Jamani kulala na watoto kutatuadhiri siku moja

Hahaha! Yuko kliniki, safari ya mikumi ilizaa matunda. Naona anatema mate mara kwa mara na kula vitu vichachu!

Wewe si umesema kuwa una vibinti 2 vinakutosha au? Nilishaanza kutafuta jinsi ya kukupata ili niwaandalie madume wangu 3 njia!!!
 
Wewe si umesema kuwa una vibinti 2 vinakutosha au? Nilishaanza kutafuta jinsi ya kukupata ili niwaandalie madume wangu 3 njia!!!

Hahaha! Mkuu anza kabisa kukata mahari mapema. Afu tubinti twenyewe tuzuri mpaka natuonea wivu!
 
Kazi ya kufanya hiyo assessment tuachie sisi. Wewe jitahidi ili visijekuwa mali isiyolika!!

Vitu vingine havina haja ya kuvifanyia asesimenti.Ni full biutiful mazee! We anza kukata mapema. Nakuahidi ful sekyurite.
 
Hiyo sentensi ni hatari sana. Kama ungekuwa waziri, kesho nisingeshangaa kuona mamia wanaandamana ili uachie ngazi.

Mkuu kuzaa haiwezi kuwa kazi ya wenye uwezo. Kwanza watu wenye uwezo wenyewe wana matatizo kibao. Wengine libido zimekufa mpaka wakapepewe kwa sangoma Na wengine sperm count imeshuka kiasi kwamba wanatoa hewa tu kama vile wanacheua. Hawa watu wa Uswazi ni muhimu sana kuhakikisha kuwa hiki kizazi hakiangamii. Ni jukumu la wasomi na watu wengine wenye uwezo na upeo kuwasaidia ili wasiharibu watoto.

ha ha ha ha! LOL. Hakuna siku umasikini utaisha duniani labda YESU arudi. Class hili neno ni kama mwiba kila mahala lipo hata mbinguni lipo Tuna malaika kama Gabriel malaika mkuu na wengine wadogo, Kwenye utatu mtakatifu tuna Mungu then Roho mtakatufu na Yesu Kristo. Sioni solution ya karibu ya umasikini kama viongozi waliko Africa hawataki kuachia ngazi na wakitoka lazima amwachie mtoto wake au ndg.
 
Ni kweli mkuu. Hasa inapotokea kuwa mtu anapanga chumba kimoja, hakina ceiling board na ndiyo anakitumia kwa kila kitu, yaani sitting room, dining n.k. Kama ingewezekana kwamba angalau chumba kina usiri kidogo, basi labda wangejaribu kuwa kama Wahindi ili watimize amri ya Mwenyezi Mungu mchana. Lakini hiyo ni ngumu sana kwani mtu wa namna hiyo atakuwa na kazi nyingi mchana (mfano kusomba zege) na mama anaweza kuwa na mishughuliko ya kuongezea kipato (mfano mama ntilie). Na kwa hiyo lazima wangoje usiku na hawawezi kusubiri sana kwa kuwa watakuwa wamechoka. Kuwahi asubuhi pia inaweza kuwa ngumu kwa sababu mama yawezekana anawahi samaki ferry! Kweli kuna watu wanakumbana na mitihani ya maisha. Na afadhali hawa wana watoto wadogo. Wengine wana watoto wakubwa kidogo (12-16 years) ambao wanaweza kugoma kulala makusudi ili wasilikize. Ukifikiri sana maisha ya namna hii unaweza kuwa kichaa au kutafuta ganja ili kuondoa soni na hivyo kuendelea tu hata watoto wakisikia shauri yao.:confused:

hapa ndio penye mdadavuo kamili wa mkasa huu.

ukweli wa maisha ni kuwa, kama watu masikini wasingekuwa wanzaa watoto, kiwango cha maovu kama mauaji matumizi ya madawa ya kulevya nk yangezidi sana.

nasisitiza si ujinga na wala uzazi wa mpango hauwezi kusaidia kitu! sana sana utaongeza uendawazimu kama ilivyo sehemu nyingine za dunia. wale wenye nafuu idogo ya maisha tukumbuke kuna wenzetu usiku ukiingia mawazo, mchana ukikaribia mawazo!

tuwakumbuke hasa tunapopata nafasi za uongozi zenye madaraka na maamuzi ya msingi
 
Vitu vingine havina haja ya kuvifanyia asesimenti.Ni full biutiful mazee! We anza kukata mapema. Nakuahidi ful sekyurite.

