Jamani wanaume wasomi mna nini?

Jamani wanaume wasomi mna nini?

Queen Horse umenipasua pwaaaaa......

Kumbe rafiki yako kaja kukuambia yoote? Leo atanitambua na tabia yake ya kuanika mambo ya ndani..... Hivi vyuo vya katavinatuharibia wanawake..

Ulitegemea asiniambie wakati humpi nafasi ya kukwambia yanayomsibu.. Nadhan ujumbe umefika badilika dikembe
 
Last edited by a moderator:
Nakwambia acha bibie mpaka kaloose weight chezea manyanyaso ya kauli wewe.. Anakula vizuri, analala vizuri, usafiri upo ila akimfikiria mumewe nguvu zinaishaa anakosa hata amani ya kumwambia mambo yanayomuhusu
Atakuja kufarijiwa na mchepuko soon
 
inferiority complex hata angekuwa mwanamme wa elimu ya kawaida engemchenjia
 
huyo msomi ndani ya wiki 563 atakuwa amefilisika, usijali shosti wangu.
 
Waliosoma sana kwenye mahusiano ni zero. Halafu mara nyingi wanaamini wewe ndio unatakiwa kujikomba kwao. Yaani kuwa na wewe ni kama amekupa msaada. Ni sheeeeda hao watu.
 
Mwidiwee.. Namahorooo wana JF
Bado Niko najiuliza maswali juu ya wanaume wasomi hasa hasa kuanzia level ya masters, PhD hadi kule kwenye ukuta ulioandikwa elimu tena basi kwanini wengi wao wanakuwa wanatabia ya kupenda kuwadharau wake zao hasa ukikuta wamewapita kiwango cha elimu mfano mke ana diploma yake ya ualimu au digrii yake ya course ya kuchechemea.

Naongea hivi kwa experience kwa sababu nimekutana na kesi kama tatu zenye kufanana lakini hii ya nne too much.
Haya yamemkuta shosty wangu mmoja hivi mwenye degree yake ya sociology na GPA ya kuchechemea na mchuchu wake mwenye PHD ya mambo ya planning.

Sikutaka kuchukua details nyingi kwa sababu elimu yake hainisaidii wala kuniletea hela ya ugali
Back to the topic, shosty kipindi kabla hajaolewa mapenzi yamechanua kama maua ya saa nne alikuwa anajisifia kweli na mchuchu wake mara wanaume waliosoma sana waelewa sana, Mara mimi degree holder wenzangu nimpeleke wapi.

Maneno kibao kudharau waume za wenzie na kujifanya wa kwake ndio bora sana kama tunavyojua masikini akipata masaburi hulia mbwata, sie tena wenye vicertificate holder vyetu tukawa tuna zip our mouth shut tunajipa moyo maisha hayapimwi kwa wingi Wa makaratasi ya vyeti.

Basi bwana Shoga yule mwaka juzi kaolewa kwa shangwe na vigelele na sisi mashabiki kama kawa tupo mbele kumpa kampani, ndoa sasa ina miaka mitatu ndo anaona chungu ya ndoa mkaka kawa na dharau kila analoliongea mkewe sharti liwe prove intelectually with high thinking capacity, akikosea kidogo matusi najuta kukuoa kilaza mkubwa wewe degree yenyewe umeipata kwa bahati, mara mimi siwezi kukaa na kujadili maisha na watu ambao sio ma critical thinker, mara sasa utanishauri nini wewe na akili yako ndogo na maneno mengine ya maudhi.

Sasa juzi ndo ilikuwa komesha shoga kaingiza loss katika biashara ya familia ambayo mkaguzi ni Mr.

Alioona junijulai alitukanwa mpaka aliiona ardhi ngumu kuikanyaga kupooza machungu kabaki anatupigia simu mashoga zake kutupa mkasa na maneno ya najuuta kibao nikamwambia shoga vumilia ndo ndoa ilivyo vumilianeni kila mtu ana kasoro zake.

Back to my question: kwani mahusiano yanahitaji akili ya kukariri vitabu?

