Jaji Werema akipona katika hili la IPTL natembea uchi

Jaji Werema akipona katika hili la IPTL natembea uchi

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
27,412
Reaction score
28,456
Naapa kwamba ikiwa Jaji Werema atanusurika kuangukiwa na rungu kufuatia skandali ya UFISADI wa ESCROW, nitatembea uchi barabarani kutoka nyumbani kwangu Pugu hadi Kivukoni.

Nimemkamia sana Werema kuliko wahusika wengine kwa sababu ya kiburi chake na kwa kuwa ameisababishia serikali hasara kubwa zaidi ukilinganisha na mafisadi wenzake waliohusika katika skandali nzima.

Sababu ya pili ya kumkamia huyu MWIZI inatokana na jinsi alivyokuwa akimkomalia Mh Kafulila na kumuita TUMBILI hadi mishipa inamtoka na macho kuwa mekundu huku akijua kwamba ameiibia serikali mabilioni ya shilingi.

Yaani wananchi wanakufa kama nzige mahospitalini kwa sababu serikali haina fedha za kununulia dawa wakati tumbili huyu ameipotezea serikali mabilioni ya shilingi!

Ndugu watanzania, endapo bunge halitamuwajibisha Werema na baadaye Profesa Kikwete kumfuta kazi na serikali kumfunga jela, sote tuandamane uchi kwenda Dodoma tukalichome moto jengo la bunge. Hakuna haja ya kuwepo kwake ikiwa haliwezi kumuwajibisha huyu MWIZI.

:israel:
 
Wewe anza kuchojoa, tayari tumeshasikia mahojiano ya takua ya siri, wenye akili wanajua nini kinafuata na mazingira gani yana tengenezwa hapo.
 
sasa tukichoma bunge si hasara nyingine? ukiibiwa bora hata ungesema tuwachome wabunge. Ukiibiwa unachoma mwizi sio, sio mali zako tena.
Halafu mambo ya kutembea uchi tena jitahihidi iwe usiku, mchana watoto wetu mkuu watakosa amani kuona viungo vya uzazi vya mtu mzima.
 
Na serikali imeshindwa kulipa wastahafu stahili zao kwa ajili ya mwizi huyu,no lazima aende segerea, kama sio leo,kesho.
Naapa kwamba ikiwa Jaji Werema atanusurika kuangukiwa na rungu kufuatia skandali ya UFISADI wa ESCROW, nitatembea uchi barabarani kutoka nyumbani kwangu Pugu hadi Kivukoni.

Nimemkamia sana Werema kuliko wahusika wengine kwa sababu ya kiburi chake na kwa kuwa ameisababishia serikali hasara kubwa zaidi ukilinganisha na mafisadi wenzake waliohusika katika skandali nzima. Sababu ya pili ya kumkamia huyu MWIZI inatokana na jinsi alivyokuwa akimkomalia Mh Kafulila na kumuita TUMBILI hadi mishipa inamtoka na macho kuwa mekundu huku akijua kwamba ameiibia serikali mabilioni ya shilingi. Yaani wananchi wanakufa kama nzige mahospitalini kwa sababu serikali haina fedha za kununulia dawa wakati tumbili huyu ameipotezea serikali mabilioni ya shilingi!

Ndugu watanzania, endapo bunge halitamuwajibisha Werema na baadaye Profesa Kikwete kumfuta kazi na serikali kumfunga jela, sote tuandamane uchi kwenda Dodoma tukalichome moto jengo la bunge. Hakuna haja ya kuwepo kwake ikiwa haliwezi kumuwajibisha huyu MWIZI.

:israel:
 
sasa tukichoma bunge si hasara nyingine? ukiibiwa bora hata ungesema tuwachome wabunge. Ukiibiwa unachoma mwizi sio, sio mali zako tena.
Halafu mambo ya kutembea uchi tena jitahihidi iwe usiku, mchana watoto wetu mkuu watakosa amani kuona viungo vya uzazi vya mtu mzima.

sawa mkuu, ila ni bora hilo bunge lichomwe kwa kuwa halina faida yoyote kwa watanzania. ikiwa wabunge wanaoketimo hawawezi kutusaidia kumuwajibisha MWIZI kuna haja gani ya kuwepo kwa hiyo 'white elephant'? inauma sana kuona jinsi mafisadi yanavyotafuna fedha za umma wakati wakifa muhimbili kwa kukosa dawa!
 
sawa mkuu, ila ni bora hilo bunge lichomwe kwa kuwa halina faida yoyote kwa watanzania. ikiwa wabunge wanaoketimo hawawezi kutusaidia kumuwajibisha MWIZI kuna haja gani ya kuwepo kwa hiyo 'white elephant'? inauma sana kuona jinsi mafisadi yanavyotafuna fedha za umma wakati wakifa muhimbili kwa kukosa dawa!

kaza moyo, tufanye mpango wa kuwachoma wabunge, lile jengo letu wenyewe tukichoma tutajenga tena kwa hela zetu wenyewe, hapo na sisi tuna IPTL nyingine. hasara yetu tuweke kwenye kuelimisha wasioelewa na kwenye kupiga kura, sio kuchoma nyumba, hawa jamaa hela zao zipo swis mambo yakiwa hovyo wanatambaa faster, mimi na wewe tunabaki na magofu.
 