Hapana mkuu. Hiyo ni lazima sana, kwani hata kama Watanzania ni wajinga, lakini tuko makini kwenye mambo binafsi. Hakuna mtu anafanya mzaha na mkewe au watoto. Kwa hiyo siweze kukubali wanangu wanunue mbuzi kwenye gunia. Tutafanya tu hata kama hupendi au wewe umeridhika!!
 
hapa ndio penye mdadavuo kamili wa mkasa huu.

ukweli wa maisha ni kuwa, kama watu masikini wasingekuwa wanzaa watoto, kiwango cha maovu kama mauaji matumizi ya madawa ya kulevya nk yangezidi sana.

nasisitiza si ujinga na wala uzazi wa mpango hauwezi kusaidia kitu! sana sana utaongeza uendawazimu kama ilivyo sehemu nyingine za dunia. wale wenye nafuu idogo ya maisha tukumbuke kuna wenzetu usiku ukiingia mawazo, mchana ukikaribia mawazo!

tuwakumbuke hasa tunapopata nafasi za uongozi zenye madaraka na maamuzi ya msingi

Asafi kabisa. Nimekutemea senksi! Ila hiyo ndo nini?
 
Hapana mkuu. Hiyo ni lazima sana, kwani hata kama Watanzania ni wajinga, lakini tuko makini kwenye mambo binafsi. Hakuna mtu anafanya mzaha na mkewe au watoto. Kwa hiyo siweze kukubali wanangu wanunue mbuzi kwenye gunia. Tutafanya tu hata kama hupendi au wewe umeridhika!!

HAHAHA! Hapa naona imekula kwangu!
 
ha ha ha ha! LOL. Hakuna siku umasikini utaisha duniani labda YESU arudi. Class hili neno ni kama mwiba kila mahala lipo hata mbinguni lipo Tuna malaika kama Gabriel malaika mkuu na wengine wadogo, Kwenye utatu mtakatifu tuna Mungu then Roho mtakatufu na Yesu Kristo. Sioni solution ya karibu ya umasikini kama viongozi waliko Africa hawataki kuachia ngazi na wakitoka lazima amwachie mtoto wake au ndg.

Kweli kabisa. Matatizo mengi ya Afrika yanasababishwa na viongozi wetu. Wengine hadi wanasema kuwa hawajui chanzo cha umasikini wa watu wao.. big shame.

Kwa hiyo masikini wana pua, kwa maana hiyo wananusa na milango mingine ya fahamu na wanatamani kama mtu mwingine. Lazima watapata wenzi wao na mwisho wa siku watapata watoto. Inawezakana baba na mama wasiweze kusaidika tena, lakini watoto wanaweza kupewa msaada na wengine kuwa mamilionea. Wengine ndiyo yalikuwa mazingira yetu hayo wakati tunakua. Tunatakiwa kuwasaidia na hasa hasa wale waliopewa jukumu la kutuongoza!
 
Wazazi ni wajinga kbsa hawa, na baadhi ya ambao hawajatajwa hapa, kama huna uwezo unazaa ya nini? ili kusumbua watoto sio? na wengine hata kuwalisha hatuwezi. Ni aibu. Oaneni na msizae mleeane tu.


Nguli ndugu yangu mlaani shetani haya uyasemayo ni ya watu waliozoea kukufuru wewe hayakufai!
 
Maisha magumu sana kiasi kwamba inatisha kwa baadhi ya watanzania. Mbaya zaidi kwa vyumba vya kupanga ambavyo kwanza ni vidogo sana. Hivi hizi hela zote za mafisadi na nyinginezo ambazo tunazisemea kuwa zimetumika vibaya si zingeweza kujenga hata makazi nafuu kwa watanzania?? Nashangaa bado watanzania hao hao ambao maisha ni magumu bado siku ya uchanguzi wanapoteza muda wao kuchagua viongozi wa chama ambacho mpaka leo hii hakijaweza kuondoa watanzania wengi katika umaskini uliokithiri. Wanachokifanya ni kuwakumbatia mafisadi kwa kuwa wanawachangia fedha za uchaguzi. Hivi yale ya kuli "YANA MWISHO HAYA" yatatimia lini?
 
Poor Iribini na advance ulikuwa umeiiingiza kwenye mahesabu ya krisimasi....

Umeistukia hiyoe? Naona tarehe zinazidi kwenda mbele na nauli ya daa eksipressi inazidi kupanda! Usisahau wakati nazaliwa kuna coin ilidondoka sakafuni. Tangu wakati huo nimekuwa na mahaba ya dhati na fweza!
 
Nguli ndugu yangu mlaani shetani haya uyasemayo ni ya watu waliozoea kukufuru wewe hayakufai!

Ndg yangu Mungu anisamehe kama nimekufuru ila DUNIA ya enzi hizo ulikuwa unaweza kuishi kwa hunting & gathering, sasa hivi zunguka dar maeneo ya posta ona ombax2 walizunguka mapaka wengine wazuga vidonda na ukilema ili waombe.

Mimi naomba Mungu anisimamie mawazo yangu niwe na watoto 2 tu. Mungu akinizidishia kipato nita adopt mtoto 1.
 
Umeistukia hiyoe? Naona tarehe zinazidi kwenda mbele na nauli ya daa eksipressi inazidi kupanda! Usisahau wakati nazaliwa kuna coin ilidondoka sakafuni. Tangu wakati huo nimekuwa na mahaba ya dhati na fweza!
washtaki kwa majembe a.k.a vijana wa kazi
 
Back
Top Bottom