Un-employment
- De-motivated Doctors and Teachers

And much more. Would anyone know how and where to start solving the issues mentioned?
Shukran, unajua ni Ujinga mkubwa sana kuendelea kubishana kuhusu maendeleo ikiwa nchi haina mambo hayo muhimu. Yaani tunawafanya wasomaji wengi kujiuliza upeo wa elimu zetu ktk kuelewa.
 
Tunaendelea kuichambua nyaraka na kuna wakati nanijitahidi sana kutafuta 'element' za ukabila au udini nakiri sijaziona.
Kama yupo anayeziona tufunguane macho. Kila ninachokiona kina sababu za msingi sana.

Nimejiuliza kwanini Mwanga na Same hazikuonekana sana katika mipango ya hospitali, nikapata jibu Mwanga walikuwa na hospitali ya serikali Usangi ingawa ilikuwa ndogo na hospitali za misheni nyingi kama ilivyokuwa Same. Wagonjwa wa TB walikuwa wanapelekwa ima Kibong'oto au Korogwe.

Je Muheza kwetu Bonde, nikaona walikuwa na hospitali ya Ubwari iliyojengwa na mjerumani na Hospitali ya misheni Magila ambayo ilikuwa na Specialist Surgeon Marion Butlet kuanzia 1948. Wagonjwa wa TB walipelekwa Korogwe.

Mbona Songea hakukuwa na mkakati? huko kulikuwa na Hospital ya serikali na ile ya Peramiho ambayo ina hadhi ya hospitali ya rufaa kuanzia enzi hizo hadi asubuhi hii ya leo. Nikafahamu kwanini project iliekekezwa Kilwa na Mtwara to some extent.

Urba water supply Pg 41 (ii) ....Make water more readily to poorer sections of community by extending the use of automatic kiosk on fulltime operation throughtout 24 hours
Automatic Kiosk ilikuwa 'ATM' ya maji unatumbukiza senti unapata ndoo yako. Hadi late 70's kiosk zilionekana sehemu ambazo maji yalikuwa shida. Inashangaza leo watu wanaambiwa wachimbe visima, yaani turudi nyuma!! hivi Manzese utapata mita ya ardhi kuchimba kisima?
matokeo yake ni milipuko ya maradhi na serikali kutumia fedha nyingi bila kuelewa 'prevention is better tha cure'.

TANESCO Pg 45: .....has decided not to apply for the licence and it is intended, therefore, to install a government operated supply in Tukuyu to cater for 103 quarters, flats and 4 mills.
Kwamba TANESCO ilikuwa inafanya kazi independently na pale ilipokuwa haina pesa basi serikali iliingilia kati kutoa umeme kama tunavyoona pia kule Musom n.k Hapa ndipo unaona serikali ilivyokuwa inajali, mfano mzuri ni wa Tukuyu.
Tanesco haikuwa na tatizo la kutoa umeme hadi 1996(Makamba Jr) amethibitisha leo. Sasa haya ya mgao yanaponasibishwa na ujamaa au kufeli kwa mwalimu, kama si chuki za kukalihwa darasani ni nini?

Cooperative college pg 63: 2. .......At present students from Tanganyika are sent to cooperative college Loughborough England. ......proposed similar college to be established in Tanganyika.
Kiongozi yeyeto mwenye elimu ya cooperative alipelekwa kusoma nje kwa mpango huu. Ama chuo cha Ushirika kilipokamilika kikaanza kutoa wataalam tena katika hadhi ya Loughborough kwa kutambuliwa. Chuo hicho ndicho kimegeuzwa kuwa chuo kikuu cha ushirika Moshi(Mucco ??). Wanapobadili majina wanasema wamejenga halafu wanamtupia Nyerere lawama kafeli.

Trade Representative Abroad pg 77: .......office accomodation and equipment for trade representative
Hapa tunaona mpango mzima ulikuwa unaandaa ofisi za trade representative katika nchi za nje.
Alipokuja mkapa akasema siasa yetu ya nje ni ya 'diplomasia ya uchumi' watu tukaona ni jambo geni wakati mwalimu si kuwa aliwatumia mabalozi tu bali alikuwa na trade representative pekee.
Wanachokifanya akina JK na BWM ni kubadili maneno lakini concept nzima ilikuwa ya Nyerere.
Nani amefli wao wanao kopi au aliyebuni?

Education pg 85:1 .......Degree course in law will start in temporary accomodation in Dar es salaam in 1961.
Hatukuwa na hata university college, chuo klikuwa Makerere college.
Hiyo temporary accomodation ilikuwa katika jengo la SUKITA Mzee Warioba anajua nini kilikuwemo humo. Ni kwa sababu ya msingi mzuri wa chuo hadi leo sifa moja ya UDSM ni kutoa wanasheria walioiva vema (sijui miaka ya karibuni).
Kama wewe ni mtu wa UDSM basi elewa faculty of law (school of law) ndio 'school mama'a chuo.
Kuna majaji wakuu wa nchi 4 za Afrika mashariki ambao ni wahitimu akiwemo yule wa Kenya Kivuitu. Lazima tukumbuke kwenye msafara wa mamba kenge wamo pia. Mbona hatumsusii Chenge.

