Jaji mstaafu Mark Bomani naye atoa mpya..

Kichekesho kipo kwa Dr. Slaa kususa ilhali wenzake wanakula!

Kibs bana... wewe unachojua ni kula na kunywa tu!! talking about mkulima kula mbegu, ndiyo maana hata mbegu za demokrasia nchini CCM wameamua kuzibugia!!! :)
 
Imebidi nikugongee ka button ka thank mhe. Kichuguu. Bado siamini kama ni mwalimu. Maana unavyochambua sheria kama lwyer vile. Au mwalimu wa sheria?
 
Duh hapa Mkuu wangu Bomani kachemsha.. Dr.Slaa na wengine wote wanaweza kupinga uchaguzi wowote ule kulingana na ushahidi uliopo. Sidhani kama anaelewa kwamba hao hao Wabunge wanatetea nafasi walizogombania na wapo wasiokubali matokeo ya ngazi walizogombea.

Sasa ni maajabu sana kuona Jaji Bomani akimzungumzia Dr.Slaa ambaye ndiye mgombea kutotambua matokeo ya Urais kiti ambacho aligombea. Mbona hakumzungumziakina Mpendazoe na wengine waliopinga pia matokeo yao? au alitaka Dr.Slaa awe msemaji mkuu wa wabunge na madiwani wote waliopinga matokeo?
 
It takes courage to listen to this ageing zinjanthropus. One of the main characteristics of zinjanthropus (in this case Bomani) was a very small brain. Therefore their logical thinking was impaired. Nafikiri wakati umefika hawa wasomi wasiojua dot com watuachia tuamue mustakabali wetu
 
It takes courage to listen to this ageing zinjanthropus. One of the main characteristics of zinjanthropus (in this case Bomani) was a very small brain. Therefore their logical thinking was impaired. Nafikiri wakati umefika hawa wasomi wasiojua dot com watuachia tuamue mustakabali wetu

How I wish this was possible.............................................
 
Kichekesho kipo kwa Dr. Slaa kususa ilhali wenzake wanakula!

Wewe ndo unaliwa na utaliwa kwa miaka mitano ijayo. Acha uchama wewe! Watanzania wanaumia afu unaleta ujinga! We ndo unafikiri Slaa ndo anaumia hapa? Kuna watu wananiudhi humu ndani!
 
Ni mtizamo tu, Maalim Seif - CUF alipokataa uchaguzi wa urais Zanzibar pia wajumbe wa baraza la wawakilishi walienda kuapishwa kisha wakaweka mgomo moja kwa moja wa kutoshirikiana na serikali ya rais wasiyemtambua kwa sababu kwa kushirikiana na serikali yake bungeni ni sawa na KUHALALISHA KUWEPO kwa hiyo serikali haramu. To me it make a lot of sense. kwa sababu hamna " half pregnancy" its either you are pregnant or you are not. Au naweza kusema kwa lugha nyingine umempa msichana mimba unaikataa kabisa mtoto akizaliwa wewe unaenda kumpa jina na matumizi ukiambiwa unapeleka, its no sense. Haiwezekani umkatae rais halafu mnakaa bungeni na huyo rais kupanga mipango ya maendeleo, bajeti n.k.
Pamoja na kwamba kuna watakao bisha saaaana kwa kushindwa kuwaza 'outside the box' sababu ya fikra zao kuwa ndani ya box la Dr Slaa akili na vichwa vyao havifikiri, ukweli utabaki pale pale kwamba CHADEMA ni dhaifu sana katika kuchambua mambo na wabinafsi ndiyo maana wanamkataa rais JK lakini wamempigia kura spika, waziri mkuu na watashirikiana na serikali. mimi naona ni UTOTO sana kwa wale wenye akili tumeisha dharau kauli ya eti hawamtambui JK. Pia hii ni moja ya sababu CUF wamewaona CHADEMA ni wachemshaji hivyo kuona hamna sababu ya kuungana nao kwavile ni kondoo tu.
 
