Jamani nimetapeliwa

Jamani nimetapeliwa

Mbona umeibiwa kirahisi sana, mnapaswa kushirikisha watu wa karibu unapoona jambo ambalo halipo sawa. Sio kufanya maamuzi kimya kimya.
 
Siku za karibuni wadada wengi wa kibongo wamepigwa na matapeli wanaoshirikiana na wazungu au wanaigiza wazungu.
Wanaanzisha urafiki kwenye mitandao kisha whatsapp unamuona kabisa.

Mdada anaongopewa kapendwa na mzungu anataka amuoe.
Anamwambia kamtumia zawadi kama mleta mada, kisha anaambiwa mzigo upo Zanzibar au mbali na mji wa mtapeliwa, anaambiwa alipie pesa za kuondoa mzigo na kodi kisha aende akachukue mzigo.

Wadada kwa tamaa wanawaonesha wenzao wamepata mchumba mzungum na picha za zawadi.
Pesa ya kulipia mzigo wanakopa madeni makubwa na kuuza vitu. Mwisho aibu kubwa huko ugenini Zanzibar wanapojikuta wamepigwa, hawana nauli ya kurudia wala mahali pa kuishi.

Jamaa yangu kawasaidia wadada watatu siku kama 7 zilizopita.
Kwa jinsi utapeli ulivyotamalaki usishangae hao wadada watatu unaowasema ndiyo wamemtapeli huo jamaa yako kwa kusingizia kwamba wametapeliwa na hivyo kujifanya kuomba msaada kwake!
 
unapungukiwa sifa za kuwa member wa JF,unapeliwaje kishamba pa1 na kupata exposure humu JF
 
Kwa jinsi utapeli ulivyotamalaki usishangae hao wadada watatu unaowasema ndiyo wamemtapeli huo jamaa yako kwa kusingizia kwamba wametapeliwa na hivyo kujifanya kuomba msaada kwake!
Nakuhakikishia walitapeliwa, na wao sio wa kwanza.
Hali ni mbaya sana kwa sasa.
 
Kamanda yaani ukishasikia mtu anakwambia mambo ya UN ujue ni utapeli . UN haifanyi kazi hivyo na pia issue ya mizigo hutanguliwa na documents za mzigo na si vinginevyo . Nakupongeza kwa ujasiri wa kusema ukweli na kukubali kukosea .Next time ukipata issue kama hiyo tafuta ushauri kwa mamlaka husika .
hapo ndo sikuwa makini nilitakiwa nijiridhishe kwanza haswa kwa mtu ambaye simjui

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kama unaishi dunia ya 3 wewe bado ni mgeni wakila kitu maana huko dunia ya 1utapeli huu n levek ya chini sana
Dunia ya sasa unatapeliwa kijinga hivyo?

U need a time to learn about this world unaonekana umgeni wa dunia ya sasa hata washauri huna..
 
Mwanangu Kangungo,

Alipata dili la kupiga mpunga mrefu ndani ya 24 hours akafanya siri..

Na yeye Akazuliwa gharama za kufaulisha mzigo kedekede kama mtoa mada hapa.

Hela yenyewe ya kufaulisha mzigo alikuwa hana..

Ila kwa sbb dili lilimtoa mate, anaona kabisa ukwasi huu hapa tena within 24 hours.. 😂😂😂

Akasema usinitanie weeh..!

Akawachek wadau kadhaa fasta wamkopeshe kwa ahadi ya kuwapa riba ya maana..

Hata kama ni wewe, mtu anakuambia nikopeshe 100,000/= kesho nakurejeshea 130,000/= huwezi acha..

Akakusanya M kadhaa..!! 😂

Kesho Ilipofika Kangungo macho yalimtoka jaman..

Ninavyozungumza sasa hivi, Kangungo boom lake likitoka analifwd kulipa deni..!

Alikuja kuniambia maji yalishamfika shingoni..

Nakubaliana na ushauri wa kutofanya siri.

Pole sana Mtoa mada.
 
Siku za karibuni wadada wengi wa kibongo wamepigwa na matapeli wanaoshirikiana na wazungu au wanaigiza wazungu.
Wanaanzisha urafiki kwenye mitandao kisha whatsapp unamuona kabisa.

