Jamaa aliyetaka kutapeliwa akashtuka akamtapeli mtapeli

Jamaa aliyetaka kutapeliwa akashtuka akamtapeli mtapeli

Niliwahi kusoma novel moja ilikuwa ni true story ya mtu aliyekuwa tapeli mkubwa anasema ili umtapeli mtu lazima yule mtu awe na tamaa, kilichokuokoa hukuwa na tamaa Ila mke wako alishaingia mkenge
Akikutana na shemeji akamwomba maongezi ya kushtakia ulivyovuruga urafiki kumwibia elfu hamsini(pesa ndogo sana imevunja urafiki,hapo anatia chumvi)na kumpakazia utapeli?, na pia akampa laki 2 nyingine ya zawadi ya watoto itakuwaje?😃😃
 
wanawake wanatapeliwa sana kuliko wanaume
Nimecheka sana kwenye huu mstari kuhusu wife: “wife nikimsimulia ananambia kazi niache hata siku hiyo nikapige pesa.”
Yani hawa viumbe wenzetu wanavyopendaga short cut! Hapo tayari alikuwa ameshajenga image ya u bilionea na jinsi Mungu alivyowashushia Neemana angekuwa ni wife wako ndo anacheza hilo insue sijui kilio chake nani angemtuliza all in all big up kwa kustukia mchezo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo wafuasi wa chadema walivyo kama huyo jamaa ,ukiwaangalia wanavyoongea utafikiri wana uchungu mno na wananchi, kumbe ni utapeli mtupu.

Sent using Jamii Forums mobile app
😀😀😀😀😀😀 wewe ni Genius sana. You Got to the real point.
Kuna Jamaa huku Kigoma aliwaambia waziwazi Wapiga kura akiwa kwenye Mkutano wa hadhara huko Kata ya Businde-Buhanda aliyowahidi 2015 zilikuwa ni siasa na aliwataka Wapiga kura wake wawaulize CCM. Na baada ya kuanza CCM kuitekeleza Miradi Mikubwa haohao wakarudi tena wanaotekeleza ni Act wazalendo tunatekeleza, Cha Ajabu mtu anapiga picha na kupost kwenye mitandao anayeitwa Hussein KALYANGO wakati alihakikishiwa na boss wake wanaoweza kutekeleza ni CCM akieleza kwenye Kampeni walitaka Wachaguliwe tu. Ukifika mtaa wa Mjimwema nyumbani kwa Kalyango Barabara haipitiki imejaa mashimo gali saloon ndogo hazipiti kiurahisi lakini utasikia eti Barabara za Lami anajenga.😅🤣🤣🤣😅
 
Chai imeharibiwa na chumvi ya mawe.

Everyday is Saturday................... 😎
 
Huyo tapeli hawezi kuangalia nyuma.

Ili kuilinda familia yako vizuri mchukulie RB kabisa ili ajue kuna polisi wanamfuatili.

Hata kaa akukumbuke wala kuisogelea familia yako.

Ila siku nyingi usipende kumtambulisha mtu kwa familia yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna watu ni walipizi kisasi, yaani kulipiza kwake ni lazima, anawashwa kabisa hakai kwa amani, anataka tu alipize though ni kweli kuna uwezekano huyu asiangalie nyuma.

Ila ni upuuzi kutatua uovu kwa kufanya uovu halafu ujisifie. Kulikuwa hakuna sababu ya kula elfu hamsini ya jamaa, na pia kulikuwa hakuna sababu ya kumpeleka nyumbani.
 
Muda anampeleka nyumban alikuwq kwenye rada tayari.. Huyo kaja kushtuka baadaye kwenye habari ya ujenzi, mtoa mada naye ni dizain ya watu wenye tamaa..
Kuna watu ni walipizi kisasi, yaani kulipiza kwake ni lazima, anawashwa kabisa hakai kwa amani, anataka tu alipize though ni kweli kuna uwezekano huyu asiangalie nyuma.

Ila ni upuuzi kutatua uovu kwa kufanya uovu halafu ujisifie. Kulikuwa hakuna sababu ya kula elfu hamsini ya jamaa, na pia kulikuwa hakuna sababu ya kumpeleka nyumbani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muda anampeleka nyumban alikuwq kwenye rada tayari.. Huyo kaja kushtuka baadaye kwenye habari ya ujenzi, mtoa mada naye ni dizain ya watu wenye tamaa..

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeongea point mkuu. Kuna ukweli flani hivi, tamaa ndo imemfanya kutaka kusimamia sight ya stranger labda kuna kitu angepata. Kwa hali ya kawaida sidhani kama alienda kuchunguza kama kweli kuna mafundi, kuna uwezekano alienda kucheki progress ili atoe ripoti ya kazi kwa jamaa ila kuwakosa ndo kukatriger swali la huyu ni tapeli nn? Angewapata labda angepiga simu na kumwambia jamaa aisee nipo sight hapa, kuna hili na lile bla bla bla.
 
Chumguza simu ya wife jamaa anaweza akakurudia kivingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata mpaka kumjua jamaa inawezekana wife wake kahusika sana, si unaona alikuwa anamshauri aache kazi.. tapeli akikujia sio kwamba eti kakukuta kweye meza kaja tu bahati mbaya, ni kuwa ana taarifa zako na kakuweka kwenye target. Jamaa ajiulize sana, unaweza shangaa mke ndio alimwambia mwalike jamaa aje nyumbani, kumbe ni rafiki wa mkewe.
Atuambie mkewe kabila gani? 😉
 
Kupona kwenye utapeli ni bahati sana. Kama unajijua una tamaa hata kidogo ni heri kuchunguza sana kila unachoambiwa.

