Jamani andikeni wosia mapema!

Jamani andikeni wosia mapema!

GAZETI

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
5,292
Reaction score
6,768
Kwani hamjui Kuwa mtakufa? Au hamuoni umuhimu kwa kuwa yenu
yameisha?

Unakuta Mtu anafariki bila kuacha wosia wowote hili ni tatizo kinachokera
zaidi kabla mgao haujaanza hapo ndo huibuka watoto wa marehemu ambao
inasemekana kazaa nje ya ndoa na wengine sijui alikosea wakati yuko shule
ya msingi........ hivi na vile... basi tu....

Nafikiri kulikuwa na umuhimu ili kupunguza migogoro watu tukaandika wosia
ambao kama utabahatika kumaliza mwaka una UPDATE..... kama una watoto
wa nje ni bora ukawaandalia mazingira mapema ili wasjekusumbua kwenye
Mirathi.

Unachotakiwa kufanya ni kujenga taswira kuwa umeshakufa na Mungu amekupa
nafasi ya kusimamia mgao wa mali zako.

Hapo unaanza...... (Mfano)
1. Hii nyumba ya Kongowe isiuzwe wapewe yatima (Hiyo inaweza kuwa sadaka au toba
Kwa Sababu inawezekana uliipata nyumba hiyo kwa njia ya dhuluma mfano
Kukaba, kubambikia watu kesi n.k) Kama una imani ya dini basi unaamua kupunguza
Mzigo.
2.........................................................................................................
Ingekuwa vema pia serikali ikasimamia utaratibu wa watu kuandika wosia wanapofikisha
miaka fulani, hii ingesaidia sana kupunguza migogoro.
 
Nilishaandika kitambo na kuwaambia nishawaambia, nikifa nusu ya mali waiuze pesa iwekwe benk kwa ajili ya Paka wangu ale chakula kizuri na matibabu (kwa kupata minyoo tu hakajambo) mpk siku na yeye akifa au pesa zikiisha.


Sent from my Siemens kidole juu using JamiiForum mobile app.
 
Nilishaandika kitambo na kuwaambia nishawaambia, nikifa nusu ya mali waiuze pesa iwekwe benk kwa ajili ya Paka wangu ale chakula kizuri na matibabu (kwa kupata minyoo tu hakajambo) mpk siku na yeye akifa au pesa zikiisha.


Sent from my Siemens kidole juu using JamiiForum mobile app.
Hata mtt wa miaka 7 anamuuwa huyo paka! anabeba fedha sabuni ya roho
 
Sawa tutajihidi na hata bima ya mazishi itabidi tuweke ili tutakao waacha wasipate tabu kutuzika
 
11bc826e52c1a0c6464ef7408b771573--real-estate-forms-legal-separation.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ukiandika wosia si unauficha watu wasiuone??
Ukifa watajuaje ulipo?
lazma will iwe na Proof ya mwanasheria, na mwanasheria anakua na copy, so ukifa ye ndo anakuja na ushahidi maana ni kazi yake kusimamia ulicho kiandika kitekelezeke. so will haifichwi bali hukaa kwa mwanasheria.
 
lazma will iwe na Proof ya mwanasheria, na mwanasheria anakua na copy, so ukifa ye ndo anakuja na ushahidi maana ni kazi yake kusimamia ulicho kiandika kitekelezeke. so will haifichwi bali hukaa kwa mwanasheria.

Anhaaa.. mwanasheria yoyote?
 
Unaweza kuuhifadhi kwa mwanasheria wako au benki yako na juu ya bahasha huandikwa
"TO BE OPENED ON THE EVENT OF MY DEATH"

Sent using Jamii Forums mobile app


Sasa Mwanasheria au Bank watajuaje kama nimekufa??

yess, yule ambae anatambulika kisheria. kuna wapo wamebobea kene izo fani lakin nadahan mwanasheria yoyote anaweza kusimamia ili mradi tu anatambulika kwa mujib wa kanuni na vigezo vya fani yake
 
Back
Top Bottom