Jambo Usilolijua: Nyerere alipokea Taifa la namna gani? Mpango wa Kwanza wa Maendeleo 1961

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
JFKPOF-124-013-p0089.jpg

Mojawapo ya hoja ambazo hatuzikii mara nyingi kwa wale ambao wanambebesha Nyerere lawama na mzigo wa taifa letu kuwa ni yeye ndiye aliyelivuruga ni kuwa Nyerere alipokea taifa lenye hali gani ile Disemba 9, 1961. Tunapoelekea miaka hamsini ya Uhuru wa Tanzania bara na hasa baada ya kupitishwa kwa mpango wa "nane" wa maendeleo chini ya serikali ya CCM ni vizuri kurudi nyuma kabisa tuone tulipoanzia.

Wiki iliyopita niliwaletea sehemu tu ya mapokezi ya Rais Nyerere Ikulu ya Marekani wakati huo chini ya Rais J. F. Kennedy. Mkutano wao ulikuwa ni mwaka 1963. Hata hivyo kabla ya hapo viongozi hao wawili walikuwa na mawasiliano ya karibu sana. Kuelekea Uhuru serikali chini ya Nyerere ilikaa na kuandaa mpango wa miaka mitatu (ambao ndio mpango wa kwanza wa maendeleo) wa taifa huru. Mpango huu ulikuwa na mambo mengi na ulikuwa na lengo moja tu nalo ni kujaribu kuleta taifa hilo changa katika karne ya ishirini.

Uzuri wa mpango huu unatupa mwanga wa hali ilikuwaje 1961 katika Tanganyika na mzigo mkubwa ambao Nyerere alibebeshwa na wananchi wenzake. Tunapojaribu kumhukumu leo hii kuwa aliiacha nchi katika "hali mbaya" - kitu ambacho si cha kweli - ni lazima tujaribu kujibu swali pia nchi aliyoipokea ilikuwaje? Changamoto za taifa changa hilo ilikuwaje (wengine wanafikiria hali ilivyokuwa Dar ndivyo ilivyokuwa mikoani). Hivyo kwa kupitia mpango huu utaweza kupata mwanga kidogo wa hali yetu ya kiuchumi ilikuwaje, kijiografia ilikuwaje na raslimali watu ilikuwaje.

Ukishapitia mpango huu swali moja ni LAZIMA ujiulize: Watendaji wa kutekeleza mpango huu walikuwa watoke wapi? Na je walikuwepo?

Wiki ijayo, inshallah tutaangalia nyaraka za CIA kuhusu Nyerere. Yote hii ni katika kuelekea kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika. Please do Enjoy. Kama umepitia mpango "wao" wa maendeleo wa miaka mitano unaweza kulinganisha kitu ambacho naweza kukiita 'motivation' ya mipango hii miwili ni nini. Only then you'll glance (like from a far) the thinking and making of a great leader. Kumbuka hakukuwa na MKUKUTA wala MKURABITA kabla yake.

NB:
1. Nashauri uongeze ukubwa wa PDF wakati unaangalia kwa karibu 700% kuweza kusoma vizuri.
2. Mistari iliyopigwa kwenye kijitabu hiki ni reaction ya serikali ya Marekani walipopitia mpango huu.
 

Attachments

  • TanganyikaDEVPLAN1961.pdf
    7 MB · Views: 776
Mzee mwanakijiji nakupongeza sana kwa taarifa zako nzuri. Wewe ni mzalendo na mpenda nchi.....
 
Kitila Mkumbo ibebe hii maana nyaraka nyingine ktk maktaba yetu ya Mlimani hazipatikani. Ukizingatia wewe ni mwalimu...au uliishaacha. Nakuaminia rais wangu miaka ile.. UDSM ikiwa UDSM kweli
 
View attachment 32526

Mojawapo ya hoja ambazo hatuzikii mara nyingi kwa wale ambao wanambebesha Nyerere lawama na mzigo wa taifa letu kuwa ni yeye ndiye aliyelivuruga ni kuwa Nyerere alipokea taifa lenye hali gani ile Disemba 9, 1961. Tunapoelekea miaka hamsini ya Uhuru wa Tanzania bara na hasa baada ya kupitishwa kwa mpango wa "nane" wa maendeleo chini ya serikali ya CCM ni vizuri kurudi nyuma kabisa tuone tulipoanzia.

Wiki iliyopita niliwaletea sehemu tu ya mapokezi ya Rais Nyerere Ikulu ya Marekani wakati huo chini ya Rais J. F. Kennedy. Mkutano wao ulikuwa ni mwaka 1963. Hata hivyo kabla ya hapo viongozi hao wawili walikuwa na mawasiliano ya karibu sana. Kuelekea Uhuru serikali chini ya Nyerere ilikaa na kuandaa mpango wa miaka mitatu (ambao ndio mpango wa kwanza wa maendeleo) wa taifa huru. Mpango huu ulikuwa na mambo mengi na ulikuwa na lengo moja tu nalo ni kujaribu kuleta taifa hilo changa katika karne ya ishirini.