Duh hapa Mkuu wangu Bomani kachemsha.. Dr.Slaa na wengine wote wanaweza kupinga uchaguzi wowote ule kulingana na ushahidi uliopo. Sidhani kama anaelewa kwamba hao hao Wabunge wanatetea nafasi walizogombania na wapo wasiokubali matokeo ya ngazi walizogombea.

Sasa ni maajabu sana kuona Jaji Bomani akimzungumzia Dr.Slaa ambaye ndiye mgombea kutotambua matokeo ya Urais kiti ambacho aligombea. Mbona hakumzungumziakina Mpendazoe na wengine waliopinga pia matokeo yao? au alitaka Dr.Slaa awe msemaji mkuu wa wabunge na madiwani wote waliopinga matokeo?
Niliposikia habari hizi zikisomwa katika gazeti asubuhi, nilianza kujiuliza kwamba kama hawa ndio majaji wetu, then ndio sababu tunapata shida na ile tunayoiona hata pale NEC. Na kama ulifuatilia utetezi wa Kiravu siku anaulizwa maswali na waandishi kuhusu efficiency na credibility ya NEC wakati wote alitaka kusogeza sura za wakina Makame kama watu waliotukuka kazini na wana credibility ya hali ya juu kwa hiyo tuone kuwa NEC ni chombo safi.
Niliona Mh Bomani amepotoka au amejaribu tu kudanganya as usual ili tuone DR Slaa hana uhalali wa kutomtambua rais aliyewekwa kwa matokeo ya kuchakachuliwa.
Kwanza sijui anajua kuwa kwa sheria zetu mbovu ambazo yeye binafsi kashindwa kuzipigia kelele, Dr Slaa hana jinsi nyingine yoyote ya kujitetea akionewa kwa kutopewa haki. Na kwa sababu hana haki hiyo, kwa hiyo lazima akubali kuonewa? Si ni afadhali hata kama kanyimwa haki aseme tu nimeonewa na kufanya kama tulivyokuwa tunafanya tukiwa wadogo, unazila kula? kitu ambacho amekifanya?
Lakini pia ajue wabunge wana haki tofauti kisheria maana wao wanaweza ku petition mahakamani wakionewa! Lakini si Dr Slaa! Ingawa bado yeye kama mwanasheria sijui kama anajua kuna kesi za uchaguzi za 2005 bado hazijatolewa hukumu na mahakama na hawezi kusema lolote kuhusu uonevu, hujuma na dhuluma kama hizo wakati kuna kesi za wakina Mramba karibu hukumu zinatoka? Huu si uzee sijui niite ni nini! Naomba Mungu asinipe uzee uliopunguzwa hekima.
Sawa bwana ngoja tumuache mzee naona hekima inaondoka na anaweza kusimama kutetea dhuluma. For whose interest? nadhani anajua mwenyewe.
 
Ni mtizamo tu, Maalim Seif - CUF alipokataa uchaguzi wa urais Zanzibar pia wajumbe wa baraza la wawakilishi walienda kuapishwa kisha wakaweka mgomo moja kwa moja wa kutoshirikiana na serikali ya rais wasiyemtambua kwa sababu kwa kushirikiana na serikali yake bungeni ni sawa na KUHALALISHA KUWEPO kwa hiyo serikali haramu. To me it make a lot of sense. kwa sababu hamna " half pregnancy" its either you are pregnant or you are not. Au naweza kusema kwa lugha nyingine umempa msichana mimba unaikataa kabisa mtoto akizaliwa wewe unaenda kumpa jina na matumizi ukiambiwa unapeleka, its no sense. Haiwezekani umkatae rais halafu mnakaa bungeni na huyo rais kupanga mipango ya maendeleo, bajeti n.k.
Pamoja na kwamba kuna watakao bisha saaaana kwa kushindwa kuwaza 'outside the box' sababu ya fikra zao kuwa ndani ya box la Dr Slaa akili na vichwa vyao havifikiri, ukweli utabaki pale pale kwamba CHADEMA ni dhaifu sana katika kuchambua mambo na wabinafsi ndiyo maana wanamkataa rais JK lakini wamempigia kura spika, waziri mkuu na watashirikiana na serikali. mimi naona ni UTOTO sana kwa wale wenye akili tumeisha dharau kauli ya eti hawamtambui JK. Pia hii ni moja ya sababu CUF wamewaona CHADEMA ni wachemshaji hivyo kuona hamna sababu ya kuungana nao kwavile ni kondoo tu.
Out of point. Sijui unazungumzia nini. Jamani nisaidieni nimuelewe naona sijui hajui tunachozungumza?
 
