Jakaya Kikwete ndani ya Ifakara

ifa96

JF-Expert Member
Jul 25, 2014
435
222
Wakuu,

Mkuu wa kaya leo yupo Kilombero Mahenge,kesho atakuwa Ifakara kuzindua ujenzi wa daraja la mto Kilombero.

Mishemishe zilzokuwepo hapa sio mchezo, mkuu wa mkoa,mkuu wa wilaya mkurugenzi makada wanapitapita NAWAONA MAAFISA USALAMA KAMA 10.

Ninachojiuliza je, hizi pilka za polisi wilaya zote na mkoa pamoja na msafara wa magari yasiyopungua 50 fedha za wafuja jasho ndio zinatumika?

========

Rais azindua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa daraja la Kilombero


Magari yakivuka juu ya daraja la muda la Mto Kilombero lililojengwa kurahisisha kazi za ujenzi wa daraja la kudumu katika wilaya ya Kilombero Mkoa wa Morogoro, wakati wa sherehe za uwekaji jiwe la msingi wa ujenzi wa darajan hilo na Rais Jakaya Mrisho Kikwete Agosti 20, 2014.
PICHA NA IKULU

Magari yakivuka juu ya daraja la muda la Mto Kilombero lililojengwa kurahisisha kazi za ujenzi wa daraja la kudumu katika wilaya ya Kilombero Mkoa wa Morogoro, wakati wa sherehe za uwekaji jiwe la msingi wa ujenzi wa darajan hilo na Rais Jakaya Mrisho Kikwete Agosti 20, 2014.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipungia wananchi kwa furaha wakati akielekea ukingoni mwa Mto Kilombero kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la kudumu juu ya mto Kilombero Agosti 20, 2014. Anaoongozana nao ni pamoja na Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuri (kushoto kwa Rais), Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Mbunge wa Ulanga Mashariki Mhe. Celina Kombani (kulia), Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Joel Bendera (kushoto) na Mama Salma Kikwete (nyuma ya Rais)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishangiliwa baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la kudumu juu ya mto Kilombero Agosti 20, 2014. Pamoja naye ni Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuri (kushoto kwa Rais), Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Mbunge wa Ulanga Mashariki Mhe. Celina Kombani (kulia), Mbunge wa Mama Salma Kikwete (nyuma ya Rais), Mbunge wa Ulanga Magharibi Dkt Haji Ponda (kulia) na Mbunge wa Kilombero Mhe Abdul Mteketa (kulia kwa Rais)



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo toka Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Bw. Patrick Mfugale juu ya ujenzi wa daraja la kudumu juu ya mto Kilombero Agosti 20, 2014. Kushoto ni Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe, Magufuri akifuatiwa na Mama Salma Kikwete


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la kudumu juu ya mto Kilombero wilayani Kilombero mkoa wa Morogoro Agosti 20, 2014

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wananchi baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la kudumu juu ya mto Kilombero wilayani Kilombero mkoa wa Morogoro



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akijaribu madawati mapya ya shule ya msingi ya Epauko wilayani Mahenge baada ya shule hiyo kukabidhiwa msaada wa madawati 500 na Kampuni ya Kibaran Resources Ltd inayojishughulisha na uchimbaji wa madini aina ya Graphite na Nickel mkoani wa Morogoro Agosti 20, 2014



Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete na mmoja wa wanafunzi wa shule ya msingi ya Epauko wilayani Mahenge baada ya shule hiyo kukabidhiwa msaada wa madawati 500 na Kampuni ya Kibaran Resources Ltd inayojishughulisha na uchimbaji wa madini aina ya Graphite na Nickel mkoani Morogoro


KABLA YA UZINDUZI
UJENZI+WA+DARAJA+LA+MUDA+MTO+KILOMBERO..JPG
DARAJA+LA+MUDA+KILOMBERO..JPG

03++Kilombero+River.jpg



 
Kesho wakuu fuatilien uzi huu tutaendelea kuwajuza kila litakalojir
 
kwa hiyo ulitaka JK aende kwa daladala au unamahanisha magari ni mengi wengepunguza?
 
