Danny greeny
JF-Expert Member
- Feb 6, 2014
- 3,856
- 1,648
Umoja Kamili wa Wapumbavu = UKAWA oyooooooooooooooooooooooooo Wapumbavuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu (in Mkapa's Voice)
Ikumbukwe kuwa Jaji Warioba alikuwa akizunguka kutoa elimu ya uraia pamoja na kueleza wananchi jinsi maoni yao yalivyotupwa kwenye rasimu ya katiba jambo ambalo lilifanya atukanwe, adhihakiwe, adharauliwe na hata kudaiwa kupigwa.
Kilichonishangaza ni yeye kusimama jana na kupiga kampeni kwa wagombea, wakati kwanza chama hicho ndo kilihusika kusigina maoni ya wananchi, pili mmoja wa wagombea alikuwa makamu mwenyekiti bunge la katiba sasa Mh. Warioba ulikuwa unazunguka kufanya nini kwa wananchi ikiwa leo una wanadi waliosigina maoni ya wananchi?
Sikutegemea kwa kweli, sasa vipi ile rasimu ya wananchi ndo huitetei tena? Nimewaza kwa sauti wajamaeni.
Ana umezo Wa kukududua hata saa nzimaYani mnaomshabikia lowassa poleni hata sijui kama atweza kuongea hata dk 30
Umepena kuyasema hayo! mimi si ccm kamwe na sijawai kuwa ccm wala cdm ispokuwa natambua mtamsema vibaya yeyote yule atakae wakosoa, siasa ni kukosoana sasa mnapo panic mkosolewapo hamjui siasa mnafuata mkumboHii ndio ajira yako wengi tunalijua hilo. Hivi kama tukiamua wote humu ndani kussupport cCM kwa kila Jambo utalipwaje?
huyu si ndio maana alipigwa na makonda, asipoangalia atadundwa tena
Huyu Huyu Mzee Warioba Ndiye Alipigwa Na MaCCM Wenzake Kwa Sababu ya Kushaabikia rasimu yake ya Katiba. Leo Ni
Kimbembele wa Kuishaabikia CCM. Kweli CCM Ni Ile Ile..Do Hata Dr. Magufuli Hawezi Lolote Kwa MiCCM.
Alicho fanya mzee warioba nisahihi kwakuwa hakuna chama cha upinzani ndio maana amepanda ktk jukwa la ccm A kama alivyo sema mzee mwinyi.
Laiti wapinzani wasinge uza vyama vyao kwa maccm B mzee warioba asingeweza kufanya alivyo fanya.
Jaji Warioba aliongoza tume kukusanya maoni ya wananchi na kuandaa rasimu kwa kuzingatia maoni hayo. Kazi ambayo aliifanya kwa umakini na uaminifu mkubwa na ameingia katika vitabu vya historia ya Tanzania kwa mchango wake huo mkubwa na uliotukuka, na ndio maana rasimu hiyo itaendelea kurejelewa kama 'Rasimu ya Warioba' hata baada ya miaka mia. Lakini hiyo haina maana kuwa ni mali yake au yaliyomo ni mawazo ya Warioba au ya mwanaTume ye yote, bali ni maoni ya wananchi wa Tanzania. Kwa hivyo hata akihama nchi au kuchukua uraia wa Rwanda (kwa mfano), hayo maoni yataendelea kuwa ya wananchi wa Tanzania na mali ya Wananchi. Kwa hivyo basi kujiunga kwake tena na timu ya kutetea mafisadi wa CCM (kumbuka na yeye hajawahi kuikana CCM), haihalalishi UKAWA waache kutetea maoni ya wananchi. Ni mtu mwenye uelewa wa kiwango cha chini anayeweza kunena kuwa "Ukawa haina pakusimamia, imekufa kabla hata ya Oktoba kufikia, tunashukuru kuona wazee kama hawa wakijitokeza na kuwaumbua hadharani hawa watu." Na mtu mwenye fikira kama hizi si kosa lake, bali ni matokeo kuntu ya elimu za kata (sekondari na vyuo). Mzee Warioba ni haki yake kupigia kampeni CCM kama UKAWA walivyo na haki yao kutetea na kupigania maoni ya Wananchi kuzingatiwa katika Katiba mpya.S
Kifupi ni kwamba UKAWA imekufa na imepoteza uhalali wake kimantiki tokea siku ile ilipoanza kukumbatia watu wenye tuhuma mbali mbali kama watu wake wa karibu. Jambo hili si dogo na limemfanya mwasisi wa madai yao kuwakana hadharani.
Ni jambo la heri mno kwa Mh. jaji Mstaafu kuona kua kikundi hicho ni cha wababaishaji, na watumiaji wa uelewa mdogo wa wananchi katika mambo flani kujinufaisha kisiasa kwa malengo binafsi.
Ukawa haina pakusimamia, imekufa kabla hata ya Oktoba kufikia, tunashukuru kuona wazee kama hawa wakijitokeza na kuwaumbua hadharani hawa watu.
Fisadi gani huyo? Ni yule/wale waliohusishwa na ESCROW scandal; maana hao bado wamo ndani ya chama kilichochoka. Gamba ambalo "tayari limevuka" halikushiri escrow hivyo mchawi anayeiua CCM bado yungalimo ndani ya CCM.Amefnya hivyo kwa sababu gamba tayari limevuka, Fisadi hayupo tena CCM, Nachama kimebaki salama