Jaji Sinde Warioba kanishangaza

Jaji Sinde Warioba kanishangaza

Wachawi walishaondoka ccm sasa safi tunajimwayamwaya magufuli ndio rais anasubiri kuapishwa tu
 
hasara ambayo mimi nimeipata kutokana na warioba kufungamana na ccm haisemeki , wakati wa vuguvugu la katiba mpya mke wangu alijifungua mtoto wa kiume , kwa heshima ya huyu mzee nikampachika mwanangu jina la warioba , sasa katika hali kama hii nafanyaje ?
 
ikumbukwe kuwa jaji warioba alikuwa akizunguka kutoa elimu ya uraia pamoja na kueleza wananchi jinsi maoni yao yalivyotupwa kwenye rasimu ya katiba jambo ambalo lilifanya atukanwe, adhihakiwe, adharauliwe na hata kudaiwa kupigwa.

Kilichonishangaza ni yeye kusimama jana na kupiga kampeni kwa wagombea, wakati kwanza chama hicho ndo kilihusika kusigina maoni ya wananchi, pili mmoja wa wagombea alikuwa makamu mwenyekiti bunge la katiba sasa mh. Warioba ulikuwa unazunguka kufanya nini kwa wananchi ikiwa leo una wanadi waliosigina maoni ya wananchi?

Sikutegemea kwa kweli, sasa vipi ile rasimu ya wananchi ndo huitetei tena? Nimewaza kwa sauti wajamaeni.

siasa za ukanda ndo zinazomgharimu ivi hamjashtuka tu jamani mbona iko wazi magufuli naye ana harufu ya ukanda wa ziwa
 
hasara ambayo mimi nimeipata kutokana na warioba kufungamana na ccm haisemeki , wakati wa vuguvugu la katiba mpya mke wangu alijifungua mtoto wa kiume , kwa heshima ya huyu mzee nikampachika mwanangu jina la warioba , sasa katika hali kama hii nafanyaje ?

Moja.

Nani kakutuma umpe mtu jina la mtu ambaye hajafa bado na historia yake bado inaandikwa?

Pili,

J. S Warioba does not own that name. Kuna kina Warioba mpaka kina Ryoba.

Sasa tatizo lako liko wapi?
 
Ikumbukwe kuwa Jaji Warioba alikuwa akizunguka kutoa elimu ya uraia pamoja na kueleza wananchi jinsi maoni yao yalivyotupwa kwenye rasimu ya katiba jambo ambalo lilifanya atukanwe, adhihakiwe, adharauliwe na hata kudaiwa kupigwa.

Kilichonishangaza ni yeye kusimama jana na kupiga kampeni kwa wagombea, wakati kwanza chama hicho ndo kilihusika kusigina maoni ya wananchi, pili mmoja wa wagombea alikuwa makamu mwenyekiti bunge la katiba sasa Mh. Warioba ulikuwa unazunguka kufanya nini kwa wananchi ikiwa leo una wanadi waliosigina maoni ya wananchi?

Sikutegemea kwa kweli, sasa vipi ile rasimu ya wananchi ndo huitetei tena? Nimewaza kwa sauti wajamaeni.

Hoja yako haina mashiko, jaji warioba hakuwa upande wa upinzani hara mara moja,alitimiza wahibu wake kwa wananchi si kwa ukawa pekee(tafadhali usizingatie tafsiri ya ukawa hapa).
Baada ya kumaliza kazi anawajibu kwa chama chake na sasa anatimiza wajibu wake sasa wewe kipi kilichokusukuma uamini kuwa Warioba alipaswa kuwa upinzani?
Labda uniambie kuwa ulikuwa hujui jjukumu alilopewa Jaji Warioba na wenzake!
 
Ulitakiwa uaenze kujishangaa wewe mwenyewe kwa kushangilia watu mliowatukana kwa miaka mingi na leo ndo wanaongoza chama
 
Namuheshimu sana Jaji Warioba, lakini kwa hili la kukubali kutumika pamoja na kutukanwa sana na kupigwa kwa baraka ya chama hicho hicho, na bado akasimama nao jana linampunguzia sana heshima kwangu.. Nakumbuka Bulembo alivyomtukana huyu mzee and yet jana wakawa jukwaa moja..!

Limempunguzia heshima kwa nani, ukawa au ccm. Kwani ukawa mambo ya ccm yanawahusu nini. Warioba kasema chadema walisusia bunge la katiba na ajenda yao ni kuvunja muungano tu. Ccm bado tunamuheshimu sana, si mlitaka agombee kupitia chadema akagoma, mkaona mumsubiri mpiga dili.
 
Anatumika kwa sababu ya mwanae anayegombea ubunge, sio mzalendo kivile nae ni mchumia tumbo
 
Ccm wote sasa wanapigania maslahi yao,baada ya kustaafu wanalipwa peasa nyingi na kusaidiwa,wanaogopa nchi ikichukuliwa na upande wa pili maslahi yao yote yataangaliwa upya au yatapotea kabisa,tumbo kwanza
 
Je UKAWA iliyowaita Sumaye na Lowassa ni mafisadi si wanafiki..!!? Hekima ya Warioba ni kubwa kuliko watu wengi wanaochangia hii mada. Kila mtu anautashi wake wa kufikiri mambo.
 
kuna kijana 1 alisema kama wangejua huyu mzee ni msanii. Wangemwacha siku ile Makonda amnyooshe Bara Bara.
 
Moja.

Nani kakutuma umpe mtu jina la mtu ambaye hajafa bado na historia yake bado inaandikwa?

Pili,

J. S Warioba does not own that name. Kina kina Warioba mpaka kina Ryoba.

Sasa tatizo lako liko wapi?
asante nimechukua hiyo ya pili maana imeifuta ile ya kwanza .
 
Back
Top Bottom