Uzuri wa mpango huu unatupa mwanga wa hali ilikuwaje 1961 katika Tanganyika na mzigo mkubwa ambao Nyerere alibebeshwa na wananchi wenzake. Tunapojaribu kumhukumu leo hii kuwa aliiacha nchi katika "hali mbaya" - kitu ambacho si cha kweli - ni lazima tujaribu kujibu swali pia nchi aliyoipokea ilikuwaje? Changamoto za taifa changa hilo ilikuwaje (wengine wanafikiria hali ilivyokuwa Dar ndivyo ilivyokuwa mikoani). Hivyo kwa kupitia mpango huu utaweza kupata mwanga kidogo wa hali yetu ya kiuchumi ilikuwaje, kijiografia ilikuwaje na raslimali watu ilikuwaje.


Ukishapitia mpango huu swali moja ni LAZIMA ujiulize: Watendaji wa kutekeleza mpango huu walikuwa watoke wapi? Na je walikuwepo?

Wiki ijayo, inshallah tutaangalia nyaraka za CIA kuhusu Nyerere. Yote hii ni katika kuelekea kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika. Please do Enjoy. Kama umepitia mpango "wao" wa maendeleo wa miaka mitano unaweza kulinganisha kitu ambacho naweza kukiita 'motivation' ya mipango hii miwili ni nini. Only then you'll glance (like from a far) the thinking and making of a great leader. Kumbuka hakukuwa na MKUKUTA wala MKURABITA kabla yake.

NB: Nashauri uongeze ukubwa wa PDF wakati unaangalia kwa karibu 700% kuweza kusoma vizuri.


Nyerere alikuwa na muda kuchange plan zote za economic, pale tu alipoona hazina maendeleo na Taifa. Kwa mfano, plan yake ya agriculture ilkuwa ni kuwahamisha Wananchi kwa nguvu, na kuwapeleka vijijini bila ya mpango maalum wa maendeleo. Utalima vipi wakati huna maji? nyenzo muhimu za kilimo, nk.

Pili, huwezi kusema kama Nyerere libebeshwa mzingo mkubwa wakati ni yeye mwenyewe Nyerere ndiyo alikuwa anataka kuimplement kila law ya nchi. Viongozi wengine hawakuweza kuinput chochote kwa Nyerere, kutokana na ubabe aliokuwa nao.
 
Nyerere alikuwa na muda kuchange plan zote za economic, pale tu alipoona hazina maendeleo na Taifa. Kwa mfano, plan yake ya agriculture ilkuwa ni kuwahamisha Wananchi kwa nguvu, na kuwapeleka vijijini bila ya mpango maalum wa maendeleo. Utalima vipi wakati huna maji? nyenzo muhimu za kilimo, nk.

Pili, huwezi kusema kama Nyerere libebeshwa mzingo mkubwa wakati ni yeye mwenyewe Nyerere ndiyo alikuwa anataka kuimplement kila law ya nchi. Viongozi wengine hawakuweza kuinput chochote kwa Nyerere, kutokana na ubabe aliokuwa nao.

bonge la point, incredibly so deep. Kudos.
 
View attachment 32526

Mojawapo ya hoja ambazo hatuzikii mara nyingi kwa wale ambao wanambebesha Nyerere lawama na mzigo wa taifa letu kuwa ni yeye ndiye aliyelivuruga ni kuwa Nyerere alipokea taifa lenye hali gani ile Disemba 9, 1961. Tunapoelekea miaka hamsini ya Uhuru wa Tanzania bara na hasa baada ya kupitishwa kwa mpango wa "nane" wa maendeleo chini ya serikali ya CCM ni vizuri kurudi nyuma kabisa tuone tulipoanzia.

Wiki iliyopita niliwaletea sehemu tu ya mapokezi ya Rais Nyerere Ikulu ya Marekani wakati huo chini ya Rais J. F. Kennedy. Mkutano wao ulikuwa ni mwaka 1963. Hata hivyo kabla ya hapo viongozi hao wawili walikuwa na mawasiliano ya karibu sana. Kuelekea Uhuru serikali chini ya Nyerere ilikaa na kuandaa mpango wa miaka mitatu (ambao ndio mpango wa kwanza wa maendeleo) wa taifa huru. Mpango huu ulikuwa na mambo mengi na ulikuwa na lengo moja tu nalo ni kujaribu kuleta taifa hilo changa katika karne ya ishirini.

Uzuri wa mpango huu unatupa mwanga wa hali ilikuwaje 1961 katika Tanganyika na mzigo mkubwa ambao Nyerere alibebeshwa na wananchi wenzake. Tunapojaribu kumhukumu leo hii kuwa aliiacha nchi katika "hali mbaya" - kitu ambacho si cha kweli - ni lazima tujaribu kujibu swali pia nchi aliyoipokea ilikuwaje? Changamoto za taifa changa hilo ilikuwaje (wengine wanafikiria hali ilivyokuwa Dar ndivyo ilivyokuwa mikoani). Hivyo kwa kupitia mpango huu utaweza kupata mwanga kidogo wa hali yetu ya kiuchumi ilikuwaje, kijiografia ilikuwaje na raslimali watu ilikuwaje.

