Jakaya Mrisho Kikwete, Mungu atakulipa!

Jakaya Mrisho Kikwete, Mungu atakulipa!

Huyu Mzee wa toka enzi za Nyerere, wakati wa Nyerere na suit hizi wapi na wapi? ilifaa waelimishwe kuvaa suti, kwanza suti hizi hazifungwi vifungo vyote hufungwa kimoja tu cha kati ikibidi.

Huyo ni punguani asiyejuwa kuvaa suti kama mapunguani wengine, lakini umeshamuona mwenyewe toto la Bwagamoyo likitia suti? Utapenda uwe kama yeye. Wapiiiiiiiiii?
Mmekosa watu wengine wakuwaweka?? Bora mgemuacha kule Ikulu aendelee kugawa chai na Juice!
 
Mmekosa watu wengine wakuwaweka?? Bora mgemuacha kule Ikulu aendelee kugawa chai na Juice!

Huyo mzee hata akikosea akaingia ofisini bila nguo bado anawahenyesha chadema, alikotokea. Sasa ulitegemea nini alikotokea ni magwanda kwa kwenda mbele. Baada ya hapo tukampeleka kijana ma fashion ampe darsa, hujaona?
 
Mleta mada unaugonjwa mbaya sana wa kumpenda Kikwete mpaka kupitiliza..,

Ni wakati wa Kikwete wapinzani wamebambikiwa kwesi zisizo na idadi kuanzia, Mbowe,Slaa,Zitto na wengineo, ni wakati huu mauji ya kisiasa kuanzia Mwangosi,Mgimwa jaribio la kuuwawa Kibanda, Kufungiwa kwa Gazeti la Mwana.ha.lisi. Mauaji ya Kisiasa pale Olasiti Arusha ni wakati huu Msamiari wa Ugaidi umeibuliwa chini ya Mwigulu kwa lengo la kupakaza matopew upinzani hususani Chadema bila Mafanikio.

Watu wamelala ndani kwa kesi za kijinga kuanzia kina kilewo na wenzake, Mauaji ya kina mama na wananchi wa Mtwara kwa vitu vya kijinga sana.

Hiyo unayoiita demokrasia unaijua wewe.?
Koma komaa

Hakuna ambacho kimefanywa na Kikwete kikakamilika kwa asilimia mia.Hili la Katiba lilikuwa jambo la kumtoa lakini kiko wapi???

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
Pia kaongeza kushuka kwa thamani ya shilingi from 1/1000 to 1/1850. Kwa hili Mungu ambariki sana. Tofauti ya 850 ni kwamba amefanya juhudi kubwa kutufikisha hapo.

Niyeye alitupandisha kielimu mpaka division 5. Huu ni uzalendo uliotukuka.

Hakuishia hapo. Sukari sasa tunanua 2000-2500 p/kg. Huu ubunifu wake binafsi.

Akakuza harufu Kali kati ya waislamu na wakristu lakini pia baina ya madhehebu mbalimbali ndani ya dini moja. Kwa hili kamfunika Nyerere.

Kwa huruma zake sasa tunaweza kuvuta bangi kituo cha polisi tusikamatwe, ikuku unaweza unaweza kupiga bongo fleva, rushwa tunagawa hadharani usiulizwe, wakoloni wamerudi kwa kasi ya ajabu na wanatuibia rasilimali chini ya mwamvuli wa uwekezaji, ukiuliza utaambiwa tunavutia mazingira yakiuwekezaji. Awamu ya 4 tumeshuhudia umafia kwa waandishi ya habari, polisi kuua raia na waandishi wa habari, tumeshuhudia serikali yake ikiunda Chama Cha siasa cha polisi ambacho kazi yake kuua upinzani nchini japo amefeli kwa hila zake chafu wacheni ni msifu kwakuwa sili kwao.

Ikafika wakati, wanafunzi 20,000 wenye sifa yakujiunga chuo kikuu kukosa mikopo, bila aibu akajisifu hadharani.Bila abu, Ni yeye pekee ananunua suti Kariakoo anaenda kujaribisha ulaya ilimradi kuvunja rekodi ya safari.

Huku tukijisifu Uhuru wa Vyombo vya habari, kule anafungia Vyombo vya habari eti kisa vimefichua maovu ya Vyombo vyake vya usalama(-----------), huu ni udikiteta.

Tukashuhudia chama chake kinateka nyara mchakato wa katiba mpya bila maridhiano. Huu ni uhuni. Akaizindua kwa mbwembwe bila kupima upepo wa kisiasa pande mbili zinaunda muungano. Akajipa madaraka yakutunga katiba bila ridhaa ya wananchi as if anapanga bajeti ya familia yake.