Na hata ukichunguza ukiona kuna uelekeo unaosomeka usikubali kuingia kwenye transaction bila kufuata taratibu zote za kisheria.

Pia usiingie kwenye transaction na mtu usiyemfahamu mpaka nyumbani kamwe. Pia huyo unayeingia naye kwenye transaction ufuatilie background yake kwa undani kupitia watu wengine wanaoweza kumfahamu ambao siyo walio karibu naye.
 
Wadau tuwekane hapa wazi kwa sisi ambao tumewahi shtukia matapeli.

Mwaka juzi kuna jamaa mmoja ilitokea tulikutana bar. Alikuja meza yangu akakaa tukaongea ongea na kuwa friends.alinambia yeye ni mgeni dar anakuwa sana arusha.

Anafanya biashara ya madini so akija huwa anafikia hotel...katika maongezi tukafahamiana sana.alilipia mpaka beers zangu.nlimkatalia sana akaomba alipe sababu amefurahi kupata rafiki mwema.

Nikajiwazia nikasema tu moyoni hiiiii "yaani mimi ni mwema?"

Basi akanipa ni biznez kadi yake tukaagana tena akimwita dereva aje pia anifahamu.akiwa dar huwa anakuwa na dereva wake.

Tukawa friends after some weeks nlimkaribisha hadi home.alipapenda sana home.siku amekuja alinunua zawadi kwa watoto na wife.almost alitumia kama 200,000+

Jamaa alikuwa mpole sana anaongea kwa upole and very smart. Anapiga sana suit alikuwa akija anatumia uber au prado moja kali sana na dereva wake.

Alinambia anajenga mbezi beach alinunua kiwanja milion 150. So ujenzi unaendelea weekend moja akaniomba akanioneshe hiyo nyumba maana akiwa nje ya nchi anakosa mtu wa kumwangalizia.

Alinipeleka mbezi beach nikakuta mafundi wapo wamechangamka wakimwita mzee na kumweleza mahitaji.fundi akasema wapewe milion 8 kuna vitu vya kununua.akaomba account ya bank ya fundi akasema ataenda mtumia jumatatu.ila kwa siku hiyo akamtumia tsh mil 1 ya matumizi tu wagawane weekend.

Jamaa alikuwa fresh sana.alianza kunipa stories za biashara ya madini.akitaka niweke mtaji hata wa mil 30 ngepata mil 45 ndani ya week tu.akinishauri niende naye arusha tukanunue dhahabu then anapoenda South Afrika twende sote akanioneshe wateja.

Hapo akili ilianza ku alert.jamaa alikuwa busy na simu kuongea na wateja sometimes aliweka tu loud speaker.nlianza kushtuka kuwa jamaa yupo fast sana kunishawish.wife nikimsimulia ananambia kazi niache hata siku hiyo nikapige pesa.

Nikawa namwambia si rahisi kiivyo asubiri nifanye utafiti kwanza. Weekend moja nikapita mbezi nikakumbuka mjengo wa jamaa.kupita ile sehemu hakuna mafundi.

Nikauliza kwa vijana jirani kuwa ile nyumba nliitamani nikitaka kupata ramani yake mwenyewe yu wapi.wakanambia mwenye nayo alifungwa kwa madawa ya kulevya toka mwaka 2016. Na haijawahi guswa tena.

Nliwadodosa sana jamaa wakasema imeachwa hivyo tu ila kuna siku jamaa mmoja alikuja wakaja na mafundi wakapotea tena.

Nliporudi home nikawasiliana na jamaa.nikamuuliza ujenzi unaendeleaje.akasema safi kabisa mafundi toka siku ile wanapiga kazi mchana na usiku na jana tu alikuwa nao.anataka iishe ndani ya miezi 3. Ahamie dar.coz ana nyumba dar na south afrika.

Kesho yake nikapita tena ile sehemu.nikakuta kimya hakuna fundi hata mmoja.

Nikamuuliza tena vipi speed ya mafundi wake nataka nami nije niwatumie.akasema wapo vizuri leo tu kawapelekea vifaa vya mil 10. Hapo ndo nikashtuka zaidi.jamaa alikuwa mwongo.

After two days nikaonana naye town.nlimwambia anisaidie 50,000 ya haraka ntampatia nikifika ofisini nmesahau biz cards zangu zote aliniazima. Nlipofika ofisini nilimwambia nmempiga picha nmetuma kwa jamaa yangu polisi akatafute mtu mwingine wa kumtapeli.

Kuanzia muda huo hakupatikana tena.sijui alihamia wapi.ila niseme jamaa alikuwa vizuri.anaongea kiingereza vizuri.anajua nchi nyingi duniani.

Jamaa alikuwa amejipanga vizuri sana.alinikosa kosa sababu mimi kwenye issues za pesa huwa nachunguza sana.mzito kuamua ghafla.

Siamini katika deals ambazo zinaleta pesa kirahisi rahisi sana.ambazo hesabu zke hazimake sense.

Walinishinswa forever living,wakanishindwa gnld,wakanishindwa wazee wa goodmorning all time. Sipatikani katika kutapeliwa.

Tupeane shuhuda mbalimbali za kutapeli na kutapeliwa.mimi nlimtapeli jamaa 50,000. Na kumuingiza hasara kwa zawad ambazo alileta kwa wife na watoto wangu.

Ntaleta kisa kingine cha bi dada mmoja ambaye alitaka kunitapeli kupitia mapenzi.
Huu uandishi ni kama ule wa Ile ID moja maarufu ya kujimwambafai humu jeiefu.
 
Back
Top Bottom