Ukishapitia mpango huu swali moja ni LAZIMA ujiulize: Watendaji wa kutekeleza mpango huu walikuwa watoke wapi? Na je walikuwepo?

Wiki ijayo, inshallah tutaangalia nyaraka za CIA kuhusu Nyerere. Yote hii ni katika kuelekea kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika. Please do Enjoy. Kama umepitia mpango "wao" wa maendeleo wa miaka mitano unaweza kulinganisha kitu ambacho naweza kukiita 'motivation' ya mipango hii miwili ni nini. Only then you'll glance (like from a far) the thinking and making of a great leader. Kumbuka hakukuwa na MKUKUTA wala MKURABITA kabla yake.

NB:
1. Nashauri uongeze ukubwa wa PDF wakati unaangalia kwa karibu 700% kuweza kusoma vizuri.
2. Mistari iliyopigwa kwenye kijitabu hiki ni reaction ya serikali ya Marekani walipopitia mpango huu.


Rick-Ross-psd35691.png



My Name is Rick Ross n I approve the above post
 
Wakati huo Paundi moja ilikuwa TSH. 20! mmh kazi kwelikweli
Hali hiyo ingekuwa leo wabongo tungekuwa mbali. Vile vita vya kumuondoa Iddi amini vimeturudisha nyuma sana hata huwa nazaniaga kunamabepari walifurahi tulivyo poromoka….
 
Duh! nimesoma mpaka nimetikisa kichwa ina maana barabara nyingi possibly more than 95% za changarawe kupita tarafa na tarafa mpaka kijiji na kijiji hazikuwepo before 1961. Mpaka the famous Tanzam highway ilikuwa lami mpaka Morogoro tu! kweli tumetoka mbali.
 
In the other hand naanza kuamini amini kwamba kifo cha Keneddy JF kiliathiri kiasi flani uelekeo wa taifa letu! I got this from some very old man anayeamini kwamba JFK asingekufa very likely Nyerere asingeenda kwenye ile direction ya ujamaa. Maana JFK ndiye alikuwa kiasi flani adviser wa Mwalimu and they used to admire each other so much.
 
Mpango wa miaka mitano wa nyerere ulikua mzuri tu lakin sasa ndio hivyo hatukua na wasomi wa kutosha.....
 
Nimeuprinti nikausome kwa kina baadaye...halafu niwape na mabinti zangu nao wausome........ watamjua Nyerere vizuri... RIP JKN!
 
Mwanakijiji ahsante sana kwa hii nyaraka, tutaimega kidogo kidogo ili twende sambamba sote. Mambo ni mazito na hayawezekani kuchambuliwa mara moja na wale wanaomtuhumu Mzee wa watu wakawa on the same page.

Dalili za jinsi alivyoichukua nchi.
Page 8 paragraph 1 and 2: '' ........... there is a most pressing need to provide cadres of trained people necessary for technical, clerical and skilled work both in government and in the private sector''
Pg 16: '............purchase of photographic and projection equipments and .........modern printing equipment"
Kwamba nchi wakati huo ilikuwa inahitaji technical staff na clerical na sio professionals kwa sababu hata hao hawakupatikana.

Page 8 paragraph 3: ".............. short term will be that of laying foundation growth of output and incomes rather than immediate increase......'
Tumeeleza katika mijadala mbali mbali kuwa kazi ya Nyerere hatuwezi kuifananisha na waliofuata kwasababu yeye alikuwa ana 'lay foundation"

Hoja inaungwa mkono zaidi na Paragraph 4 ya ukurasa huo huo:
''It must not be forgotten that a large proportion of the expenditure is being devoted to training and to the provision of institutions necessary.................The economic effect of the former will be felt in the long run and in the case of the later it will be indirect or relatively small'

Page 7 last paragraph:
"The devolpment of communication and in particular feeder roads in rural areas"
Pg13 last paragraph: "The size of feeder road programme is limited by number of surveyors available, a factor not affecting the main trunk road programme which will be carried out by contractors"

Katika viongozi waliofuata nani alianza na technical staff? Leo kuna professionals wangapi?
Kiongozi gani anajenga training institutions for technical cadres ukiacha alizojenga Nyerere
Kiongozi gani anajenga feeder road sasa kama zilishajengwa na Nyerere?
Angalia mgawanyo wa rasilimali kidogo ulivyozingatia umuhimu wa ujenzi wa bara bara.

Tuendelee kuchambua
 
In the other hand naanza kuamini amini kwamba kifo cha Keneddy JF kiliathiri kiasi flani uelekeo wa taifa letu! I got this from some very old man anayeamini kwamba JFK asingekufa very likely Nyerere asingeenda kwenye ile direction ya ujamaa. Maana JFK ndiye alikuwa kiasi flani adviser wa Mwalimu and they used to admire each other so much.
Hawatakawia kukwambia walikuwa karibu kwa sababu ya UKATOLIKI wao. Maadui wa Mwalimu tuko wengi.
 
Back
Top Bottom