Pamoja kwamba ni mkurya mwenzangu ila hii ni aibu ya kufunga mwaka
Ila pia kila aliyehusika afungwe jela
 
Hii ni Tanzania bana maandamano wanayaweza wenzetu ambako kuna uzalendo wa kweli kama Hong Kong, n.k, Watanzania wengi tatizo njaa na tamaa badala ya kuandamana kweli mnaaza kuiba vitu vya wanyonge hao hao mnaodai kuwatetea sasa sijui utakuwa na tofauti gani wewe na Werema maana ultimately wote ni wezi, tu.
 
kumbe ndio maana Werema alikuwa mkali sana kipinfi kile na kumuita Kafulila tumbili...okweeeey
 
Naapa kwamba ikiwa Jaji Werema atanusurika kuangukiwa na rungu kufuatia skandali ya UFISADI wa ESCROW, nitatembea uchi barabarani kutoka nyumbani kwangu Pugu hadi Kivukoni.

Nimemkamia sana Werema kuliko wahusika wengine kwa sababu ya kiburi chake na kwa kuwa ameisababishia serikali hasara kubwa zaidi ukilinganisha na mafisadi wenzake waliohusika katika skandali nzima. Sababu ya pili ya kumkamia huyu MWIZI inatokana na jinsi alivyokuwa akimkomalia Mh Kafulila na kumuita TUMBILI hadi mishipa inamtoka na macho kuwa mekundu huku akijua kwamba ameiibia serikali mabilioni ya shilingi. Yaani wananchi wanakufa kama nzige mahospitalini kwa sababu serikali haina fedha za kununulia dawa wakati tumbili huyu ameipotezea serikali mabilioni ya shilingi!

Ndugu watanzania, endapo bunge halitamuwajibisha Werema na baadaye Profesa Kikwete kumfuta kazi na serikali kumfunga jela, sote tuandamane uchi kwenda Dodoma tukalichome moto jengo la bunge. Hakuna haja ya kuwepo kwake ikiwa haliwezi kumuwajibisha huyu MWIZI.

:israel:

Bunge halina madaraka/mamlaka ya kumuwajibisha Werema (AG), mwenye madaraka ya kumuwajibisha Werema ni RAIS!

Bunge linayo madaraka/mamlaka ya kumuwajibisha RAIS au Waziri Mkuu lakini sio AG
 
Mimi nafatilia kwa karibu aliyesema makaratasi yetu niya kufungia vitumbua. Hivi mkoa wa Mara wote ni ma Tyson.Je aliyetaka kupigana anasema nini na uongo wake?
 
Bunge halina madaraka/mamlaka ya kumuwajibisha Werema (AG), mwenye madaraka ya kumuwajibisha Werema ni RAIS!

Bunge linayo madaraka/mamlaka ya kumuwajibisha RAIS au Waziri Mkuu lakini sio AG

Kwani kwenye Richmond ilikuwa je? Si alipiga kelele nimedhalilishwa sana na kuonewa sana,halafu akatokomea leo eti awe mkuu wa nchi.Huyu mwingine atakumbuka miziga yake ya asali,acha Waziri mkuu akaline asali si ataitwa waziri mkuu MSTAAFU.
 
Kiongozi jiangalie sana pale Gongolamboto kuna wahuni watataka hiyo nnya halafu ikawa balaa mkuu wangu. Hivi unajua kuwa anayeongoza mahojiano na Werema naye aliwahi kuhojiwa kuhusu mabilioni ya uswisi na akakiri mbele ya kiapo kuwa hana jina hata moja analolijua na kwamba mabilioni ilikuwa ni mbwembwe tu.

Sasa mkuu wangu wewe uko nyumbani kwako Pugu wenzio wako Dodoma tena ndani ya USIRI mkubwa then utembee uchi na kuweka nnya yako rehani!!! Think twice kiongozi jiangalie
 
Usijiapize mkuu serikali ya mafisadi si wajinga kiasi hicho, lolote laweza fanywa na baada ya uchaguzi suala hilo likawa limesahauliwa kabisa.
 
....bunge litachomwa moto endapo wanamuokoa tumbilies
 
Werema ni jitu la hovyo kabisa! limesoma lkn hajaelimika hata chembe. Kafulila alionyesha ni mtu mwerevu zaidi ya huyu aliyepewa dhamana kubwa lkn bure kabisa.
 
Back
Top Bottom