Jaji Sinde Warioba kanishangaza

Jaji Sinde Warioba kanishangaza

Nashindwa kumuelewa jaji Warioba kuhusu katiba yeye kasimamia wapi maana anaowanadi sasa hivi walimtukana mpaka kumpiga kisa alikuwa na msimamo juu ya katiba ya wananchi.

Ebu tujadili; je, na yeye kakubali katiba pendekezwa?
Umuelewi kivipi wakati Warioba ni kada wa CCM muda mrefu wewe ulidhani yupo Ukawa?
 
Unachoshindwa kumuelewa ni kipi hasa?

Msimamo wake kuhusu katiba kabadilisha?

Hawezi kukiunga mkono chama chake katika kampeni za urais kama anatofautiana nacho kuhusu katiba?

Kuna watu ili akuelewe ni lazima ufanye kama anavyotaka/anavyofikiri yeye hata kama haelewi kwanini wewe unafanya hivyo!
 
Nashindwa kumuelewa jaji Warioba kuhusu katiba yeye kasimamia wapi maana anaowanadi sasa hivi walimtukana mpaka kumpiga kisa alikuwa na msimamo juu ya katiba ya wananchi.

Ebu tujadili; je, na yeye kakubali katiba pendekezwa?

Kwani Chadema na Ukawa wanaongelea nini kuhusu katiba mpya? Lowasa ana msimamo gani?
 
Wamesaliti kazi yao iliyo bora,Wamewasaliti wananchi Maskini NA sasa hawazungumzii tena katiba mpya zaidi ya kupambana NA LOWASSA. Magufuli akishinda Urais hawezi kubadilisha msimamo WA bunge maalum LA katiba lililo pitisha katiba pendekezi zaid ya kufanya referendum.WARIOBA NA POLEPOLE wametuacha kwenye mataa sisi wakulima maskini.hawatakua NA jipya kwa wananchi tena zaidi ya sisi kuwaona wasaliti.

Wasalaam
Abel sere from Moshi
Chadema ndiyo wamewasaliti upinzani na kuungana na mafisadi
 
Hata Saed kubenea, waliomwagia tindikali ndio hao sasa anawaandika vizuri, kwahiyo ushishangae ya Warioba anza kwanza na ya kubenea. hii ndio tz kama huijui


Duh!
Mkuu umenimaliza sana kwa kicheko.
 
Namuheshimu sana Jaji Warioba, lakini kwa hili la kukubali kutumika pamoja na kutukanwa sana na kupigwa kwa baraka ya chama hicho hicho, na bado akasimama nao jana linampunguzia sana heshima kwangu.. Nakumbuka Bulembo alivyomtukana huyu mzee and yet jana wakawa jukwaa moja..!

......... vipi kwa Ukawa kuchukuwa makapi ya CCM ambao walishiriki kuipiga chini Katiba ya Wananchi !?? sosoliso
 
Last edited by a moderator:
Sio Siri..Jaji Warioba ameingia chaka.Ni dhahiri huyu bwana ni kigeugeu.Bora angekaa kimya kama mawiri wakuu wastaafu wenzake kama Salim Ahmed Salim,Msuya na Malecela.
#Hapa Kazi tu..kula kwenu.
 
pochi imebadilisha upepo!


Chambia Chadema.JPG
 
pochi imebadilisha upepo!

Kama pochi imebadili upepo, ina maana kuwa hata ule upepo wa awali wa kuilika ccm na serikali ulikuwa umesababisabishwa ba pochi.
Basi pochi limezidiwa na pochi.
Cheni feki kwa pesa feki.
 
Sio Siri..Jaji Warioba ameingia chaka.Ni dhahiri huyu bwana ni kigeugeu.Bora angekaa kimya kama mawiri wakuu wastaafu wenzake kama Salim Ahmed Salim,Msuya na Malecela.
#Hapa Kazi tu..kula kwenu.

Hujaeleza ameingia chaka kivipi na kwa nini ni kigeu geu.

Inawezekana unashindwa kumuelewa kwa kukosa uchambuzi wa kina utakaoweza kuelewa kwamba mtu anaweza kutokubaliana na chama chake kwenye masuala fulani lakini pia akaona hakijapata mbadala na hivyo kuamua kukiunga mkono katika kampeni na kubaki kama chachu ya mabadiliko kutoka ndani ya chama hicho.

Usichoelewa hapo ni nini?

Au wewe kumuelewa mtu ni lazima afikiri kama wewe na kuunga mkono fikra unazounga mkono wewe?
 
Hujaeleza ameingia chaka kivipi na kwa nini ni kigeu geu.

Inawezekana unashindwa kumuelewa kwa kukosa uchambuzi wa kina utakaoweza kuelewa kwamba mtu anaweza kutokubaliana na chama chake kwenye masuala fulani lakini pia akaona hakijapata mbadala na hivyo kuamua kukiunga mkono katika kampeni na kubaki kama chachu ya mabadiliko kutoka ndani ya chama hicho.

Usichoelewa hapo ni nini?

Au wewe kumuelewa mtu ni lazima afikiri kama wewe na kuunga mkono fikra unazounga mkono wewe?

Mkuu Kiranga utakesha bure na hawa vijana wa Bavicha.Wao akili zao washaweka mfukoni,Mbowe ndo anaamua.
 
Last edited by a moderator:
Fisadi gani huyo? Ni yule/wale waliohusishwa na ESCROW scandal; maana hao bado wamo ndani ya chama kilichochoka. Gamba ambalo "tayari limevuka" halikushiri escrow hivyo mchawi anayeiua CCM bado yungalimo ndani ya CCM.

Hujui chanzo cha escrow ww? Mulize fisadi papa.
 
Mlidgani warioba ni mpumbavu na lofa kama nyinyi?

Acha utovu wa nidhamu. Hivi unajua kuwa nchi hii imedumu hadi wewe kuzaliwa kutokana na hekima, busara na subira za watu kama mzee warioba?! Hivi unajua kuwa endapo watu fasta fasta kama wewe wangekuwa wengi kungekuwa hakuna hata nchi kama hii ambayo kila mtu akiamka anatukana wakunga uzazi ungalipo? Subiri kitambo si kidogo yaja nchi kama hiyo ambapo wewe utakuwa umezeeka na ndiyo hapo utakapokiri na kuomba msamaha kimya kimya kuwa heri waendao kuliko wajao. Tema mate chini upesi!!!!
 
Fisadi gani huyo? Ni yule/wale waliohusishwa na ESCROW scandal; maana hao bado wamo ndani ya chama kilichochoka. Gamba ambalo "tayari limevuka" halikushiri escrow hivyo mchawi anayeiua CCM bado yungalimo ndani ya CCM.

Chanzo cha escrow ni nini!?
 
Back
Top Bottom