Nilipoleta Uzi kuhusu Utata wa Umri wa Jaji Mkuu, sikuwa na shaka kuwa sheria inasema ajiuzulu akiwa na miaka 65. Tatizo kubwa katika mjadala wote tangu jana, ni baadhi ya wachunguzi wakiwemo wa Idara yake kusema kuwa alizaliwa 4/9/1949, lakini kutokana sababu ambazo bado hazijawa wazi, wakati jaji Mkuu Augustino Ramadhani anastaafu, kuna Jaji Mwingine aliarifiwa kuwa angekuwa Jaji Mkuu. Haikujulikana ni kwa sababu zipi, kwa ushauri wa ndugu yake, Rashid Othman, Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa, ilibadilishwa ghafla, akateuliwa Jaji Mohamed Othman Chande, na tarehe ikawa 1/1/1952. Utata ulianzia hapa, kama alizaliwa mwaka 1952, na kusoma hadi kumaliza Chuo Kikuu akiwa na miaka 22 mwaka 1974, ukikokotoa vema ikaonena kuwa jaji Mkuu alianza shule akiwa na miaka minne. hofu ikaongezeka baada ya kuonekana kuwa Wenakae wote waliosoma naye darasa moja wanastaafu 2013, iweje sasa kustaafu kwake kuwe 2017? Iweje taarifa zake zikawa siri kuna nini kinafichwa? Je Ndugu yake ambaye ni Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa haionekani kuwa kulikuwa na Mgongano wa kimaslahi katika kumteua mdogo wake baada ya kumshauri Rais kama katiba inavyoelekeza. Huu ndio Mjadala, watu wajitokeze ili tusiingize nchi katika Historia ya Kughushi hadi Umri wa jaji Mkuu. Na kama amedanganya Umri ni kwa ajili ya nini?.......... mwaga jamvini.............