Kama mnaona vitabu ni mali si mngekaa single mkaendelea kukariri.

Najua wengi mko humu wenye hizo tabia acheni dharau ishini na familia zetu kwa amani, kama mkeo ana weakness mu encourage aweze vile unavyotaka kumnyanyasa kisaikolojia sio vizuri.

Unasababishia makovu moyoni ambayo inawezekana hata we huyajui.

dah, umezunguka-zunguka weeee, kumbe hata paragraph moja ingefikisha ujumbe

nice try, ukikazana hivi miezi 24 utaweza kuandika hadithi fupi

swali: sasa wanaume wasomi wasipokua arrogant nani awe hivyo?? umesahau tuna division of labor na arrogant nayo kazi?
 
sa kama amekosea asiambiwe, umeleta hasara kwenye biashara unataka nikubembeleze tena.... hiyo kitu haipo, tusipokuwa wakali mtatupanda kichwani, lazima upige biti ata kidogo!!! Ilitakiwa ampe na vibao hata viwili kabisa sio maneno matupu

Tatizo siyo kumkosoa mtu, issue ni namna unavyomkosoa. Iko njia ya kuzungumza na mwenzi wako, siyo kukoroma as if unaongea na mtoto wako. Huyo bwana anajidanganya tu kwa sababu kama kusoma ingelikuwa ndo kuyapatia maisha, basi professors wengelikuwa millionare. Lakini tunao huku kitaa na kila siku wanatupinga mizinga tu.
 
Aise mpe pole sana, kuna watu wapo hivyo, ni selfish na insecure, yaani ni mtu kasoma lkn ana low self esteem kwa hiyo ili ajiskie vizuri na kujiamini lazima atafute mtu wa kumput dowm sasa yeye kaona ni mke, na watu wa mimi, mimi, mimi, hawafanyi effort yeyote kusaidi wanaonaga matatizo yapo kwa mtu mwingine, hata kitandani wakiunder perform ni rahisi kusema mwanamke ndo anasababisha ila wao hawana kasoro..
Ni kweli kabisa nimeshuhudia hii kitu. Alafu mtu wa namna hii si kwa mkewe tu ila mkewe ndio anakua mhanga namba moja. Na mtu wa namna hii kila kosa hata la kibinadamu ambalo naye humtokea huwaona wengine wajina ila akifanya yeye atalaumu mwingine sababu yeye hawezi kukosea. Na hata siku moja hawezi kuwa na kasoro kwamba inabidi ajirekebishe hapana, wengine ndio inabidi wajirekebishe na wengine ndio wanamuhitaji hata mkewe yeye hana shida nao. Ila malezi pia huchangia, na umasikini sababu mwengine si msomi ila ametokea kwenye ufukara lakini akafanikiwa alafu aoe mke aliyetoka tu hata familia ya kawaida basi atamnyanyasa mpaka basi. Kikubwa wanawake tuchunguze kabla ya kuingia ndoani, na mtu anayekudharau na kukuabuse kwa maneno au vipigo kamwe hawezi badilika hivyo ukiona dalili hizi ni vema kusonga mbele unaweza kuumizwa mpaka ukajiua kwa depression.
 
Mtasingizia na jirani zangu bure lkn tatizo ni huyo dada.........
Kuleta loss isiyo na maelezo ni sawa na kuukaribisha umaskini ktk familia!!!!!!!! hii ni inatokana na kutoa hela za biashara kufanyia mambo binafsi
 
Sio suala la 'usomi', kuna baadhi tumeumbwa kama perfectionists and we get upset (or well, bitter) when someone does n't understand & follow simple facts..pengine bahati mbaya 'wasomi' wengi wanaangukia hapo. Mfano, majuzikati nilikua nasafiri na mwenzangu mmoja, nikamwambia safari ni ndefu tugawane hizo kilomita at least 150-150 ili tusichoke na kueza kufuata vyema alama za barabarani...jamaa akakomaa eti aendeshe yeye akivuta distance alafu eti zitakazobakia aniachie, ajafika mbali kapigwa bao na trafiki kwa kuovateki sehemu isio na kuzidisha spidi ya 50, alafu mmlipaji rushwa ni mimi.. niliboreka lakini, sometimes perfectionists are tired of being right quietly and all the time. so u may find some of them speaking their minds loudly!
Ushauri:Kimsingi mtu mwene umakini mdogo aolewe na mwene umakini mdogo mwenzake ili kupunguza threads kama hizi JF.
 
