Kuna jamaa yangu kipindi fulani cha miaka ya 90 mwishoni, aliamua kwenda Kagera, akaenda akakaa kwa jamaa fulani halafu akawa anavaa Lubega nyeusi, miguuni amejipaka masizi meusi, akijidai kuwa ni mgonjwa halafu huyo jamaa yake akawa anigiza kuwa ndiyo mganga wa kienyeji. Watu kuona hivyo wakawa wanamiminika kwa wingi nyumbani hapo, kwa ajili ya kupata tiba ya miguu na mambo mengine, huku yeye akiwashuhudia kuwa alifika akiwa ana hali mbaya lakini mganga amemsaidia sana kuimarisha afya yake. Walipiga hela ndefu halafu baadaye akapotea. Baadhi ya wagonjwa walikuja kustuka baadaye, kuja kuonana naye walipomuuliza, akawaambia kuwa hata yeye alienda pale kupata tiba kama wao walivyokuwa wakifanya kwa hiyo yeye hakuwa tapeli isipokuwa yule mganga, kwa hiyo akawa anawaelekeza waende wakamuulize mganga wao aliyekuwa akiwatibu.
Kesi nyingine tena akawa yuko anasafiri kwa Baiskeli iliyokuwa imechoka sana, alikuwa anaeleka Magu. Kukaribia Magu akawa amekamatwa kwa kutokuwa amekata kodi ya Baiskeli, kipindi hicho baiskeli zilikuwa zinakatiwa kodi kwa mwwaka. Wakamataji wakamlazimisha aidha akate kodi pamoja na kutoa faini, au aiache Baiskeli akatafute hela halafu akipata, arudi aje achukue Baiskeli. Jamaa kuona hivyo akaona ni dili kama la "900 itapendeza", akawaachia Baiskeli na hawakuandikishana. Akatembea kwa mguu mpaka Magu mjini. Kufika mjini akaenda kwenye duka la rafiki yake, akaomba kuandikiwa risiti ya Baiskeli mpya aina ya Phoenix, halafu tarehe za risiti zikarudishwa nyuma miezi kadhaa. Kesho yake akawarudia watoza ushuru, akawapa hela yao ya faini, akalipia na kodi ya Baiskeli, halafu akawaomba sasa wamrudishie Baiskeli yake. Walivyoileta Baiskeli ile ile aliyokuwa amewaachia jana yake, akaikataa, akasema kuwa yeye Baiskeli yake ilikuwa ni mpya aina ya Phoenix, akawaonyesha na risiti akidai kuwa ameinunua siku siyo nyingi na ndiyo maana hata risiti yake huwa anatembea nayo siku zote. Kilichotokea baada ya mvurugano huo, ilibidi wahusika wakanunue Baiskeli mpya aina ya Phoenix, wakamkabidhi akaondoka na Baiskeli mpya, akawaachia mkweche.
Hata hivyo huyu ni tapeli perce na utapeli wake haufanani na ule wa kwako