Hakika anastahili pongezi.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
 
Kwakweli rais wetu amefanya kazi kubwa sana,hadi kuweza kuziona billion 300 ni fedha za madafu amejitahidi sana???watu wamepigwa hadi kusokomewa vijiti kwenye nyeti zao(operation tokomeza)amejitahidi sana kuwakenulia wezi rais wetu mpendwa sio eti???Nashindwa kuelewa mnaposifu akili zenu huwa mnaficha kwapani au???

lukeblair;
Usifadhaike; akili zao hazipo walipo, zimeachwa stoo pale Lumumba, mpaka jioni ili mlipa buku 7 asipate shida kuhesabu ni vichwa vingapi vilibaki pale ofisi ndogo mpaka jioni.
Faiza Foxy anasema hakuna aliyewahi kufanya makuu ka JK. Naona uzi huu kaandika yeye na kujijibu yeye. Haikosi huyu ni bi mkuu
 
Huyo mzee hata akikosea akaingia ofisini bila nguo bado anawahenyesha chadema, alikotokea. Sasa ulitegemea nini alikotokea ni magwanda kwa kwenda mbele. Baada ya hapo tukampeleka kijana ma fashion ampe darsa, hujaona?

Hueleweki. Umekaa ki nafiki nafiki tu. JK ni rais wa hovyo kuwahi kutokea duniani
 
Huyu Mzee wa toka enzi za Nyerere, wakati wa Nyerere na suit hizi wapi na wapi? ilifaa waelimishwe kuvaa suti, kwanza suti hizi hazifungwi vifungo vyote hufungwa kimoja tu cha kati ikibidi.

Huyo ni punguani asiyejuwa kuvaa suti kama mapunguani wengine, lakini umeshamuona mwenyewe toto la Bwagamoyo likitia suti? Utapenda uwe kama yeye. Wapiiiiiiiiii?

Dini ya Wassira ndio kigezo cha wewe kumporomoshea mitusi?
 
Hueleweki. Umekaa ki nafiki nafiki tu. JK ni rais wa hovyo kuwahi kutokea duniani

Sitegemei punguani kama wewe kunielewa.

Kikwete ndiye Rais pekee na wa kwanza Tanzania aliyepata tuzo ya utawala bora, kumbuka hilo.

Kikwet endiye wa kwanza kualikwa rasmi na Obama kutokea Afrika alipochukuwa madaraka USA.

Kikwete ndiye Rais wa kwanza dunia aliyeweza kuwakutanisha Marais wanne kwa pamoja Afrika kwa wakati mmoja, Obama, Bush, Clinton na Jimmy Carter. Haijwahi kutokea kwingine.

Na mengine mengi ya kwanza ya Kikwete nikianza kuyaweka hapa tutakesha.
 
Mafanikio ya kiongozi yeyote, hasa rais hupimwa kwa sentensi moja tu:
Je maisha ya watu ni bora zaidi hivi sasa kuliko wakati wa aliyemtangulia? Naweza kusema ndiyo kwa Rwanda.
 
Huo ndiyo ukisikia ufupi wa mawazo.

Na wewe uliamini jina Kigoma litageuka kuwa Dubai?

Hivi hizo shule huwa mnaenda kusomea ujinga?

Alitakiwa asimwamini Kikwete kwakuwa haaminiki. Si unaona na zile meli alidanganya? Sasa hivi tunadaiwq Bilioni 600 na PSPF pekee. Alhaji Dau hajasema anadai sh ngapi. Madeni yameongezeka, meli hakuna, barabara ndo zile zinajengwa na wachina, wiki mbili tu mashimo kibao, ahule ndio hizo za kata, mtoto hajui hata bunsen burner. Albino wanazidi kupukutika. Migomo na maandamano yamezidi, kina Mboni Mhita ndo wanaong'ara ki ccm ccm. Katiba imekula bilioni 100+ lakini ni likatiba la hovyo. Pasco anaiita bora katiba. Mvutano ndani ya chama chake kwenye maslahi unazidi kurindima. Tishio la kupasuka kwa CCM ni dhahiri. Mijizi imeshirikiana nae kuiba fedha za Escrow. Yani ni hatari
...!!
 
Last edited by a moderator:
lukeblair;
Usifadhaike; akili zao hazipo walipo, zimeachwa stoo pale Lumumba, mpaka jioni ili mlipa buku 7 asipate shida kuhesabu ni vichwa vingapi vilibaki pale ofisi ndogo mpaka jioni.
Faiza Foxy anasema hakuna aliyewahi kufanya makuu ka JK. Naona uzi huu kaandika yeye na kujijibu yeye. Haikosi huyu ni bi mkuu

Kumbe wanalipwa hawa jamaa???ndo maana nashangaa binadamu wa kawaida kufikiri kidogo kiasi cha kusifu upuuzi..huo Uhuru wa vyama vya siasa ndio ule wakuwapiga wanaoandamana hadi kuwang'oa meno???
 
Sitegemei punguani kama wewe kunielewa.

Kikwete ndiye Rais pekee na wa kwanza Tanzania aliyepata tuzo ya utawala bora, kumbuka hilo.

Kikwet endiye wa kwanza kualikwa rasmi na Obama kutokea Afrika alipochukuwa madaraka USA.

Kikwete ndiye Rais wa kwanza dunia aliyeweza kuwakutanisha Marais wanne kwa pamoja Afrika kwa wakati mmoja, Obama, Bush, Clinton na Jimmy Carter. Haijwahi kutokea kwingine.