Pia kuna another possibility. Kuna watu wana inferirity complex. Unaweza ukawa hujamtakia neno lolote baya. Mfano unapingana tu na kitu fulani. Sababu ana inferiity complex anaanza kusema unanipinga sababu sijasoma au sababu wewe umesoma sana. Yaani huwa inakuwaga hivyo soemtimes. Au chochote utachosema anakuwa offended.
 
Yaani kama uliingia mdomoni kwa huyo mkaka uka copy na kupaste.... Yaan anajiona yeye ndo muhimili wa Shoga angu mie bila yeye nyumba itaanguka.. Inafika stage anamwambia shukuru mungu umezaa na intellect kizazi chako kitakuwa na watoto wanaojielewaa ungezaa na vilaza wenzio ungetoa waokota makopo.. Mmh kweli is it fair??

Duh, this is too much aisee!
 
Naomba sana yasimkute dada,ndugu au rafiki
yangu duh......
 
huyo mwenzio yamemkuta kama malipo ya kujidai na kuwadharau wenzake.. wacha apate tamu yake.
 
Ni kweli kabisa nimeshuhudia hii kitu. Alafu mtu wa namna hii si kwa mkewe tu ila mkewe ndio anakua mhanga namba moja. Na mtu wa namna hii kila kosa hata la kibinadamu ambalo naye humtokea huwaona wengine wajina ila akifanya yeye atalaumu mwingine sababu yeye hawezi kukosea. Na hata siku moja hawezi kuwa na kasoro kwamba inabidi ajirekebishe hapana, wengine ndio inabidi wajirekebishe na wengine ndio wanamuhitaji hata mkewe yeye hana shida nao. Ila malezi pia huchangia, na umasikini sababu mwengine si msomi ila ametokea kwenye ufukara lakini akafanikiwa alafu aoe mke aliyetoka tu hata familia ya kawaida basi atamnyanyasa mpaka basi. Kikubwa wanawake tuchunguze kabla ya kuingia ndoani, na mtu anayekudharau na kukuabuse kwa maneno au vipigo kamwe hawezi badilika hivyo ukiona dalili hizi ni vema kusonga mbele unaweza kuumizwa mpaka ukajiua kwa depression.

umeongea yote kabisa, sema wakina dada na mapenzi inakuwa shida, mtu anakuja stuka kasha chaka, dalili ya kwanza kabisa ya watu wa aina hii ni maneno hasa ya kuabuse, wakati wa kudate inatakiwa mwanamke akiona hiyo akimbie vibaya mno
 
Mtasingizia na jirani zangu bure lkn tatizo ni huyo dada.........
Kuleta loss isiyo na maelezo ni sawa na kuukaribisha umaskini ktk familia!!!!!!!! hii ni inatokana na kutoa hela za biashara kufanyia mambo binafsi

Unajua sisi watanzania wengi, tumelelewa kwa kusolve matattizo either kwa kulalamika, KULAUMU, kushout au kupigana..tunakuwa watu ambao tunaona matatizo hasa ya kawaida kama mwisho wa kila kitu, yaani unaweza kukuta mtu na mkewe, mke anafanya makosaa ya kawaida(si makosa makubwa kama kuchepuka) ya kawaida tu lakini badala ya kukaa chini kutafuta solution mtu anapanick atamtukania mama yake, atamuita kilaza, mshenzi, ni ile tu sisi wabongo hatuna utamaduni wa kukabili matatizo strategically na kusolve rather than kulalamika na kulaumu....vitu kama hasara vipo...watu wanafilisika mabilioni bana na wanarudi ndo iwe hasara ngapi sijui....
 
Back
Top Bottom