Community center pg 95:
Nikikumbuka machozi yananitoka. Kwa wale wa enzi hizo mnakumbuka mahali palipokuwa panaitwa ' olfea' (welfare). Hata wilayani zilikuwepo, leo hata jiji la DSM halina community center, kama zipo ni zile alizojenga Mwalimu. Nchi za wenzetu bado ni kitu muhimu sisi tukitaka kukutana na madiwani basi tunakodi ukumbi wa baa, mungu jalia ukuta usijeanguka!
Bado hatufikiri haya tumejikita kumtafutia Nyerere sababu.

Ukweli kwa kile alichoshindwa usemwe kama ukweli kwa alichoshinda, inasikitisha hata yale mema tumeamua kuweka tongo tongo mchana ili tu tupate mahali pa kumchafua. Yaani si kwa mabaya yake bali dhamira na chuki, tena chuki za kufundishwa.

Bahati mbaya walimu wa chuki hizi ni wasomi wazuri sana na wanatumia usomi wao kuwapumbuza watu ima wauze vitabu au nyaraka zao wakificha ukweli tena nyuma ya mgongo wa ukabila na dini.

Wamewafundisha hadi mmoja wa wana JF ameandika thread kwa kujiamini kabisa baada ya kufuzu somo la chuki ikisema ' Nyerere aling'oa reli ya Mtwara- Dar'!!!!!!!!! kwamba chuki imechukua nafasi ya kufikiri bila hata kujiuliza ilikatiza daraja gani la Rufiji endapo lililopo lina miaka 10?

Ndiyo maana nasema nyaraka hii hapa ambayo inaonyesha dhamira ya Nyerere kwa wema au uovu, basi tuichambue na kufahamishana.
 
Mgodi mkubwa kabisa wa Almasi kule mwadui hivi unamilikiwa na nani na Tanzania inamiliki asilimia ngapi za mapato yote nasiki 25% tuliutaifisha ukatushinda, kisha ukarudishwa kwa wenyewe.

Tulitaifisha na tukawa tunawauzia hao hao tulio wanyanganya (Nadhani tulitaifisha management tu).

Tumbaku, tulikuwa tukiwauzia Afrika kusini na Zimbambwe na tukiagiza Landrover kutoka kwao, upande wa pili akiwasema kuwa ni makaburu.

Makabila 120 ya Tanganyika Nyerere akuyaunganisha, Nyerere alikuta tayari tuna utamaduni wa kutembeleana na kuchangayika, tofauti na nchi zenye makabila machache, uko kenya, Rwanda, burundi na Uganda yanawashinda kwa sababu makabila makubwa yapo machache na inakuwa rahisi kwa kabila moja kutawala nchi, sasa kwa nchi kama tanzania ni kabila gani lenye uwezo wa kupata kura za kuongoza nchi?
X-Paster,
Hata Wakenya walikuwa wakitembeleana na kuchanganyika. Lakini ni siasa za Kenyatta za ukabila zilizoleta mtafaruku na utengamano ambao matokeo yake tuliyaona 2007. Nyerere alisaidia kujenga umoja wetu kupitia harakati za TANU, lugha ya Kiswahili na Azimio la Arusha. Huo ni ukweli usiopingika.
PS. Tulikuwa tunauza tumbaku na mbao Afrika kusini. Lakini Mwalimu alisitisha biashara na utawala wa Makaburu mwaka 1962.
 
Nguvuri, aisee umenikumbusha mbali sana kwenye hizi Community Centers.. zilikuwa nyingi sana, ndio maeneo bendi mbalimbali zikija kule wilayani zilikuwa zikipiga, I still remember matangao ya kuja kwa DDC Kibisa, enzi za kina Bandari Theater Group n.k wengine tulichezaga sarakasi pale Makorola (Makorola Dancing Troupe) duh!!
 
Nguvuri, aisee umenikumbusha mbali sana kwenye hizi Community Centers.. zilikuwa nyingi sana, ndio maeneo bendi mbalimbali zikija kule wilayani zilikuwa zikipiga, I still remember matangao ya kuja kwa DDC Kibisa, enzi za kina Bandari Theater Group n.k wengine tulichezaga sarakasi pale Makorola (Makorola Dancing Troupe) duh!!

Ukisikia mikutano ya wazazi ni 'olfea', bendi madisco ya space 1900 ni huko. Yaani ukipita community center ni shughuli tu zinaendelea.
Siku hizi nyingi zimegeuzwa ofisi zingine hatujui wanakaa akina nani, atashangaa mzee anakitambi anaingia na kutoka humjui.
Hao DDC wakiingia ndani ya muji wana bus lao mkitaka kuwaona akina Reheani, Bitchuka n.k lazima muwahi community center.
Acha tu!
 
Back
Top Bottom