Na mengine mengi ya kwanza ya Kikwete nikianza kuyaweka hapa tutakesha.
Siamini kama una akili fupi hivyo, siku zote nilikuwa jabizana na wewe nikidhani una uelewa mzuri wa mambo kumbe nilikuwa najidanganya. Sitajibizana tena na wewe, malizia ni rais pekee aliyepata uprofesa china. Utawala bora upi upo tanzania wewe, umesoma ripoti za taasisi za kimataifa. Tuzo ni nini? Unajifanya hujui lengo la wanaompa. Kuitwa na obama umeona ni hatari sana, inaelekea wewe ni mpenda mteremko sana.
 
Wewe hata unachokibishia hukielewi ni nini.

Development ya Tanzania wakati wa Kikwete inaongelewa Kimataifa ni kati ya nchi 20 zinazo develop kwa haraka duniani:

Fastest-Growing Economies Through 2015 - Business Insider

Hivi hizo shule huwa mnaenda kusomea ujinga?

Hizi ni takwimu zilizotayarishwa na wamarekani na washirika wake. Unazikubali kumbe? Kumbe makafiri unawaheshimu eeh? Kesho wakija na idadi kubwa ya Wakristo kuzidi waislam uzifanye raference pia
 
Sawa bwana najua saa hizi mko Mbeya mnapanga mikakati ya kulazimisha matokeo uchaguzi mkuu 2015. Imekula kwenu!. Mtakutana sana!. Ninyi ni weupe peeee!

Hi
You must be "old school"
Freedom of speech ? ==>> explosion of Internet even the Great Wall of china have failed; the power of VPN etc etc please; don't live in dark
That is all ranting
 
As you signing off Sir keepon praying for your nation ili kikombe cha siasa chafu ya wasaka madaraka hali mikono yao ikinuka rushwa, kiliepushe taifa kuingia kwenye machafuko.
Nimeguswa!.

P.
 
Watakuja watu kubeza hayo mafanikio. Mimi huwa nnawaambia wachanganye awamu zote waone kama Kikwete hajafanya zaidi ya wote.

Sikusikia mfumko wa bei wala wakati wa Mkapa kama ilivyo sasa.
Je hazina anaiacha vipi.Anapoondoka. Amejitahidi kwa sehemu yake na kila aliyepita ana mazuri na mabaya pia. Hivyo siwezi kubeza wala kumpa credit kwamba kafanya zaidi ya waliomtangulia nitakuwa nampaka mafuta na kuwa mshabiki tu.
 
Awamu ya nne imewajenga watanzania vibaya .kujikomba ili liende. kashateua ndugu.
 
Kwakweli rais wetu amefanya kazi kubwa sana,hadi kuweza kuziona billion 300 ni fedha za madafu amejitahidi sana???watu wamepigwa hadi kusokomewa vijiti kwenye nyeti zao(operation tokomeza)amejitahidi sana kuwakenulia wezi rais wetu mpendwa sio eti???Nashindwa kuelewa mnaposifu akili zenu huwa mnaficha kwapani au???

watoe majibu hao wanaosifia jamaa kuteua mademu zake kuwa DC
 
Tukumbushane jamani; watanzania tulio wengi uelewa wetu unatia mashaka kutokana na elimu tuliyopatiwa. Kumbuka population statistics zinasema zaidi ya 55% tumezaliwa baada ya mwaka 1980.
Sasa wanaomlaumu au kuponda 'mafanikio' ya JK sio kuwa hawaoni majengo, mabarabara, madaraja, mabehewa ya TRL nk, la hasha wanayaona haya lakini hili ni kundi dogo lenye uelewa na upeo.
Hawa ndio wanaziona barabara huku wakizilinganishan na madeni yaliyokopwa kuzijenga wakijua wazi utakuwa mzigo zaidi ya faida zake. Hawa ndio wanaona jinsi udini unavyolinyemelea taifa, hawa ndio wanaweza kujiuliza kuwa kama serikali inashindwa kuwalinda Albino wasiofikia 35,000 nchi nzima kuwa tukishambuliwa sote 45,000,000 kwa wakati mmoja itakuwaje.
Pia marais waliotangulia 'walitupa shida' katika kuhakikisha kuwa tufanye kazi kwa bidii na maarifa ili kula tulivyozalisha laikini yeye anasema kuwa ziko pesa nyingi sana huko nje na kinachotakiwa ni jinsi unavyojipanga kuwaomba hao 'wafadhili', wala hawakunyimi! Na sisi tulivyo wavivu wa kazi tunafurahia maendeleo ya 'kuwekwa rehani' bila kuiwaza kesho.
Lakini kubwa kabisa wanaweza kuwa wanaangalia regime inayojigamba kwa rekodi ya kutoa wahitimu 600,000 wa Form IV huku hawajui hesabu za darasa la tano!!!!
Ni kweli hakuna mkamilifu, lakini.....
 
Back
Top Bottom