Bramo
JF-Expert Member
- Oct 21, 2009
- 13,250
- 10,233
Mwandishi wa Mwananchi alifika katika Hospitali ya Ubalozi Medical Clinic iliyopo mita 200 kutoka vilipo viwanja vya Leaders na kukutana na Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Dk Aneth Rwebembela ambaye alisema hakuna mgonjwa aliwalalamikia wala kuzimia kutokana na muziki.Kweli ule msemo kuwa ukimchekea sana mbwa atakufuata msikitini nimeuelewa.
Nakumbuka mwaka Jana au juzi kiongozi wetu wa nchi alielezea suala la Tigo fiesta kwa wananchi kwamba ni ubunifu mzuri wa ajira na akawasifu sana Clouds.
Ilifika hata akatangaza kuwaongezea muda wa onyesho. Jee wakati huo hakukuwa na wagonjwa?
Leo hii RC wa Dar kwanza kawatia moyo CMG na Tigo kuwa hii itakuwa kubwa kuliko na watu waka invest vya kutosha fedha nyingi, lakini Makonda na uongozi wake wa Dar walikuwa wanajua nini wamepanga. 24 hours before event wakawaonyesha kuwa wao ndio wababe wa Jiji hata kama Rais aliwahi kutamka kuwa shughuli hizo ni nzuri na halali, nani kama Paul Makonda Dar es salaam?
Mheshimiwa Rais, hizi aibu unazopewa na huyu kijana wako utazifumbia macho hadi lini? Visasi vyake na hao Clouds sii ulishawashikisha mikono Tanga mbona sasa anatumia ofisi kuendeleza ubabe?
Kumbuka huo msemo wa waswahili kuhusu muislamu na mbwa wake!
Tamasha la Fiesta laacha simanzi, maswali lukuki