Ivi senesence si ndio negative growth jamani kwa biologia yangu ndogo
 
Kuna wakati wazee kama hawa inabidi watafakari kwanza kabla ya kuingia na kujadili masuala..kuna 'ujinga' wa kudhani kuwa kila watakachoongea kina 'busara'..ni 'ujinga' tu kufikiri na kuamini hivyo..Huyu huyu Bomani na wenzake (wasomi wengine wa kanda ya Ziwa wa Zamani) WAMEKAA TU NA KUBWETEKA WAKATI ULE WOTE WALIPOKUWA NA POWER ya kuweza 'kuchambua na kushauri' vema wakubwa wa nchi hii..na hata kushinikiza..uchoporaji,ubakaji na unyonyaji wa rasilimali za huko, huku watanzania kwa ujumla hawanufaiki, wakibaki maskini wa kutupwa..Sasa wafikie mahali 'wakiri kuwa hawakutimiza wajibu wao ipasavyo..plz mzee nyamaza
 
mpuuzeni wee kwa nyie wenye akili, ila mwananchi wa kawaida sana naye anachanganyikiwa kuhusu hii issue ya chadema, kuwa rais kateua jina la waziri mkuu, Tundu Lissu anaambiwa akahesabu kura na anakubali anaenda, the very same president ambaye hawamtambui, this issue ikijadiliwa kwa ushabiki tu ni kupeana moyo, ila critically kuna ya kufanya, kukataa matokeao ya urais na rais husika , ni jambo zito ambalo inabidi liende kwa vitendo!!
 
Out of point. Sijui unazungumzia nini. Jamani nisaidieni nimuelewe naona sijui hajui tunachozungumza?

huwezi kujua kwa sababu uko ndani ya 'box' la dr slaa hivyo uwezo wa kufikiri umeisha. try to get out of the box and think objectively as a learned brother
 
......Hivyo ana masilahi mazito ya ubia ................................Ama kwa hakika Jaji Mstaafu Mark Bomani ametoa mpya hii ya kujidhalilisha machoni mwa jamii........


kwenye bold: Safari, kilimanjaro,ndovu, castle, bingwa, castle lite, milk stout, reds, ............to mention a few
 
Jaji Bomani, ni mtu anayeheshimika katika jamii yetu na hivyo sio wa kupuuzwa hata kama ametofautiana na msimamo wa Chadema, the same applies to Jaji Warioba, Jaji Mfalila, Salim Salim, Ibrahim Kaduma etc, wale waumini wazuri wa Mwalimu Nyerere.

Pasco
Hakuna waumini wa nyerere, kama kweli wangekuwa waumini wa Nyerere wasingekubali kuiona tanzania inakuwa hivi ilivyo sasa na wao wakiangalia au kuchangia kuiangamiza TZ.
 
Jaji Bomani, ni mtu anayeheshimika katika jamii yetu na hivyo sio wa kupuuzwa hata kama ametofautiana na msimamo wa Chadema, the same applies to Jaji Warioba, Jaji Mfalila, Salim Salim, Ibrahim Kaduma etc, wale waumini wazuri wa Mwalimu Nyerere.

Hivi heshima ni kukubali asemacho au afanyacho mtu hata kama sio sawa???:doh:

Nwyz kama wengine Mzee anafuata nyuki ale asali.....bila hata kua na uhakika kama atapata hiyo asali au ataambulia kung'atwa!!!
 
Back
Top Bottom