Kwani maafisa wa usalama wana sare hadi kuwatambua na kujua idadi yao? Ndo kazi ya bunge la bajeti. Hao wote wanao husika na hilo tukio pamoja na hivyo vitendea kazi na magari yakiwemo, bunge la bajeti lilipitisha kabla ya mwaka wa fedha 2014/2015.
 
Mkuu Felix kwa msafara mkubwa kama huo na mafuta yanayotumika kwa sababu zisizokuwa na msing ni bora apunguze msafara
 
Last edited by a moderator:
Mkuu gfesto we na ww gamba nn?Maana yake inaoneka ww huna huruma na fedha za wavuja jasho wa inch hii
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Felix kwa msafara mkubwa kama huo na mafuta yanayotumika kwa sababu zisizokuwa na msing ni bora apunguze msafara

hapo nimekusoma mkuu, mambo mengine wala si rais anataka migari yote hiyo. ni waandaji tu wa msafara hili wachakachuemo mafuta.
 
Mkuu gfesto we na ww gamba nn?Maana yake inaoneka ww huna huruma na fedha za wavuja jasho wa inch hii

Unadhani hilo fungu la hiyo ziara limetoka kwenye mfuko gani ambao pesa zake hazikuidhinishwa na bunge?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Felix kwa msafara mkubwa kama huo na mafuta yanayotumika kwa sababu zisizokuwa na msing ni bora apunguze msafara


Ukimuona amefanya ziara ya huko mikoani ujue kisha panga safari ya kwenda Ulaya/marekani na bila shaka akitoka huko tu utasikia yuko washington D.C.!!! Huyu Vasco Dagama hazionei huruma hizi hela za kodi yetu kwa vile yeye na ukoo wake wananjia za kuchota fedha kutoka vyanzo wanavyovijua wao ; baya zaidi afadhali hiyo misafara yake ingekuwa hapa hapa nchini tu lakini hata anapokwenda huko nje anatutia shoti kweli kwani huwa anaongozana na watu chungu nzima mpaka wapiga ramli wake anawabeba!!!
 
Raisi wa Tanzania hatumii magari mengi kama maraisi wengine, raisi wetu anapanda commercial
 
Mkuu gfesto kuidhinishwa na bunge c tatizo kwan we hutambui kuwa hata hizo zilizoizinishwa ni kod za wavuja jasho wa nchi hii?
 
Last edited by a moderator:
Ukimuona amefanya ziara ya huko mikoani ujue kisha panga safari ya kwenda Ulaya/marekani na bila shaka akitoka huko tu utasikia yuko washington D.C.!!! Huyu Vasco Dagama hazionei huruma hizi hela za kodi yetu kwa vile yeye na ukoo wake wananjia za kuchota fedha kutoka vyanzo wanavyovijua wao ; baya zaidi afadhali hiyo misafara yake ingekuwa hapa hapa nchini tu lakini hata anapokwenda huko nje anatutia shoti kweli kwani huwa anaongozana na watu chungu nzima mpaka wapiga ramli wake anawabeba!!!

Tehe teh teh mkuu anabeba mpaka wapiga raml? Jamaa kiboko
 
Mkuu @bules ulijuaje kesho 2 utaskia yuko urus au marekan
 
Wakuu mkuu wa kaya leo yupo kilombero mahenge,kesho atakuwa ifakara kuzindua ujenz wa daraja la mto kilombero,mishemishe zilzokuwepo hapa c mchezo mkuu wa mkoa,mkuu wa wilaya mkurugenz makada wanapitapita NAWAONA MAAFISA USALAMA KAMA 10 ninachojiuliza je iz pilka za polis wilaya zote na mkoa pamoja na msafara wa magar yasiyopungua 50 je hiz c fedha za wafuja jasho??

Posho mkuu
 
Kwani maafisa wa usalama wana sare hadi kuwatambua na kujua idadi yao? Ndo kazi ya bunge la bajeti. Hao wote wanao husika na hilo tukio pamoja na hivyo vitendea kazi na magari yakiwemo, bunge la bajeti lilipitisha kabla ya mwaka wa fedha 2014/2015.

ndio maafisa usalama wana sare mkuu au hujui polisi wana sare mbona
 
Back
Top Bottom