Mdada anaongopewa kapendwa na mzungu anataka amuoe.
Anamwambia kamtumia zawadi kama mleta mada, kisha anaambiwa mzigo upo Zanzibar au mbali na mji wa mtapeliwa, anaambiwa alipie pesa za kuondoa mzigo na kodi kisha aende akachukue mzigo.

Wadada kwa tamaa wanawaonesha wenzao wamepata mchumba mzungu na picha za zawadi.
Pesa ya kulipia mzigo wanakopa madeni makubwa na kuuza vitu. Mwisho aibu kubwa huko ugenini Zanzibar wanapojikuta wamepigwa, hawana nauli ya kurudia wala mahali pa kuishi.

Jamaa yangu kawasaidia wadada watatu siku kama 7 zilizopita.
Matapeli yamegundua dawa ni kujifanya wazungu ilihali ni vijana wa Tz au Kenya
 
Pole mkuu mtakubaliana na mm , kwa sasa mm niliekataa...kabisa !! Kuhusu kuamin ...mawasiliano na mtu nisiyemjua !! Halafu eti akufadhili kirahic tu hiyo haipo

sent from toyota Allex
 
Yaani wabongo mkisikia mzungu basi mnajua ela ipo aseeh..

Imeisha hiyo mkuu
 
Kuna mzungu tapeli anayejita Gambler Erik number zake za simu +41779140475 tulikuwa marafiki kwenye mtandao wa LinkedIn kama marafiki wa kawaida akaonyesha kuja kuwekeza Tanzania.... Akasema kabla ya kuja Tanzania atanitumia machine zake za kutengeneza lotion na cream kwangu sikumbili kabla ya yeye mwenyewe kuja Tanzania. Na kwenye hiyo mizigo kaweka dola za kulipia pango la nyumba na maswala mengine

Akanijulisha wiki iliyopita atatuma mizigo kwenye ndege za UN na mara moja mzigo utanifikia kwangu kwa kupitia wakala.

Nilichoshangaa jumatatu ya wiki hii Kuna mwanamama kanipigia kwa number 0758392082 jina inasoma Emmanuel Tesha... At Mimi nilipe Kodi ya hizo bidhaa zilizokuja Tanzania kwa jina langu. Nikamwuuliza huyo Tapeli Gambler hivi Ni sahihi akaniambia wewe lipa nitakurudishia. Kumbe ndio nimeanza kuliwa kekundu hapo.

Hiyo ilikuwa Ni Kasulu Kigoma nikashangaa kwa Nini mzigo utuwe Kasulu na siyo DSM? Baada ya kulipa $ hiyo number haipatikani hewani. Nikajiuliza Toka jumatatu mpaka Alhamisi hakuna dalili yoyote ya kupokea mzigo ilikhali huyo mama Tapeli ananiaminia kwamba huo mzigo upo na utanifikia kwangu bila tatizo. Jana kaibuka Tapeli mwingine mwenye number 0758727527 jina la usajili Swaum Mena.

Akaniambia kiswahili kwamba mzigo umekwama Arusha ati nilipe $500 ili mzigo unifikie... Leo saa sita mchana.... Hapo ndio nikashtuka na kujuwa Kuna utapeli na hiyo pesa sijaituma. Na nikamtumia msg huyo mama kwamba Ni Tapeli anirudishie pesa zangu

Nimetuma ujumbe huu na hizo number za simu ili wengine yasiwapate kama Mimi yalivyonisibu
Nawatakia Ijumaa khereem

Sent using Jamii Forums mobile app

hiyo namba na simu usajili pia .....kuna mengi utawapata tz polisi watakusaidia cyber


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kuna mmoja alitaka kunipiga nilichomwambia ngoja niwasiliane na Interpool hata alipoishia sijui.
Watu hamtumiagi akili, we na exposure yote hii hadi leo hujui hizo mambo za kujidai sijui anataka wekeza blah blah, ila ndio ushajifunza, hamna uwekezaji wa mitandaoni sawa? Mtu akutumie eti mashine bila hata kukuona, kufanya utafiti, kupata vibali nk... Ushajifunza ila na hiyo hela jiesabie tu maumivu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom