Jamani nimetapeliwa

Jamani nimetapeliwa

Pole kwa kutapeliwa kijinga, hivi unaliavipi mzigo ambao huna document zake? Hivi huwa hausikii kitu kinaitwa GOVERNMENT ELECTRONIC PAYMENTS GATE WAY (GEPG) yaani mfumo wa malipo ya serikali kwa njia ya electronic? pole sana jifunze siku nyingine kuwa makini hata jirani yako anauwezo wa kuweka profile ya mzungu akajifanya anaishi Ulaya au Amerika kumbe ni mgogo/Mchaga jirani yako.
 
Asante kwa taarifa itayookoa wengine kuchapiwa kwa staili hii. Ndio faida ya Jamiiforums hii.

Kwa taarifa tu ni kwamba huyo mzungubalikuwa ni mbongo wa hapa hapa, naona hii staili inakuja kwa kazi kuna Mdada flani alikuwa anatumiwa video za saa za dhahabu na tapeli aliehifanya ni tajiri yupo nje, basi yule tapeli akamwambia anamtumia saa ile kwasababu wamekuwa marafiki siku ya siku Dada anapokea simu anaambiwa atume laki 3 mzigo upo airport dar huwezi kuingia bila kulipia, Dada yule ana bahati tulimfumbua kuwa jamaa ni tapeli
 
hawa matapeli wanapenda sana jamaa ambao ni mandezi, wajanja wajanja kama mie hawawezi kujaribu hapa! pambafff! acha mliwe labda mtatia akili siku moja!
 
Kuna jirani yangu namuona anakaribia kutapeliwa na watu wa design hiyo lakini mwenyewe anafanya siri.
 
Pole sana Mkuu ila Ndiyo hivyo umekuja JF kwenye watu wenye akili zao nyingi na ambao hawajawahi kutapeliwa kabisa

Pole sana tunajifunza kutokana na Makosa lakini tusifanye makosa yatakayo tufunza kutupoteza
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom